Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kuadhimisha Ukumbusho—Ijumaa, Aprili 3, 2015

Kuadhimisha Ukumbusho—Ijumaa, Aprili 3, 2015

JUMAMOSI ya Machi 7, 2015, makutaniko ulimwenguni pote yalianza kampeni ya majuma manne ya kuwaalika watu wengi kadiri iwezekanavyo kuhudhuria ukumbusho wa kifo cha Yesu Kristo na kusikiliza hotuba iliyozungumzia jinsi tunavyofaidika na kifo chake. Mamilioni ya watu walipewa mialiko moja kwa moja, kupitia simu, au barua pepe. Matokeo yangekuwaje? Mashahidi wa Yehova walifurahia sana kuwakaribisha watu 19,862,783 siku ya Ijumaa Aprili 3, katika tukio hilo takatifu. Sasa jitihada nyingi zinafanywa ili kuwasaidia wote waliohudhuria Ukumbusho washirikiane na watu wa Yehova kwa ukawaida ili kumwabudu Mungu wa kweli, na kufurahia upendo na baraka zake nyingi.—Mika 4:2.