Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Kuheshimia Wakati

Kuheshimia Wakati

Hata watu wenye wanazoea kuchelewa wanaamini kama ni muzuri kuheshimia wakati. Biblia inatoa mashauri yenye hekima kuhusu jambo hilo.

Ni jambo la lazima kuheshimia wakati?

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA?

Watu fulani wameona kama kufika mbele ya wakati mahali penye walipanga kukutana na mutu ao watu fulani, kunatuliza akili. Mutu mwenye kuheshimia wakati anapata sifa nzuri zaidi kutoka kwa watu wengine. Namna gani?

Kuheshimia wakati kunaonyesha kama uko na uwezo wa kupanga mambo muzuri. Kama unaheshimia wakati, unaonyesha kwamba unajikaza kupanga mambo yote katika maisha yako, kuliko kuruhusu hali fulani zikuzuie kufanya mambo yenye unapenda.

Kuheshimia wakati kunaweza kufanya wengine wakutumainie. Watu wengi hawatimize ahadi zao na wanavunja mapatano, kwa hiyo, watu wanafurahia wale wenye kutimiza ahadi zao. Watu wenye kutumainika wanaheshimiwa na marafiki wao na watu wa familia yao. Wakubwa wa kazi wanapendezwa na watu wenye wanafika kwa wakati kwenye kazi na ambao wanaheshimia wakati wenye walipewa ili kumaliza kazi fulani. Wakubwa hao wanaweza hata kuwaongezea mushahara na kuwatumainia sana.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

Biblia iko na Maandiko yenye kutusaidia kuelewa mambo fulani juu ya kuheshimia wakati. Kwa mufano, Biblia inasema hivi: ‘Mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mupango.’ (1 Wakorintho 14:40) Wakati watu wanapanga kukutana mahali na saa fulani, ni jambo la adabu na lenye kufaa waheshimie wakati. Biblia inasema tena hivi: “Kuna wakati uliowekwa wa kila kitu, hata kuna wakati wa kila jambo chini ya mbingu.” (Mhubiri 3:1) Andiko lenye kufuata kisha andiko hilo, linasema kama kuko “wakati wa kupanda na wakati wa kungoa.” (Mhubiri 3:2) Walimaji wanapanda mimea kwa wakati wenye kufaa ili waweze kupata mavuno mengi. Ni kusema, mulimaji anapata matokeo ya muzuri kwa sababu ya kuheshimia wakati.

Biblia inatoa sababu ingine ya maana zaidi ya kuheshimia wakati: Kuheshimia wakati kunaonyesha kwamba tunaheshimia wengine na wakati wao wenye kuwa wa lazima. (Wafilipi 2:3, 4) Lakini, wale wenye wanazoea kuchelewa wanaiba wakati wa wengine.

‘Mukiendelea kuangalia, si faida za kibinafsi za mambo yenu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.’​Wafilipi 2:4.

Unaweza kufanya nini ili kuheshimia wakati?

MAMBO BIBLIA INASEMA:

Biblia inatutia moyo kupanga mambo mbele ya wakati. (Methali 21:5) Kama unazoea kuchelewa, pengine uko na mambo mengi sana ya kufanya. Ni muzuri uondoe mambo yenye haiko ya lazima yenye kula wakati. Ujiwekee wakati wa kutosha mbele ya saa yenye mulipanga kukutana na mutu ao watu fulani, na ujikaze kufika kwa wakati. Hilo litakusaidia wakati mambo yenye hautazamie yanatokea, kama vile musongamano wa motokari ao hali ya hewa yenye kuwa mubaya.

Pia Biblia inatutia moyo tukuwe na kiasi. (Methali 11:2) Hilo linamaanisha kujua mipaka yako. Mbele ya kukubali kama utaweza kuwa mahali fulani kwa wakati fulani ao utaweza kumaliza kazi fulani kwa muda wenye ulipewa, chunguza programu yako ili ujue ikiwa inawezekana kabisa. Ikiwa unakubali ao unapanga kufanya mambo mengi yenye hautaweza, unajiongezea mahangaiko ya akili wewe mwenyewe na wengine pia!

Tena, Biblia inatuambia tutumie muzuri sana wakati wetu. (Waefeso 5:15, 16) Utie mambo ya lazima zaidi pa nafasi ya kwanza. (Wafilipi 1:10) Kwa mufano, wakati uko katika motokari za kusafirisha watu, unaweza kutumia wakati huo ili kusoma ao kupanga mambo yenye utafanya wakati mwingine.

‘Mipango ya mwenye bidii bila shaka inaleta faida.’​Methali 21:5.