Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Tuliona Katika Njia Nyingi Fazili za Mungu Zenye Hatustahili

Tuliona Katika Njia Nyingi Fazili za Mungu Zenye Hatustahili

ARTHUR, baba yangu alikuwa kijana mwenye kumupenda Mungu. Kwa hiyo, alitaka kuwa muhubiri wa dini ya Methodiste. Lakini alibadilisha uamuzi wake wakati alisoma vichapo fulani vya Wanafunzi wa Biblia na akaanza kujiunga nao. Baba yangu alibatizwa katika mwaka wa 1914, wakati alikuwa na miaka 17. Wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, aliombwa aingie katika jeshi, lakini alikataa kupigana. Kwa hiyo, alihukumiwa kifungo cha miezi kumi katika gereza la Kingston katika Ontario, Kanada. Kisha kuachiliwa katika gereza, akakuwa kolportere, ni hivyo mapainia walikuwa wanaitwa zamani.

Katika mwaka wa 1926, baba yangu alioa Hazel Wilkinson. Mama ya Hazel alijifunza kweli katika mwaka wa 1908. Nilizaliwa tarehe 24 Mwezi wa 4, 1931, nilikuwa mutoto wa pili katika familia ya watoto ine. Baba yangu alipenda na kuheshimia Biblia, na alitufundisha kufanya hivyo pia. Kuabudu Yehova lilikuwa jambo la maana zaidi katika maisha yetu. Familia yetu ilikuwa inafanya mahubiri ya nyumba kwa nyumba kwa ukawaida.—Matendo 20:20.

KAMA BABA YANGU, SIKUJIINGIZA KATIKA MAMBO YA POLITIKE NA NILIFANYA KAZI YA UPAINIA

Katika mwaka wa 1939, Vita ya Pili ya Ulimwengu ilianza. Mwaka wenye ulifuata, kazi ya Mashahidi wa Yehova ilikatazwa katika Kanada. Kwenye masomo, watoto walisalimia bendera na kuimba wimbo wa taifa. Kwa ukawaida walimu waliniruhusu mimi na dada yangu Dorothy tuende inje wakati wa kufanya mambo hayo. Lakini siku moja, mwalimu wangu alipenda kunipatisha haya kwa kusema kama nilikuwa mwenye woga. Kisha masomo wanafunzi fulani walinishambulia, na wakanipiga na kuniangusha chini. Hilo lilinifanya niazimie zaidi ‘kumutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.’—Matendo 5:29.

Mwezi wa 7, 1942, wakati nilikuwa na miaka 11, nilibatizwa katika shamba fulani la kuchungia wanyama katika tangi ya maji. Wakati tulikuwa tunafunga masomo nilifurahia kufanya kazi ya upainia wa wakati wa mapumuziko. Leo tunaita kazi hiyo upainia musaidizi. Mwaka moja nilienda na ndugu wengine watatu katika Ontario ya kaskazini, kwenye tulihubiria watu wenye kufanya kazi ya kukata miti.

Tarehe 1 Mwezi wa 5, 1949, nilianza kufanya kazi ya upania wa kawaida. Kisha nilialikwa kusaidia katika kazi ya ujenzi kwenye biro ya tawi ya Kanada na kisha nikafikia kuwa mwanabeteli katika Beteli ya Kanada. Nilipewa mugawo wa kutumika mahali pa kuchapishia vichapo, kwenye nilijifunza kutumia aina fulani ya mashine ya kuchapisha yenye kuitwa bapa ya kuchapa (presse cylindrique). Ninakumbuka namna nilikuwa ninatumika usiku muzima kwa majuma mengi ili kuchapisha trakte fulani yenye kuzungumuzia mateso ya watu wa Yehova katika Kanada.

Kisha, nilitumika katika Biro ya Utumishi. Nilipewa mugawo wa kuuliza maulizo mapainia wenye walikuwa wanaenda kutumika katika Quebec, kwenye kazi yetu ilipingwa sana. Kati ya mapainia hao kulikuwa Mary Zazula kutoka Edmonton, Alberta. Wazazi wake walikuwa katika Kanisa la Orthodox. Wakati Mary na mukubwa yake mwanaume walikataa kuacha kujifunza Biblia, wazazi wao waliwafukuza nyumbani. Mary na mukubwa yake walibatizwa katika Mwezi wa 6, 1951, na kisha miezi sita wakaanza kufanya kazi ya upainia. Wakati nilikuwa ninauliza Mary maulizo, niliona kuwa anamupenda Yehova sana. Ninakumbuka nilifikiri kuwa yeye ndiye dada mwenye ningependa kuoa. Kisha miezi kenda, tulioana; ilikuwa tarehe 30 Mwezi wa 1, 1954. Juma moja kisha ndoa yetu, mimi na Mary tulialikwa ili kufuata mazoezi ya kufanya kazi ya muzunguko. Kwa miaka mbili yenye ilifuata tulifanya kazi ya muzunguko kaskazini mwa Ontario.

Kadiri kazi ya kuhubiri katika dunia yote iliendelea kuongezeka, kulikuwa lazima ya wamisionere wengi zaidi. Mimi na Mary tulifikiri kuwa ikiwa tuliweza kuvumilia baridi kali katika kipindi cha baridi na imbu zenye kusumbua katika kipindi cha joto katika Kanada, tungeweza kuishi mahali popote. Tulisoma darasa la 27 la Masomo ya Gileadi, na tukamaliza katika Mwezi wa 7, 1956. Kufikia Mwezi wa 11 tulikuwa katika makao yetu ya mupya, katika Brazili.

KAZI YA UMISIONERE KATIKA BRAZILI

Wakati tulifika Brazili, tulianza kujifunza luga ya Kireno (Portugais). Kwanza, tulijifunza njia nyepesi za kuanzisha mazungumuzo. Kisha, tuliweka katika akili namna fupi ya kutolea watu magazeti. Kisha, tulienda katika mahubiri na tukakutana na mwanamuke mumoja mwenye alipendezwa na ujumbe wetu. Tulikuwa tumeamua kwamba ikiwa musikilizaji fulani angependezwa, tungesoma andiko lenye kuonyesha namna maisha yatakuwa katika Ufalme wa Mungu. Kwa hiyo, nilisoma andiko la Ufunuo 21:3, 4, kisha nikazimia! Sikukuwa ninazoea hali ya hewa yenye joto. Hali hiyo ya joto iliendelea kuwa tatizo kwangu.

Tulipewa mugawo wa kufanya kazi ya umisionere katika muji wa Campos. Leo, katika muji huo, kuko makutaniko 15! Lakini wakati tulifika huko, kulikuwa tu kikundi kimoja chenye kuwa mbali katika muji huo na kulikuwa pia nyumba ya wamisionere yenye ilikuwa na dada ine: Esther Tracy, Ramona Bauer, Luiza Schwarz, na Lorraine Brookes (mwenye sasa anaitwa Wallen). Kazi yangu katika nyumba ya wamisionere ilikuwa kusaidia kufua manguo na kuleta kuni za kutumia ili kupika. Usiku moja wa Siku ya Kwanza kisha funzo la Munara wa Mulinzi, Mary alikuwa anapumuzika kwenye kiti na kuweka kichwa chake kwenye musegemeo (coussin). Tulikuwa tunazungumuzia muchana wetu. Wakati Mary alisimama, nyoka alitoka chini ya musegemeo huo! Mugeni huyo mwenye hatukutazamia alileta wasiwasi sana mupaka wakati nilimuua.

Kisha kujifunza Kireno kwa mwaka moja, tulianza kazi ya muzunguko. Tulitumika katika maeneo yenye hayakukuwa na moto wa umeme. Tulikuwa tunalala kwenye mikeka na kusafiri kwa kutumia gari lenye kukokotwa na farasi. Wakati moja tulisafiri katika treni ili kuenda katika muji wenye kuwa kwenye milima ili kuhubiri katika eneo fulani la mbali. Tulikamata chumba cha kulipia huko. Biro ya tawi ilitutumia magazeti 800 ya kutumikisha katika kazi ya kuhubiri. Mara nyingi tulipaswa kufanya safari ya kuenda kwenye biro ya poste ili kuchukua karto za magazeti.

Katika mwaka wa 1962, Masomo ya Huduma ya Ufalme yalifanywa katika inchi yote ya Brazili. Kwa miezi sita, nilipewa mugawo wa kusafiri mimi mwenyewe kwenye masomo mbalimbali. Nilifundisha masomo hayo katika Manaus, Belém, Fortaleza, Recife, na Salvador. Wakati nilikuwa katika Manaus, nilifanya matayarisho ya mukusanyiko katika jumba fulani la opera lenye kujulikana sana. Kwa sababu ya mvua kubwa, hakukuwa maji ya mingi ya kunywa yenye kuwa safi, na hatukukuwa na nafasi ya muzuri kwenye ndugu na dada wangekulia chakula wakati wa mukusanyiko. Niliongea na mukubwa mumoja wa jeshi na kumuelezea tatizo letu. Kwa upendo, alifanya mipango ili kutupatia maji ya kunywa wakati wote wa mukusanyiko. Pia, alituma maaskari wakuje wajenge hema mbili kubwa, zenye tulitumia kuwa nafasi ya kupikia chakula na nafasi ya kukulia.

Wakati nilisafiri, Mary alihubiri katika nafasi ya biashara kwenye hakuna mutu mwenye alipenda kuzungumuza juu ya Biblia. Watu hao walitoka Portugal ili kutafuta feza katika Brazili. Mary alivunjika moyo na kuambia marafiki wake fulani hivi: “Fasi ya mwisho kwenye ningependa kuishi katika dunia ni katika inchi ya Portugal.” Muda mufupi tu kisha hapo, tulipata barua fulani. Ilikuwa mugawo wa kutumikia Portugal, kwenye kazi yetu ya kuhubiri ilikuwa imekatazwa. Mary alishangaa sana! Lakini tulikubali mugawo huo na tukahamia Portugal.

MUGAWO WETU KATIKA PORTUGAL

Tulifika katika muji wa Lisbon, Portugal, katika Mwezi wa 8, 1964. Polisi wa siri walikuwa wanasumbua sana ndugu zetu katika muji huo. Kwa hiyo, tuliona kuwa ni jambo la hekima tusitafute kwanza Mashahidi wa eneo hilo. Kwanza, tuliishi katika chumba cha kulipia. Kisha wakati tulipata viza zetu, tulikamata nyumba ya kulipia. Kisha miezi tano, hatukuogopa tena kuzungumuza na ndugu kwenye biro ya tawi. Mwishowe, tulifurahi sana wakati tuliweza kuenda kwenye mikutano!

Kwa sababu kazi yetu ilikuwa imekatazwa, Majumba ya Ufalme yalifungwa na mikutano ya kutaniko ilikuwa inafanywa katika nyumba za ndugu. Mara kwa mara nyumba zao zilichunguzwa na polisi. Mamia ya ndugu na dada walipelekwa kwenye biro za polisi ili kuulizwa maulizo. Polisi waliwatendea mubaya kisha walijaribu kuwakaza watoe majina ya ndugu wenye kuwa na madaraka. Kwa hiyo, ili ndugu walinde ndugu wenzao, waliacha kuitana kwa majina yao ya jamaa na wakaanza kuitana kwa majina yao mengine tu.

Kusudi letu kubwa lilikuwa kuhakikisha kama ndugu wangeendelea kupata vichapo vyenye vingewasaidia kuvumilia. Kwa kutumia mashine, Mary alikuwa anaandika habari za kujifunza za Munara wa Mulinzi na vichapo vingine kwenye karatasi fulani ya pekee. Kisha karatasi hiyo ilitumiwa ili kufanya kopi nyingi kwa ajili ya ndugu na dada.

KUTETEA HABARI NJEMA KWENYE TRIBINALI

Katika Mwezi wa 6, 1966, kesi kubwa ilifanywa kwenye tribinali katika Lisbon. Mashahidi wote 49 wa Kutaniko la Feijó walishitakiwa kuwa walihuzuria mukutano wenye haukubaliwe na sheria katika nyumba ya mutu fulani. Ili kuwatayarisha kwa ajili ya kusamba, nilijifanya kuwa mwanasheria (avocat) mwenye angejaribu kuonyesha kama ndugu walikuwa na makosa. Lakini, kama vile tu tulikuwa tunafikiri, hatukupata ushindi. Ndugu na dada hao 49 walifungwa kwa wakati fulani katika gereza, kuanzia siku 45 mupaka miezi tano na nusu. Lakini tulitoa ushahidi mukubwa wakati tulikuwa tunasamba. Mwanasheria wetu alitaja hata maneno ya Gamalieli yenye kuwa katika Biblia. (Matendo 5:33-39) Kisha, vyombo vya kutangaza habari vilizungumuzia jambo hilo. Tulifurahi sana wakati mwanasheria wetu alianza kujifunza Biblia pamoja na sisi na kuanza kukusanyika.

Katika Mwezi wa 12, 1966, nilipewa mugawo wa kuwa musimamizi wa biro ya tawi na nilitumia wakati mwingi ili kushugulikia mambo ya kisheria. Tulifanya yetu yote ili kutoa sababu za kisheria zenye kuonyesha sababu gani Mashahidi wa Yehova walipaswa kukubaliwa kuabudu kwa uhuru katika Portugal. (Wafilipi 1:7) Mwishowe, tarehe 18 Mwezi wa 12, 1974, tulikubaliwa na sheria. Ndugu Nathan Knorr na Frederick Franz walitoka kwenye makao makubwa ili kuja kufurahi pamoja na sisi. Tulifanya mukutano wenye hatuwezi kusahau katika muji wa Oporto na Lisbon na watu 46870 walihuzuria.

Yehova alisaidia pia kazi ya kuhubiri ifike katika visiwa kwenye watu wanasema Kireno, kama vile kisiwa cha Açores, Cap-Vert, Madère, na Sao Tomé-et-Principe. Kadiri hesabu ya Mashahidi iliongezeka katika maeneo hayo, tulikuwa na lazima ya Beteli kubwa zaidi. Kisha Beteli hiyo kujengwa, Ndugu Milton Henschel alitoa hotuba ili kuitoa kwa Yehova tarehe 23 Mwezi wa 4, 1988. Ndugu na dada 45522 walikuwa kwenye tukio hilo, kutia ndani wamisionere 20 wenye walikuwa wametumikia Portugal wenye walikuja tena katika inchi hiyo kwa ajili ya tukio hilo

MIFANO YA WATUMISHI WAAMINIFU ILITUFUNDISHA

Kwa miaka mingi, mimi na Mary tumefurahia kabisa kujifunza mambo mbalimbali kutoka kwa ndugu waaminifu. Kwa mufano, wakati nilitumika pamoja na Ndugu Theodore Jaracz katika ziara ya mwangalizi wa eneo la dunia, nilijifunza jambo la maana. Tawi yenye tulikuwa tunatembelea ilikuwa na tatizo kubwa, na ndugu wa Halmashauri ya Tawi walikuwa wamejikaza sana ili kusaidia. Walihuzunika kwa sababu hawangeweza kufanya mengi zaidi. Kwa hiyo, Ndugu Jaracz aliwatia moyo kwa kusema hivi: “Sasa ni wakati wa kuachia roho takatifu nafasi ya kutenda.” Pia, sitasahau hata siku moja jambo lenye Ndugu Franz alisema kumepita miaka mingi wakati mimi na Mary tulitembelea Brooklyn. Pamoja na watu wengine, tulimuomba mashauri, na akatuambia hivi: “Pendekezo langu ni hili: Mushikamane na tengenezo lenye kuonekana la Yehova hata katika magumu. Ni tengenezo hilo tu ndilo linafanya kazi yenye Yesu aliamuru wanafunzi wake wafanye; kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu!”

Kufanya hivyo kumetusaidia mimi na Mary tukuwe wenye furaha sana. Pia, tunaendelea kukumbuka mambo mengi ya muzuri yenye tuliona wakati tulikuwa tunafanya ziara ya mwangalizi wa eneo la dunia katika tawi mbalimbali katika dunia. Tulifurahia kukutana na watumishi wa Yehova wa miaka mbalimbali na kuwahakikishia kuwa utumishi wao kwa Yehova unaonwa kuwa wa maana. Sikuzote, tuliwatia moyo waendelee kumutumikia Yehova.

Kumepita miaka mingi, na sasa sisi wawili tuko na miaka 80 hivi. Mary iko na matatizo mbalimbali ya afya. (2 Wakorintho 12:9) Tumepata magumu mengine. Lakini magumu hayo yametia nguvu imani yetu na kutufanya tuazimie zaidi kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova. Wakati tunaangalia miaka yenye tumemutumikia Yehova, tunaona kama kwa fazili zake zenye hatustahili, ametubariki katika njia nyingi sana. *—Soma maelezo ya chini.

^ fu. 29 Wakati habari hii ilikuwa inatayarishwa ili kutolewa, Douglas Guest alikufa muaminifu kwa Yehova tarehe 25 Mwezi wa 10, 2015.