MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Januari 2014

Toleo hili linathibitisha kwamba Yehova amekuwa Mfalme sikuzote. Linatusaidia pia kuuthamini zaidi Ufalme wa Kimasihi na mambo ambayo umetimiza.

Walijitoa Wenyewe kwa Hiari—Afrika Magharibi

Ni nini kilichowachochea baadhi ya watu kutoka Ulaya kuhamia Afrika Magharibi na wamenufaika jinsi gani?

Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele

Kujifunza jinsi Yehova alivyotenda akiwa Baba na jinsi ambavyo ametumia mamlaka yake kutatuchochea kumkaribia zaidi.

Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme—Inakuhusuje?

Utawala wa Ufalme unaweza kutunufaishaje? Ona jinsi Mfalme wa Kimasihi anavyowasafisha, kuwafundisha, na kuwapanga raia zake.

Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana

Vijana wengi Wakristo waliojiweka wakfu wanapata mambo yaliyoonwa yenye kusisimua wanapowasaidia wengine. Utafanya nini ili ushiriki kikamili zaidi katika utumishi wa Yehova?

Kumtumikia Yehova Kabla Siku Zenye Msiba Hazijaja

Wakristo waliozeeka wana fursa gani za pekee za kupanua huduma yao?

“Ufalme Wako na Uje”—Lakini Utakuja Lini?

Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba hivi karibuni Mfalme aliyetiwa mafuta na Mungu atachukua hatua ili mapenzi ya Mungu yatimizwe kikamili duniani?

Uamuzi Niliofanya Utotoni

Mvulana mdogo kutoka Columbus, Ohio, Marekani aliamua kujifunza Kikambodia. Kwa nini? Uamuzi wake ulikuwa na matokeo gani maishani mwake?