Biblia Inatufundisha Nini?

Kitabu hiki cha kujifunzia Biblia kimekusudiwa kukusaidia ujifunze Biblia inasema nini kuhusu mambo mbalimbali, kutia ndani kwa nini tunateseka, inakuwaje tunapokufa, jinsi ya kuwa na familia yenye furaha, na mengine mengi.

Mungu Alituumba kwa Kusudi Gani?

Huenda ukashangaa kwa nini kuna matatizo mengi leo. Biblia inafundisha kwamba hivi karibuni Mungu atachukua hatua ili kuwaondolea wanadamu matatizo kama vile kuteseka, magonjwa, na kifo.

SURA YA 1

Mungu Ni Nani?

Je, unaamini kwamba Mungu anakujali? Jifunze kuhusu utu wake na jinsi unavyoweza kuwa rafiki ya Mungu.

SURA YA 2

Biblia​—Kitabu Kutoka Kwa Mungu

Biblia inaweza kukusaidia jinsi gani kukabili matatizo? Kwa nini unaweza kuutumaini unabii wa Biblia?

SURA YA 3

Kusudi la Mungu kwa Wanadamu Ni Nini?

Maisha yatakuwaje katika ulimwengu mpya dunia itakapokuwa paradiso?

SURA YA 4

Yesu Kristo Ni Nani?

Jifunze mambo yanayothibitisha kwamba Yesu alikuwa Masihi, alitoka wapi, na kwa nini anaitwa Mwana mzaliwa pekee wa Yehova?

SURA YA 5

Fidia​—Zawadi Bora Kutoka kwa Mungu

Fidia ni nini? Fidia inaweza kukufaidi jinsi gani?

SURA YA 6

Tukifa Tunaenda Wapi?

Jifunze yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu wafu waliko na kwa nini wanadamu hufa.

SURA YA 7

Kutakuwa na Ufufuo!

Je, umewahi kufiwa na mpendwa wako? Je, inawezekana kumwona tena? Jifunze yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu ufufuo

SURA YA 8

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Watu wengi wanaijua ile Sala ya Bwana. Maneno: “Ufalme Wako na Uje” yanamaanisha nini?

SURA YA 9

Je, Mwisho wa Dunia Uko Karibu?

Chunguza jinsi matendo na mitazamo ya watu wanaotuzunguka inavyothibitisha kwamba tunaishi mwishoni mwa siku za mwisho wa dunia, kama Biblia ilivyotabiri.

SURA YA 10

Ukweli Kuhusu Malaika

Biblia inazungumzia kuhusu malaika na roho waovu. Je, viumbe hao roho ni halisi? Je, wanaweza kutusaidia au kutudhuru?

SURA YA 11

Kwa Nini Kuna Mateso Mengi Ulimwenguni?

Watu wengi wanafikiri kwamba Mungu ndiye wa kulaumiwa kwa sababu ya mateso yote ulimwenguni. Wewe una maoni gani? Jifunze yale ambayo Mungu anasema kuhusu sababu za kuteseka.

SURA YA 12

Jinsi Unavyoweza Kuwa Rafiki ya Mungu

Tunaweza kuishi maisha yanayompendeza Yehova. Bila shaka, unaweza kuwa rafiki yake.

SURA YA 13

Heshimu Zawadi ya Uhai

Mungu anahisije kuhusu, kutoa mimba, kutiwa damu mishipani, na uhai wa wanyama?

SURA YA 14

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha

Waume, wake, wazazi, na watoto wanaweza kuiga mfano wa Yesu katika kuonyesha upendo. Tunajifunza nini kutoka kwa Yesu?

SURA YA 15

Jinsi ya Kumwabudu Mungu Kwa Njia Inayofaa

Jifunze mambo sita yanayotambulisha dini ya kweli.

SURA YA 16

Amua Kumwabudu Mungu

Huenda ukakabili upinzani gani unapowaambia wengine imani yako? Unaweza kufanya hivyo jinsi gani bila kuwaudhi?

SURA YA 17

Zawadi ya Sala

Je, Mungu anasikiliza unaposali? Ili kujibu swali hilo unahitaji kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu sala.

SURA YA 18

Je, Ninapaswa Kujiweka Wakfu kwa Mungu na Kubatizwa?

Ni hatua gani zinahitajiwa ili kustahili kwa ajili ya ubatizo wa Kikristo? Jifunze kile unachowakilisha na jinsi unavyopaswa kufanywa.

SURA YA 19

Kaa Karibu na Yehova

Tunawezaje kuonyesha upendo na shukrani kwa mambo yote ambayo Mungu ametufanyia?

Maelezo ya Ziada

Maana ya maneno na vifungu vya maneno yaliyotumiwa katika kitabu Biblia Inatufundisha Nini?