JANUARI 21, 2022
URUSI
Mashahidi wa Yehova Katika Eneo la Irkutsk Wadumisha Uaminifu Licha ya Kuvamiwa kwa Ukatili Nyumbani
Oktoba 4, 2021, nyumba za Mashahidi wa Yehova zilivamiwa katika eneo la Irkutsk. Maofisa wa polisi waliwahoji na kuwapiga kikatili. Mashahidi sita wa Yehova walipelekwa mahabusu kwa sababu tu ya kushiriki imani yao ya Kikristo kwa amani.