Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 12

Rĩ, Nũkwona Mantũ Jarĩa Zekaria Oonere?

Rĩ, Nũkwona Mantũ Jarĩa Zekaria Oonere?

“No ũntũ bwa kĩrundu gĩakwa,’ nĩu Mwathani wa Njũũrĩ augĩte.’​—ZEK. 4:6.

RWĨMBO 73 Tupe Ujasiri

MUHTASARI *

1. Ayahudi barĩa baataĩtwe baarĩ na wĩrĩgĩĩro bũrĩkũ bwa kũgwĩrania?

 WAYAHUDI walikuwa wamesisimka sana. Yehova Mungu alikuwa ‘ameichochea roho ya Mfalme Koreshi wa Uajemi’ awaachie huru Waisraeli, ambao walikuwa utekwani Babiloni kwa miaka mingi. Mfalme alitangaza kwamba Wayahudi wangerudi katika nchi yao na “kujenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli.” (Ezra 1:1, 3) Agizo hilo lilisisimua sana! Lilimaanisha kwamba ibada ya Mungu wa kweli ingerudishwa upya katika nchi ambayo alikuwa amewapatia watu wake.

2. Ayahudi barĩa baataĩtwe bagũcooka Jerusalemu boombanĩre kũthithia atĩa mbere?

2 Katika mwaka wa 537 K.W.K., kikundi cha kwanza cha Wayahudi wahamishwa kiliwasili Yerusalemu, lililokuwa jiji kuu la ufalme wa kusini wa Yuda. Wayahudi hao waliorudi walianza haraka kazi ya ujenzi wa hekalu, na kufikia mwaka 536 K.W.K., tayari walikuwa wamejenga msingi wake!

3. Nĩ ũregani bũrĩkũ Ayahudi bacemanĩrie nabu?

3 Hata hivyo, mara tu walipoanza kujenga upya hekalu wahamishwa hao wa zamani walianza kukabiliana na upinzani mkubwa. Mataifa yaliyowazunguka ‘yalizidi kuwavunja moyo watu wa Yuda na kuwakatisha tamaa ili wasijenge.’ (Ezra 4:4) Hiyo ilikuwa hali mbaya sana kwa Wayahudi. Hata hivyo, mambo yalizidi kuwa mabaya. Katika mwaka 522 K.W.K., Artashasta mfalme mpya wa Uajemi, alianza kutawala. * Wapinzani waliona mabadiliko hayo ya uongozi kuwa fursa yao ya kusitisha kabisa kazi ya ujenzi kwa ‘kutunga matatizo kwa kutumia sheria.’ (Zab. 94:20) Walimwambia Mfalme Artashasta kwamba pamoja na mambo mengine, Wayahudi walikuwa wanapanga kumwasi. (Ezra 4:11-16) Mfalme aliamini uwongo wao, naye akapiga marufuku ujenzi wa hekalu. (Ezra 4:17-23) Kwa sababu hiyo, wajenzi hao ambao mwanzoni walikuwa na furaha waliacha kujenga hekalu.​—Ezra 4:24.

4. Nĩatĩa Jehova aathĩthĩrie bwegie ũreganĩ bwa gwakwa gwa kĩũrũ? (Isaya 55:11)

4 Wakaaji wapagani wa nchi hiyo na baadhi ya viongozi wa serikali ya Uajemi, walikuwa wameazimia kusitisha kazi ya kujenga upya hekalu. Lakini Yehova alikuwa ameazimia kuufanya mradi wa ujenzi uendelee kusonga mbele, naye sikuzote hutimiza kusudi lake. (Soma Isaya 55:11.) Yehova alimwinua nabii asiye na woga aliyeitwa Zekaria na kumpatia mfululizo wa maono manane yenye kusisimua, ambayo alipaswa kuwapa Wayahudi ili kuwatia moyo. Maono hayo yenye kutia moyo yaliwasaidia waone kwamba hawakupaswa kuwaogopa wale waliowapinga na kuwahimiza waendelee kufanya kazi ya Yehova. Katika maono ya tano, Zekaria aliona kinara cha taa na mizeituni.

5. Nĩmbĩ tũkairitana kĩthoomone gĩkĩ?

5 Sisi sote huvunjika moyo pindi fulani. Hivyo, tunaweza kunufaika kwa kuchunguza jinsi Yehova alivyowatia moyo Waisraeli kupitia maono ya tano ya Zekaria. Kuelewa maono hayo kunaweza kutusaidia kumtumikia Yehova kwa uaminifu tunapokabiliana na upinzani, tunapokabiliana na mabadiliko na tunapopokea mwongozo ambao hatuuelewi.

KŨŨMBANA NA ŨREGANI

Zekaria aliona maono ya mizeituni miwili inayopeleka mafuta kwenye kinara cha taa kilichokuwa na taa saba (Tazama fungu la 6)

6. Nĩatĩa Ayahudi boonere ũcamba kuumania na kĩoneki kĩa gĩtugi kĩa tawa na mĩzeituni ĩĩrĩ ĩrĩa ĩtaarĩrĩĩtue kĩrĩ Zekaria 4:1-3? (Tega Mbica karatacine ka mbere.)

6 Soma Zekaria 4:1-3. Maono ya kinara cha taa na mizeituni miwili, yaliwapa Wayahudi ujasiri wa kushinda upinzani. Jinsi gani? Je, umetambua kwamba kinara cha taa kilikuwa na chanzo cha mafuta kisichokoma? Mizeituni miwili ilipeleka mafuta kwenye chombo kilicho kama bakuli, ambacho kilipeleka mafuta kwenye kila moja ya taa saba zilizokuwa kwenye kinara cha taa. Mafuta hayo yalifanya taa hizo ziendelee kuwaka bila kuacha. Zekaria aliuliza hivi: “Vitu hivi vinamaanisha nini?” Malaika alimjibu hivi kwa ujumbe kutoka kwa Yehova: “‘Si kwa jeshi, wala si kwa nguvu, bali kwa roho yangu,’ asema Yehova wa majeshi.” (Zek. 4:4, 6) Mafuta kutoka kwenye miti hiyo yalifananisha roho takatifu ya Yehova yenye nguvu ambayo haiwezi kuisha kamwe. Jeshi lote lenye nguvu la Milki ya Uajemi lilikuwa si kitu kwa kulinganisha na nguvu za roho ya Mungu. Yehova akiwa upande wao, wajenzi hao wa hekalu wangeweza kupinga upinzani wowote na kukamilisha kazi yao. Huo ulikuwa ujumbe wenye kutia moyo sana! Jambo ambalo Wayahudi walihitaji kufanya ni kumtumaini Yehova na kuendelea na kazi. Na hivyo ndivyo walivyofanya hata ingawa walikuwa wamepigwa marufuku.

7. Nĩ ũgarũrũku bũrĩkũ bwatũmĩre aakĩ ba kĩũrũ boothĩrwa nĩ mantũ?

7 Badiliko fulani liliwaletea kitulizo wajenzi wa hekalu. Badiliko gani? Mwaka 520 K.W.K, Uajemi ilikuwa ikitawaliwa na mfalme mpya, Dario wa Kwanza. Katika mwaka wa pili wa utawala wake, aligundua kwamba marufuku ya ujenzi wa hekalu haikuwa halali kisheria. Hivyo, Dario akaruhusu ujenzi ukamilishwe. (Ezra 6:1-3) Habari hizo pekee zilitosha kumstaajabisha kila mtu​—lakini kulikuwa na habari zaidi. Mfalme aliamuru kwamba mataifa yaliyokuwa yakizunguka eneo hilo yaache kuingilia kazi ya kujenga upya na watoe pesa na vifaa ili kutegemeza kazi hiyo! (Ezra 6:7-12) Matokeo ni kwamba Wayahudi walikamilisha kujenga hekalu miaka minne hivi baadaye, katika mwaka wa 515 K.W.K.​—Ezra 6:15.

Tegemea nguvu za Yehova unapokabili upinzani (Tazama fungu la 8)

8. Nĩkĩ ũũmba kwĩthĩrwa na ũcamba rĩrĩa wacemania na ũregani?

8 Leo pia, waabudu wengi wa Yehova wanakabili upinzani. Kwa mfano, baadhi yao wanaishi katika nchi ambazo kazi yetu imewekewa vizuizi. Katika nchi hizo, huenda akina ndugu wakakamatwa na ‘kupelekwa mbele ya magavana na wafalme’ ili kuwatolea ushahidi. (Mt. 10:17, 18) Nyakati nyingine, mabadiliko ya utawala huenda yakaleta kitulizo. Au huenda hakimu asiye na upendeleo akatoa uamuzi ambao unaunga mkono kazi yetu. Mashahidi wengine wa Yehova wanakabili upinzani wa aina tofauti. Wanaishi katika nchi ambayo watu wa Yehova wana uhuru wa kuabudu, lakini bado wanakabili upinzani kutoka kwa watu wa familia ambao wameazimia kuwazuia kumtumikia Mungu wao. (Mt. 10:32-36) Katika visa vingi, wapinzani wanapogundua kwamba jitihada zao za kuwavunja moyo watu wao wa ukoo ambao ni Mashahidi hazitafaulu, wanaacha kuwapinga. Na katika baadhi ya visa, wale ambao pindi fulani walikuwa wapinzani wakali, baadaye walikuja kuwa Mashahidi wenye bidii. Unapokabili upinzani, usife moyo! Uwe jasiri. Yehova anakusaidia kupitia roho yake takatifu yenye nguvu, hivyo, usiogope kitu chochote!

KŨŨMBANA NA ŨGARŨRŨKU

9. Nĩkĩ Ayahudi bamwe baunĩkĩre nkoro rĩrĩa mũcingi jwa kĩũrũ gĩkĩerũ jwakĩrwe?

9 Msingi wa hekalu jipya ulipojengwa, baadhi ya Wayahudi wenye umri mkubwa walilia. (Ezra 3:12) Walikuwa wameona utukufu wa hekalu lililojengwa na Sulemani, na walihisi kwamba hekalu jipya walilokuwa wakijenga lilikuwa ‘duni likilinganishwa’ na la awali. (Hag. 2:2, 3) Walilemewa na huzuni walipolinganisha hekalu jipya na hekalu la zamani. Maono ya Zekaria yangewasaidia washinde hisia zao za kuvunjika moyo. Jinsi gani?

10. Nĩatĩa biugo bia Mũraĩka kĩrĩ Zekaria 4:8-10 biatetherie Ayahudi kũũmbana na kuunĩka nkoro?

10 Soma Zekaria 4:8-10. Malaika alimaanisha nini aliposema kwamba Wayahudi ‘wangeshangilia na kuona timazi mikononi mwa [gavana wa Wayahudi] Zerubabeli’? Timazi ni kifaa kinachotumika kupima kitu kilichonyooka wima. Hivyo, malaika alikuwa akiwahakikishia watu wa Mungu kwamba, ingawa hekalu halikuwa la kifahari kama wengine walivyoona, lingekamilika na lingetimiza viwango vya Yehova. Yehova angefurahishwa nalo, basi wao pia walipaswa kufurahishwa nalo. Jambo lililokuwa muhimu kwa Yehova ni kwamba ibada iliyofanywa katika hekalu hilo jipya ilipatana na matakwa yake. Ikiwa Wayahudi wangekazia fikira ibada ya Yehova inayokubalika na kupata kibali chake, shangwe yao ingerudi.

Sitawisha mtazamo unaofaa unapokabili mabadiliko (Tazama fungu la 11 na 12) *

11. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ bamwe ba athaathayia ba Jehova bacemanagia najo narua?

11 Ni vigumu kwa wengi wetu kukabiliana na mabadiliko. Baadhi ya ndugu na dada ambao wametumikia katika utumishi wa pekee wa wakati wote kwa muda mrefu, wamepata badiliko la migawo. Wengine wamelazimika kuacha mgawo fulani walioupenda kwa sababu umri wao umesonga. Ni jambo la kawaida kuvunjika moyo tunapopata badiliko kama hilo. Mwanzoni, huenda tusielewe kikamili uamuzi huo au kukubaliana nao. Huenda tukatamani maisha yetu ya zamani. Na huenda tukavunjika moyo na kuhisi kwamba thamani yetu imepungua machoni pa Yehova. (Met. 24:10) Maono ya Zekaria yanaweza kutusaidiaje tuendelee kumpa kilicho bora Mungu wetu?

12. Nĩatĩa kĩoneki kĩa Zekaria kĩũmba gũtũteethia tũũmbana na kuunĩka nkoro rĩrĩa mantũ jeetũ jagarũka?

12 Ni rahisi kukabiliana na mabadiliko ikiwa tutaona mambo kama Yehova anavyoyaona. Anatimiza mambo mengi leo, na tuna pendeleo la pekee la kuwa wafanyakazi wenzi wake. (1 Kor. 3:9) Huenda majukumu yetu yakabadilika, lakini upendo wa Yehova kwetu hautabadilika. Hivyo, ikiwa mabadiliko katika tengenezo yatakuathiri wewe binafsi, epuka kutumia muda mwingi kuwazia mambo ambayo huenda yalisababisha mabadiliko hayo. Badala ya kutamani “siku za zamani,” mwombe Yehova akusaidie kutumia mambo mazuri ya badiliko hilo. (Mhu. 7:10) Badala ya kufikiria mambo ambayo huwezi kufanya kwa sasa, fikiria mambo unayoweza kufanya. Kutokana na maono ya Zekaria, tunajifunza umuhimu wa kudumisha mtazamo mzuri. Hivyo, tutaendelea kuwa na shangwe na kuwa waaminifu hata hali zetu zinapobadilika.

RĨRĨA BŨRĨ BŨBŨŨMŨ KŨTHĨNGATA ŨTONGEERIA

13. Nĩkĩ Aisraeli bamwe baĩgĩrue atĩ ĩtua rĩa gwaka kĩũrũ kaĩrĩ rĩarĩ rĩthũũku?

13 Kazi ya kujenga upya hekalu ilipigwa marufuku. Hata hivyo, wanaume waliowekwa rasmi kuongoza kazi, yaani, Kuhani Mkuu Yeshua (Yoshua) na Gavana Zerubabeli ‘walianza kujenga upya nyumba ya Mungu.’ (Ezra 5:1, 2) Huenda baadhi ya Wayahudi walihisi kwamba uamuzi huo ulikuwa mbaya. Hawangeweza kuficha kazi ya kujenga hekalu na maadui zao wangefanya kila walichoweza ili kusimamisha kazi hiyo. Yoshua na Zerubabeli, wanaume waliokuwa wamewekwa rasmi ili kuwaongoza watu, walihitaji kuhakikishiwa kwamba Yehova angewasaidia. Naye aliwasaidia. Jinsi gani?

14. Kũringana na Zekaria 4:12, 14, Joshua Mũthĩnjĩri ũ-Mũnene na Ngavana Zerubabeli boonere ũrikithia bũrĩkũ?

14 Soma Zekaria 4:12, 14. Katika sehemu hii ya maono ya Zekaria, malaika anamfunulia nabii mwaminifu wa Mungu kwamba mizeituni miwili inawakilisha “watiwa-mafuta wawili”​—Yoshua na Zerubabeli. Malaika alisema kwamba, wanaume hao wawili ni kana kwamba walikuwa ‘wamesimama kando ya Bwana wa dunia yote,’ Yehova. Hilo lilikuwa pendeleo kubwa sana! Yehova alikuwa anawatumaini. Hivyo, Waisraeli wenzao walikuwa na kila sababu ya kuwa na uhakika katika maamuzi yao na katika mwongozo wa Mungu, haidhuru mwongozo huo ungehusisha mambo gani.

15. Nĩatĩa twonanagia atĩ nĩtũgũtĩĩa ũtongeeria bwa Jehova bũrĩa bwonoraga rũtetone rwawe?

15 Njia moja ambayo Yehova anaendelea kutoa mwongozo kwa watu wake leo, ni kupitia Neno lake Biblia. Katika kitabu hicho kitakatifu, anatuambia jinsi ya kumwabudu kwa njia inayokubalika. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaheshimu mwongozo tunaopata kutoka katika Neno la Mungu? Ni kwa kusoma kwa makini na kutumia muda ili kuelewa. Jiulize, ‘Ninaposoma Biblia au mojawapo ya machapisho yetu, je, ninatua na kutafakari? Je, ninatafuta maana ya kweli za Biblia ambazo ni “vigumu kuzielewa”? Au je, ninasoma habari hizo haraka-haraka?’ (2 Pet. 3:16) Ikiwa tunatumia muda kutafakari kuhusu mambo ambayo Yehova anatufundisha, tutaweza kufuata mwongozo wake na kutimiza kazi yetu ya kuhubiri.​—1 Tim. 4:15, 16.

Tumaini mwongozo unaopata kutoka kwa mtumwa mwaminifu na mwenye busara (Tazama fungu la 16) *

16. Rĩrĩa tũtĩgũciũkĩrwa bwega nĩ ũtongeeria bũrĩa twaewa nĩ “nthũmba mbĩtĩkua na ĩnjũme,” nĩmbi bĩgatũtethia tũbũthĩngatĩĩra?

16 Njia nyingine ambayo Yehova anatoa mwongozo ni kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Nyakati nyingine, huenda mtumwa huyo akatoa mwongozo ambao hatuuelewi kikamili. Kwa mfano, huenda tukapewa maagizo hususa ambayo yamekusudiwa kutuandaa kwa ajili ya kuokoka majanga ya asili ambayo tunafikiri kwamba hayawezi kutokea katika eneo letu. Au huenda tukahisi kwamba mtumwa anahangaikia hali ya janga kupita kiasi. Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunahisi kwamba maagizo hayo si ya hekima? Tunaweza kufikiria jinsi Waisraeli walivyonufaika kwa kufuata shauri walilopewa kupitia Yoshua na Zerubabeli. Tunaweza pia kufikiria masimulizi mengine ya Biblia ambayo tumesoma. Nyakati nyingine watu wa Mungu walipata mwongozo ambao ulionekana haufai kulingana na maoni ya binadamu, lakini ukawa wenye kuokoa uhai.​—Amu. 7:7; 8:10.

ONA KĨRĨA ZEKARIA ONERE

17. Kĩoneki kĩa gĩtugi kĩa tawa na mĩzeituni ĩĩrĩ gĩatetherie atĩa Ayahudi?

17 Maono ambayo Zekaria aliona huenda yalikuwa mafupi, lakini yaliwasaidia Wayahudi kuwa na mtazamo mzuri kuhusu kazi yao na ibada yao. Lakini walipotumia masomo waliyojifunza kutokana na maono ya Zekaria, waliona jinsi Yehova anavyowasaidia na kuwaongoza kwa upendo. Kupitia roho yake takatifu yenye nguvu, Yehova aliwasaidia waendelee na kazi yao na kupata tena shangwe yao.​—Ezra 6:16.

18. Nĩatĩa kĩoneki kĩa Zekaria gĩgũkũringithia?

18 Maono ya Zekaria ya kinara cha taa na mizeituni miwili, yanaweza kukusaidia sana maishani mwako. Kama tulivyozungumzia, yanaweza kukusaidia kupata nguvu unazohitaji ili kukabiliana na wapinzani, shangwe unayohitaji ili kukabiliana na hali zinazobadilika maishani, na uhakika unaohitaji ili kutii unapopata mwongozo ambao hauelewi. Unapaswa kufanya nini unapopitia mabadiliko maishani? Kwanza, ona jambo ambalo Zekaria aliona—uthibitisho kwamba Yehova anawajali watu Wake. Kisha, tenda kulingana na mambo unayoona kwa kumtumaini Yehova na kuendelea kumwabudu yeye kwa moyo wako wote. (Mt. 22:37) Ukifanya hivyo, Yehova atakusaidia umtumikie kwa shangwe milele.​—Kol. 1:10, 11.

RWĨMBO 7 Yehova, Nguvu Yetu

^ Yehova alimpatia nabii Zekaria mfululizo wa maono yenye kusisimua. Mambo ambayo Zekaria aliona yalimpa yeye na watu wa Yehova nguvu za kushinda changamoto walizokabiliana nazo, walipokuwa wakipambana ili kurudisha upya ibada safi. Maono hayo yanaweza kutusaidia sisi pia kumtumikia Yehova kwa uaminifu licha ya changamoto tunazokabili. Katika makala hii, tutazungumzia masomo muhimu tunayoweza kujifunza kutokana na maono ambayo Zekaria aliona yaliyohusisha kinara cha taa na mizeituni.

^ Miaka kadhaa baadaye, wakati wa utawala wa Gavana Nehemia, mfalme mwingine aliyeitwa Artashasta alikuwa mwenye fadhili sana kwa Wayahudi.

^ MAELEZO YA PICHA: Ndugu anaona kwamba anahitaji kukubaliana na hali zinazosababishwa na umri kusonga na afya mbaya.

^ MAELEZO YA PICHA: Dada anatafakari uhakika wa kwamba Yehova anamsaidia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kama alivyofanya kwa Yoshua na Zerubabeli.