Ona video zinazopatikana

SEHEMU YA 5

Ukweli Juu ya Uchawi na Ulozi

Ukweli Juu ya Uchawi na Ulozi

1. Ni kwa kadiri gani watu wanaamini uchawi na ulozi?

 KITABU African Traditional Religion inasema kama “mu Afrika haiko hata lazima kuuliza kama wachawi wanakuwaka. Waafrika wa hali zote wanaamini sana uchawi.” Ikuwe walisomaka ao hapana, wote wanaamini uchawi na ulozi. Viongozi wa dini ya Waislamu na Wakristo, wote wanaamini uchawi na ulozi.

2. Watu wengi wanaamini kama nguvu za uchawi zinatokaka wapi?

2 Mu Afrika, watu wengi wanaamini kama kuko nguvu fulani ya uchawi yenye iko na uwezo sana. Wanaamini kama Mungu njo anaongozaka ile nguvu. Viumbe wa roho na roho za wafu wanaweza kutumia ile nguvu. Na wanaamini pia kama wanadamu fulani wanaweza kuitumia juu ya kufanyia watu mambo ya muzuri ao ya mubaya.

3. Watu wanaamini kama uchawi mubaya njo nini, na wanaamini nini juu ya ule uchawi?

3 Uchawi mubaya ao ulozi unatumiwaka juu ya kufanyia maadui mambo ya mubaya. Watu wanaamini kama wale wenye kufanya ule uchawi, wanatumaka ndege, popo, na inzi, na wanyama wengine, juu wafanyie watu mambo ya mubaya. Wanaamini pia kama ule uchawi njo unaletaka vita, unafanyaka wanamuke wasizale, unaletaka magonjwa na hata kifo.

4. Watu wengi wanaamini nini juu ya wachawi, na watu fulani wenye walikuwa wachawi zamani walisemaka nini?

4 Wengine wanaamini kama wachawi wanaweza kutendea watu mubaya. Wanaamini kama muchawi anaachaka mwili yake usiku na anaruka juu ya kuenda kukutana na wachawi wenzake, ao juu ya kuua watu. Lakini hakuna ushuhuda wenye unahakikisha ile jambo. Ni watu tu wenye walikuwaka wachawi zamani njo wanaelezeka zile habari. Kwa mufano, gazeti moja ya Afrika ilionyesha maneno ya watu wenye walikuwaka wachawi zamani, zaidi sana vijana wanamuke. Walisema hivi: “Niliua watu 150 kwa kufanya pikipiki zifanye aksida.” “Niliua watoto 5 kwa kuwanyonya damu yote.” “Niliua wanaume 5 juu walinikatala.”

5. Watu wanaamini kama uchawi muzuri njo nini, na wenye kufanya ule uchawi wanafanyaka nini?

5 Watu wanaamini kama uchawi muzuri njo uchawi wenye unalindaka watu juu mambo ya mubaya isiwafikie. Wale wenye kufanya ule uchawi wanavalaka pete na vikomo vya uchawi. Wanakunywaka dawa za kuwalinda ao kuzipakala ku mwili wao. Wanafichikaka vitu mu nyumba na mu udongo juu viwalinde. Wanatumainia hirizi zenye kuwa na maneno ya Biblia ao ya Korani.

Mambo ya Uongo Kabisa

6. Shetani na pepo wake wachafu walifanya nini zamani, na tunapaswa kuona namna gani nguvu zao?

6 Ni kweli kama Shetani na pepo wake wachafu ni maadui, na wanaweza kutendea wanadamu mubaya. Wako na uwezo wa kuvuruga akili na maisha ya watu. Zamani waliingia hata mu watu na mu wanyama. (Matayo 12:43-​45) Hatupaswe kuzarau uwezo wao. Lakini pia hatupaswe kuwaza kama wako na nguvu zenye hazina mipaka.

7. Shetani anapenda tuamini nini, na ni mufano gani unaweza kutusaidia tuelewe ile jambo?

7 Shetani anajua kudanganya sana. Anafanya watu waamini kama iko na nguvu zenye hana. Kwa mufano mu inchi fulani ya Afrika, wakati wa vita maaskari walitumia vyombo vya kuongeza sauti juu ya kuogopesha maadui wao. Mbele ya kushambulia, walikuwa napiga rekodi za bunduki kubwa-kubwa. Walipenda maadui wao wawaze kama wako nashambuliwa na jeshi yenye kuwa na bunduki za mingi tena kubwa-kubwa. Vile njo Shetani naye anafanyaka. Anapenda watu waamini kama iko na nguvu zenye hazina mipaka. Anafanyaka vile juu ya kuogopesha watu ili wafanye mapenzi yake, hapana mapenzi ya Yehova. Tuone mambo tatu ya uongo yenye Shetani anapenda watu waamini.

8. Uongo wa kwanza wenye Shetani anapenda watu waamini ni nini?

8 Uongo wa kwanza: Hakuna jambo ya mubaya yenye inajitokeza. Kama kunatokea jambo fulani ya mubaya, ni kusema kuko mutu ao nguvu fulani yenye iliitokeza. Kwa mufano tuseme mutoto anagonjwa malaria kisha anakufa. Mama yake anaweza kujua kama imbu njo inaletaka malaria. Lakini, anaweza pia kuamini kama kuko mutu mwenye aliomba muchawi atume imbu juu ilume mutoto wake.

Wakati fulani mambo ya mubaya inafikaka tu

9. Biblia inasema nini yenye inaonyesha kama haiko Shetani njo analetaka kila jambo ya mubaya?

9 Ni kweli kama Shetani iko na uwezo wa kuleta magumu fulani. Lakini ni makosa kuwaza kama yeye njo analetaka kila jambo ya mubaya. Biblia inasema hivi: “Haiko wenye mbio ndio wanashinda kila mara katika mbio, wala haiko wenye nguvu ndio wanashinda katika vita, wala haiko wenye hekima ndio wanapata kila mara chakula, wala haiko wenye akili ndio wanakuwa kila mara na utajiri, wala haiko wenye ujuzi ndio wanafanikiwa kila mara, kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe yanafikia wote.” (Muhubiri 9:11) Mu mashindano, mukimbiaji fulani anaweza kuwa na mbio kuliko wengine. Lakini inawezekana asipate ushindi. ‘Tukio yenye haitazamiwe’ inaweza kufanya asipate ushindi. Pengine anakwala na kuanguka, anagonjwa, ao anavunjika. Ile mambo inaweza kufikia kila mutu. Haiko kusema kama Shetani ao muchawi fulani njo alifanya mambo ikuwe vile. Mambo ya vile inafikaka tu.

10. Watu wanasemaka nini juu ya walozi na nini njo inaonyesha kama ni uongo?

10 Uongo wa pili: Usiku walozi wanaachaka mwili wao juu ya kuenda kukutana na walozi wenzao ao juu ya kuenda kunyonya damu ya maadui wao ao kuwakula. Sasa ujiulize hivi: ‘Kama walozi wanaweza kufanya vile, nini njo inatokaka mu mwili na kuenda? Sawa vile tumeona, nafsi njo mutu. Haiko kitu yenye inatokaka mu mutu. Tena roho ni nguvu yenye inasaidiaka mwili uendelee kuishi na haiwezi kufanya kitu inje ya mwili.

Wachawi hawawezi kuacha mwili wao

11. Nini njo inatusaidia kujua kama walozi hawawezi kuacha miili yao, na unaamini ile?

11 Ikuwe nafsi ao ikuwe roho, hakuna yenye inatokaka mu mwili juu ya kuenda kufanya jambo ya muzuri ao ya mubaya. Njo maana walozi hawawezi kuacha mwili wao. Kusema kweli, hawafanyake mambo yenye wanasemaka kama walifanya ao yenye wanawazaka kama walifanya.

12. Shetani anaweza kutumia nini juu ya kufanya watu waamini kama walifanya mambo yenye hawakufanya?

12 Sasa, tuseme nini juu ya mambo yenye wale wenye walikuwaka walozi zamani wanasemaka kama walikuwaka wanafanya? Shetani anaweza kufanya watu waamini kama walifanya mambo yenye hawakufanya. Shetani anaweza kutumia maono juu ya kufanya watu wawaze kama wameona, wamesikia, na kufanya mambo yenye hawakufanya. Shetani anafanyaka vile juu anatumaini kama ile itafanya watu wamuache Yehova na kufanya watu wawaze kama mambo yenye Biblia inasema haiko ya kweli.

13. (a) Uchawi muzuri ni kosa? (b) Biblia inasema nini juu ya uchawi?

13 Uongo wa tatu: Watu wanawazaka kama uchawi muzuri haiko kosa juu unaweza kumaliza nguvu ya uchawi mubaya. Biblia haionyeshe kama kuko tofauti kati ya uchawi muzuri na uchawi mubaya. Inakataza kila namna ya uchawi. Ona sheria fulani zenye Yehova alipatiaka taifa ya Israeli kuhusu uchawi na wale wenye kufanya uchawi:

  •   “Hamupaswe . . . kufanya uchawi.”​—Mambo ya Walawi 19:26.

  •   “Kila mwanaume ao mwanamuke mwenye kupashana habari na pepo wachafu ao mwenye kutabiri matukio anapaswa kabisa kuuawa.”​—Mambo ya Walawi 20:27.

  •   “Asipatikane katikati yako . . . mutu yeyote mwenye kufanya uchawi, mutu yeyote mwenye kutafuta alama za mambo yenye yatatokea, mulozi, mutu yeyote mwenye anafunga wengine kwa uchawi.”​—Kumbukumbu la Torati 18:10-​14.

14. Juu ya nini Yehova alipatiaka watu wake sheria zenye zinakataza uchawi?

14 Zile sheria zilionyesha wazi kama Mungu hapendi watu wake wafanye uchawi. Yehova alipatiaka watu wake zile sheria juu aliwapenda. Na hakutaka wakuwe wanaishi mu woga na ushirikina. Hakutaka mashetani wawatese.

15. Namna gani Biblia inaonyesha kama Yehova iko nguvu sana kupita Shetani?

15 Biblia haizungumuzie sana mambo yenye mashetani wanaweza kufanya na yenye hawawezi kufanya. Lakini inaonyesha kama Yehova Mungu iko na nguvu mingi sana kupita Shetani na mashetani wake. Yehova alifukuza Shetani mbinguni. (Ufunuo 12:9) Tena, Shetani aliomba Mungu ruhusa ya kumujaribu Yobu na alitii wakati Mungu alimuambia asiue Yobu.​—Yobu 2:4-6.

16. Tunapaswa kutumainia nani juu atulinde?

16 Mezali 18:10 inasema hivi: “Jina la Yehova ni munara wenye nguvu.Mwenye haki anakimbilia ndani na kupata ulinzi.” Yehova tu njo anaweza kutulinda. Njo maana watumishi wa Yehova hawatumiake hirizi ao dawa ya kujilinda ili wasishambuliwe na Shetani na mashetani wake, na hawaogopake ulozi. Wanaamini hii maneno ya Biblia: Kwa maana macho ya Yehova yanaenda huku na huku katika dunia yote ili kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale wenye moyo wao ni kamili kumuelekea yeye.”​—2 Mambo ya Nyakati 16:9.

17. Yakobo 4:7 inatuhakikishia nini, lakini tunapaswa kufanya nini?

17 Na weye unaweza kuwa hakika na ile maneno kama unamutumikia Yehova. Yakobo 4:7 inasema hivi: “Mujitiishe wenyewe kwa Mungu; lakini mumupinge Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.” Kama unamutumikia Yehova Mungu wa kweli na kumutii, ukuwe hakika kama atakulinda.