Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 32

Antũ Babeethĩ—Menya Bũtiga Kũthithia Wĩti na Mbere Nyuma ya Kũbatithua

Antũ Babeethĩ—Menya Bũtiga Kũthithia Wĩti na Mbere Nyuma ya Kũbatithua

‘Tũrĩ na wendo tũkũreni na njĩra cionthe.’​—AEF. 4:15, Kimeru Bible, 2010.

WIMBO 56 Fanya Kweli Iwe Njia Yako ya Maisha

MUHTASARI a

1. Nĩ mantũ jarĩkũ jameega antũ babaingĩ babeethĩ barĩĩkĩtie gũkinyĩra?

 KILA mwaka, maelfu ya vijana Wakristo hubatizwa. Je, wewe umechukua hatua hiyo? Ikiwa ndivyo, ndugu na dada zako wa kiroho wanafurahi kwa ajili yako, na Yehova anashangilia pia! (Met. 27:11) Kwa Mfano, fikiria mambo ambayo umetimiza kufikia sasa. Umejifunza Biblia kwa bidii, labda kwa miaka kadhaa. Mambo uliyojifunza yamekusadikisha kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Zaidi ya hayo, umejua na kumpenda Mtungaji wa kitabu hicho kitakatifu. Upendo wako kwa Yehova umeimarika sana hivi kwamba sasa wewe ni mmoja wa watumishi wake aliyejiweka wakfu na kubatizwa. Umefanya vema sana!

2. Nĩmbi tũkaarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

 2 Bila shaka, imani yako ilijaribiwa kwa njia mbalimbali ulipokuwa ukifanya maendeleo ili kufikia hatua ya ubatizo. Lakini kadiri unavyozidi kukua, utakabili majaribu mengine. Shetani atajaribu kudhoofisha upendo wako kwa Yehova na pia atajaribu kukufanya uache kumtumikia Yehova. (Efe. 4:14) Usiruhusu jambo hilo litukie. Ni nini kinachoweza kukusaidia uendelee kuwa mshikamanifu kwa Yehova na kutimiza ahadi uliyotoa ulipojiweka wakfu? Ni lazima uendelee kufanya maendeleo, yaani, ‘usonge mbele’ kuelekea ukomavu wa Kikristo. (Ebr. 6:1) Lakini unawezaje kufanya hivyo?

ŨRĨ MŨKRISTŨ NĨATĨA ŨŨMBA KŨTHITHIA WĨTI NA MBERE?

3. Nĩ wĩti na mbere bũrĩkũ Akristũ bonthe babuĩrĩte kũthithia nyuma ya kũbatithua?

3 Baada ya kubatizwa, sisi sote tunahitaji kufuata ushauri ambao mtume Paulo aliwapa Wakristo wenzake huko Efeso. Aliwatia moyo wawe Wakristo ‘waliokomaa kabisa.’ (Efe. 4:13) Kwa maneno mengine, ni kama aliwaambia hivi: ‘Endeleeni kufanya maendeleo.’ Tunaweza kuelewa jambo ambalo Paulo alimaanisha alipolinganisha ukuzi wa kiroho na ukuzi wa kimwili wa mtoto. Wazazi wanampenda na kujivunia mtoto wao mchanga. Lakini hataendelea kuwa mtoto mchanga sikuzote. Baada ya muda, atalazimika kuacha “tabia za mtoto.” (1 Kor. 13:11) Hivyo ndivyo ilivyo kwa Wakristo. Baada ya kubatizwa, ni lazima tuendelee kufanya maendeleo. Acheni tuzungumzie baadhi ya mapendekezo yatakayotusaidia kufanya hivyo.

4. Nĩ nkuma irĩkũ ciũmba gũgũtethia kũthithia wĩti na mbere gĩkĩrundu? Tarĩĩria. (Afilipi 1:9)

4 Imarisha upendo wako kwa Yehova. Tayari unampenda Yehova sana. Lakini upendo wako kwake unaweza kuongezeka hata zaidi. Jinsi gani? Mtume Paulo alitaja njia moja kwenye andiko la Wafilipi 1:9. (Soma.) Paulo alisali kwamba upendo wa Wafilipi uwe “mwingi zaidi na zaidi.” Basi, upendo wetu kwa Yehova unaweza kuongezeka. Tunaweza kufanya hivyo kwa kujipatia “ujuzi sahihi na utambuzi kamili.” Kadiri tunavyozidi kumjua Yehova, ndivyo tunavyozidi kumpenda na kuthamini sifa zake na njia yake ya kufanya mambo. Tamaa yetu ya kumfurahisha inaongezeka, na tunajitahidi kuepuka kufanya jambo lolote ambalo halitampendeza. Tunajitahidi kutambua mapenzi yake na jinsi tunavyoweza kumtii.

5-6. Nĩatĩa tũũmba gũkũria wendo bwetũ kwerekera Jehova? Tarĩĩria.

5 Upendo wetu kwa Yehova unaweza kukua ikiwa tutajitahidi kumfahamu vizuri zaidi Mwana wake, ambaye anaiga kikamilifu sifa za Baba yake. (Ebr. 1:3) Njia bora zaidi ya kumjua Yesu ni kwa kujifunza masimulizi ya vitabu vinne vya Injili. Ikiwa bado hujasitawisha zoea zuri la kujifunza Biblia kila siku, kwa nini usianze sasa? Unapojifunza masimulizi kumhusu Yesu, kazia fikira sifa zake. Alikuwa mwenye kufikika na aliwakumbatia watoto wadogo kwa upendo. (Marko 10:13-16) Aliwastarehesha wanafunzi wake; walijihisi huru kueleza maoni yao walipokuwa pamoja naye. (Mt. 16:22) Kwa njia hiyo, Yesu alimwiga Baba yake wa mbinguni. Yehova pia ni mwenye kufikika. Tunaweza kuzungumza naye kupitia sala. Tunaposali, tunaweza kummiminia moyo wetu. Tuna hakika kwamba hatatuhukumu. Anatupenda na kutujali.​—1 Pet. 5:7.

6 Yesu aliwahurumia watu. Mtume Mathayo alisema hivi: “Alipoona umati akausikitikia, kwa sababu walikuwa wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.” (Mt. 9:36) Naye Yehova anahisije? Yesu alisema hivi: “Baba yangu aliye mbinguni hapendi hata mmoja wa hawa wadogo aangamie.” (Mt. 18:14) Hilo linatutia moyo sana! Tunapomjua Yesu vizuri zaidi, upendo wetu kwa Yehova unaongezeka.

7. Nĩatĩa kũgwatanĩra na Akristũ baagimaru kũũmba gũgũtethia?

7 Unaweza pia kujifunza kuonyesha upendo zaidi na kufanya maendeleo ukiwa Mkristo, kwa kuwafahamu vizuri zaidi ndugu na dada wakomavu katika kutaniko lenu. Ona jinsi walivyo na shangwe. Hawajutii uamuzi wao wa kumtumikia Yehova. Waombe wakusimulie baadhi ya mambo waliyojionea katika utumishi wao kwa Yehova. Ikiwa unahitaji kufanya uamuzi muhimu, waombe ushauri. Kumbuka kwamba “washauri wengi huleta mafanikio.”​—Met. 11:14.

Unawezaje kujitayarisha kukabiliana na fundisho la mageuzi shuleni? (Tazama fungu la 8 na 9)

8. Nĩatĩa ũũmba kũthithia ũkeeja kwĩthĩrwa ũrĩna nkaaja bwegie jarĩa Bibiria yugaga?

8 Shinda shaka ulizo nazo. Kama ilivyotajwa kwenye  fungu la 2, Shetani atajaribu kukuzuia kufanya maendeleo zaidi ya kiroho. Njia moja anayoweza kufanya hivyo ni kwa kufanya utilie shaka baadhi ya mafundisho ya Biblia. Kwa mfano, pindi fulani huenda utasikia kuhusu fundisho la mageuzi ambalo linamvunjia Mungu heshima. Labda hukukazia fikira jambo hilo ulipokuwa mdogo, lakini kwa kuwa sasa umri wako umeongezeka, huenda unakabili fundisho hilo moja kwa moja shuleni. Mambo ambayo walimu wako wanasema ili kuunga mkono mageuzi, huenda yakaonekana yanapatana na akili na yenye kusadikisha. Hata hivyo, inawezekana kwamba hawajawahi kuchunguza kwa makini uthibitisho unaoonyesha kwamba kuna Muumba. Kumbuka kanuni inayotajwa kwenye Methali 18:17: “Mtu wa kwanza kuwasilisha kesi yake huonekana kuwa sahihi, mpaka mwingine anapokuja na kumuuliza maswali.” Badala ya kukubali bila kuchunguza kwa makini mambo unayojifunza shuleni na kuyaona kuwa ya kweli, chunguza kwa makini kweli zinazopatikana katika Neno la Mungu, Biblia. Fanya utafiti kwa kutumia machapisho yetu. Zungumza na ndugu na dada ambao zamani waliamini fundisho la mageuzi. Waulize kuhusu jambo linalowasadikisha kwamba kuna Muumba anayewapenda. Mazungumzo kama hayo yenye kujenga yanaweza kukusaidia ukazie fikira mambo yaliyo ya kweli.

9. Nĩmbi ũkwiritana kuumania na jarĩa Melissa aakũrũkĩrĩĩre?

9 Dada anayeitwa Melissa alinufaika sana alipofanya utafiti kuhusu uumbaji. b Alisema hivi: “Shuleni, fundisho la mageuzi hufafanuliwa kwa njia inayoonekana kuwa yenye kusadikisha sana. Mwanzoni niliogopa kuchunguza shaka nilizokuwa nazo. Nilikuwa na wasiwasi kwamba ikiwa ningefanya utafiti, ningegundua kwamba mambo niliyoamini si ya kweli. Lakini nilijiambia kwamba Yehova hataki tumtumikie bila kuwa na uthibitisho kuhusu mambo tunayoamini. Basi, nilifanya utafiti kuhusu mambo niliyotilia shaka. Nilisoma kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? na broshua Uhai​—Ulitokana na Muumba? na Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai. Hiyo ndiyo habari niliyohitaji hasa. Laiti ningefanya hivyo mapema.”

10-11. Nĩmbi biumba gũgũtethia gũtũũra ũrĩna mĩtugo ya wagĩru? (1 Athesalonike 4:3, 4)

10 Epuka mwenendo mbaya. Wakati wa kubalehe, tamaa ya kufanya ngono inaweza kuongezeka sana, na huenda ukashinikizwa sana ufanye uasherati. Shetani anataka ushindwe na tamaa yako. Ni nini kinachoweza kukusaidia uendelee kuwa safi kiadili? (Soma 1 Wathesalonike 4:3, 4.) Katika sala zako za kibinafsi, mweleze Yehova hisia zako. Mweleze kihususa jinsi unavyohisi, na umwombe akuimarishe. (Mt. 6:13) Kumbuka kwamba Yehova anataka kukusaidia, si kukuhukumu. (Zab. 103:13, 14) Pia, unaweza kupata msaada katika Neno la Mungu. Melissa, aliyetajwa awali, alipambana ili kushinda mawazo yasiyo safi. Anasema hivi: “Kusoma Biblia kila siku kulinisaidia nisikate tamaa. Kulinisaidia kukumbuka kwamba mimi ni mali ya Yehova na ninataka awe sehemu ya maisha yangu.”​—Zab. 119:9.

11 Usijaribu kutatua matatizo yako wewe mwenyewe. Zungumza na wazazi wako kuhusu changamoto unazokabili. Bila shaka, si rahisi kuzungumzia mambo kama hayo ya kibinafsi, lakini ni muhimu kufanya hivyo. Melissa, anasema hivi: “Nilisali ili nipate ujasiri, kisha nikazungumza na baba yangu kuhusu tatizo langu. Baada ya hapo, nilifarijika sana. Nilijua kwamba nilikuwa nimemfurahisha Yehova.”

12. Nĩatĩa ũũmba kũthithia matua jameega?

12 Ongozwa na kanuni za Biblia. Kadiri unavyozidi kukua, ndivyo utakavyokuwa na uhuru zaidi wa kujifanyia maamuzi yako mwenyewe. Lakini bado huna uzoefu mwingi maishani. Unawezaje kuepuka kufanya kosa ambalo litaathiri uhusiano wako na Yehova? (Met. 22:3) Dada anayeitwa Kari anaeleza jambo lililomsaidia kufanya maamuzi mazuri. Alitambua kwamba Wakristo wakomavu hawahitaji sheria inayoongoza kila jambo wanalofanya. Anasema hivi: “Nilihitaji kuelewa kanuni za Biblia, badala ya kufuata sheria tu.” Unaposoma Biblia, jiulize hivi: ‘Mistari hii inanifundisha nini kuhusu njia ya Yehova ya kufikiri? Je, kuna kanuni zinazoweza kunisaidia kuwa na mwenendo mzuri? Ikiwa ndivyo, nitanufaikaje kwa kuzitumia?’ (Zab. 19:7; Isa. 48:17, 18) Ukisoma Biblia na kutafakari kanuni zilizomo, itakuwa rahisi zaidi kwako kufanya maamuzi yanayomfurahisha Yehova. Unapozidi kufanya maendeleo, utatambua kwamba huhitaji sheria kuhusu kila hali unayokabili kwa sababu utaelewa njia ya Yehova ya kufikiri kuhusu mambo.

Dada mmoja kijana alichagua marafiki wa aina gani? (Tazama fungu la 13)

13. Acoore babeega bomba kwĩthĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ kĩrĩwe? (Njuno 13:20)

13 Chagua marafiki wanaompenda Yehova. Kama ilivyotajwa awali, marafiki unaochagua wanaweza kuwa na uvutano mkubwa sana katika maendeleo unayofanya ukiwa Mkristo. (Soma Methali 13:20.) Dada anayeitwa Sara alianza kupoteza shangwe yake. Kisha jambo fulani likamsaidia kubadili mtazamo wake. Sara anasema hivi: “Nilipata marafiki wazuri kwa wakati unaofaa kabisa. Mimi na dada mmoja kijana tulikutana kila juma ili kujifunza gazeti la Mnara wa Mlinzi. Rafiki mwingine alinisaidia nianze kutoa maelezo kwenye mikutano. Kwa sababu ya kushirikiana na rafiki zangu, nilianza kujifunza kibinafsi na kusali kwa bidii. Nilianza kusitawisha uhusiano wa karibu zaidi na Yehova, na nikaanza tena kuwa na shangwe.”

14. Nĩatĩa Julien aatumĩre ũcoore na antũ babeega?

14 Unawezaje kusitawisha urafiki na watu ambao watakusaidia? Julien, ambaye sasa anatumikia akiwa mzee wa kutaniko, anasema hivi: “Nilipokuwa kijana nilisitawisha urafiki pamoja na wale nilioshirikiana nao katika huduma. Marafiki hao walikuwa wenye bidii na walinisaidia kufurahia huduma. Hivyo, nilijiwekea lengo la kuanza utumishi wa wakati wote. Nilitambua kwamba nilikuwa nikikosa kushirikiana na marafiki wazuri, kwa kuchagua tu marafiki wenye umri wangu. Baadaye, nilipata marafiki wazuri Betheli. Mfano wao ulinisaidia kuchagua vizuri zaidi burudani, na hilo liliimarisha uhusiano wangu na Yehova.”

15. Nĩ mũkaana jũrĩkũ Paũlũ aaere Timotheo jwegie barĩa arĩngĩgwatanĩra nabo? (2 Timotheo 2:20-22)

15 Utafanya nini ukitambua kwamba mtu fulani kutanikoni si rafiki anayekufaa? Paulo alijua kwamba baadhi ya watu katika kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza hawakuwa na mtazamo unaofaa wa kiroho, basi akamwonya Timotheo ajiepushe nao. (Soma 2 Timotheo 2:20-22.) Uhusiano wetu na Yehova ni wenye thamani. Hatupaswi kumruhusu mtu yeyote adhoofishe uhusiano wa karibu ambao tumejitahidi sana kusitawisha pamoja na Baba yetu wa mbinguni.​—Zab. 26:4.

GŨCIĨKĨRA MĨOROTO NĨATĨA KŨŨMBA GŨGŨTETHIA KŨTHITHIA WĨTI NA MBERE GĨKĨRUNDU?

16. Nĩ mĩoroto ĩrĩkũ ũbuĩrĩte kũthingatĩĩra?

16 Jiwekee malengo yanayofaa. Chagua malengo ambayo yataimarisha imani yako na kukusaidia uwe Mkristo mkomavu. (Efe. 3:16) Kwa mfano, unaweza kuamua kuboresha ratiba yako ya kujifunza kibinafsi na kusoma Biblia. (Zab. 1:2, 3) Au unaweza kujitahidi kuboresha sala zako na kusali mara nyingi zaidi. Labda unahitaji kusitawisha zaidi sifa ya kujizuia inapohusu burudani unazochagua na jinsi unavyotumia wakati wako. (Efe. 5:15, 16) Yehova atafurahi anapoona ukijitahidi kufanya maendeleo zaidi.

Dada huyu kijana alijiwekea lengo gani? (Tazama fungu la 17)

17. Nĩatĩa ũgunĩkaga rĩrĩa watethia bangĩ?

17 Utazidi kuwa Mkristo mkomavu unapowasaidia wengine. Yesu alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Utanufaika sana ikiwa utatumia wakati na nguvu zako za ujana kuwasaidia wengine. Kwa mfano, unaweza kujiwekea lengo la kuwasaidia waliozeeka na wenye matatizo ya afya katika kutaniko lenu. Labda unaweza kuwasaidia kufanya ununuzi au kuwasaidia kutumia vifaa vya kielektroni. Ikiwa wewe ni ndugu, jiwekee lengo la kuwa mtumishi wa huduma, ukiwa na nia ya kuwatumikia ndugu na dada zako. (Flp. 2:4) Pia, waonyeshe upendo watu wasio Mashahidi kwa kuwahubiria habari njema za Ufalme. (Mt. 9:36, 37) Ikiwa inawezekana, jiwekee lengo la kushiriki katika aina fulani ya utumishi wa wakati wote.

18. Nĩatĩa gũtumĩka ũrĩ mũtungatĩri wa ĩgiita rĩonthe kũũmba gũgũtethia gũkũra gĩkĩrundu?

18 Utumishi wa wakati wote unaweza kukupatia fursa nyingi sana za kufanya maendeleo ya kiroho. Kutumikia kama painia kunaweza kukufungulia mlango wa kuhudhuria Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Huenda ukatumikia Betheli au kwenye miradi ya ujenzi ya kitheokrasi. Dada kijana painia anayeitwa Kaitlyn, anasema hivi: “Kutumia muda katika huduma pamoja na ndugu na dada wenye uzoefu kulinisaidia sana kukomaa kiroho baada ya kubatizwa. Mfano wao ulinichochea kuongeza ujuzi wangu wa Biblia na kuboresha uwezo wangu wa kufundisha.”

19. Nĩ itharimo birĩkũ ũkagwĩrĩrua o ũrĩa ũgeeta ũkĩthithagia wĩti na mbere gĩkĩrundu?

19 Unapozidi kufanya maendeleo ya kiroho, utapata baraka nyingi sana. Utaepuka kupoteza ujana wako kwa kufuatia malengo yasiyo na thamani. (1 Yoh. 2:17) Utaepuka maumivu yanayosababishwa na kufanya maamuzi yasiyofaa. Badala yake, utapata mafanikio ya kweli na furaha. (Met. 16:3) Mfano wako mzuri utawatia moyo Wakristo wenzako, vijana kwa wazee. (1 Tim. 4:12) Na jambo muhimu zaidi, utapata amani na kuridhika kwa sababu ya kumfurahisha Yehova na kuwa na uhusiano wa karibu pamoja naye.​—Met. 23:15, 16.

WIMBO 88 Nijulishe Njia Zako

a Watumishi wote wa Yehova hufurahi vijana wanapobatizwa. Bila shaka, baada ya kubatizwa, ni lazima wanafunzi wapya waendelee kufanya maendeleo ya kiroho. Makala hii itatusaidia sisi sote kutanikoni kuona jinsi vijana waliobatizwa hivi karibuni, wanavyoweza kukua kufikia ukomavu wa Kikristo.

b Baadhi ya majina yamebadilishwa.