Esta 8:1-17

  • Mordekai apandishwa cheo (1, 2)

  • Esta amsihi mfalme (3-6)

  • Mfalme atoa agizo lingine (7-14)

  • Wayahudi wapata kitulizo na kushangilia (15-17)

8  Siku hiyo Mfalme Ahasuero akampa Malkia Esta nyumba* ya Hamani+ aliyekuwa adui ya Wayahudi;+ naye Mordekai akaja mbele ya mfalme, kwa maana Esta alikuwa amemfunulia kuhusu uhusiano wao wa kifamilia.+  Kisha mfalme akavua pete yake ya muhuri+ aliyokuwa amempokonya Hamani, akampa Mordekai. Naye Esta akamweka Mordekai kuwa msimamizi wa nyumba ya Hamani.+  Zaidi ya hayo, Esta akazungumza tena na mfalme. Akaanguka chini miguuni pake, akalia na kumsihi mfalme akomeshe madhara ya Hamani Mwagagi na njama aliyopanga dhidi ya Wayahudi.+  Mfalme akamnyooshea Esta fimbo ya ufalme ya dhahabu,+ naye Esta akainuka na kusimama mbele ya mfalme.  Esta akasema: “Ukipenda Ee mfalme na ikiwa nimepata kibali chako, na ikiwa ni jambo jema kwako mfalme, nawe umependezwa nami, acha agizo liandikwe la kufuta barua za njama ya Hamani+ mwana wa Hamedatha Mwagagi,+ alizoandika ili kuwaangamiza Wayahudi katika mikoa yote ya* mfalme.  Kwa maana ninawezaje kuvumilia kuona msiba utakaowapata watu wangu, na ninawezaje kuvumilia kuona watu wangu wa ukoo wakiangamizwa?”  Basi Mfalme Ahasuero akamwambia Malkia Esta na Mordekai Myahudi: “Tazama! Nimempa Esta nyumba ya Hamani,+ naye Hamani ametundikwa mtini,+ kwa sababu alipanga njama ya kuwashambulia* Wayahudi.  Sasa andikeni katika jina la mfalme jambo lolote mnaloona linafaa kwa niaba ya Wayahudi nanyi mlitie muhuri kwa pete ya mfalme, kwa maana agizo lililoandikwa katika jina la mfalme na kutiwa muhuri kwa pete ya mfalme haliwezi kufutwa.”+  Ndipo waandishi wa mfalme wakaitwa wakati huo katika mwezi wa tatu, yaani, mwezi wa Sivani,* siku ya 23, wakaandika mambo yote ambayo Mordekai aliwaamuru Wayahudi, na pia maliwali,+ magavana, na wakuu wa mikoa*+ kuanzia India mpaka Ethiopia, mikoa* 127, kila mkoa* kwa mwandiko wake wenyewe* na kila kikundi cha watu kwa lugha yao wenyewe na kwa Wayahudi katika mwandiko wao wenyewe* na lugha yao. 10  Aliandika agizo hilo katika jina la Mfalme Ahasuero na kulitia muhuri kwa pete ya mfalme,+ kisha akatuma barua za agizo hilo kupitia wajumbe walioendesha farasi; farasi hao wenye mbio walitumiwa kusafirisha barua, nao walizalishwa kwa ajili ya utumishi wa mfalme. 11  Katika barua hizo mfalme aliwaruhusu Wayahudi katika majiji yote wakusanyike ili walinde uhai wao* na kuangamiza, kuua, na kuharibu jeshi lolote la taifa lolote au mkoa* ambao huenda ungewashambulia wao, kutia ndani wanawake na watoto wao, na kuchukua mali zao.+ 12  Wangefanya hivyo siku ileile katika mikoa yote ya* Mfalme Ahasuero, siku ya 13 ya mwezi wa 12, yaani, mwezi wa Adari.*+ 13  Maandishi* ya agizo hilo yalipaswa kutangazwa kuwa sheria katika mikoa yote.* Watu wote walipaswa kutangaziwa agizo hilo, ili Wayahudi wajitayarishe siku hiyo kulipiza kisasi dhidi ya maadui wao.+ 14  Wajumbe walioendesha farasi wa kusafirisha barua waliotumiwa katika utumishi wa mfalme wakaondoka haraka na kwa kasi kulingana na agizo la mfalme. Sheria hiyo ilitangazwa pia katika ngome ya* Shushani.*+ 15  Naye Mordekai akatoka mbele ya mfalme akiwa amevaa mavazi ya kifalme ya rangi ya bluu na nyeupe, taji kubwa la dhahabu, na joho la kitambaa bora cha sufu ya zambarau.+ Na jiji la Shushani* likapiga kelele kwa shangwe. 16  Wayahudi wakapata kitulizo,* wakafurahi, wakashangilia, na kupata heshima. 17  Na katika mikoa yote* na majiji yote, popote ambapo agizo la mfalme na sheria yake ilifika, Wayahudi walifurahi na kushangilia, wakafanya karamu na kusherehekea. Watu wengi wa mataifa yaliyokuwa nchini walikuwa wakijitangaza kuwa Wayahudi,+ kwa maana waliwaogopa Wayahudi.

Maelezo ya Chini

Au “mali yote.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Tnn., “aliunyoosha mkono wake kwa nguvu dhidi ya.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “mtindo wao wenyewe wa kuandika.”
Au “mtindo wake wenyewe wa kuandika.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “wilaya za utawala.”
Au “nafsi zao.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “wilaya zote za utawala za.”
Au “wilaya zote za utawala.”
Au “Nakala.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “Susa.”
Tnn., “wakaona nuru.”
Au “wilaya zote za utawala.”