Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 36

Antũ ba Jehova Nĩbendete Mantũ ja Wagĩru

Antũ ba Jehova Nĩbendete Mantũ ja Wagĩru

“Kitharimo-ri, ni kiri baria bari na mpara na nyonta ni untu bwa mantu jaria jaagirite.”​—MAT. 5:6.

WIMBO 9 Yehova Ni Mfalme Wetu!

MUHTASARI a

1. Nĩ kĩgerio kĩrĩkũ Jusufu aakũrũkĩrĩre, na nĩatĩa aathithĩrie?

 YOSEFU, mwana wa Yakobo alikabili jaribu gumu. Mwanamke fulani alimwambia: “Lala nami.” Alikuwa mke wa Potifa, bwana wake. Yosefu alikataa ombi lake. Leo, huenda mtu akajiuliza, ‘Kwa nini Yosefu alipinga kishawishi hicho?’ Potifa hakuwepo. Isitoshe, Yosefu alikuwa mtumwa katika nyumba hiyo; mwanamke huyo alikuwa na uwezo wa kufanya maisha ya Yosefu yawe magumu ikiwa angekataa ombi lake. Hata hivyo, Yosefu aliendelea kukataa mwanamke huyo aliposisitiza. Kwa nini? Yosefu alisema: “Ninawezaje kufanya uovu huu mkubwa na kwa kweli nimtendee Mungu dhambi?”​—Mwa. 39:7-12.

2. Nĩatĩa Jusufu aamenyere atĩ ũthũngĩĩri nĩ wĩyia methone ja Mũrungu?

2 Yosefu alijuaje kwamba Mungu wake angeona uzinzi kuwa ‘uovu mkubwa’? Sheria ya Musa ambayo ilikuwa na amri hii iliyo wazi, “Usifanye uzinzi,” iliandikwa miaka mia mbili baadaye. (Kut. 20:14) Hata hivyo, Yosefu alikuwa na ujuzi wa kutosha kumhusu Yehova na alielewa jinsi ambavyo alihisi kuhusu mwenendo mpotovu. Kwa mfano, bila shaka Yosefu alijua kwamba Mungu alikusudia ndoa iwe kati ya mwanamume mmoja na mwanamke mmoja. Na huenda alikuwa amesikia jinsi ambavyo katika pindi mbili tofauti, Yehova aliingilia kati ili kumlinda Sara, nyanya yake, alipokabili hatari ya kutendewa vibaya. Vivyo hivyo, Mungu aliingilia kati ili kumlinda Rebeka, mke wa Isaka. (Mwa. 2:24; 12:14-20; 20:2-7; 26:6-11) Yosefu alipotafakari mambo hayo, alitambua mambo yanayofaa na yasiyofaa machoni pa Mungu. Kwa kuwa Yosefu alimpenda Mungu, alipenda pia viwango vya Yehova vya uadilifu na alikuwa ameazimia kuvifuata.

3. Nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

3 Je, unapenda uadilifu? Bila shaka, unaipenda sifa hiyo. Lakini sisi sote hatujakamilika, na tusipokuwa waangalifu mtazamo wa ulimwengu kuhusu uadilifu unaweza kutuathiri kwa urahisi. (Isa. 5:20; Rom. 12:2) Hivyo, tutachunguza maana ya uadilifu na jinsi tunavyonufaika kwa kuipenda sifa hiyo. Kisha tutazungumzia hatua tatu tunazoweza kuchukua ili kuvipenda zaidi viwango vya Yehova.

WAGĨRU NĨMBI?

4. Nĩ mwonere jũrĩkũ jũtĩbui babaingĩ bethagĩrwa naju jwegie wagĩru?

4 Watu wanaposikia kuhusu mtu mwadilifu, huenda wengi wakafikiri ni mtu mwenye majivuno, anayewachambua wengine, au anayejiona kuwa mwadilifu kupita kiasi. Lakini sifa hizo hazimpendezi kamwe Mungu. Yesu alipokuwa duniani, aliwashutumu kwa ukali viongozi wa kidini wa siku zake ambao walijiwekea viwango vyao wenyewe vya uadilifu. (Mhu. 7:16; Luka 16:15) Mtu anayeonyesha uadilifu wa kweli hajioni kuwa mwadilifu kupita kiasi.

5. Kũringana na Bibiria, wagĩru nĩmbi? Ejana ngerekano.

5 Uadilifu ni sifa yenye kupendeza. Kwa ufupi, inamaanisha kufanya mambo yaliyo sawa machoni pa Yehova Mungu. Katika Biblia, maneno yanayotafsiriwa “uadilifu” yanatokeza wazo la kuishi kulingana na viwango vya juu zaidi, yaani, viwango vya Yehova. Kwa mfano, Yehova aliagiza kwamba wafanyabiashara wanapaswa kutumia ‘mawe ya kupimia yaliyo ya haki.’ (Kum. 25:15) Neno la awali la Kiebrania lililotafsiriwa “haki,” pia linaweza kutafsiriwa “uadilifu.” Basi, Mkristo ambaye anataka kuwa mwadilifu machoni pa Mungu, atatenda kwa unyoofu kabisa katika shughuli zake zote za kibiashara. Pia, mtu mwadilifu anapenda haki, hapendi kuona mtu mwingine akitendewa isivyo haki. Na “ili kumpendeza [Yehova] kikamili,” mtu ambaye ni mwadilifu kikweli anafikiria jinsi Yehova atakavyoona maamuzi anayofanya.​—Kol. 1:10.

6. Nĩkĩ tũũmba kwĩthĩrwa tũtĩ na nkaanja kĩrĩ mawaatho ya Jehova jegie weega na wũũi? (Isaya 55:8, 9)

6 Biblia inamfafanua Yehova kuwa Chanzo cha uadilifu. Hiyo ndiyo sababu anaitwa “makao ya uadilifu.” (Yer. 50:7) Akiwa Muumba, Yehova peke yake ndiye anayeweza kuweka viwango vinavyofaa kuhusu yaliyo sawa na yasiyo sawa. Kwa kuwa Yehova ni mkamilifu, maoni yake kuhusu mambo yaliyo sawa na mambo yasiyo sawa yako juu sana kuliko maoni yetu, ambayo mara nyingi yanaathiriwa na hali ya kutokamilika na dhambi. (Met. 14:12; soma Isaya 55:8, 9.) Hata hivyo, kwa kuwa tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, tunaweza kuishi kulingana na viwango vyake vya uadilifu. (Mwa. 1:27) Na tunapenda kufanya hivyo. Upendo wetu kumwelekea Baba yetu, unatuchochea kumwiga kwa uwezo wetu wote.​—Efe. 5:1.

7. Nĩkĩ tũkũbatara mawaatho jakwĩrĩgĩrĩka? Tarĩĩria.

7 Tunanufaika tunapofuata viwango vya Yehova kuhusu mambo yaliyo sawa na yasiyo sawa. Kwa nini tunasema hivyo? Wazia hali ingekuwaje ikiwa kila benki ingejiwekea viwango vyake vya thamani ya pesa au ikiwa kila kampuni ya ujenzi ingejiwekea viwango vyake vya vipimo. Hilo lingesababisha mvurugo. Na ikiwa madaktari hawangefuata viwango hususa vya matibabu, huenda baadhi ya wagonjwa wangekufa. Bila shaka, viwango vinavyotegemeka hutulinda. Vivyo hivyo, viwango vya Yehova kuhusu mambo yaliyo sawa na yasiyo sawa hutulinda.

8. Nĩ itharimo birĩkũ antũ barĩa bendeete mantũ jarĩa meega berĩgĩĩrĩte?

8 Yehova huwabariki wale wanaojitahidi kuishi kulingana na viwango vyake. Anaahidi hivi: “Waadilifu wataimiliki dunia, nao wataishi humo milele.” (Zab. 37:29) Je, unaweza kuwazia jinsi wanadamu watakavyokuwa na umoja, amani, na furaha wakati kila mtu ataishi kulingana na viwango vya Yehova? Yehova angependa ufurahie maisha hayo. Bila shaka, kila mmoja wetu ana sababu nzuri za kupenda uadilifu! Tunawezaje kuipenda sifa hii hata zaidi? Acheni tuchunguze hatua tatu tunazoweza kuchukua.

ĨKĨRA INYA WENDO BWAKU KWEREKERA MAWAATHO YA JEHOVA

9. Nĩmbi bigatũtethia kwenda mantũ ja wagĩru?

9 Hatua ya 1: Mpende Yule anayeweka viwango hivyo. Ili tupende uadilifu tunahitaji kuimarisha upendo wetu kumwelekea Yule anayeweka viwango vya mambo yaliyo sawa na yasiyo sawa. Kadiri tunavyozidi kumpenda Yehova, ndivyo tutakavyotamani hata zaidi kuishi kulingana na viwango vyake vya uadilifu. Fikiria jambo hili: Ikiwa Adamu na Hawa wangempenda Yehova, wangetii amri yake.​—Mwa. 3:1-6, 16-19.

10. Nĩatĩa Iburahimu oombĩre gũkũria ũmenyo bwawe kwerekera Jehova?

10 Bila shaka, hatungependa kufanya kosa ambalo Adamu na Hawa walifanya. Tunaweza kuepuka matokeo hayo mabaya ikiwa tutaendelea kujifunza kumhusu Yehova, kuthamini sifa zake, na kujitahidi kuelewa njia yake ya kufikiri. Tunapofanya hivyo, bila shaka tutaimarisha upendo wetu kwa Yehova. Mfikirie Abrahamu. Alimpenda sana Yehova. Hata ilipokuwa vigumu kwake kuelewa maamuzi ambayo Yehova alifanya, Abrahamu hakuasi. Badala yake, alijitahidi kumjua Yehova vizuri zaidi. Kwa mfano, aliposikia kuhusu uamuzi wa Yehova wa kuangamiza Sodoma na Gomora, mwanzoni Abrahamu aliogopa kwamba “Mwamuzi wa dunia yote” angefagilia mbali waadilifu pamoja na waovu. Abrahamu aliona hilo kuwa jambo lisilowezekana, basi kwa unyenyekevu alimuuliza Yehova maswali kadhaa. Yehova alimjibu kwa subira. Mwishowe, Abrahamu alitambua kwamba Yehova anachunguza moyo wa kila mwanadamu na kwamba hawaadhibu kamwe watu wasio na hatia pamoja na wenye hatia.​—Mwa. 18:20-32.

11. Nĩatĩa Iburahimu oonanĩrie neendete Jehova na namwĩrĩgagĩĩra?

11 Abrahamu alichochewa sana na mazungumzo kati yake na Yehova kuhusu majiji ya Sodoma na Gomora. Bila shaka, alimpenda na kumheshimu Baba yake hata zaidi kuliko mwanzoni. Miaka mingi baadaye, uwezo wa Abrahamu wa kumtumaini Yehova ulijaribiwa kwa njia kubwa. Yehova alimwagiza amtoe dhabihu Isaka, mwana wake mpendwa. Sasa Abrahamu alikuwa amemfahamu vizuri zaidi Mungu wake. Basi, pindi hii hakumuuliza maswali. Abrahamu alifanya kama Yehova alivyomwagiza. Hata hivyo, wazia uchungu aliohisi moyoni alipokuwa akijitayarisha kufanya jambo hilo! Ni lazima Abrahamu alifikiria kwa kina mambo ambayo alikuwa amejifunza kumhusu Yehova. Alijua kwamba Yehova hangeweza kamwe kufanya jambo lisilo la uadilifu au lisilo la upendo. Kulingana na mtume Paulo, Abrahamu alifikia uamuzi kwamba Yehova angeweza kumfufua mwana wake mpendwa, Isaka. (Ebr. 11:17-19) Na kwa kweli, Yehova alikuwa ameahidi kwamba Isaka angetokeza taifa, na kufikia wakati huo Isaka hakuwa na watoto. Abrahamu alimpenda Yehova, basi alikuwa na uhakika kwamba Baba yake angetenda kwa uadilifu. Kwa imani, alitii ingawa haikuwa rahisi.​—Mwa. 22:1-12.

12. Nĩatĩa tũũmba kwigerekania na Iburahimu? (Zaburi 73:28)

12 Tunawezaje kumwiga Abrahamu? Kama Abrahamu, tunapaswa kuendelea kujifunza kumhusu Yehova. Tunapofanya hivyo, tutazidi kumkaribia na kumpenda hata zaidi. (Soma Zaburi 73:28.) Dhamiri yetu itazoezwa kutenda kulingana na njia ya Yehova ya kufikiri. (Ebr. 5:14) Matokeo ni kwamba ikiwa mtu atajaribu kutushawishi tufanye jambo lisilo sawa, tutakataa. Tutachukia hata kuwazia kufanya jambo lolote ambalo litamuumiza Baba yetu na kuharibu uhusiano wetu pamoja naye. Hata hivyo, tunaweza kuonyesha kwa njia gani nyingine kwamba tunapenda uadilifu?

13. Nĩatĩa tũũmba kũthingatĩĩra mantũ ja wagĩru? (Njuno 15:9)

13 Hatua ya 2: Jitahidi kupenda uadilifu siku baada ya siku. Tunaweza kusitawisha upendo kuelekea viwango vya uadilifu vya Yehova kama tunavyofanya ili kuimarisha misuli, yaani, kupitia jitihada zinazofanywa kwa ukawaida na kwa kuendelea. Hilo ni jambo ambalo unaweza kufanya kila siku. Yehova ni mwenye usawaziko, na hatarajii kamwe tufanye mambo yanayozidi uwezo wetu. (Zab. 103:14) Anatuhakikishia kwamba yeye “humpenda mtu anayefuatia uadilifu.” (Soma Methali 15:9.) Ikiwa tunafuatia lengo hususa katika utumishi wa Yehova, sisi huendelea kufanya jitihada ili kutimiza lengo hilo. Tunafanya hivyo pia tunapofuatia uadilifu. Na kwa subira, Yehova atatusaidia kufanya maendeleo ili tuendelee kuboresha sifa hiyo hatua kwa hatua.​—Zab. 84:5, 7.

14. “Mathaga ja wagiru” ja ‘kibara’ nĩmbi, na nĩkĩ tũkũjabatara?

14 Kwa upendo, Yehova anatukumbusha kwamba sifa ya uadilifu si mzigo mzito. (1 Yoh. 5:3) Kinyume chake, sifa hiyo inatulinda, na tunahitaji ulinzi huo kila siku. Kumbuka mavazi kamili ya silaha za kiroho ambayo mtume Paulo alizungumzia. (Efe. 6:14-18) Ni sehemu gani iliyolinda moyo wa mwanajeshi? Ni “bamba la kifuani la uadilifu,” ambalo linafananisha viwango vya uadilifu vya Yehova. Kama vile bamba la kifuani linavyolinda moyo halisi, ndivyo viwango vya uadilifu vya Yehova vinavyolinda moyo wetu wa mfano, yaani, yule mtu wa ndani. Basi, jitahidi kuhakikisha kwamba vazi lako kamili la silaha linatia ndani bamba la kifuani la uadilifu!​—Met. 4:23.

15. Nĩatĩa ũũmba gwĩkĩra mathaga ja wagĩru ja kĩbara?

15 Unawezaje kuvaa bamba la kifuani la uadilifu? Unaweza kufanya hivyo kwa kuzingatia viwango vya Mungu katika maamuzi unayofanya kila siku. Unapofikiria mambo utakayozungumzia, muziki utakaosikiliza, burudani utakayotazama, au vitabu utakavyosoma, kwanza jiulize hivi: ‘Nitaulisha nini moyo wangu? Je, habari hizi zitanisaidia kupata kibali cha Yehova? Au je, zinaendeleza ukosefu wa maadili, ukatili, pupa, ubinafsi​—mambo ambayo Yehova anaona kuwa yasiyo ya uadilifu?’ (Flp. 4:8) Ikiwa maamuzi unayofanya yanapatana na mapenzi ya Yehova, utakuwa ukiruhusu viwango vyake vya uadilifu viulinde moyo wako.

Uadilifu wako unaweza kuwa “kama mawimbi ya bahari” (Tazama fungu la 16 na 17)

16-17. Nĩatĩa Isaya 48:18 ĩgũtũrikithĩria atĩ no tũũmbe gũtũũra kũringana na mawaatho ya Jehova kenya na kenya?

16 Je, wakati mwingine wewe huwa na wasiwasi ikiwa utaendelea kuishi kulingana na viwango vya Yehova siku baada ya siku, na mwaka baada ya mwaka? Fikiria mfano ambao Yehova alitumia kwenye Isaya 48:18. (Soma.) Yehova anaahidi kwamba uadilifu wetu unaweza kuwa “kama mawimbi ya bahari.” Wazia kwamba umesimama kando ya bahari kubwa ukitazama mawimbi yanayoendelea kuja kwenye ufuo, wimbi moja baada ya lingine. Ukiwa katika mazingira hayo matulivu, je, unaweza kuwa na wasiwasi kwamba siku moja mawimbi hayo yataacha kuja? Hapana! Unajua kwamba mawimbi yamekuwa yakija kwenye ufuo huo kwa maelfu ya miaka, na yataendelea kuja.

17 Uadilifu wako unaweza kuwa kama mawimbi ya bahari! Jinsi gani? Kabla ya kufanya uamuzi wowote, kwanza fikiria jambo ambalo Yehova angependa ufanye. Kisha ufanye jambo hilo. Hata uamuzi huo uwe mgumu jinsi gani, Baba yako mwenye upendo atakuwepo sikuzote ili kukusaidia uendelee kuwa imara na thabiti na kuishi maisha yako siku baada ya siku kulingana na viwango vyake vya uadilifu.​—Isa. 40:29-31.

18. Nĩkĩ tũtĩbuĩrĩte kũgambithia bangĩ tũgĩtumagĩra ithimi bietũ?

18 Hatua ya 3: Mwachie Yehova kazi ya kuhukumu. Ingawa tunajitahidi sana kuishi kulingana na viwango vya uadilifu vya Yehova, ni lazima tuepuke kuwahukumu wengine na kujiona kuwa waadilifu kupita kiasi. Badala ya kuwadharau wengine kana kwamba tuna haki ya kuwahukumu kwa kutegemea viwango vyetu wenyewe, tunapaswa kukumbuka kwamba Yehova ndiye “Mwamuzi wa dunia yote.” (Mwa. 18:25) Yehova hajatupatia kazi ya kuwahukumu wengine. Isitoshe, Yesu alituamuru hivi: “Acheni kuhukumu ili msihukumiwe.”​—Mt. 7:1. b

19. Nĩatĩa Jusufu oonanĩrie neetĩkĩtie njĩra ya Jehova ya gũtua ĩgamba?

19 Tufikirie tena mfano wa mwanamume mwadilifu Yosefu. Aliepuka kuwahukumu wengine, hata wale waliomtendea vibaya. Ndugu zake mwenyewe walimtendea vibaya, wakamuuza utumwani, na kumsadikishia baba yao kwamba Yosefu alikuwa amekufa. Miaka mingi baadaye, Yosefu aliungana tena na familia yake. Sasa akiwa kiongozi wa nchi mwenye nguvu, Yosefu angeweza kuwahukumu ndugu zake kwa ukali na kulipiza kisasi. Ndugu za Yosefu waliogopa kwamba angetenda hivyo, ingawa walikuwa wamejuta kutoka moyoni kwa mambo waliyokuwa wamefanya. Lakini Yosefu aliwapa uhakikisho huu: “Msiogope. Je, nimechukua nafasi ya Mungu?” (Mwa. 37:18-20, 27, 28, 31-35; 50:15-21) Kwa unyenyekevu, Yosefu alimwachia Yehova kazi ya kuhukumu.

20-21. Nĩatĩa ũũmba gũciebania na mwerekera jwa gũciona ũrĩ ũmwagĩru nkũrũki ya kĩthimi?

20 Kama Yosefu, tunamwachia Yehova kazi ya kuhukumu. Kwa mfano, tunaepuka kufikiria kwa kimbelembele kwamba tunajua jambo linalowachochea ndugu na dada zetu watende kwa njia fulani. Hatuwezi kusoma mioyo; ‘Yehova tu ndiye anayechunguza nia.’ (Met. 16:2) Anawapenda watu wa kila aina, kutoka malezi na tamaduni mbalimbali. Na Yehova anatutia moyo ‘tufungue kabisa mioyo yetu.’ (2 Kor. 6:13) Tunajitahidi kuwapenda wote katika familia yetu ya kiroho, si kuwahukumu.

21 Pia, hilo linamaanisha kwamba hatupaswi kuwahukumu wale walio nje ya kutaniko. (1 Tim. 2:3, 4) Je, unaweza kumhukumu mtu wako wa ukoo ambaye si Shahidi wa Yehova ukisema, “Mtu huyu hatawahi kukubali kweli”? Hapana, huo ni mtazamo wa kimbelembele na wa kujiona kuwa mwadilifu kupita kiasi. Bado Yehova anawapa “wanadamu wote kila mahali” nafasi ya kutubu. (Mdo. 17:30) Sikuzote kumbuka kwamba Yehova anawaona kuwa wasio waadilifu, wale wanaojiona kuwa waadilifu kupita kiasi.

22. Nĩkĩ gwe ũtuĩte ĩtua rĩa kwenda mantũ ja wagĩru?

22 Acheni upendo wetu kwa viwango vya Yehova vya uadilifu uendeleze shangwe na kuwachochea wengine, ukiwasaidia watukaribie hata zaidi sisi na Mungu wetu. Tusiache kamwe kuwa na “njaa na kiu ya uadilifu.” (Mt. 5:6) Uwe na hakika kwamba Yehova anaona jitihada zako na sikuzote anafurahia maendeleo unayofanya. Hata ulimwengu huu unapozidi kukosa uadilifu, usife moyo! Sikuzote kumbuka kwamba “Yehova anawapenda waadilifu.”​—Zab. 146:8.

WIMBO 139 Wazia Wakati Vitu Vyote Vitakuwa Vipya

a Katika ulimwengu huu mwovu, si rahisi kupata watu waadilifu. Ingawa hivyo, leo mamilioni ya watu wanaishi maisha ya uadilifu. Bila shaka, wewe ni mmoja wao. Unaishi maisha hayo kwa sababu unampenda Yehova, na Yehova anapenda uadilifu. Tunawezaje kuipenda hata zaidi sifa hii maridadi? Katika makala hii, tutachunguza maana ya uadilifu na jinsi tunavyonufaika kwa kuipenda sifa hiyo. Pia, tutazungumzia hatua tunazoweza kuchukua ili kuipenda zaidi sifa hii.

b Wakati mwingine wazee wa kutaniko wanalazimika kuhukumu katika visa vinavyohusu dhambi nzito na toba. (1 Kor. 5:11; 6:5; Yak. 5:14, 15) Hata hivyo, kwa unyenyekevu wanakumbuka kwamba hawawezi kusoma mioyo na kwamba wanahukumu kwa ajili ya Yehova. (Linganisha 2 Mambo ya Nyakati 19:6.) Wanatumia kwa makini viwango vya Mungu vya haki, vyenye usawaziko na rehema.