MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 11, 2014

Gazeti hili lina habari za kujifunza za tarehe 29 Mwezi wa 12, 2014 mupaka tarehe 1 Mwezi wa 2, 2015.

Ufufuo wa Yesu Una Maana Gani Kwetu?

Kuko sababu ine zenye zinatuhakikishia kwamba Yesu alifufuliwa. Kuamini kwamba Yesu alifufuliwa kuna matokeo gani juu yetu?

Sababu Gani Tunapaswa Kuwa Watakatifu

Je, umekwisha kuchanganyikiwa ao kuvunjika moyo kwa sababu haukuelewa kitabu cha Mambo ya Walawi? Mambo mazuri sana yenye kupatikana katika kitabu hicho yanaweza kukusaidia umutolee Yehova utumishi mutakatifu.

Tunapaswa Kuwa Watakatifu Katika Mwenendo Wetu Wote

Kuna upatano gani kati ya kuendelea kuwa mushikamanifu, kumutolea Yehova kulingana na uwezo wetu, na kula chakula kigumu cha kiroho?

“Watu Ambao Mungu wao Ni Yehova”

Je, Mungu anakubali watu wenye mioyo mizuri ambao wanapatikana katika dini zote?

“Sasa Ninyi Ni Watu wa Mungu”

Namna gani tunaweza kuwa na kuendelea kuwa “Watu wa Mungu”?

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Namna gani wazee na watumishi wa huduma wanawekwa katika kila kutaniko? Mashahidi wawili ambao wanazungumuziwa katika Ufunuo sura 11 ni nani?

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Kweli ya Biblia Inafika Katika Inchi ya Japani

Magari yenye inaitwa “Yehu” yalijengwa ili kusaidia kazi ya kuhubiri Ufalme isonge mbele katika inchi ya Japani.