Ona video zinazopatikana

Mawazo ya Biblia—Inafaa Kabisa Kucheza “michezo hatari?”

Mawazo ya Biblia—Inafaa Kabisa Kucheza “michezo hatari?”

Mawazo ya Biblia—Inafaa Kabisa Kucheza “michezo hatari?”

“LEO, WATU WENGI HAWATOSHEKE TU NA KUANGALIA MICHEZO HATARI, SAWA VILE KURUKA MU PARACHUTE, KUPANDA MILIMA, KUTEREMUKA KU MAPOROMOKO YA MAJI MU MASHUA YA KIDOGO, AO KUOGELEA KATIKATI YA PAPA AO REQUINS. LAKINI WAO WENYEWE WANAFANYA ILE MAMBO JUU TU YA KUJIFURAHISHA.​—GAZETI YA WILLOW GLEN RESIDENT.

MANENO ya ile gazeti inaonyesha mawazo yenye watu wengi wako nayo juu ya michezo. Watu wengi zaidi wanafurahia michezo ya kutia maisha mu hatari, sawa vile kujitupa mu hewa na parachute, kupanda ku milima ya barafu, kuruka kutoka kwenye milima, majengo ya murefu, na vilalo, kwa kutumia parachute. Tena, watu wanafanyaka mambo ya hatari kwa kutumia ubao wa kusaidia kutereza ku teluji, kinga za kutembeza fasi yoyote, ubao wenye magurudumu, na viato vyenye magurudumu. Sawa vile gazeti Times inaonyesha, juu watu wengi sana wanapenda kufanya “michezo hatari,” ile inaonyesha kuwa mamilioni ya watu wanafanyaka ile michezo juu ya kumaliza woga na kufanya maisha yao ichangamuke zaidi.

Lakini, ile kupenda sana michezo hatari imeleta pia magumu mingi sana. Juu michezo hatari imeenea sana, hata michezo ya kawaida, watu wanaifanya mu njia yenye kuwa hatari, na ile imefanya watu wengi waumie sana. Mu 1997 mu Amerika, hesabu ya watu wenye walipelekwa ku hopitale juu waliumia wakati walikuwa wanatumia ubao wenye magurudumu, iliongezeka kufikia 33%, na hesabu ya watu wenye waliumia kwa sababu ya kutumia ubao wa kutereza ku teluji, iliongezeka kufikia 31%, na hesabu ya watu wenye waliumia wakati walikuwa napanda milima iliongezeka kufikia 20%. Na kuko michezo ingine yenye kuwa hatari sana, yenye inafikiaka hata kuua watu. Watu wenye wanafanyaka ile michezo, wanajua kama wanatiaka uzima wao mu hatari. Mwanamuke fulani mwenye anachezaka muchezo hatari wa kutereza ku teluji anasema hivi: “Ninajua kama ninakuwaka natembea na kifo.” Muchezaji fulani mwenye analipiwaka juu ya kutumia ubao wa kutereza ku teluji anasema kama ikiwa “hauumie, ni kusema haukujikaza sana.”

Kulingana na mambo yote yenye tumeona, Mukristo anapaswa kuwa na mawazo gani juu ya michezo hatari? Biblia inasema nini yenye inaweza kutusaidia kuamua ikiwa inafaa kucheza michezo hatari? Juu tupate majibu ya ile maulizo, tufikirie namna Mungu anaonaka uzima.

Namna Mungu Anaona Uzima

Biblia inatuambia kama Yehova ni “chemchemi ya uzima.” (Zaburi 36:9) Zaidi ya kutuumba, Yehova alitutayarishia mambo yote yenye tuko nayo lazima juu tufurahie maisha. (Zaburi139:14; Matendo 14:16, 17; 17:24-28) Ile inaonyesha kama, anapenda tuchunge muzuri zawadi ya uzima yenye ametupatia. Sheria zenye alipatia Waisraeli zinaonyesha kama anaona uzima kuwa wa maana sana.

Sheria ya Musa iliomba watu wajikaze sana juu ya kulinda uzima wa wengine. Kama Mwisraeli angeshindwa kuheshimia sheria za kulinda usalama na ile inafanya Mwisraeli mwingine akufe, ule Mwisraeli mwenye alishindwa kuheshimia zile sheria angekuwa na hatia ya damu. Kwa mufano, wakati mutu alijenga nyumba, alipaswa kujenga ukuta mufupi kuzunguka sehemu ya juu ya nyumba yake. Kama Mwisraeli hangefanya vile, na kisha mutu anaanguka kutoka kusehemu ya juu ya nyumba yake na kufa, ule Mwisraeli angekuwa na hatia ya damu. (Kumbukumbu la Torati 22:8) Kama ngombe angepiga mutu na mapembe kisha ule mutu anakufa, mwenye ile ngombe hangekuwa na hatia. Lakini kama ilijulikana kuwa ile ngombe ilikuwa hatari, na watu walikuwa walishaambia mwenye ile ngombe, lakini hakufanya jambo yoyote juu ya kuifunga muzuri, kisha ile ngombe inapiga mutu mapembe na ule mutu anakufa, mwenye ile ngombe angekuwa na hatia ya damu na angeweza kuuawa. (Kutoka 21:28, 29) Yehova alipatia Waisraeli zile sheria juu anaona uzima kuwa wa maana sana na anapenda watu waulinde.

Watumishi wa Yehova waaminifu walielewa kama ni mubaya kutia maisha yao ao ya wengine mu hatari, hata wakati hakukuwa amri yenye kuonyesha vile waziwazi. Kwa mufano, wakati fulani Daudi alisema kama anatamani ‘kunywa maji ya tangi lenye kuwa karibu na mulango mukubwa wa Betlehemu.’ Ile wakati, Betlehemu ilikuwa natawaliwa na Wafilisti. Wakati maaskari watatu wa Daudi walisikia vile, waliingia kwa kinguvu mu kambi ya Wafilisti, wakashota maji mu ile tangi ya Betlehemu, na wakailetea Daudi. Daudi alifanya nini? Hakukunywa ile maji, lakini aliimwanga chini. Alisema hivi: “Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwa upande wangu kwa maoni ya Mungu wangu kufanya jambo hilo! Je, nikunywe damu ya wanaume hawa wenye walitia uzima wao katika hatari?” Kwa maana walitia uzima wao katika hatari kwa kuenda kuyaleta.” (1 Mambo ya Nyakati 11:17-19) Daudi aliona kama ni mubaya sana kutia uzima wa wengine mu hatari juu tu ya kutimiza tamaa yake.

Yesu naye alitenda vilevile wakati Shetani alimuambia katika maono ajitupe chini kutoka kwenye munara wa hekalu, juu aone ikiwa malaika hawatamulinda ili asiumie. Yesu alijibia hivi: “Haupaswe kumujaribu Yehova Mungu wako.” (Matayo 4:5-7) Kwa kweli, Daudi na Yesu walijua kama Mungu hafurahi wakati mutu anatia uzima mu hatari wakati haiko lazima kufanya vile.

Ile mifano inaweza kufanya tujiulize hivi: ‘Nini njo itanisaidia kujua ikiwa michezo fulani inavuka mipaka ao ni hatari? Juu hata mambo ya kawaida ya kujifurahisha, yenye haiko hatari, inaweza kuwa hatari kama inapita mipaka, nini njo itanisaidia kujua mipaka yenye sipaswe kuvuka?’

Ni Lazima Kabisa Utie Uzima Wako mu Hatari?

Kuchunguza muzuri muchezo ao jambo ingine yenye tuko napanga kufanya, kutatusaidia kupata jibu ya ile ulizo. Kwa mufano, tunaweza kujiuliza, ‘Hii muchezo inafanyaka watu waumie sana? Niko na vitu vya kujizoeza navyo ao vya kunizuia nisiumie? Matokeo itakuwa nini kama ninaanguka, ao sikadirie muzuri jambo yenye ninatafuta kufanya, ao kama kitu ya kunizuia nisiumie haitumike muzuri? Nitaumia tu kidogo, ao inawezekana nitaumia sana ao hata kufa?’

Kama tunatia uzima wetu mu hatari juu tu ya kujifurahisha, tunaweza kuharibu urafiki wetu na Yehova na hatutastahili kupata mapendeleo fulani mu kutaniko. (1 Timoteo 3:2, 8-10; 4:12; Tito 2:6-8) Kwa kweli, hata wakati tuko najifurahisha, siye Wakristo hatupaswe kusahau kama Mungu anaona uzima kuwa wa maana sana.