Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

INDONESIA

Painia wa Pekee kwa Miaka Hamsini

Alisten Lumare

Painia wa Pekee kwa Miaka Hamsini
  • ALIZALIWA 1927

  • ALIBATIZWA 1962

  • HISTORIA FUPI Aliyekuwa inspekta wa polisi alitumikia akiwa painia wa pekee kwa zaidi ya miaka 50.

MWAKA wa 1964, nilipewa mgawo wa kuwa painia wa pekee huko Manokwari, West Papua, katika kutaniko dogo lililokuwa likikabili upinzani mkali wa viongozi wa kidini wa eneo hilo. Mara tu nilipowasili, mhudumu wa Kiprotestanti alivamia nyumba yangu.

Akafoka: “Nitavunja nyumba hii na kuwafutilia mbali Mashahidi wa Yehova hapa Manokwari.”

Sikuogopa kwa sababu nilikuwa nimepata mafunzo ya kijeshi. Hata hivyo, nilimjibu kwa utulivu, na mwishowe akaondoka kwa amani.—1 Pet. 3:15.

Wakati huo kulikuwa na wahubiri wanane katika eneo la Manokwari. Baada ya miaka 50 hivi, sasa kuna makutaniko saba katika eneo hilo. Zaidi ya watu 1,200 walihudhuria kusanyiko la eneo mwaka wa 2014. Ninapoona mambo ambayo Yehova ametimiza katika eneo hili la kijijini, moyo wangu unafarijika sana.