Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 52

Tethia Bangĩ Kũmĩĩria Magiita Jamoomũ

Tethia Bangĩ Kũmĩĩria Magiita Jamoomũ

“Baria baagiri kuthithirua wega ukarega kubathithiria wega, riria ukuumba kuthithaniria.”​—NJU. 3:27.

RWĨMBO 103 Wachungaji​—Zawadi Katika Wanadamu

MUHTASARI a

1. Nĩ njĩra irĩkũ Jehova atumagĩra gũcookia maromba ja nthũmba ciawe?

 JE, UNAJUA kwamba Yehova anaweza kukutumia kujibu sala ya bidii ya mtu fulani? Unaweza kusaidia iwe wewe ni mzee wa kutaniko, mtumishi wa huduma, painia, au mhubiri kutanikoni. Pia, unaweza kusaidia iwe wewe ni kijana au una umri mkubwa, au iwe wewe ni ndugu au dada. Mtu anayempenda Yehova anapomlilia akiomba msaada, mara nyingi Mungu wetu huwatumia wazee wa kutaniko na watumishi wengine waaminifu wawe “chanzo cha faraja nyingi” kwa mtu huyo. (Kol. 4:11) Ni pendeleo kubwa kumtumikia Yehova na ndugu zetu katika njia hiyo! Tunaweza kusaidia kunapokuwa na mlipuko wa ugonjwa, msiba wa asili, au mateso.

TETHIA BANGĨ RĨRĨA MŨRIMO JWAUMĨRA

2. Nĩkĩ bũmba kwĩthĩrwa bũrĩ bũbũũmũ gũtethia bangĩ rĩrĩa mũrimo jwaumĩra?

2 Kunapokuwa na mlipuko wa ugonjwa fulani, inaweza kuwa vigumu kwetu kuwasaidia wengine. Kwa mfano, huenda tukatamani kuwatembelea rafiki zetu, lakini isiwe salama kufanya hivyo. Huenda tukatamani kuwaalika wale ambao wanakabili matatizo ya kifedha wajiunge nasi kwa ajili ya chakula, lakini huenda hilo lisiwezekane pia. Huenda tukatamani kuwasaidia wengine, lakini inaweza kuwa changamoto ikiwa watu wa familia yetu wenyewe wanateseka. Ingawa hivyo, tunataka kuwasaidia ndugu zetu na Yehova anafurahi tunapofanya yale tunayoweza ili kuwasaidia. (Met. 3:27; 19:17) Tunaweza kufanya nini?

3. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ngerekano ya akũrũ ba kĩũthũrano kĩaba Desi? (Jeremia 23:4)

3 Mambo ambayo wazee wanaweza kufanya. Ikiwa wewe ni mzee wa kutaniko, wafahamu kondoo wako vizuri. (Soma Yeremia 23:4.) Desi, dada aliyenukuliwa katika makala iliyotangulia, anasema hivi: “Wakati uliopita, wazee katika kikundi chetu cha utumishi walijiunga pamoja nami na wengine kwa ajili ya huduma na tafrija.” b Jitihada za wachungaji hao zilifanya iwe rahisi kwao kumsaidia Desi baada ya janga la COVID-19 kutokea na alipopoteza baadhi ya watu wa familia yake kwa sababu ya virusi hivyo.

4. Nĩkĩ akũrũ boombĩre gũtethia Desi, na nĩmbi tũkwiritana?

4 Desi anaeleza hivi: “Kwa kuwa tayari niliwaona wazee kuwa rafiki, ilikuwa rahisi kwangu kuwaambia jinsi nilivyohisi na mambo yaliyonihangaisha.” Wazee wanapata somo gani? Wachungeni wale walio chini ya utunzaji wenu kabla ya hali ngumu kutokea. Uwe rafiki yao. Ikiwa kuna mlipuko wa ugonjwa unaokuzuia kuwatembelea kibinafsi, wasiliana nao kupitia njia nyingine. Desi anasema hivi: “Wakati mwingine wazee tofauti-tofauti walinipigia simu au kunitumia ujumbe siku ileile. Maandiko waliyoshiriki pamoja nami yalinigusa moyo, ingawa niliyajua maandiko hayo vizuri.”

5. Nĩatĩa akũrũ bomba kũmenya jarĩa ataana na aarĩ-ba-baaba bakũbatara nĩkenda babatethia?

5 Njia moja ambayo unaweza kujua mahitaji ya ndugu na dada zako ni kwa kuwauliza maswali kwa busara. (Met. 20:5) Je, wana chakula cha kutosha, dawa, na bidhaa nyingine? Je, wanakabili hatari ya kupoteza kazi au hata nyumba yao? Je, tunahitaji kuwaonyesha jinsi ya kutuma maombi serikalini ili kuomba msaada? Desi alipokea msaada wa kimwili kutoka kwa waabudu wenzake. Lakini ni msaada wa kihisia na wa kiroho aliopata kutoka kwa wazee wa kutaniko ambao ulimsaidia hasa akabiliane na majaribu yake. Anasema hivi: “Wazee walisali pamoja nami. Ingawa siwezi kukumbuka hasa mambo waliyosema, ninakumbuka jinsi nilivyohisi. Ni kana kwamba Yehova alikuwa akiniambia, ‘Huko peke yako.’”​—Isa. 41:10, 13.

Ndugu anayeongoza sehemu mkutanoni anafurahi kusikia maelezo yenye kutia moyo kutoka kwa wengi waliohudhuria mkutano na kutoka kwa ndugu mgonjwa ambaye amelazimika kushiriki kupitia video (Tazama fungu la 6)

6. Nĩatĩa ataana na aarĩ-ba-baaba bomba kũthithia nĩkenda batethia bangĩ? (Tega mbica.)

6 Mambo ambayo wengine wanaweza kufanya. Tunatarajia kwamba wazee watasaidia ndugu na dada kutanikoni. Lakini Yehova anatualika sisi sote tuwatie moyo na kuwasaidia wengine. (Gal. 6:10) Hata kuonyesha upendo kwa njia ndogo kunaweza kumsaidia sana mtu ambaye ni mgonjwa. Mtoto anaweza kutuma kadi au mchoro ili kumtia moyo ndugu fulani. Huenda kijana akamsaidia dada kufanya ununuzi. Namna gani kutayarisha chakula na kukipeleka kwa njia salama nyumbani kwa mtu ambaye ni mgonjwa? Bila shaka, ikiwa ugonjwa fulani umeenea sana, kila mtu kutanikoni atahitaji kutiwa moyo. Labda tunaweza kubaki kwa muda mrefu baada ya mkutano ili kuzungumza na ndugu na dada, iwe ni uso kwa uso au kupitia video. Na wazee wa kutaniko wanahitaji kutiwa moyo pia. Baadhi ya Mashahidi wamewatumia wazee barua ya shukrani, kwa sababu wanakuwa na shughuli nyingi sana kunapokuwa na mlipuko wa ugonjwa. Ni jambo zuri tunapofanya sehemu yetu ili “[kuendelea] kutiana moyo na kujengana”!​—1 The. 5:11.

TETHIA BANGĨ RĨRĨA KŨRĨ NA ŨGWATI

7. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ joomba kuumĩra nyuma ya ũgwati?

7 Msiba wa asili unaweza kuvuruga maisha ya mtu ghafla. Huenda watu wakapoteza mali zao, nyumba zao, au hata wapendwa wao. Ndugu na dada zetu Wakristo hupatwa pia na mambo hayo. Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia?

8. Akũrũ ba biũthũrano na biongo bia nja bomba kũthithia atĩa mbere ũgwati buumĩra?

8 Mambo ambayo wazee wanaweza kufanya. Wazee wa kutaniko, wasaidieni ndugu zenu wajitayarishe kabla ya msiba kutokea. Hakikisheni kwamba wote kutanikoni wanajua mambo wanayopaswa kufanya ili wawe salama na kuwasiliana na wazee wa kutaniko. Margaret aliyenukuliwa katika makala iliyotangulia, anasema hivi: “Wazee katika kutaniko letu walitayarisha sehemu ya mahitaji ya kutaniko, na kutuonya kwamba msimu wa moto wa msituni haukuwa umekwisha. Walisema kwamba ikiwa wenye mamlaka wangetuamuru tuondokee au ikiwa hali zingekuwa hatari, tunapaswa kuondoka mara moja.” Habari hiyo ilitolewa kwa wakati unaofaa kwa sababu majuma matano baadaye moto hatari wa msituni ulitokea. Wakati wa ibada ya familia, vichwa vya familia wanaweza kuzungumzia mambo ambayo kila mshiriki wa familia atafanya. Ikiwa wewe na watoto wako mmejitayarisha, inaelekea mtaendelea kuwa watulivu msiba wa asili unapotokea.

9. Akũrũ bomba atĩa kwithuranĩra gũtethia bangĩ mbere na nyuma ya ũgwati?

9 Ikiwa wewe ni mwangalizi wa kikundi, usisubiri hadi msiba utokee ili kuhakikisha kwamba una habari sahihi za mawasiliano za wote katika kikundi chako cha utumishi. Andika orodha na uhakikishe kwamba ina habari za karibuni zaidi. Kisha msiba unapotokea, itakuwa rahisi kwako kuwasiliana na kila mhubiri na kuchanganua mahitaji yake. Wasilisha habari hizo mara moja kwa mratibu wa baraza la wazee, ambaye atawasiliana na mwangalizi wa mzunguko. Ndugu hao wanaposhirikiana pamoja, kunaweza kuwa na matokeo mazuri sana. Baada ya moto huo, mwangalizi wa mzunguko wa kutaniko ambalo Margaret anashirikiana nalo alikaa macho kwa saa 36, akielekeza jitihada za wazee za kuwasiliana na kuwatunza ndugu na dada 450 hivi waliolazimika kuondoka nyumbani kwao. (2 Kor. 11:27) Hivyo, wote waliohitaji mahali pa kukaa waliandaliwa makao.

10. Nĩkĩ akũrũ bonaga ndiũnga cia ũtegeeri irĩ cia gĩtũmi? (Johana 21:15)

10 Wazee Wakristo wana jukumu la kuandaa msaada wa kiroho na kihisia. (1 Pet. 5:2) Msiba unapotokea, kwanza wazee wanapaswa kuhakikisha kwamba kila ndugu na dada yuko salama na wana chakula, mavazi, na makao. Lakini kwa miezi mingi baada ya hapo, inaelekea kwamba ndugu na dada watahitaji msaada wa kiroho na kihisia. (Soma Yohana 21:15.) Ndugu Harold, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ambaye amekutana na ndugu na dada wengi walioathiriwa na misiba ya asili, anasema hivi: “Muda unahitajika ili kurudia hali ya kawaida. Huenda wakaanza kuishi maisha ya kawaida tena, lakini wanaweza kuendelea kuwa na kumbukumbu za wapendwa wao waliokufa, vitu vyenye thamani walivyopoteza, au hali hatari waliyokabili. Kumbukumbu hizo zinaweza kusababisha tena hisia za majonzi. Hisia hizo hazimaanishi kwamba hawana imani, bali ni hali ya kawaida kwa wanadamu.”

11. Nĩ mantũ ta jarĩkũ nja ikũbatara gwĩta na mbere gũtetherua kĩrĩjo?

11 Wazee wa kutaniko wanatumia shauri la “[kulia] na wale wanaolia.” (Rom. 12:15) Wazee wanapaswa kuwahakikishia ndugu na dada hao waliopatwa na misiba kwamba bado Yehova anawapenda na pia ndugu na dada zao Wakristo. Wazee watajitahidi kusaidia familia zidumishe ratiba yao ya kiroho, kutia ndani kusali, kujifunza, kuhudhuria mikutano, na kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Wazee wanaweza kuwatia moyo pia wazazi wawasaidie watoto wao kukazia fikira mambo ambayo hayawezi kuharibiwa na msiba wowote. Wazazi, wakumbusheni watoto wenu kwamba sikuzote Yehova atakuwa rafiki yao na kwamba sikuzote atawasaidia. Na mhakikishe mnawaeleza kwamba sikuzote watakuwa na familia ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada ambao wako tayari kuwasaidia.​—1 Pet. 2:17.

Je, unaweza kujitolea kusaidia baada ya msiba wa asili kutokea katika eneo lenu? (Tazama fungu la 12) e

12. Nĩatĩa bangĩ bomba kũthithia nĩkenda batethania ĩgiita rĩa ũgwati? (Tega mbica.)

12 Mambo ambayo wengine wanaweza kufanya. Msiba unapotokea karibu na eneo lenu, waulize wazee jinsi unavyoweza kusaidia. Labda unaweza kuandaa makao ya muda kwa wale waliolazimika kuhama, au kwa ajili ya wajitoleaji wa ujenzi. Huenda ukasaidia kupeleka chakula na bidhaa kwa wahubiri wenye uhitaji. Msiba unapotokea katika eneo lililo mbali zaidi, bado unaweza kusaidia. Jinsi gani? Kwa kusali kwa ajili wale walioathiriwa. (2 Kor. 1:8-11) Huenda ukaunga mkono kifedha kazi ya kutoa msaada kwa kutoa mchango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. (2 Kor. 8:2-5) Ikiwa unaweza kusafiri kwenda eneo lililoathiriwa, waulize wazee wa kutaniko kuhusu jinsi unavyoweza kujitolea. Ombi lako likikubaliwa, inaelekea kwamba utapata mazoezi fulani ili utumike katika sehemu ambayo msaada wako unahitajika zaidi.

TETHIA ATAANA NA AARĨ-BA-BAABA KŨMĨĨRIA RĨRĨA BAKŨTHANGĨKUA

13. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ ataana-ba-baaba bakũrũkagĩĩra nthĩgũrũ irĩa ngũgĩ yeetũ ĩrigĩĩrĩtue?

13 Katika nchi ambazo kazi yetu imepigwa marufuku, mateso hufanya maisha yawe magumu zaidi. Bado akina ndugu katika nchi hizo wanakabili changamoto za kifedha, wanakuwa wagonjwa, na kuwapoteza wapendwa wao katika kifo. Lakini kwa sababu ya marufuku, huenda wazee wa kutaniko wasiwatembelee au kuwasiliana kwa uhuru na wale ambao wanahitaji kutiwa moyo. Ilikuwa hivyo kwa Andrei, aliyetajwa katika makala iliyotangulia. Dada mmoja katika kikundi chao cha utumishi alikuwa na matatizo ya kifedha. Kisha akapatwa na aksidenti ya gari. Alihitaji kufanyiwa upasuaji mbalimbali na hangeweza kufanya kazi. Licha ya vizuizi na janga la COVID-19, akina ndugu walifanya yale waliyoweza ili kumsaidia, na Yehova aliona jitihada zao.

14. Nĩatĩa akũrũ ba kĩũthũrano bomba gwĩka ngerekano ĩnjega yegie kwĩrĩgĩĩra Jehova?

14 Mambo ambayo wazee wanaweza kufanya. Andrei alisali na akafanya mambo aliyoweza. Yehova alimjibuje? Aliandaa waabudu wenzake ambao walikuwa na uhuru mwingi zaidi wa kufanya mambo. Baadhi yao walimpeleka dada huyo hospitalini. Wengine walitoa msaada wa kifedha. Yehova aliwachochea kufanya yale ambayo wangeweza, naye akabariki jitihada zao za umoja na za ujasiri. (Ebr. 13:16) Wazee, kazi yetu inapowekewa vizuizi, wakabidhini wengine majukumu. (Yer. 36:5, 6) Zaidi ya yote, mtegemeeni Yehova. Anaweza kuwasaidia kutimiza mahitaji ya ndugu na dada zetu.

15. Nĩatĩa tũũmba gũkaria ũrũmwe bwetũ bwa Gĩkristũ rĩrĩa tũkũthangĩkua?

15 Mambo ambayo wengine wanaweza kufanya. Tunapokuwa chini ya marufuku huenda tukalazimika kukutana katika vikundi vidogo zaidi. Basi, ni jambo muhimu sana kuendelea kudumisha mahusiano yenye amani. Adui yetu ni Shetani, bali si ndugu na dada zetu. Usikazie fikira makosa ya ndugu zako, na ujitahidi kusuluhisha upesi hali zozote za kutoelewana. (Met. 19:11; Efe. 4:26) Muwe tayari kusaidiana. (Tito 3:14) Msaada ambao wengine walimpa yule dada aliyekuwa na uhitaji, ulikuwa na matokeo mazuri katika kikundi chao cha utumishi. Uhusiano wao ulikuwa wa karibu zaidi, kama wa familia.​—Zab. 133:1.

16. Kũringana na Akolosai 4:3, 18, nĩatĩa tũũmba gũtethia ataana na aarĩ-ba-baaba barĩa bakũthangĩkua?

16 Makumi ya maelfu ya ndugu na dada zetu Wakristo wanamtumikia Yehova licha ya kuwekewa vizuizi na serikali. Baadhi yao wamefungwa gerezani kwa sababu ya imani yao. Tunaweza kusali kwa ajili yao, kwa ajili ya familia zao, na kwa ajili ya wale wanaohatarisha uhuru wao wenyewe ili kuwaandalia ndugu na dada hao msaada wa kiroho, kimwili, na kisheria. c (Soma Wakolosai 4:3, 18.) Usipuuze kamwe nguvu za sala zako!​—2 The. 3:1, 2; 1 Tim. 2:1, 2.

Unawezaje kuitayarisha familia yako sasa kwa ajili ya mateso? (Tazama fungu la 17)

17. Nĩatĩa ũũmba kwithuranĩra nandĩ tontũ bwa mĩthangĩko?

17 Wewe na familia yako mnaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya mateso. (Mdo. 14:22) Usijaribu kuwazia mambo yote mabaya yanayoweza kutokea. Badala yake, imarisha urafiki wako pamoja na Yehova na uwasaidie watoto wako wafanye hivyo pia. Ikiwa nyakati nyingine unahisi wasiwasi, mmwagie Mungu moyo wako. (Zab. 62:7, 8) Mkiwa familia, zungumzieni sababu zote zinazofanya mmtumaini Yehova. d Kama ilivyo kuhusiana na misiba ya asili, ikiwa mtajitayarisha kibinafsi na kumtumaini Yehova, hilo litawasaidia watoto wenu kusitawisha ujasiri na kuwa na amani wanapokabili mateso.

18. Nĩ mantũ jarĩkũ twĩrĩgĩĩrĩte ĩgiita rĩĩjĩte?

18 Amani ya Mungu hufanya tujihisi salama. (Flp. 4:6, 7) Kupitia amani hiyo, Yehova huutuliza moyo wetu licha ya magonjwa, misiba ya asali, na mateso ambayo huenda yakatupata leo. Anawatumia wazee wa kutaniko wenye bidii kutuchunga. Na anatupatia sisi sote pendeleo la kusaidiana. Amani tunayofurahia sasa itatusaidia kukabiliana na majaribu makubwa zaidi wakati ujao, kutia ndani “dhiki kuu.” (Mt. 24:21) Wakati huo, tutahitaji kudumisha amani yetu na kuwasaidia wengine kufanya hivyo pia. Lakini baada ya tukio hilo, hatutakabili tena hali ngumu ambazo zitatufanya tuwe na wasiwasi. Hatimaye tutafurahia jambo ambalo sikuzote Yehova ametaka tuwe nalo​—amani kamilifu inayodumu.​—Isa. 26:3, 4.

RWĨMBO 109 Pendaneni Sana Kutoka Moyoni

a Mara nyingi Yehova hutumia watumishi wake waaminifu kuwasaidia wale wanaokabiliana na hali ngumu. Anaweza kukutumia wewe ili kuwatia moyo ndugu na dada zako. Acheni tuone jinsi tunavyoweza kuwasaidia wengine wanapohitaji msaada.

b Baadhi ya majina yamebadilishwa.

c Haiwezekani kwa ofisi ya tawi au kwa wale walio kwenye makao makuu ya ulimwenguni pote kutuma barua za watu binafsi kwa ndugu na dada ambao wamefungwa gerezani.

d Tazama makala “Jitayarishe Sasa kwa Ajili ya Mateso” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 2019.

e MAELEZO YA PICHA: Wenzi wa ndoa wanailetea chakula familia iliyo kwenye makao ya muda baada ya kupatwa na msiba wa asili.