MATUKO MUHIMU YA MWAKA ULIOPITA
Nuru Yazidi Kuongezeka
KWA KUWA waabudu wa kweli wanaamini kwamba Yehova ni Chanzo cha nuru ya kiroho, husali kwa bidii ‘nuru na kweli’ ya Mungu iwaongoze. (Zab. 43:3) Ingawa ulimwengu uko katika giza zito la kiroho, Mungu wa kweli anaendelea kuwaangazia nuru watu wake. Hivyo, njia yao ni ‘ni kama nuru inayong’aa na inayozidi kuongezeka.’ (Met. 4:18) Nuru ya Yehova inayoongezeka inaendelea kuwaangazia kitengenezo, kimafundisho na kimaadili. Ni baadhi ya uelewaji gani mpya ambao tumepata hivi karibuni?