Ona video zinazopatikana

SEHEMU YA 6

Yobu Anaendelea Kuwa Mushikamanifu

Yobu Anaendelea Kuwa Mushikamanifu

Shetani alisema kama Yobu hataendelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova, lakini Yobu anaendelea kuwa mushikamanifu

MWANADAMU anaweza kuendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu kama maisha yake iko mu hatari, na kama hapate faida yoyote kwa sababu ya kumutii Mungu? Mambo yenye ilimufikia mwanaume mwenye kuitwa Yobu, ilisaidia kujibia ile ulizo.

Yobu alikuwa mutu wa jamaa ya Abrahamu, na alikuwa anaishi Arabia wakati Waisraeli walikuwa wangali watumwa Misri. Ile wakati, malaika walikusanyika mbele ya Mungu, na Shetani malaika muasi, naye alikuwa pale. Yehova alisifu ushikamanifu wa Yobu mbele ya malaika wote. Alisema kama ku dunia hakukukuwa mutu mwingine mwenye alikuwa mushikamanifu sawa Yobu. Lakini, Shetani alisema kama Yobu alikuwa namutumikia Mungu juu tu Mungu alikuwa namubariki na kumulinda. Na alisema kama ikiwa Yobu anapoteza mali yake yote, atamukana Mungu.

Mungu aliruhusu Shetani afanye Yobu apoteze mali yake yote na watoto wake na kisha akamuruhusu amuletee ugonjwa. Yobu hakujua kama Shetani njo alimuletea ile magumu yote. Kwa hiyo hakuelewa juu ya nini Mungu alikuwa naruhusu apate ile magumu. Lakini, Yobu hakumukana Mungu.

Marafiki tatu wa Yobu walikuya kumutembelea, lakini walimushitaki mambo ya uongo. Waliambia Yobu kama Mungu njo alikuwa namupatia malipizi juu ya zambi zenye alishakafichika. Na hata, walisema kama Mungu hapendi na hatumainiake watumishi wake. Yobu hakukubali ile mawazo yao ya uongo. Aliwaambia kama ataendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu mupaka kifo!

Lakini Yobu alikosea, alijitetea-tetea sana. Kisha kijana Elihu, mwenye alikuwa nasikiliza mazungumuzo yao, akaanza kuzungumuza. Alimurekebisha Yobu juu Yobu alikuwa najihangaikia sana na kujitetea kuliko kumutetea Yehova. Elihu alirekebisha pia marafiki wa Yobu.

Yehova naye alizungumuza na Yobu, na akamusaidia kurekebisha mawazo yake. Alitumia uumbaji juu ya kumuonyesha kama wanadamu ni wa hali ya chini sana kwa kulinganishwa na Mungu. Yobu alijishusha na akakubali Mungu amurekebishe. Na juu Yehova ni “mwenye upendo mwingi sana na mwenye rehema,” alimurudishia Yobu afya yake, akamurudishia mali yake mara mbili, na akamupatia watoto kumi. (Yakobo 5:11) Yobu aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova hata wakati alipata majaribu. Kwa kufanya vile, alionyesha kama Shetani alikosea wakati alisema kama hakuna mwanadamu mwenye anaweza kuendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu, wakati anajaribiwa.

​—Hii Habari inategemea kitabu ya Yobu.