Ona video zinazopatikana

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Biblia haizungumuzie tabia ya kugongesha virauli, sasa juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawafanyake vile?

Kugongesha virauli vya divai (ao pombe ingine) ni tabia ya zamani sana na yenye imeenea sana. Mu maeneo mbalimbali watu wanaifanyaka mu njia tofauti-tofauti. Wakati fulani watu hawagongeshake virauli, lakini wanaviinuaka tu na kutakiana maisha yenye furaha, afya ya muzuri, maisha ya murefu, na mambo ingine ya vile. Wengine wenye kuwa pale wanaweza kusema kwa sauti kama wanakubaliana na ile maneno ao wanaweza kupandisha virauli vyao na kunywa divai kidogo. Watu wengi wanaona kama kufanya vile haiko mubaya, ni njia tu ya kuonyesha wengine heshima. Lakini Mashahidi wa Yehova wako na sababu zenye zinawachochea wasifanye vile.

Haiko kusema kama Wakristo hawapendi wengine wakuwe na furaha, ao na afya ya muzuri. Wakati baraza yenye kuongoza ya kwanza-kwanza iliandikia makutaniko barua, ilimalizia na maneno yenye inaweza kutafsiriwa “afya njema kwenu,” “mukuwe salama,” ao “tunawatakia mambo ya muzuri.” (Matendo 15:29) Zaidi ya ile, waabudu fulani wa Yehova waliambia hivi wafalme: “Bwana wangu Mufalme . . . aishi milele” ao “Mufalme aishi siku nyingi.”​—1 Wafalme 1:31; Nehemia 2:3.

Lakini, tabia ya kugonganisha virauli ilitoka wapi? Mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 1, 1968, mulikuwa hii maneno ya kitabu The Encyclopædia Britannica (1910), mu Buku ya 13, ukurasa wa 121: “Inaonekana kabisa kama desturi ya kugonganisha virauli juu ya kutakia wazima ‘afya’ ya muzuri ilitokana na desturi ya zamani ya kidini ya kunywa kwa ajili ya miungu na wafu. Wakati ya kula, Wagiriki na Waroma walikuwa wanamwanga kinywaji chini kwa ajili ya miungu yao, na wakati ya sikukuu zao walikuwa wanakunywa juu ya kuonyesha heshima ile miungu na wafu.” Ile kitabu iliongeza tena hivi: “Inawezekana watu walikuwa wanakunywa na kutakiana afya ya muzuri wakati walikuwa wanafanya vile.”

Halafu leo? Kitabu International Handbook on Alcohol and Culture yenye ilitolewa mu 1995 inasema hivi: “Leo, wakati watu wanagonganisha virauli, hata kama hawafanye vile juu ya sababu za kidini, inawezekana ile tabia inatokana na desturi ya zamani ya kutolea miungu kinywaji takatifu, ni kusema damu ao divai, na pia kutakiana mambo ya muzuri kwa kutumia maneno sawa vile ‘ukuwe na maisha ya murefu!’ ao ‘ukuwe na afya ya muzuri!’”

Kwa kweli, haimaanishe kama juu tu kitu fulani ilikuwa natumiwa zamani mu dini ya uongo, ni kusema ni ya mubaya. Fikiria mufano wa tunda yenye kuitwa komamanga. Kitabu fulani yenye kuzungumuzia Biblia inasema hivi: “Inaonekana kama komamanga ilikuwa pia alama takatifu mu dini za kipagani.” Lakini, Mungu aliamuru makomamanga yenye kutengenezwa na uzi iwekwe ku upinde wa nguo ya kuhani mukubwa, na makomamanga ilipamba nguzo za shaba za hekalu ya Sulemani. (Kutoka 28:33; 2 Wafalme 25:17) Zaidi ya ile, wakati fulani pete ya ndoa ilikuwa na maana ya kidini, lakini watu wengi leo hawaionake vile. Wanaionaka tu kuwa alama ya kuonyesha kama mutu fulani ameoa ao kuolewa.

Biblia inasema nini kuhusu kutumia divai mu ibada ya miungu ya uongo? Kwa mufano, siku fulani, wanaume wa Shekemu wenye kuabudu Baali ‘waliingia katika nyumba ya mungu wao, wakakula na kunywa na kumulaani Abimeleki,’ mwana wa Gideoni. (Waamuzi 9:22-28) Unawaza muabudu muaminifu wa Yehova angeweza kunywa ile divai na kumuomba Baali alaani Abimeleki? Kuhusu wakati fulani yenye Waisraeli waliacha kumutii Yehova, Amosi anasema hivi: “Wanajinyoosha karibu na kila mazabahu juu ya nguo zenye walinyanganya ili zikuwe kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo; na divai yenye wanakunywa katika nyumba ya miungu yao.” (Amosi 2:8) Unawaza waabudu wa kweli wangefanya vile? Wangemwanga divai kuwa toleo ao kuikunywa ili kuonyesha miungu heshima? (Yeremia 7:18) Ao unawaza muabudu wa kweli anageinua juu kirauli ya divai na kuomba miungu ibariki mutu fulani?

Inafurahisha kujua kama, wakati fulani watumishi wa Yehova waliinua mikono yao juu ili kuomba Mungu awafanyie mambo ya muzuri. Waliinua mikono yao kwa Mungu wa kweli. Biblia inasema hivi: “Sulemani akasimama mbele ya mazabahu ya Yehova mbele ya kutaniko lote la Israeli, na akanyoosha mikono yake kuelekea mbinguni; na akasema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe . . . na usikie ukiwa katika makao yako mbinguni; ndiyo, usikie na usamehe.’” (1 Wafalme 8:22, 23, 30) Vilevile, ‘Ezra alimusifu Yehova . . . kisha watu wote wakajibu, ‘Amina! Amina!’ nao wakainua mikono yao juu. Kisha wakainama na kushusha nyuso chini mbele ya Yehova.’ (Nehemia 8:6; 1 Timoteo 2:8) Ni wazi kama wale watumishi wa Yehova waaminifu hawakuinua mikono kuelekea mbinguni juu ya kuomba baraka kutoka kwa miungu fulani wa bahati.​—Isaya 65:11.

Leo, watu wengi wenye wanainuaka virauli vyao na kuvigongesha, hawajuake kama wako naomba jibu ao baraka kutoka kwa miungu fulani. Lakini pia hawawezi kufasiria juu ya nini wanainuaka virauli vyao vya divai kuelekea mbinguni. Siye Wakristo wa kweli hatupaswe kuwaiga juu tu hawajue sababu gani wanafanyaka vile.

Mara mingi, hata mu mambo ingine, Mashahidi wa Yehova wanajizuiaka kufanya mambo fulani yenye watu wengi wanafanyaka. Kwa mufano, watu wengi wanafanyaka alama fulani juu ya kusalimia bendera. Hawaonake kama kufanya vile ni kuabudu bendera. Wakristo wa kweli hawazuiake wengine kufanya zile alama. Lakini wao hawazifanyake. Ikiwa wanajua wakati ile mambo itafanywa, Mashahidi wengi wanajikazaka wasikuwe pale. Lakini kama hali inawalazimisha wakuwe pale, hawafanyake alama yoyote ya kutukuza taifa, yenye inapingana na kanuni za Biblia. (Kutoka 20:4, 5; 1 Yohana 5:21) Leo watu wengi hawaonake kama kugonganisha virauli ni tendo ya kidini. Lakini, Wakristo wako na sababu za muzuri zenye zinawachochea wasifanye vile. Wanajua kama ile tabia ilitokana na dini za uongo za zamani. Na hata leo, kufanya vile ni kuomba baraka kutoka kwa ‘mbingu’ ao kwa nguvu fulani yenye haiko ya kawaida.​—Kutoka 23:2.