MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 3, 2014

Katika gazeti hili, utajifunza namna ya kuendelea kuonyesha roho ya kujitoa na kuendelea kuwa na maoni yanayofaa. Utaona pia na tunaweza kuwatunza ndugu na dada zetu na watu wa jamaa wenye kuzeeka.

Namna ya Kugusa Mioyo ya Watu wa Jamaa Wasio Mashahidi

Namna ambavyo Yesu aliwatendea watu wa jamaa yake inatufundisha nini? Namna gani tunaweza kuelezea watu wa jamaa mambo tunayoamini, ao hata wale wasiokuwa na dini?

Endelea Kuonyesha Roho ya Kujitoa

Kuna adui anayeweza kuharibu roho yetu ya kujitoa bila sisi kujua. Habari hii inatuonyesha adui huyo na namna Biblia inaweza kutusaidia tupambane naye.

Endelea Kuwa na Maoni Yanayofaa

Sababu watu wengi wanapambana na maoni yasiyofaa? Habari hii itakuonyesha namna Biblia inaweza kutusaidia tuendelee kuwa na maoni yanayofaa juu ya hali yetu.

Ibada ya Familia—Namna Gani Unaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?

Ona namna familia za inchi mbalimbali zinavyofanya ili ujue namna wewe pia unaweza kufanya.

Tuwaheshimu Ndugu na Dada Zetu Wenye Kuzeeka

Chunguza namna Mungu anavyowaona ndugu na dada wenye kuzeeka. Watoto ambao wamekuwa watu wazima wana madaraka gani kuelekea wazazi wao wenye kuzeeka? Namna gani kutaniko linaweza kuwaheshimu ndugu na dada wenye kuzeeka?

Namna ya Kuwatunza Watu Wenye Kuzeeka

Wazazi na watoto wanaweza kufanya mipango na kuchukua maamuzi mbele ya ‘siku zenye musiba.’ Namna gani wanaweza kupambana na matatizo ya kuwatunza wazazi wenye kuzeeka?

Je, Neno Lako Ni ‘Ndiyo, na Pia Siyo’?

Wakristo wanapaswa kutimiza mambo wanayosema na hawapaswe kusema ‘ndiyo na pia siyo.’ Namna gani ikiwa tunaona ni lazima tuvunje mapatano fulani? Mutume Paulo alituachia mufano muzuri.