MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Machi 2014

Katika toleo hili, jifunze jinsi ya kudumisha roho ya kujidhabihu na maoni yanayofaa. Tunawezaje kuwatunza waamini wenzetu na watu wa ukoo waliozeeka?

Kuifikia Mioyo ya Watu wa Ukoo Wasio Waamini

Tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Yesu alivyowatendea watu wake wa ukoo? Tunawezaje kuwaambia watu wetu wa ukoo wenye imani tofauti au wasio na dini yoyote kuhusu tunayoamini?

Jinsi ya Kudumisha Roho ya Kujidhabihu

Tunakabili adui mwenye hila anayeweza kudhoofisha roho yetu ya kujidhabihu. Makala hii inamtaja adui huyo na kuonyesha jinsi tunavyoweza kutumia Biblia kupambana naye.

Jinsi Tunavyoweza Kudumisha Maoni Yanayofaa

Kwa nini watu wengi hupambana na maoni yasiyofaa? Makala hii inatuonyesha jinsi tunavyoweza kutumia Biblia ili itusaidie kudumisha maoni yanayofaa kujihusu.

Ibada ya Familia—Je, Mnaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?

Hebu chunguza uone jinsi ibada ya familia inavyofanywa katika nchi mbalimbali na upate madokezo unayoweza kutumia.

Waheshimuni Ndugu na Dada Waliozeeka

Chunguza na uone maoni ya Mungu kuhusu waliozeeka. Watoto wana wajibu gani kuelekea wazazi wao waliozeeka? Makutaniko yanawezaje kuwaheshimu ndugu na dada waliozeeka?

Kuwatunza Waliozeeka

Wazazi waliozeeka na watoto wanaweza kukutana ili kuzungumzia matayarisho na maamuzi wanayoweza kufanya mapema kabla “siku zenye msiba” hazijaja. Wanawezaje kukabiliana na changamoto hizo?

Usemi Wako—Je, Unamaanisha “Ndiyo na pia Siyo”?

Wakristo wanapaswa kutimiza ahadi zao na hawapaswi kamwe kusema “ndiyo na pia siyo.” Namna gani tukilazimika kuvunja mpango fulani? Jifunze kutokana na mfano wa Mtume Paulo.