Ona video zinazopatikana

Alipata Kusudi mu Maisha

Alipata Kusudi mu Maisha

Ripoti ya Waeneza-injili wa Ufalme

Alipata Kusudi mu Maisha

Yesu alisema kama anajua kondoo wake. (Yohana 10:14) Kama mutu iko na moyo muzuri na anapenda amani na haki, atafurahia wafuasi wa Yesu. Atapata kusudi mu maisha, sawa vile mufano wa mwanamuke fulani wa inchi ya Ubelgiji unaonyesha. Hii njo habari juu ya maisha yake:

“Wakati Mashahidi wa Yehova waligonga ku mulango yangu, nilikuwa navunjika moyo sana na nilikuwa nafikiria kujiua. Nilifurahia wakati Mashahidi wa Yehova waliniambia kama magumu yote yenye iko mu hii dunia itaisha. Lakini sikufurahi kujua kama Mungu njo ataimaliza. Kulikuwa kulishapita miaka munane tangu niache kuenda ku kanisa, juu nilichukia unafiki wenye nilikuwa naona mule. Lakini wakati nilizungumuza na Mashahidi wa Yehova, nilitambua kama walikuwa wanafundisha mambo ya kweli, na nilielewa kama kuishi bila kumutegemea Mungu ni bure.

“Lakini, kisha wakati fulani, Mashahidi waliacha kunitembelea. Ile ilifanya nihuzunike sana. Nilikuwa navuta paketi mbili za sigareti kwa siku na hata nilianza kutumia dawa za kulewesha. Juu nilipenda kuzungumuza na tate yangu mwanaume mwenye alikuwa alishakufa, nilijiingiza mu mambo ya uchawi. Kwa hiyo, pepo wachafu walianza kunitendea mubaya usiku wakati nilikuwa miye peke, na ile ilifanya niogope sana! Ile hali iliendelea kwa miezi mingi. Kila mangaribi, niliogopa sana kuwa miye peke.

“Kisha, siku moja nilienda tembea kidogo na nikapitia mu njia yenye sikukuwa nazoea. Nikafika fasi fulani kwenye watu walikuwa wanajenga. Nilishangala sana kuona watu wengi pale. Wakati nilikaribia, niliona kama walikuwa Mashahidi wa Yehova wenye walikuwa najenga Jumba ya Ufalme. Nilikumbuka namna Mashahidi wa Yehova walikuwa nanitembelea, na nikajiambia kama dunia ingekuwa muzuri sana ikiwa watu wote wangeishi kama Mashahidi wa Yehova.

“Nilipenda Mashahidi waanze kunitembelea tena, kwa hiyo nilizungumuza na Mashahidi fulani wenye walikuwa najenga ile jumba ya Ufalme. Nilisali kwa Mungu, na kisha siku kumi, mwanaume mwenye alinitembeleaka mara ya kwanza aligonga ku mulango yangu. Aliniambia tuanze tena kujifunza Biblia, na nilikubali kwa furaha. Bila kukawia, alinialika ku mikutano ku Jumba ya Ufalme na niliitika. Nilikuwa siyaona watu wenye kupendeza vile! Maisha yangu yote, nilikuwa nimetafuta watu wenye kupendana na wenye kuwa na furaha. Na sasa nilikuwa nimewapata!

“Kisha pale, nilianza kuenda ku mikutano yote. Na kisha majuma tatu hivi, niliacha kuvuta tumbako. Nilitupa vitabu na miziki ya mambo ya uchawi, na nilianza kuona kama pepo wachafu hawakukuwa nanisumbua tena. Nilianza kutumikisha kanuni za Yehova mu maisha yangu, na kisha miezi tatu, nikaanza kuhubiri habari njema. Kisha miezi sita nilibatizwa. Na siku mbili kisha kubatizwa, nikakuwa painia musaidizi.

“Ninashukuru Yehova sana juu ya mambo yote ya muzuri yenye amenifanyia. Sasa maisha yangu iko na kusudi. Kwa kweli, jina ya Yehova ni munara wenye nguvu, kwenye nilikimbilia juu nipate ulinzi. (Mezali 18:10) Ninakubaliana kabisa na hii maneno yenye muandikaji mumoja wa Zaburi aliandika mu Zaburi 84:10. Aliandika hivi: ‘Kwa maana siku moja katika viwanja vyako inapita siku elfu moja (1 000) mahali pengine popote! Ninachagua kusimama kwenye muingilio wa nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya uovu.’”

Ule mwanamuke munyenyekevu alipata kusudi mu maisha. Na kila mutu mwenye anatafuta kabisa Yehova kwa moyo wote, naye anaweza kupata kusudi mu maisha.