Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo yenye Saa ya Mwisho wa Dunia inatabiri hayatatimia kwa sababu Mungu anaahidi wakati wenye kuja wenye furaha kwa ajili ya wanadamu na dunia

HABARI KUBWA | DUNIA HII ITAOKOKA?

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

HALI ya mubaya yenye kuwa katika dunia ilitabiriwa na Biblia kumepita miaka mingi. Zaidi ya hilo, Biblia ilitabiri pia wakati wenye kuja wenye furaha kwa ajili ya wanadamu. Hatupaswe kukataa mara moja mambo yenye Biblia inasema, kwa sababu mambo yenye ilitabiri yanatimia hata katika mambo madogo-madogo.

Kwa mufano, fikiria unabii mbalimbali wa Biblia wenye kufuata:

  • “Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya nchi mahali pamoja baada ya pengine.”​—Mathayo 24:7.

  • ‘Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi, wanaopenda raha badala ya kumupenda Mungu.’​—2 Timotheo 3:1-4.

Unabii huo unaonyesha hali ya dunia hivi kwamba watu fulani wanaweza kusema kwamba dunia inaendelea kuwa mubaya zaidi kwa njia yenye haiwezi kuzuiwa. Kwa njia fulani, wanadamu hawawezi tena kuongoza ulimwengu wetu. Kulingana na Biblia, wanadamu hawana hekima na uwezo wa kumaliza magumu hayo kwa njia yenye kudumu. Jambo hilo linaonyeshwa katika maandiko yenye kufuata:

  • “Kuna njia ambayo imenyooka mbele ya mwanadamu, lakini njia za kifo ndizo mwisho wake baadaye.”​—Methali 14:12.

  • ‘Mwanadamu amemutawala mwanadamu kwa kumuumiza.’​—Mhubiri 8:9.

  • “Mwanadamu . . . hana uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—Yeremia 10:23.

Kama wanadamu wanaendelea kufanya mambo yenye wanataka, dunia inaweza kabisa kupata musiba mukubwa. Lakini, hilo halitatokea! Sababu gani? Biblia inasema hivi:

  • Mungu ‘ameiwekea dunia musingi juu ya mahali pake palipofanywa imara; haitatikiswa mupaka wakati usio na kipimo, au milele.’​—Zaburi 104:5.

  • ‘Kizazi kinaenda, kizazi kinakuja; lakini dunia inasimama mupaka wakati usio na kipimo.’​—Mhubiri 1:4.

  • “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.”​—Zaburi 37:29.

  • “Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko.”​—Zaburi 72:16.

Mafundisho hayo ya Biblia yanaleta majibu yenye kuwa wazi. Wanadamu wote hawatakufa kwa sababu ya kuchafuliwa kwa mazingira, kukosekana kwa chakula ao maji, ao kwa sababu ya magonjwa yenye yataenea katika dunia yote. Dunia haitaangamizwa katika uharibifu mukubwa wa kinyuklia. Sababu gani? Wakati wenye kuja wa dunia yetu uko katika mikono ya Mungu. Ni kweli kwamba Mungu ameruhusu wanadamu watumie uhuru wao wa kuchagua. Lakini watavuna matokeo ya maamuzi yao. (Wagalatia 6:7) Dunia haiko kama treni yenye imeharibika katika mwendo, yenye haiwezi tena kuongozwa, na yenye kungojea tu musiba. Mungu ameweka mipaka kuhusu kiasi cha magumu yenye wanadamu wanaweza kujiletea.​—Zaburi 83:18; Waebrania 4:13.

Lakini Mungu atafanya zaidi ya hilo. Ataleta “wingi wa amani.” (Zaburi 37:11) Mambo mazuri yenye kuonyeshwa katika habari hii ni mambo madogo tu kati ya mambo mengi yenye mamilioni ya Mashahidi wa Yehova wamejifunza kupitia funzo la Biblia.

Mashahidi wa Yehova wenye kuwa katika dunia yote ni wanaume na wanawake wa miaka yote na wenye walikomaa katika hali mbalimbali za maisha. Wanaabudu Mungu mumoja wa kweli ambaye jina lake ni Yehova, kama vile Biblia inaonyesha. Hawaogope wakati wenye kuja kwa sababu Biblia inasema: ‘Yehova, Muumba wa mbingu, Yeye Mungu wa kweli, Mufanyizaji wa dunia na Mutengenezaji wake, Yeye aliyeifanya imara, ambaye hakuiumba tu bila sababu, ambaye aliiumba ili ikaliwe na watu, amesema hivi: Mimi ni Yehova, wala hakuna mwingine.’​—Isaya 45:18.

Habari hii imezungumuzia mafundisho fulani ya Biblia kuhusu wakati wenye kuja wa dunia na wa wanadamu. Ili kupata habari zaidi, ona somo la 5 la broshua Habari Njema Inayotoka Kwa Mungu! yenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na yenye kupatikana kwenye www.pr418.com

Unaweza pia kuangalia video Sababu Gani Mungu Aliumba Dunia? yenye kupatikana kwenye www.pr418.com. (Fungua kichwa VICHAPO > VIDEO)