Hamia kwenye habari

FEBRUARI 11, 2021
LIBERIA

Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Yatolewa Katika Kikisi

Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Yatolewa Katika Kikisi

Februari 7, 2021, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa katika lugha ya Kisi. Watafsiri walifanya kazi ya kutafsiri kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu.

Ndugu Joseph Mensah ambaye ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Liberia alitoa Biblia hiyo katika programu iliyorekodiwa mapema.

Biblia zilizochapishwa zilisafirishwa kutoka ofisi ya tawi ya Ulaya ya Kati hadi Guinea, Liberia, na Sierra Leone. Wahubiri 1,200 hivi wanaozungumza Kikisi walipewa Biblia hizo huku miongozo ya kujilinda dhidi ya ugonjwa wa COVID-19 ikizingatiwa.

Kikundi cha watafsiri watatu kilifanya kazi ya kutafsiri. Mmoja wa watafsiri hao alisema hivi: “Akina ndugu wanaozungumza Kikisi watafurahi kusoma Biblia hii kwa sababu ni rahisi kuielewa. Itawasaidia watu wa Kisi kujifunza kweli na kuipenda.”

Mtafsiri wa pili anasema hivi: “Biblia hii ni zawadi ya pekee kutoka kwa Yehova, ambayo kwa upendo amenipa mimi na watu wote wanaozungumza lugha ya Kisi.”

Tuna uhakika kwamba toleo hili litawasaidia ndugu zetu waendelee kuwa wasikiaji na watendaji wa neno la Mungu.—Yakobo 1:22.