Ona video zinazopatikana

Nilifikia Kujua Mwenye Anaweza Kuleta Haki ku Dunia

Nilifikia Kujua Mwenye Anaweza Kuleta Haki ku Dunia

Nilifikia Kujua Mwenye Anaweza Kuleta Haki ku Dunia

Ursula Menne anaeleza maisha yake

Nakumbuka kama tangu zamani nimetamani sana kuona watu wanatendewa muzuri na kwa haki. Ile tamaa ilifanya hata nipelekwe mu gereza mu Alemanye ya Mashariki ya Kikomunisti. Na ni kule njo nilifikia kuelewa mwenye anaweza kuleta haki ku dunia. Muache niwafasirie.

NILIZALIWA mwaka wa 1922 mu muji wa Alemanye wa Halle. Ni muji wenye umefanya miaka zaidi ya 1 200. Unapatikana ku kilometre 200 kusini-mangaribi mwa Berlin, na ulikuwa kati ya miji ya kwanza-kwanza kwenye dini ya Kiprotestanti ilitia mizizi. Dada yangu, Käthe, alizaliwa mu 1923. Baba alikuwa natumika mu kazi ya kijeshi. Mama alikuwa naimba mu jumba ya maonyesho.

Ni kwa baba yangu njo nilitosha tamaa kubwa ya kupenda kupiganisha ukosefu wa haki. Wakati baba yangu aliacha kazi ya kijeshi, aliuza duka (ao magasin). Juu wengi kati ya wenye walikuwa nakuya kuuza walikuwa maskini, baba alikuwa nawapatia vitu ku deni. Na ile ilifanya vitu viiishe mu duka. Mambo yenye ilimufikia baba ilinifundisha kama kupiganisha ukosefu wa haki ni nguvu sana kuliko vile mutu anaweza kuwazia. Lakini, mawazo yenye mutu anakuwaka nayo wakati iko kijana inakuwaka nguvu sana kuachana nayo.

Kwa mama yangu, niliriti tamaa ya kupenda kuimba na kucheza, na alinifundisha miye na Käthe muziki, wimbo, na dansi. Nilikuwa mutoto mwenye kuchangamuka na mwenye furaha, na miye na Käthe tulikuwa na maisha ya muzuri sana mupaka 1939.

Maisha Inabadilika

Kisha kumaliza masomo yangu ya musingi, nilienda ku masomo ya dansi yenye kuitwa ballet. Kule, nilijifunza pia Ausdruckstanz (dansi yenye inaomba kuonyesha hisia), na Mary Wigman njo alikuwa naifundisha. Alisaidiaka kuanzisha ile dansi yenye inaomba mutu kuonyesha hisia zake kupitia dansi. Nilianza pia kuchora picha. Kwa hiyo, miaka yangu ya ujana ilianza na furaha na iliyala mambo yenye kufurahisha na tamaa ya kujifunza mambo mingi. Lakini kisha tukafika mu mwaka wa 1939, na Vita ya Pili ya Ulimwengu ikaanza. Jambo ingine ya mubaya ilitokea mu 1941, wakati baba alikufa na kifua kikubwa.

Vita ni jambo ya mubaya sana. Hata kama nilikuwa na miaka 17 tu wakati vita ilianza, niliwaza kama dunia imepanda wazimu. Niliona watu wengi wenye mbele ya pale walikuwa na maisha ya muzuri na kisha pale Wanazi wakavuruga maisha yao. Kisha watu wakakosa mambo ya lazima, watu wengi wakauawa, na kukakuwa uharibifu. Nyumba yetu iliharibiwa sana na bombe, na wakati vita ilikuwa inaendelea, watu wengi wa familia yangu waliuawa.

Wakati vita ilimalizika mu 1945, Mama, Käthe, na miye tulikuwa tungali Halle. Lakini ile wakati, nilikuwa na bwana na mutoto mudogo mwanamuke, na ndoa yangu ilikuwa na matatizo. Tulitengana, na juu nilipaswa kujitimizia mahitaji yangu na ya mutoto wangu mwanamuke, nilifanya kazi ya kucheza dansi na kuchora picha.

Kisha vita, Alemanye iligawanywa mu sehemu ine, na muji wetu ulikuwa mu sehemu yenye ilitawaliwa na Muungano wa Sovieti. Kwa hiyo, iliomba siye wote tuzoee utawala wa Kikomunisti. Mu 1949, sehemu yetu ya Alemanye, yenye mara mingi iliitwa Alemanye ya Mashariki, ilifikia kuwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Alemanye.

Maisha mu Utawala wa Kikomunisti

Ile miaka yote, Mama aligonjwa, na nilipaswa kumuhangaikia. Nilipata kazi ya kiserikali. Ile wakati, nilifikia kujuana na wanafunzi fulani waasi wenye walikuwa najaribu kuonyesha watu hali fulani za ukosefu wa haki. Kwa mufano, kijana fulani hakukubaliwa ku masomo ya juu kwa sababu baba yake alikuwa mu chama ya Wanazi. Nilijua muzuri ule mwanafunzi, juu mara mingi tulikuwa napiga naye muziki. Nilijiuliza, ‘Juu ya nini anapaswa kuteseka juu ya mambo yenye baba yake alifanya?’ Nilianza kupenda sana kujiunga na wale wanafunzi waasi, na nikaamua kufanya maandamano ya kupinga serikali. Siku moya, nilitia hata trakti ku vipandio vya majengo ya tribinali.

Juu nilipenda haki, nilihuzunishwa sana na barua fulani zenye nilipaswa kuandika na mashini wakati nilikuwa sekretere wa Halmashauri ya Eneo ya Amani. Siku ingine, juu ya sababu za kipolitike, ile Halmashauri ilipanga kutuma habari za propaganda ya Kikomunisti kwa mwanaume moya mwenye kuzeeka mwenye alikuwa naishi mu Alemanye ya Mangaribi ili kufanya watu waanze kuwa naye mashaka. Nilikasirika sana kuona namna alitendewa bila haki na nikaficha zile habari mu biro yangu. Kwa hiyo, hawakuzitumaka.

“Mutu Mubaya Sana mu Chumba ya Gereza” Alinipatia Tumaini

Mu Mwezi wa 6, 1951, wanume wawili waliingia mu biro yangu na kuniambia: “Tunakuya kukufunga.” Walinipeleka mu gereza yenye kuitwa Roter Ochse, ao Ngombe-dume Mwekundu. Kisha mwaka moya, nilishitakiwa kama nilikuwa natafuta kuangusha serikali. Mwanafunzi fulani alinichongeaka ku Stasi, polisi ya siri, kwa kuwaambia kama zamani nilikuwa nagawia watu trakti zenye kuwa na mawazo ya kupinga serikali. Ile kesi ilikuwa tu ya jina juu hakuna mwenye alihangaikia mambo yenye nilisema juu ya kujitetea. Nilihukumiwa miaka sita mu gereza. Ile wakati, nilikuwa mugonjwa na nilipelekwa mu hopitale ya gereza pamoya na wanamuke wengine 40 hivi. Wakati niliona namna wale wanamuke wote hawakukuwa na furaha, nilianza kuogopa. Nilikimbia ku mulango na kuipiga ngumi.

Mulinzi aliniuluza, “Unapenda nini?”

Nilimuambia kwa kulalamika, “Sipaswe kubakia hapa. Munitie mu chumba ya miye peke, lakini sipaswe kubakia hapa!” Hakuhangaikia ombi yangu. Wakati kidogo kisha pale, niliona mwanamuke fulani mwenye alikuwa tofauti na wengine. Macho yake ilionyesha kama alikuwa na amani ya moyo. Kwa hiyo, niliikala pembeni yake.

Aliniambia hii mambo yenye ilinishangaza, “Kama unaikala pembeni yangu, unapaswa kuwa muangalifu.” Kisha aliongezea, “Wengine wanawazaka kama niko mutu mubaya sana mu hii chumba ya gereza juu niko Shahidi wa Yehova.”

Ile wakati, sikujua kama Mashahidi wa Yehova walionwa kuwa maadui wa serikali ya Kikomunisti. Lakini sikujua mambo mingi kuwahusu. Nilijua tu kama kulikuwaka Wanafunzi wa Biblia wawili (jina ya zamani ya Mashahidi) wenye walikuwaka namutembelea Baba yangu wakati nilikuwa mutoto. Nilikumbuka hii maneno yenye Baba alikuwa nasema, “Wanafunzi wa Biblia wanasemaka kweli!”

Nililia na kupata kitulizo wakati nilikutana na ule mwanamuke, mwenye aliitwa Berta Brüggemeier. Nilimuambia, “Tafazali, uniambie mambo fulani kuhusu Yehova.” Tangu ile wakati, tulipitisha wakati mingi pamoya na mara mingi tulizungumuzia Biblia. Kati ya mambo yenye nilijifunza, nilifikia kujua kama Mungu wa kweli, Yehova, ni Mungu wa upendo, haki, na amani. Nilijifunza pia kama ataondoa mambo yote ya mubaya yenye watu waovu na wakali wameleta. Zaburi 37:10, 11 inasema hivi: “Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena . . . Lakini wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”

Kufunguliwa na Kuhamia mu Alemaye ya Mangaribi

Nilifunguliwa mu 1956, kisha kupitisha mu gereza zaidi ya miaka tano. Siku tano kisha kufunguliwa, nilitoka mu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Alemanye na kupanda ndege ili kuenda kuishi Alemanye ya Mangaribi. Ile wakati, nilikuwa na watoto wawili wanamuke, Hannelore na Sabine, na nilienda pamoya nao. Kule, tulivunja ndoa na bwana yangu na nilikutana tena na Mashahidi. Wakati nilikuwa najifunza Biblia, nilivumbula kama nilipaswa kufanya mabadiliko ya mingi mu maisha yangu ili kuipatanisha na kanuni za Yehova. Nilifanya ile mabadiliko na kubatizwa mu 1958.

Kisha, niliolewa tena. Mara hiyo, niliolewa na Klaus Menne, Shahidi wa Yehova. Miye na Klaus tulikuwa na ndoa ya muzuri na tulizala watoto wawili, Benjamin na Tabia. Jambo ya kuhuzunisha, Klaus alikufa miaka 20 hivi mu aksida, na tangu ile wakati niko mujane. Lakini, nafarijiwaka sana na tumaini ya ufufuo, juu najua kama wafu watafufuliwa ili kuishi mu Paradiso ku dunia. (Luka 23:43; Matendo 24:15) Nafarijiwaka pia sana kuona namna watoto wangu wote ine wanamutumikia Yehova.

Kupitia funzo yangu ya Biblia, nimejifunza kama Yehova tu njo anaweza kuleta haki ya kweli. Tofauti na wanadamu, yeye anajua mambo yote kutuhusu, kwa mufano namna tulikomala, mambo yenye mara mingi wengine hawaonake. Kujua vile kunanipatia amani tangu sasa, zaidi sana wakati ninaona watu wanatendewa bila haki ao wakati natendewa bila haki. Muhubiri 5:8 inasema hivi: “Kama unaona maskini wanakandamizwa kwa njia yoyote na haki inavunjwa na uadilifu havifuatwe katika wilaya yako, jambo hilo lisikushangaze. Kwa maana ofisa mukubwa iko anaangaliwa na ule mwenye kuwa juu zaidi kuliko yeye, na kuko wengine wenye wako tena juu kuliko wao.” Kwa kweli, “mwenye kuwa juu zaidi” njo Muumbaji wetu. Waebrania 4:13 inasema hivi: “Vitu vyote viko uchi na vyenye kufunuliwa wazi mbele ya macho ya ule mwenye tunapaswa kutoa hesabu kwake.”

Kufikia Miaka 90 Yenye Imepita

Wakati fulani, watu wananiulizaka kama maisha ilikuwaka namna gani mu utawala wa Wanazi na wa Kikomunisti. Maisha haikukuwaka mwepesi mu utawala wote mbili. Na utawala wa Wanazi na wa Kikomunisti, sawa tu vile aina zote za serikali za wanadamu, zinaonyesha tu kama wanadamu hawawezi kujitawala. Biblia inasema kweli wakati inasema hivi: “Mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.”​—Muhubiri 8:9.

Wakati nilikuwa kijana na bila uzoefu, nilikuwa nawaza kama wanadamu njo wanaweza kuleta haki. Sasa nimejua. Muumbaji wetu tu njo anaweza kuleta kabisa haki ku dunia, na atafanya vile kwa kutosha mambo yote ya mubaya na kufanya Mwana wake, Yesu Kristo, kuwa mutawala wa dunia. Sikuzote Yesu anatiaka faida za wengine mbele ya faida zake. Biblia inasema hivi kuhusu Yesu: “Ulipenda haki, na ukachukia uvunjaji wa sheria.” (Waebrania1:9) Niko mwenye shukrani sana kwa Mungu kwa kunivuta kwa ule Mufalme muzuri na mwenye haki, mwenye natumainia kuishi milele mu utawala wake!

[Picha]

Pamoya na watoto wangu wanamuke Hannelore na Sabine kisha kufika mu Alemanye ya Mangaribi

[Picha]

Leo, pamoya na mutoto wangu mwanaume, Benjamin, na bibi yake, Sandra