Ona video zinazopatikana

Nilikubali Mawazo ya Mungu Juu ya Damu

Nilikubali Mawazo ya Mungu Juu ya Damu

Nilikubali Mawazo ya Mungu Juu ya Damu

Munganga anaeleza maisha yake

NILIKUWA mu jumba ya mukutano ya hopitale, nilikuwa naelezea wanganga wenzangu mambo yenye nilivumbula kisha kuchunguza maiti ya mutu fulani. Ule mutu mwenye alikufa alikuwa na kansere. Niliwaambia hivi: “Tunaweza kusema kama damu ya mingi yenye ule mugonjwa alitiwa mu mishipa, ilifanya [chembe zake nyekundu ziharibike] na [figo] zake zisitumike muzuri, na ile njo ilifanya akufe.”

Profesere fulani alisimama na kuniambia hivi kwa kasirani: “Unataka kusema haukumutia damu ya muzuri?” Nilijibia: “Haiko vile njo ninamaanisha.” Niliwaonyesha picha za sehemu za kidogo-kidogo za figo ya ule mutu. Niliongezea hivi: “Tunaona mu figo yake chembe nyekundu za mingi zenye kuharibika, kwa hiyo, tunaweza kusema kama ile njo ilifanya figo yake iache kutumika.” * Walikasirika sana, mupaka na miye nikakuwa na wasiwasi. Hata kama nilikuwa munganga kijana, na yeye alikuwa profesere, niliona kama sitabadilisha mambo yenye nilisema.

Wakati ile jambo yenye nilizungumuzia ilitokea, nilikuwa siyakuwa Shahidi wa Yehova. Nilizaliwa mu mwaka 1943 katika Sendai, muji wenye unapatikana kaskazini mu Japani. Juu baba yangu alikuwa munganga, na miye niliamua kusoma kinganga. Mu mwaka 1970, wakati nilikuwa mu mwaka wangu wa pili wa masomo ya kinganga, nilioa kijana mwanamuke mwenye kuitwa Masuko.

Ninaanza Kujifunza Magonjwa

Masuko alikuwa natumika juu tupate makuta ya kutusaidia wakati miye nilikuwa ningali nasoma. Nilifurahia sana masomo ya kinganga. Nilishangala sana kuona namna mwili wa mwanadamu umefanywa! Hata vile, sikukuwa naamini kama kunakuwaka muumbaji. Niliwaza kama uchunguzi wa kinganga ungenisaidia nikuwe na furaha mu maisha. Kwa hiyo, kisha kuwa munganga, niliamua kujifunza mambo ingine ya kinganga. Sasa nilianza kujifunza magonjwa, ni kusema nilijifunza alama za magonjwa, mambo yenye kuleta magonjwa, na hatari ya magonjwa.

Wakati nilikuwa nachunguza maiti za wagonjwa wenye walikufa na kansere, nilianza kuona kama kutiwa damu mu mishipa hakusaidiake kabisa. Wagonjwa wenye kuwa na kansere ya nguvu sana, wanaweza kuisha damu na kuwa zaifu sana, na matunzo yenye inatumiwa juu ya kutunza kansere, inaweza kufanya hali yao ikuwe mubaya zaidi. Njo maana mara mingi wanganga wanaombaka watiwe damu mu mishipa. Leo wanganga wanajua kama, wakati wanatia wagonjwa wa kansere damu mu mishipa, ile inafanyaka wakuwe zaifu zaidi, inafanyaka kansere irudie tena, na inafanyaka ikuwe nguvu kwa wale wagonjwa kupona. *

Mambo yenye nilizungumuzia ku mwanzo ilitokea mu mwaka 1975. Ule profesere njo alikuwa nashugulikia ule mugonjwa mwenye alikufaka na alisomeaka sana mambo ya damu. Njo maana haishangaze kuona kuwa alikasirika sana wakati alisikia ninasema kama damu yenye ule mugonjwa alitiwa mu mishipa njo ilifanya akufe! Lakini, niliendelea kuwaelezea mambo yenye nilivumbula na akaanza kutulia polepole.

Hakutakuwa Magonjwa ao Kifo

Ni mu ile wakati njo mwanamuke fulani mwenye kuzeeka, mwenye kuwa Shahidi wa Yehova, alitembelea bibi yangu. Alitumia jina “Yehova” mu mazungumuzo yake, na bibi yangu akamuuliza juu ya nini anatumia ile jina. Ule Shahidi alimujibia kama, “Yehova ni jina ya Mungu wa kweli.” Masuko alikuwa nasoma Biblia tangu wakati alikuwa mutoto mudogo, lakini mu Biblia yake, walikuwa walishatia jina “BWANA” pa nafasi ya jina ya Mungu. Sasa alijua kama Mungu iko na jina!

Bila kukawia, Masuko alianza kujifunza Biblia na ule Shahidi mwenye kuzeeka. Wakati nilirudia kutoka ku hopitale karibu saa saba ya usiku, bibi yangu aliniambia hivi kwa furaha: “Biblia inasema kama magonjwa na kifo havitakuwa tena!” Nikasema, “Ile ni muzuri sana!” Kisha akasema tena, “Juu dunia mupya iko karibu, sipendi upoteze wakati yako.” Niliwaza kama alimaanisha niache kuwa munganga. Kwa hiyo nilikasirika sana na tulianza kukosana sana mu ndoa yetu.

Lakini bibi yangu hakuacha kuniambia mambo yenye Biblia inasema. Aliomba Mungu amusaidie apate maandiko yenye kufaa ya kunionyesha. Maneno ya Muhubiri 2:22, 23 ilinigusa moyo sana. Ile andiko inasema hivi: “Kwa kweli mutu anapata faida gani kwa kazi yake yote ya nguvu na tamaa yenye inamuchochea kufanya kazi kwa bidii chini ya jua? . . . na hata usiku moyo wake haupumuzike. Jambo hili pia ni bure.” Ni vile nilikuwa nafanya, nilikuwa natumika usiku na muchana mu mambo ya kinganga, lakini ile haikuniletea furaha ya kweli.

Asubui fulani ya Siku ya Yenga, Mwezi wa 7, 1975, wakati bibi yangu alienda ku Jumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova, na miye niliamua kumufuata. Bibi yangu alishangala kuniona, na Mashahidi walinikaribisha kwa furaha. Kuanzia ile siku, nilianza kuenda ku mikutano kila Siku ya Yenga. Kisha mwezi moya, Shahidi fulani wa Yehova alianza kujifunza na miye Biblia. Miezi tatu kisha bibi yangu kanza kujifunza Biblia, alibatizwa.

Ninakubali Mawazo ya Mungu Juu ya Damu

Bila kukawia nilijifunza kuwa Biblia inasema kama Wakristo wanapaswa ‘kujiepusha na damu’. (Matendo 15:28, 29; Mwanzo 9:4) Juu tayari nilikuwa nawaza kama damu haisaidiake wagonjwa, ilikuwa mwepesi kukubali mawazo ya Mungu juu ya damu. Niliwaza hivi: ‘Kama kuko Muumbaji, na anasema vile, maana yake ni vile tu.’

Nilijifunza pia kama tunagonjwaka na tunakufaka juu tuliriti zambi kutoka kwa Adamu. (Waroma 5:12) Ile wakati, nilikuwa nafanya uchunguzi juu ya ugonjwa wenye unafanyaka mishipa ya damu ikuwe nguvu-nguvu na igonde. Wakati tunaendelea kukomala, mishipa yetu ya damu inakuwaka nguvu-nguvu na inagondaka na ile inaletaka magonjwa sawa vile magonjwa ya moyo, magonjwa ya mishipa ya ubongo na magonjwa ya figo. Kwa hiyo, inaeleweka kusema kama magonjwa inatokana na hali ya kutokamilika yenye tuliriti. Kisha pale, bidii yangu mu mambo ya kinganga ilipunguka. Ni Yehova tu njo anaweza kumaliza magonjwa na kifo!

Mu Mwezi wa 3, 1976, miezi saba kisha kuanza kujifunza Biblia, niliacha kufanya uchunguzi ku hopitale yenye ilikuwa ku masomo ya juu. Niliogopa kama sitapataka tena kazi ya kinganga, lakini nilipata kazi ku hopitale ingine. Nilibatizwa mu Mwezi wa 5, 1976. Niliona kama jambo ya muzuri zaidi ya kufanya mu maisha yangu ni kuwa mutumishi wa wakati wote, ni kusema kuwa painia; na nilianza upainia mu Mwezi wa 7, 1977.

Ninatetea Mawazo ya Mungu Juu ya Damu

Mu Mwezi wa 11, 1979, miye na Masuko tulihamia Chiba mu kutaniko ingine; mu ile kutaniko mulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Nilipata kazi ku hopitale fulani na ile kazi haikukuwa na nikamata wakati mingi. Siku yangu ya kwanza ku kazi, kikundi ya wanganga wenye kufanya upasuaji walinizunguka na kuniuliza hivi: “Vile uko Shahidi wa Yehova, kama kunakuya mugonjwa mwenye iko na lazima ya kutiwa damu, utafanya nini?”

Kwa heshima niliwafasiria kama nitatii mambo yenye Mungu anasema juu ya damu. Niliwafasiria kama kuko matunzo ingine yenye inaweza kutumiwa pa nafasi ya damu, na kama nitafanya yangu yote juu ya kusaidia mugonjwa. Kisha kuzungumuza nao kwa saa moya hivi, munganga mwenye kusimamia mambo ya upasuaji, alisema hivi: “Ninaelewa. Lakini kama kuko mugonjwa mwenye amepoteza sana damu, siye wenyewe tutamushugulikia.” Ule munganga mwenye kusimamia mambo ya upasuaji, alikuwa najulikana kuwa mutu mugumu. Lakini kisha ile mazungumuzo, tulifikia kuwa marafiki, na kila mara alikuwa naheshimia imani yangu.

Niliheshimia Mawazo ya Mungu Juu ya Damu Hata Wakati Ilikuwa Nguvu Kufanya Vile

Wakati tulikuwa Chiba, biro ya mupya ya Mashahidi wa Yehova katika Japani ilikuwa najengwa mu muji wa Ebina. Miye na bibi yangu tulikuwa naenda kule mara moja kwa juma juu ya kutunza Mashahidi wa Yehova wenye walikuwa nasaidia kujenga ile biro ya tawi yenye kuitwa Beteli. Kisha miezi fulani, tuliombwa tutumikie kwa wakati wote ku Beteli ya Ebina. Kwa hiyo, mu Mwezi wa 3, 1981 tulianza kuishi mu majengo ya muda ya Beteli kwenye zaidi ya wajitoleaji 500 walikuwa tayari wanaishi. Asubui, nilikuwa nasaidia kusafisha choo na fasi ya kunawia, na muchana nilikuwa natunza wagonjwa.

Mugonjwa fulani mwenye nilikuwa natunza, aliitwa Ilma Iszlaub, alitoka Australia na alikuwa misionere mu inchi ya Japani tangu mwaka wa 1949. Alikuwa na ugonjwa fulani wa damu wenye unaitwa lukemia na wanganga wake walimuambia kama anabakia na miezi fulani tu ya kuishi. Ilma alikala kutiwa damu mu mishipa juu ya kurefusha maisha yake na akaamua kupitisha siku zake za mwisho ku Beteli. Ile wakati, dawa za kusaidia mwili itengeneze chembe nyekundu za damu, hazikukuwa. Kwa hiyo, wakati fulani damu yake ilikuwa chini sana; kuko wakati alikuwa na grame 3 ao 4 tu ya damu! (Kwa kawaida mutu anakuwaka na grame 12 mupaka 15.) Lakini nilifanya yangu yote juu ya kumutunza. Ilma aliendelea kuwa na imani yenye nguvu mupaka wakati alikufa mu Mwezi wa 1, 1988; miaka saba ilikuwa imepita, tangu wamuambie kama anabakia na miezi fulani tu ya kuishi!

Kwa miaka mingi, wajitoleaji ku Beteli ya Japani, wamekuwa na lazima ya kufanyiwa upasuaji. Tuko wenye shukrani juu wanganga wa ku hopitale za karibu-karibu wamekubali kuwafanya upasuaji bila kuwatia damu. Mara mingi wameniomba nikuwe mu chumba ya upasuaji juu ya kuona namna wako nafanya upasuaji, na wakati fulani, nimesaidia kufanya upasuaji. Ninashukuru sana wanganga wenye wanaheshimia mawazo ya Mashahidi wa Yehova juu ya damu. Wakati niko natumika nao, nimepata nafasi za mingi ya kuwaelezea mambo yenye ninaamini. Hivi majuzi, munganga fulani alifikia kubatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova.

Wanganga wamejikaza kutunza Mashahidi wa Yehova bila kuwatia damu, na ile imesaidia kukuwe maendeleo mu mambo ya kinganga. Ushuhuda unaonyesha kama kuko faida za mingi wakati wagonjwa wanafanyiwa upasuaji bila kutiwa damu. Uchunguzi umeonyesha kama wale wagonjwa wanaponaka haraka, na hawakuwake na matatizo ya mingi kisha upasuaji.

Ninaendelea Kuiga Munganga Mukubwa Zaidi

Ninajikazaka kujua maendeleo yenye iko nafanywa mu mambo ya kinganga. Lakini, ninaendeleaka pia kuiga Yehova, Munganga Mukubwa Zaidi. Yeye haonake tu vile mutu anaonekana kwa inje, lakini anachunguzaka mutu kwa ujumla. (1 Samweli 16:7) Na miye, mu kazi yangu, ninajikazaka kuhangaikia hali yote ya mutu, hapana kukaza tu akili ku ugonjwa wake. Ile inanisaidiaka nimutunze muzuri.

Ningali natumikia ku Beteli, na kati ya mambo yenye inanileteaka furaha sana, ni kusaidia wengine wamujue Yehova, na wajue mawazo yake juu ya damu. Ninaombaka Yehova, Munganga Mukubwa Zaidi, atende haraka juu ya kumaliza magonjwa yote na kifo.​—Ilielezwa na Yasushi Aizawa.

[Maelezo ya chini]

^ Mu kitabu Modern Blood Banking and Transfusion Practices, muchunguzi Denise M. Harmening, anasema kama “mugonjwa mwenye alikuwa na mimba, mwenye alishakatiwa damu mu mishipa, ao mwenye alitiwa kiungo fulani mu mwili, anaweza kuwa na matatizo makubwa ya afya kama anatiwa damu mu mishipa, na chembe zake nyekundu za damu zinaweza kuharibika.” Mu hali za vile, vipimo vya damu vyenye vinafanywaka mbele mutu atiwe damu mu mishipa, havionyeshake kama kuko hatari yenye inaweza kutokea.” Kitabu Dailey’s Notes on Blood, kinasema kama “chembe nyekundu za damu zinaweza kuharibika hata wakati mutu anatiwa kiasi kidogo tu ya damu yenye haipatane na damu yake . . . Wakati figo zinaacha kutumika, haziwezi tena kusafisha damu, na ile inafanya hali ya mugonjwa ikuwe mubaya zaidi.”

^ Gazeti Journal of Clinical Oncology ya Mwezi wa 8, 1988, ilisema hivi: “Wagonjwa wa kansere wenye hawakutiwa damu mbele ya upasuaji, walikuwa na tumaini ya mingi ya kupona kuliko wagonjwa wa kansere wenye walitiwa damu mbele ya upasuaji.”

[Wazo ya fungu]

“Niliwafasiria kama kuko matunzo ingine yenye inaweza kutumiwa pa nafasi ya damu, na kama nitafanya yangu yote juu ya kusaidia mugonjwa”

[Wazo ya fungu]

“Ushuhuda unaonyesha kama kuko faida za mingi wakati wagonjwa wanafanyiwa upasuaji bila kutiwa damu”

[Picha]

Juu: Niko natoa hotuba yenye kutegemea Biblia

Kuume: Miye na bibi yangu, Masuko, leo