Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu

Biblia ina kanuni na inatufundisha viwango vya maadili vinavyoweza kutusaidia kudumu katika upendo wa Mungu.

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova linawasihi wote wanaompenda Yehova Mungu wajifunze jinsi ya kuishi kupatana na kweli ya Neno lake, Biblia.

SURA YA 1

Upendo wa Mungu Unadumu Milele

Jitihada zinahitajika ili kudumisha urafiki imara na wa karibu pamoja na Mungu. Tunaweza kufanya nini ili tufaulu kufanya hivyo?

SURA YA 2

Dhamiri Njema Mbele za Mungu

Mungu ametupa sisi sote kitu cha kutuongoza ili tujue njia tunayopaswa kufuata maishani.

SURA YA 3

Chagua Marafiki Wanaompenda Mungu

Marafiki wanaweza kutusaidia au kutudhuru. Kanuni za Biblia zinaweza kutusaidiaje tunapochagua marafiki wazuri?

SURA YA 4

Kwa Nini Unapaswa Kuheshimu Mamlaka?

Tuna sababu nzuri za kuheshimu mamlaka katika familia, kutanikoni, na katika jamii.

SURA YA 5

Jinsi ya Kujitenga na Ulimwengu

Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Ninyi si sehemu ya ulimwengu.” Huo ‘ulimwengu’ ni upi, na kwa nini Wakristo wanapaswa kujitenga nao?

SURA YA 6

Jinsi ya Kuchagua Burudani

Burudani ya ulimwengu huu ni kama tunda lililo na sehemu nzuri na nyingine zimeoza. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuchagua sehemu nzuri na kuepuka sehemu mbaya?

SURA YA 7

Je, Una Maoni Kama ya Mungu Kuhusu Uhai?

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutusaidia kufanya maamuzi mazuri kuhusu uhai na damu?

SURA YA 8

Yehova Anataka Watu Wake Wawe Safi

Viwango vya Mungu vya usafi vinahusisha mengi zaidi ya miili, mavazi, na nyumba zetu. Vinahusisha ibada, mwenendo, na hata mawazo yetu.

SURA YA 9

“Ukimbieni Uasherati!”

Uasherati ni nini, na tunaweza kuukimbiaje?

SURA YA 10

Ndoa​​—Zawadi Kutoka kwa Mungu

Ndoa ina faida zipi? Ni nini kinachoweza kukusaidia kuchagua mwenzi anayefaa? Ni nini kinachoweza kusaidia ndoa idumu?

SURA YA 11

Baada ya Siku ya Harusi

Ndoa zote hukabili matatizo mara kwa mara. Hata hivyo, hata wenzi wa ndoa ambao wamekabili matatizo mazito wanaweza kuwa na ndoa imara.

SURA YA 12

Sema Lililo “Jema kwa Ajili ya Kujenga”

Maneno yanaweza kuwatia moyo wengine au kuwadhuru. Yehova anatufundisha jinsi ya kutumia zawadi ya usemi kwa njia nzuri.

SURA YA 13

Je, Sherehe Zote Zinampendeza Mungu?

Sherehe na sikukuu ni muhimu katika maisha ya watu. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuelewa Mungu anahisije kuhusu sherehe hizo?

SURA YA 14

Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote

Fikiria maeneo manne maishani ambapo inaweza kuwa vigumu kudumisha unyoofu na faida tunazopata kwa kufanya hivyo.

SURA YA 15

Furahia Kazi Yako

Muumba anataka tufurahie kazi yetu. Kwa hiyo, ni nini kinachoweza kutusaidia tufurahie kazi yetu? Na je, kuna kazi ambazo Wakristo hawapaswi kufanya?

SURA YA 16

Mpingeni Ibilisi

Tunaishi katika ulimwengu unaodhibitiwa na Shetani. Tunawezaje kuendelea kukaa karibu na Mungu na kujilinda dhidi ya Shetani Ibilisi?

SURA YA 17

Dumu Katika Upendo wa Mungu

Mwandikaji mmoja wa Biblia aliwatia moyo Wakristo: “Jijengeni juu ya imani yenu takatifu zaidi.” Unawezaje kufanya hivyo?

Maelezo ya Ziada

Maana ya maneno yaliyo katika kitabu Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu.