Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Har–Magedoni—Watu Wana Maoni Gani?

Har–Magedoni—Watu Wana Maoni Gani?

Har–Magedoni​—Watu Wana Maoni Gani?

“Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har–Magedoni.”​—UFUNUO 16:16, Union Version.

NI JAMBO gani linalokuja akilini unaposikia neno “Har–Magedoni”? Labda unawazia msiba mkubwa sana. Ingawa neno hilo linapatikana mara moja tu katika Biblia, linatajwa mara nyingi na vyombo vya habari na hata viongozi wa kidini.

Je, maoni ya watu wengi kuhusu Har–Magedoni yanapatana na mambo ambayo Biblia inafundisha? Ni muhimu kujua jibu la swali hilo. Kwa nini? Kwa sababu ukweli kuhusu Har–Magedoni unaweza kukuondolea wasiwasi, kukusaidia uwe na maoni yanayofaa kuhusu wakati ujao, na hata kubadili maoni yako kumhusu Mungu.

Fikiria maswali matatu yanayofuata, kisha ulinganishe maoni ya watu wengi kuhusu Har–Magedoni na mambo ambayo Biblia inafundisha.

1. JE, HAR–MAGEDONI NI MSIBA UTAKAOSABABISHWA NA WANADAMU?

Mara nyingi, waandishi wa habari na watafiti hutumia neno “Har–Magedoni” kufafanua misiba inayosababishwa na wanadamu. Kwa mfano, Vita vya Kwanza na vya Pili vya Ulimwengu vimerejelewa kuwa Har–Magedoni. Baada ya vita hivyo, wanadamu walikuwa na wasiwasi kwamba nchi za Marekani na Muungano wa Sovieti zingepigana zikitumia silaha za atomi. Vyombo vya habari viliita vita hivyo ambavyo havikupiganwa, “Har–Magedoni itakayosababishwa na silaha za atomi.” Leo, watafiti ambao wana wasiwasi kuwa uchafuzi wa mazingira utasababisha mabadiliko makubwa katika hali ya hewa duniani, wanaonya kwamba hivi karibuni kutakuwa na “Har–Magedoni itakayosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa.”

Ufafanuzi wao unamaanisha nini?: Wanadamu ndio tu wanaoweza kuamua jinsi wakati ujao wa dunia na uhai utakavyokuwa. Ikiwa serikali hazitatenda kwa hekima, basi dunia itaharibiwa kabisa.

Biblia inafundisha nini?: Mungu hatawaruhusu wanadamu waiharibu dunia. Biblia inatuhakikishia kwamba Yehova * hakuiumba dunia “bila sababu,” bali aliiumba “ili ikaliwe na watu.” (Isaya 45:18) Badala ya kuruhusu dunia iharibiwe na wanadamu, Mungu “[ata]waharibu wale wanaoiharibu dunia.”—Ufunuo 11:18.

2. JE, HAR–MAGEDONI NI MSIBA WA ASILI?

Nyakati nyingine, wanahabari hutumia neno “Har–Magedoni” kumaanisha msiba mkubwa wa asili. Kwa mfano, mwaka wa 2010, ripoti moja ilizungumza kuhusu “‘Har–Magedoni’ nchini Haiti.” Ilizungumzia kuteseka, uharibifu, na vifo vilivyotokana na tetemeko kubwa la ardhi lililoikumba nchi hiyo. Wanahabari na watengeneza filamu wanatumia neno hilo wanaporejelea matukio ambayo tayari yametukia na pia yale wanayohofia kwamba yatatukia. Kwa mfano, wametumia neno “Har–Magedoni” wanaporejelea uharibifu wanaofikiri utatokea wakati jiwe fulani la angani litakapogonga dunia.

Ufafanuzi wao unamaanisha nini?: Har–Magedoni ni tukio ambalo litaangamiza watu wazuri na waovu. Huwezi kufanya lolote ili kuepuka maangamizi hayo.

Biblia inafundisha nini?: Har–Magedoni si tukio ambalo litaangamiza watu wazuri na waovu. Badala yake, watu waovu tu ndio watakaoharibiwa wakati wa Har–Magedoni. Biblia inaahidi kwamba hivi karibuni “mtu mwovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo.”—Zaburi 37:10.

3. JE, MUNGU ATAHARIBU DUNIA KWENYE HAR–MAGEDONI?

Watu wengi wa kidini wanaamini kwamba kutakuwa na vita vya mwisho kati ya wema na uovu ambavyo vitaangamiza sayari yetu. Utafiti uliofanywa nchini Marekani na Kikundi cha Watafiti cha Princeton ulisema kwamba asilimia 40 ya watu waliohojiwa wanaamini kuwa dunia itaharibiwa katika “vita vya Har–Magedoni.”

Mafundisho yao yanamaanisha nini?: Wanadamu hawakukusudiwa kuishi duniani milele, wala dunia haikukusudiwa kudumu milele. Mungu aliwaumba wanadamu akiwa na lengo la kwamba siku moja wote watakufa.

Biblia inafundisha nini?: Biblia inasema waziwazi kwamba Mungu “ameiwekea dunia msingi juu ya mahali pake palipofanywa imara; haitatikiswa mpaka wakati usio na kipimo, au milele.” (Zaburi 104:5) Kuhusu wakaaji wa duniani, Biblia inasema: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.”—Zaburi 37:29.

Ni wazi kwamba Biblia inapinga maoni mbalimbali yanayopendwa na watu wengi kuhusu Har–Magedoni. Hivyo ukweli ni upi?

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 9 Katika Biblia, jina la kibinafsi la Mungu ni Yehova.