MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Juni 2019

Toleo hili lina makala za funzo za Agosti 5 hadi Septemba 1, 2019

“Jihadharini Ili Mtu Yeyote Asiwachukue Mateka”!

Shetani ni bingwa wa kuwapotosha watu. Yeye hujaribu jinsi gani kutupotosha ili tumwache Yehova?

Pindua Kila Wazo Ambalo Ni Kinyume cha Ujuzi wa Mungu!

Njia yetu ya kufikiri huathiriwa na malezi, utamaduni, na elimu yetu. Tunaweza kung’oa jinsi gani mambo yaliyokita mizizi akilini mwetu, yaliyo kama “ngome zenye nguvu”?

Mtegemee Yehova Unapopatwa na Mkazo

Mkazo mwingi kupita kiasi au unaodumu kwa muda mrefu unaweza kutuletea madhara ya kimwili na ya kihisia. Tunaweza kujifunza mambo mengi kutokana na jinsi Yehova alivyowasaidia watumishi wake nyakati za zamani kukabiliana na mkazo.

Wasaidie Wengine Kukabiliana na Mkazo

Loti, Ayubu, na Naomi walimtumikia Yehova kwa ushikamanifu, lakini bado walilazimika kuvumilia nyakati zenye mikazo. Tunaweza kujifunza nini kutokana na hali walizokabili?

Jilinde Usinaswe na Mtego Huu wa Shetani

Ponografia imewanasa watumishi wengi wa Mungu. Tunaweza kuepukaje zoea hilo chafu?

Kitabu cha Kukunjwa cha Zamani “Chakunjuliwa””

Katika mwaka wa 1970 wachimbuzi wa vitu vya kale walichimbua kitabu cha kukunjwa kilichokuwa kimeungua nchini Israel. Kwa msaada wa programu ya kidijitali ya kusoma picha, habari za kitabu hicho zinaweza kusomwa. Teknolojia hiyo imefunua nini?