Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaweza Kufanya Mengi Zaidi ili Kuwaonya Wengine?

Unaweza Kufanya Mengi Zaidi ili Kuwaonya Wengine?

Filme nzuri ya bila sauti iliyoitwa A Trip Down Market Street iliwavutia watazamaji sana kwa sababu ilionyesha namna maisha yalivyokuwa huko San Francisco, Amerika, mwanzoni mwa miaka ya 1900. Watengenezaji wa filme hiyo waliweka kamera inayoendeshwa kwa mikono juu ya motokari na kuelekezea kamera hiyo kwenye barabara yenye kujaa watu. Filme hiyo ilionyesha mambo mengi kama vile motokari za kukokotwa na farasi na aina za kwanza​-kwanza za motokari, na vilevile watu wanaouzisha katika maduka na vijana wanaouzisha magazeti katika shuguli zao za kila siku.

Filme hiyo ilikuwa yenye kuhuzunisha sana kwa sababu ilirekodiwa kwenye video Mwezi wa 4, 1906, mbele tu ya tetemeko la dunia na mulipuko wa moto uliotokea tarehe 18 Mwezi wa 4, ambao uliua maelfu ya watu na kuharibu sehemu kubwa ya muji. Inaonekana kwamba, watu fulani walioonyeshwa katika filme hiyo walibaki tu na siku chache za kuishi. Scott Miles, ambaye ni muzao wa mumoja kati ya wale waliotengeneza filme hiyo, anasema hivi: “Watu ambao ninaona katika muji huo hawakujua jambo ambalo lingewapata kisha siku chache. Na hauwezi kuwasaidia ila tu unaweza kuwasikilia huruma.”

Tetemeko la dunia na moto ulitokea mwaka wa 1906 huko San Francisco bila kutazamia na kuharibu sehemu kubwa ya muji huo

Jambo hilo linaweza kutufanya tufikiri kwa uzito kuhusu siku zetu. Sisi pia hatuwezi kuzuia jambo litakalowapata majirani zetu. Wanaendelea kufanya shuguli zao za kila siku bila kujua musiba utakaowapata karibuni, ni kusema, uharibifu wa ulimwengu huu na matendo yake. Tofauti na tetemeko la dunia lisilotazamiwa, tungali na nafasi fupi ya kuonya majirani zetu kuhusu siku ya hukumu ya Yehova. Pengine umepanga programe ya kuhubiri nyumba kwa nyumba kila juma, lakini, unaweza kufanya mengi zaidi ili kuwaonya wengine?

YESU ALIKUWA TAYARI KUHUBIRI KILA WAKATI

Yesu alituachia mufano muzuri kwa sababu alikuwa tayari kuhubiri kila wakati. Alihubiria kila mutu aliyekutana naye. Alihubiria mutoza​-kodi aliyekutana naye katika barabara fulani, na alipokuwa akipumuzika wakati wa muchana, alimuhubiria mwanamuke mumoja kwenye kisima. (Lu. 19:1-5; Yoh. 4:5-10, 21-24) Hata wakati alipenda kupumuzika, Yesu alitumia wakati huo ili kuwafundisha wengine bila kunungunika. Alisikilia majirani zake huruma, na hilo lilimuchochea ahubiri zaidi. (Mk. 6:30-34) Bila shaka, Yesu aliona uhitaji wa kutenda kwa uharaka; namna gani tunaweza kumuiga leo?

WALITUMIA KILA NAFASI ILIYOJITOKEZA ILI KUHUBIRI

Dada Melika anaishi katika nyumba inayochungwa sana. Majirani zake wengi ni wanafunzi kutoka inchi za kigeni wanaotumia telefone za mukononi na namba zao hazipatikane katika kitabu kilicho na namba za telefone za watu wa mahali hapo. Anatumia nafasi za pekee ili kuanzisha mazungumuzo kuhusu Biblia pamoja na watu anaokutana nao kwenye mwingilio wa nyumba hiyo ao mahali ambapo kuna mashine ya kupandisha na kushusha watu. Anasema hivi: “Ninachukua nafasi hiyo kuwa eneo langu.” Melika anachukua magazeti katika luga mbalimbali, na wengi wanakubali magazeti na trakti. Anawatia moyo pia watembelee adresi yetu ya internete, jw.org. Kwa Kufanya hivyo, ameanzisha mafunzo mengi ya Biblia.

Dada Sonia pia anatumia kila nafasi ili kuhubiri. Anatumika katika hospitali fulani, na anajiwekea muradi wa kuhubiri kila mumoja kati ya wafanyakazi wenzake. Kwanza, alichukua wakati wa kufikiria mahitaji na mapendezi ya kila mumoja wao. Kisha, alikuwa akitumia pumuziko la muchana ili kuhubiria kila mumoja wao. Amepata matokeo mazuri kwa sababu alianzisha mafunzo mawili ya Biblia. Anafanya pia mipango ili kupumuzikia mahali ambapo watu wanangojea kuonana na muganga.

TUMIA KILA NAFASI INAYOJITOKEZA

Mwanaume mumoja aliyeokoka tetemeko la dunia la 1906, aliita tetemeko hilo “musiba mubaya zaidi ya misiba yote ambayo ilikuwa imekwisha tokea katika muji fulani.” Lakini, hivi karibuni kuna musiba utakaotokea ambao utashinda misiba yote ambayo imekwisha kutokea, musiba huo ni siku ya kisasi ya Yehova inayokuja juu ya wale wote ‘wasiomujua Mungu.’ (2 Thes. 1:8) Yehova anatamani sana watu wabadili akili na mioyo yao na watii maonyo ambayo Mashahidi wake wanaendelea kutoa.​—2 Pet. 3:9, Ufu. 14:6, 7.

Je, unaweza kutumia kila nafasi inayojitokeza ili kuhubiri unapofanya shuguli zako za kila siku?

Una pendeleo la kufungua watu macho ili waelewe kwamba tunaishi kipindi cha hatari na kuwasaidia waache kutafuta tu faida zao wenyewe, lakini wamutafute Yehova. (Zef. 2:2, 3) Je, unaweza kutumia kila nafasi inayojitokeza ili kuhubiria wafanyakazi wenzako, majirani zako, na wale unaokutana nao katika shuguli zako za kila siku? Je, utafanya mengi zaidi ili kuwaonya wengine?