Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 34

“Ĩtaga na Njĩra Ĩrĩa Ĩrĩ ya Mma”

“Ĩtaga na Njĩra Ĩrĩa Ĩrĩ ya Mma”

‘Itaga na njira iria iri ya mma.’​—3 JOH. 4.

WIMBO 111 Sababu za Kuwa na Shangwe

MUHTASARI a

1. Nĩatĩa tũgunĩkaga rĩrĩa tũkwaranĩria na bangĩ ũrĩa twonere ‘umma’?

 “WEWE ulipataje kweli?” Bila shaka, umejibu swali hilo mara nyingi sana. Ni moja kati ya maswali ya kwanza ambayo mwabudu mwenzetu atatuuliza tunapoanza kufahamiana naye. Tunapenda kusikia jinsi ndugu na dada zetu walivyoanza kumjua Yehova na kumpenda, na tunafurahi kuwaambia kwa nini tunaipenda kweli. (Rom. 1:11) Mazungumzo hayo yanatukumbusha jinsi kweli ilivyo yenye thamani sana. Pia, tunaazimia hata zaidi kuendelea “kutembea katika kweli,” yaani, kuendelea kuishi kwa njia ambayo itatuletea kibali na baraka za Yehova.​—3 Yoh. 4.

2. Nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

2 Katika makala hii, tutachunguza sababu zinazofanya tuipende kweli. Kisha tutachunguza jinsi tunavyoweza kuendelea kuonyesha kwamba tunaipenda zawadi hii yenye thamani. Bila shaka, mazungumzo haya yataendelea kuimarisha uthamini wetu kwa mambo ambayo Yehova amefanya ili kutuvuta katika kweli. (Yoh. 6:44) Pia, yataimarisha azimio letu la kuwafundisha wengine kweli za Biblia.

GĨTŨMI TWENDETE ‘UMMA’

3. Tũrĩna gĩtũmi kĩrĩkũ gĩkĩnene gĩa kwenda ũmma?

3 Tunaipenda kweli kwa sababu mbalimbali. Sababu muhimu zaidi ni kwamba tunampenda Yehova Mungu, ambaye ndiye Chanzo cha ile kweli. Kupitia Neno lake, Biblia, tumemjua kuwa Muumba mwenye nguvu zote wa mbingu na dunia na pia kama Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo ambaye anatujali kwa wororo. (1 Pet. 5:7) Tunajua kwamba Mungu wetu ni “mwenye rehema na huruma, si mwepesi wa hasira, [ana] upendo mwingi mshikamanifu na kweli.” (Kut. 34:6) Yehova anapenda haki. (Isa. 61:8) Anaumia anapoona tukiteseka na yuko tayari​—naam, anatamani—​kukomesha mateso yote wakati wake utakapofika. (Yer. 29:11) Huo utakuwa wakati wenye kufurahisha sana! Ndiyo sababu tunampenda sana Yehova!

Kweli ya Biblia Ni Kama . . . Nanga

Kama vile nanga inavyosaidia kudhibiti mashua, tumaini letu linalotegemea Biblia linaweza kutuimarisha tunapokabili majaribu. Pia, kweli za Biblia zinatuchochea kuwaambia wengine kuhusu tumaini letu la wakati ujao (Tazama fungu la 4 hadi 7)

4-5. Nĩatĩa Paũlũ aang’uanĩthanĩrie wĩtĩkio bwetũ na nanga?

4 Ni sababu gani nyingine inayofanya tuipende kweli? Kweli inatunufaisha kwa njia nyingi sana. Fikiria mfano mmoja. Kweli za Biblia zinatia ndani tumaini letu la wakati ujao. Ili kuonyesha thamani ya tumaini hilo, mtume Paulo aliandika hivi: “Tuna tumaini hilo kama nanga ya nafsi, likiwa hakika na imara.” (Ebr. 6:19) Kama vile nanga inavyosaidia kudhibiti mashua, tumaini letu linalotegemea Biblia linaweza kutuimarisha tunapokabili majaribu maishani.

5 Katika muktadha huu, Paulo alikuwa akizungumzia tumaini la mbinguni ambalo Wakristo watiwa-mafuta wanatazamia. Lakini maneno yake yanawahusu pia Wakristo wanaotazamia kuishi milele katika paradiso duniani. (Yoh. 3:16) Bila shaka kujifunza kuhusu tumaini la uzima wa milele kumetusaidia kuishi maisha yenye kusudi.

6-7. Nĩatĩa Yvonne aagunĩkĩre arĩkwiritana ũmma bwegie ĩgiita rĩĩjĩte?

6 Fikiria jambo ambalo dada anayeitwa Yvonne alijionea. Hakulelewa katika kweli, na alipokuwa mtoto aliogopa kifo. Anakumbuka maneno haya ambayo alisoma na yakabaki katika akili yake: “Kuna siku ambayo kesho haitafika.” Anasema hivi: “Maneno hayo yalifanya nikose usingizi usiku nikiwaza kuhusu wakati ujao. Nilijiambia ‘Ni lazima maisha yawe na kusudi fulani. Kwa nini niko hapa?’ Sikutaka kufa!”

7 Baadaye, alipokuwa tineja, Yvonne alikutana na Mashahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Nilianza kuamini kwamba ninaweza kuwa na tumaini la kuishi milele katika Paradiso duniani.” Kujifunza kweli kumemnufaishaje dada yetu? Anaongezea hivi: “Sikosi tena usingizi usiku kwa sababu ya wasiwasi kuhusu wakati ujao au kifo.” Bila shaka, Yvonne anaithamini sana kweli na anaridhika sana anapowaeleza wengine kuhusu tumaini lake la wakati ujao.​—1 Tim. 4:16.

Kweli ya Biblia Ni Kama . . . Hazina

Kumtumikia Yehova sasa na kuwa na tumaini la kufanya hivyo milele chini ya utawala wa Ufalme wake ni kama hazina. Haiwezi kulinganishwa na chochote tunachoweza kudhabihu (Tazama fungu la 8 hadi 11)

8-9. (a) Kĩrĩ njuno ĩmwe ya Jesũ, nĩatĩa muntũ mũrũme ũmwe oonanĩrie atĩ mũthithũ jũrĩa oonere nĩ jwarĩ jwa gĩtũmi? (b) Gwe-rĩ, wonaga ũmma bũrĩ bwa gĩtũmi bũng’ana?

8 Kweli za Biblia zinatia ndani pia habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu. Yesu alilinganisha kweli kuhusu Ufalme na hazina iliyofichwa. Kama ilivyoandikwa katika Mathayo 13:44, Yesu alisema hivi: “Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa katika shamba, ambayo mtu fulani aliipata na kuificha; na kwa sababu ya shangwe aliyo nayo, anaenda na kuuza kila kitu alicho nacho na kununua shamba hilo.” Ona kwamba hakuwa akitafuta ile hazina. Lakini alipoiona alikuwa tayari kudhabihu mambo makubwa ili kuipata. Na kwa kweli, aliuza kila kitu alichokuwa nacho. Kwa nini? Kwa sababu alijua hazina hiyo ni yenye thamani sana. Ilikuwa yenye thamani kuliko kitu chochote ambacho angedhabihu.

9 Je, wewe pia unahisi hivyo kuhusu kweli? Bila shaka, unahisi hivyo. Tunajua kwamba hakuna kitu chochote katika ulimwengu huu kinachoweza kulinganishwa na shangwe ya kumtumikia Yehova sasa, tukiwa na tumaini la kuishi milele wakati ujao chini ya Ufalme wa Mungu. Pendeleo letu la kuwa na uhusiano wa karibu na Yehova ni lenye thamani kuliko jambo lolote tunaloweza kudhabihu. Shangwe yetu kubwa zaidi ni “kumpendeza kikamili.”​—Kol. 1:10.

10-11. Nĩmbi biatũmĩre Michael agarũra njĩra yaawe mũtũrĩĩre?

10 Wengi wetu tumedhabihu mambo makubwa ili kupata kibali cha Yehova. Wengine wameacha kazi zenye mshahara mnono katika ulimwengu. Wengine wameacha kufuatia utajiri. Pia, wengine walibadili kabisa maisha yao baada ya kujifunza kumhusu Yehova. Hivyo ndivyo Michael alivyofanya. Yeye hakulelewa katika kweli. Alipokuwa kijana alipata mazoezi ya kupigana karate. Anasema hivi: “Jambo muhimu zaidi kwangu lilikuwa kufanya mazoezi ya kimwili. Wakati mwingine nilihisi siwezi kushindwa.” Lakini alipoanza kujifunza Biblia, Michael alitambua maoni ya Yehova kuhusu ukatili. (Zab. 11:5) Michael anasema hivi, kuhusu wenzi wa ndoa Mashahidi waliomfundisha Biblia: “Hawakuniambia kamwe niache kupigana karate. Waliendelea tu kunifundisha kweli za Biblia.”

11 Kadiri Michael alivyoendelea kujifunza kumhusu Yehova, ndivyo upendo wake Kwake ulivyoongezeka. Aliguswa moyo hasa na jinsi Yehova anavyowatendea waabudu wake kwa huruma. Baada ya muda, Michael alitambua kwamba alihitaji kufanya mabadiliko makubwa maishani. Anasema hivi: “Nilijua kwamba kuacha karate kungekuwa jambo gumu zaidi ambalo nimewahi kufanya maishani. Lakini pia, nilitambua kuwa jambo hilo lingemfurahisha Yehova, na nilisadiki kwamba kumtumikia Yehova hakungeweza kulinganishwa na jambo lingine lolote ambalo ningedhabihu.” Michael alitambua thamani ya kweli aliyokuwa amepata, na hilo lilimchochea kufanya mabadiliko makubwa maishani.​—Yak. 1:25.

Kweli ya Biblia Ni Kama . . . Taa

Taa yenye mwanga mkali hutusaidia kuona njia tunapokuwa gizani. Vivyo hivyo, Neno la Mungu hutusaidia kuona njia tunayopaswa kufuata katika ulimwengu huu wa Shetani wenye giza (Tazama fungu la 12 na 13)

12-13. Nĩatĩa ũmma bwa Bibiria bwatetherie Mayli?

12 Ili kukazia thamani ya ile kweli, Biblia inalinganisha kweli na taa inayowaka gizani. (Zab. 119:105; Efe. 5:8) Mayli anayeishi huko Azerbaijan, anathamini sana nuru ambayo amepata katika Neno la Mungu. Alilelewa katika familia iliyogawanyika kidini. Baba yake alikuwa Mwislamu, na mama yake alikuwa Myahudi. Anasema hivi: “Ingawa sikuwa na shaka kamwe kwamba Mungu yupo, kuna mambo ambayo yalinitatiza. Nilijiuliza hivi, ‘Kwa nini Mungu aliwaumba wanadamu, na kungekuwa na kusudi gani kwa mtu kuteseka maisha yake yote na kisha ateswe milele kwenye moto wa mateso?’ Kwa kuwa watu walisema kwamba kila jambo linalotokea ni mapenzi ya Mungu, nilijiuliza, ‘Je, Mungu anaongoza matendo ya wanadamu na kufurahia kuona wakiteseka?’”

13 Mayli aliendelea kutafuta majibu ya maswali yake. Baadaye, alikubali kujifunza Biblia na akawa Shahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Mafundisho ya Biblia yanayopatana na akili na yenye kusadikisha yalibadili kabisa mtazamo wangu kuhusu maisha. Ufafanuzi wenye kuaminika unaopatikana katika Neno la Mungu unaniletea amani ya moyoni.” Kama Mayli, sisi sote tunamsifu Yehova, “Yule [aliyetuita] kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.”​—1 Pet. 2:9.

14. Nĩatĩa tũũmba kwongeera wendo bwetũ kwerekera ũmma? (Tega kinya kathandũkũ “ Mantũ Jangĩ ja Gũteganĩĩria Najo.”)

14 Hiyo ni mifano michache tu inayoonyesha thamani ya ile kweli. Bila shaka, unaweza kufikiria mifano mingine mingi. Kwa nini usijiwekee lengo la kufanya utafiti katika funzo lako la kibinafsi kuhusu sababu nyingine zinazofanya tuipende kweli? Kadiri tunavyozidi kuipenda kweli, ndivyo tutakavyojitahidi kupata njia za kuonyesha kwamba tunaipenda kweli.

ŨRĨA TWONANAGIA ATĨ NĨTWENDETE ŨMMA

15. Nĩ njĩra ĩrĩkũ ĩmwe tũũmba kwonania atĩ nĩtwendete ũmma?

15 Tunaweza kuonyesha kwamba tunaipenda kweli kwa kujifunza kwa ukawaida Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia. Kwa sababu hata iwe tumekuwa katika kweli kwa muda gani, bado kuna mengi ya kujifunza. Toleo la kwanza kabisa la gazeti hili lilisema hivi: “Kama ua dogo katika jangwa la maisha, kweli imezungukwa na hata kukaribia kusongwa na magugu mengi ya makosa. Ili uipate ni lazima uwe macho wakati wote. . . . Ili uipate ni lazima uiname kuichukua. Usiridhike na ua moja la kweli. . . . Endelea kukusanya, tafuta mengine zaidi.” Kujifunza kunahitaji jitihada nyingi, lakini jitihada hizo si za bure.

16. Nĩ njĩra ĩrĩkũ ya kwiritana wonaga ĩrĩ na maumĩĩra jameega? (Njuno 2:4-6)

16 Si kila mtu anapenda kusoma na kujifunza. Lakini Yehova anatukaribisha ‘tuendelee kutafuta’ ili tupate uelewaji wenye kina zaidi wa ile kweli. (Soma Methali 2:4-6.) Sikuzote tunanufaika tunapofanya jitihada hizo. Ndugu anayeitwa Corey anasema kwamba anaposoma Biblia kibinafsi, yeye hukazia fikira mstari mmoja baada ya mwingine. Anaeleza hivi: “Ninasoma maelezo yote ya chini, marejeo yote ya pambizoni, na kufanya utafiti zaidi. . . . Ninajifunza mengi sana kwa kutumia njia hii!” Iwe tunatumia njia hiyo au nyingine, tunaonyesha kwamba tunaithamini kweli tunapotumia wakati na jitihada kujifunza kweli.​—Zab. 1:1-3.

17. Nĩkuuga atĩa gũtũũra kũringana na ũmma? (Jakubu 1:25)

17 Bila shaka, haitoshi tu kujifunza kweli. Ili tunufaike kikamili ni lazima tuishi kulingana na kweli, yaani, kutumia mambo tunayojifunza maishani mwetu. Kwa kufanya hivyo, ndipo tu kweli itakapotusaidia kuwa na furaha ya kweli. (Soma Yakobo 1:25.) Tunawezaje kuhakikisha kwamba tunaishi kulingana na kweli? Ndugu mmoja alipendekeza kwamba tunapaswa kujichunguza kibinafsi ili kutambua maeneo ambayo tunafanya vizuri na maeneo ambayo tunahitaji kufanya maendeleo. Mtume Paulo alifafanua jambo hilo hivi: “Kwa kadiri ambavyo tumefanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo huohuo.”​—Flp. 3:16.

18. Nĩkĩ tũthithagia jonthe jarĩa tũkũũmba nĩkenda twĩta na mbere ‘gwitaga na njira iria iri ya mma’?

18 Hebu wazia faida tunazopata tunapojitahidi kabisa ‘kuendelea kutembea katika kweli’! Maisha yetu yanaendelea kuwa bora hata zaidi, na tunamletea Yehova shangwe na pia waabudu wenzetu. (Met. 27:11; 3 Yoh. 4) Kwa hakika, tuna sababu nzuri sana za kuipenda kweli na kuishi kulingana na kweli!

WIMBO 144 Kaza Macho Kwenye Zawadi!

a Mara nyingi sisi huita mafundisho yetu na njia yetu ya maisha kuwa ile “kweli.” Iwe sisi ni wapya katika kweli au tumeijua kweli maisha yetu yote, tutanufaika sana kwa kuchunguza kwa nini tunaipenda kweli. Kwa kufanya hivyo, tutaimarisha azimio letu la kupata kibali cha Yehova.