Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Mashahidi wa Yehova wanapatikana ulimwenguni pote na wametoka katika jamii zote na tamaduni mbalimbali. Ni nini kinachowaunganisha?

Mapenzi ya Mungu Ni Nini?

Mungu anataka mapenzi yake yajulikane ulimwenguni pote. Mapenzi yake ni nini, na ni nani leo wanaowafundisha watu kuyahusu?

SOMO 1

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina Gani?

Unawajua Mashahidi wa Yehova wangapi? Ni mambo gani hasa unayojua kutuhusu?

SOMO 2

Kwa Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?

Chunguza sababu tatu zilizofanya tuitwe hivyo.

SOMO 3

Kweli za Biblia Zilifunuliwaje Tena?

Tunawezaje kuwa na uhakika kwamba tumeelewa kwa usahihi mambo ambayo Biblia inafundisha?

SOMO 4

Kwa Nini Tumechapisha Tafsiri ya Ulimwengu Mpya?

Ni nini kinachofanya tafsiri hii ya Neno la Mungu iwe ya pekee?

SOMO 5

Utaona Mambo Gani Katika Mikutano Yetu ya Kikristo?

Tunahudhuria mikutano ili kujifunza Maandiko na kutiana moyo. Unakaribishwa kwa uchangamfu!

SOMO 6

Tunafaidikaje kwa Kushirikiana na Wakristo Wenzetu?

Neno la Mungu linawatia moyo Wakristo washirikiane. Jifunze jinsi unavyoweza kunufaika na ushirikiano huo.

SOMO 7

Mikutano Yetu Hufanywaje?

Je, umewahi kuwazia mambo yanayofanyika katika mikutano yetu? Bila shaka utafurahi kuona elimu ya Biblia ya kiwango cha juu inayopatikana hapo.

SOMO 8

Kwa Nini Tunavalia Vizuri Tunapohudhuria Mikutano?

Je, Mungu anakazia uangalifu jinsi tunavyovaa? Jifunze kanuni za Biblia zinazotuongoza tunapochagua mavazi na mapambo.

SOMO 9

Ni Njia Gani Bora ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Mikutano?

Kujitayarisha vizuri kwa ajili ya mikutano kutatusaidia tufaidike.

SOMO 10

Ibada ya Familia Ni Nini?

Chunguza jinsi mpango huu unavyoweza kukusaidia umkaribie Mungu na kuimarisha ndoa yako.

SOMO 11

Kwa Nini Tunahudhuria Makusanyiko?

Kila mwaka, tunakutana pamoja mara tatu kwa ajili ya matukio ya pekee. Unaweza kufaidikaje na matukio hayo?

SOMO 12

Kazi Yetu ya Kuhubiri Ufalme Hufanywaje?

Sisi hufuata utaratibu ambao Yesu alitumia alipokuwa duniani. Tunahubiri wapi?

SOMO 13

Painia Ni Nani?

Baadhi ya Mashahidi hutumia saa 30, 50, au zaidi kila mwezi katika kazi ya kuhubiri. Ni nini huwachochea kufanya hivyo?

SOMO 14

Mapainia Huzoezwa Katika Shule Gani?

Wahubiri wa Ufalme wa wakati wote hupata mazoezi gani ya pekee?

SOMO 15

Wazee Hulitumikia Kutaniko Jinsi Gani?

Wazee ni wanaume wakomavu kiroho ambao wanaongoza katika kutaniko. Wazee hufanya kazi gani?

SOMO 16

Watumishi wa Huduma Wana Majukumu Gani?

Watumishi wa huduma hulisaidia kutaniko. Jifunze jinsi ambavyo kazi yao huwafaidi wote wanaohudhuria mikutano.

SOMO 17

Waangalizi wa Mzunguko Wanatusaidiaje?

Kwa nini waangalizi wa mzunguko hutembelea makutaniko? Unaweza kufaidika jinsi gani kutokana na ziara zao?

SOMO 18

Tunawasaidiaje Ndugu Zetu Wakati wa Taabu?

Janga linapotokea, mara moja sisi hupanga kutoa msaada wa kimwili na faraja ya kiroho kwa wale waliokumbwa na janga. Tunafanyaje hivyo?

SOMO 19

Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara Ni Nani?

Yesu aliahidi kwamba angemweka rasmi mtumwa ili kuandaa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa. Chakula hicho huandaliwaje?

SOMO 20

Baraza Linaloongoza Hufanyaje Kazi Leo?

Katika karne ya kwanza, kikundi kidogo cha mitume na wanaume wazee kilitumikia kikiwa baraza linaloongoza la kutaniko la Kikristo. Namna gani leo?

SOMO 21

Betheli Ni Nini?

Betheli ni eneo la pekee sana lililo na kusudi muhimu. Jifunze habari zaidi kuhusu wale wanaotumikia hapo.

SOMO 22

Ni Kazi Gani Zinazofanywa Katika Ofisi ya Tawi?

Wageni wanakaribishwa kutembelea ofisi yoyote ya tawi. Wewe pia unakaribishwa!

SOMO 23

Jinsi Machapisho Yetu Yanavyoandikwa na Kutafsiriwa

Tunatayarisha machapisho katika lugha zaidi ya 750. Kwa nini tunafanya kazi yote hiyo?

SOMO 24

Kazi Yetu ya Ulimwenguni Pote Inagharimiwaje?

Inapohusu gharama za uendeshaji, tengenezo letu lina tofauti gani na dini nyingine?

SOMO 25

Majumba ya Ufalme Yanajengwa Jinsi Gani na Kwa Nini?

Kwa nini majengo yetu ya ibada yanaitwa Majumba ya Ufalme? Jifunze habari zaidi kuhusu jinsi majengo hayo yanavyosaidia makutaniko yetu.

SOMO 26

Tunaweza Kusaidiaje Kudumisha Jumba Letu la Ufalme?

Jumba la Ufalme safi na lililodumishwa vizuri linamtukuza Mungu wetu. Ni mipango gani inayofanywa ili kutunza Jumba la Ufalme?

SOMO 27

Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutunufaisha Jinsi Gani?

Je, ungependa kufanya utafiti fulani ili uweze kuielewa Biblia vizuri? Tembelea maktaba ya Jumba la Ufalme!

SOMO 28

Ni Habari Gani Zinazopatikana Kwenye Tovuti Yetu?

Unaweza kujifunza mengi kutuhusu na kuhusu imani yetu pamoja na kupata majibu ya maswali ya Biblia.

Je, Utafanya Mapenzi ya Yehova?

Yehova Mungu anakupenda kikweli. Unaweza kuonyeshaje tamaa yako ya kufanya mapenzi Yake katika maisha yako ya kila siku?