Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 53

Atana ba Baaba Babeethĩ—Eeni Antũ Arũme Akristũ Bagimaru

Atana ba Baaba Babeethĩ—Eeni Antũ Arũme Akristũ Bagimaru

“Ugie na inya, ucionanagie ati uri muntu-murume mma.”—1 AN. 2:2.

RWĨMBO 135 Mwaliko Wenye Upendo wa Yehova: “Uwe na Hekima, Mwanangu”

MUHTASARI a

1. No mwanka muntũ mũrũme Mũkristũ athithie atĩa nĩkenda ombana?

 MFALME Daudi alimwagiza Sulemani hivi: “Uwe imara na ujithibitishe kuwa mwanamume.” (1 Fal. 2:​1-3) Ushauri huo ni muhimu kwa wanaume wote Wakristo leo. Ili wafanikiwe, ni lazima wajifunze kutii sheria za Mungu na kutumia kanuni za Biblia katika kila sehemu ya maisha yao. (Luka 2:52) Kwa nini ni muhimu sana kwa ndugu vijana kuwa wanaume Wakristo wakomavu?

2-3. Nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi mũtana wa baaba ũmwĩthĩ kwaa Mũkristũ ũmũgimaru?

2 Mwanamume Mkristo anatimiza majukumu muhimu katika familia na kutanikoni. Bila shaka, ninyi ndugu vijana mmefikiria kuhusu majukumu mnayoweza kuwa nayo wakati ujao. Huenda una lengo la kuwa mtumishi wa wakati wote, mtumishi wa huduma, na baadaye mzee wa kutaniko. Pia, huenda ukataka kufunga ndoa na kuwa na watoto. (Efe. 6:4; 1 Tim. 3:1) Ili ufikie malengo hayo na kufanikiwa, unahitaji kuwa Mkristo mkomavu. b

3 Ni nini kinachoweza kukusaidia uwe Mkristo mkomavu? Kuna stadi muhimu unazohitaji kujifunza. Hivyo, unaweza kufanya nini sasa ili kujitayarisha na kufanikiwa kutimiza jukumu lolote ambalo huenda ukawa nalo wakati ujao?

MATAGARIA JA KWAA MŨKRISTŨ ŨMŨGIMARU

Kuiga sifa za pekee za Yesu kunaweza kukusaidia kuwa mwanamume Mkristo mkomavu (Tazama fungu la 4)

4. Nĩkũ ũũmba kwona ngerekano injega cia kũthingata? (Tega kinya mbica.)

4 Chagua mifano mizuri ya kuiga. Biblia ina mifano mingi mizuri ambayo wanaume vijana wanaweza kuiga. Wanaume hao wa zamani walimpenda Mungu na kushughulikia majukumu mbalimbali ili kuwatunza watu wa Mungu. Pia, unaweza kupata mifano mizuri ya wanaume Wakristo wakomavu katika familia yenu na katika kutaniko lenu. (Ebr. 13:7) Na una mfano mkamilifu wa Yesu Kristo. (1 Pet. 2:21) Unapochunguza kwa makini mifano hiyo, fikiria sifa zao za pekee. (Ebr. 12:​1, 2) Kisha uamue jinsi utakavyowaiga wanaume hao.

5. Nĩatĩa ũũmba kũgia na ũũmbi bwa kĩmathũgaanio, na nĩkĩ ũntũ bũu bũrĩ bwa gĩtũmi? (Zaburi 119:9)

5 Sitawisha na ‘ulinde uwezo wa kufikiri.’ (Met. 3:21) Mwanamume mwenye uwezo wa kufikiri anatafakari kwa makini kabla ya kuamua atakachofanya. Hivyo, jitahidi kusitawisha uwezo huo na kuudumisha. Kwa nini? Ulimwengu huu umejaa wanaume vijana ambao wanaongozwa na mawazo yao wenyewe au wanaoruhusu hisia zao ziongoze matendo yao. (Met. 7:7; 29:11) Vyombo vya habari kama vile televisheni, sinema, intaneti, na mitandao ya kijamii inaweza kuathiri kwa njia kubwa jinsi unavyofikiri na kutenda. Lakini unawezaje kusitawisha uwezo wa kufikiri? Anza kwa kujifunza kanuni za Biblia na kufikiria kwa nini kanuni hizo zina manufaa. Kisha utumie kanuni hizo ili zikusaidie kufanya maamuzi yatakayomfurahisha Yehova. (Soma Zaburi 119:9.) Ukisitawisha uwezo huo, utakuwa umepiga hatua kubwa kuelekea kuwa mwanamume Mkristo mkomavu. (Met. 2:​11, 12; Ebr. 5:14) Fikiria jinsi uwezo wa kufikiri utakavyokunufaisha katika hali hizi mbili: (1) unaposhughulika na akina dada na (2) unapofanya maamuzi kuhusu mwonekano wako.

6. Nĩatĩa ũũmbi bwa kĩmathũgaanio bũgatethia mũtana wa baaba ũmwĩthĩ gũtĩĩa aarĩ ba baaba?

6 Uwezo wa kufikiri utakusaidia kuwaonyesha heshima wanawake. Ni jambo la kawaida na linalofaa kwa ndugu kijana kutamani kuanzisha uhusiano na dada Mkristo. Hata hivyo, mwanamume kijana mwenye uwezo wa kufikiri hatasema, kuandika, au kufanya jambo lolote linaloonyesha anavutiwa kimahaba na dada fulani isipokuwa iwe kwa kweli, anamfikiria dada huyo kuwa mwenzi wake wa ndoa wa wakati ujao. (1 Tim. 5:​1, 2) Ikiwa ameanzisha urafiki wa kimahaba na dada, atalinda sifa nzuri ya dada huyo, kwa kuepuka kabisa kuwa peke yao bila kuwa na mwandamani anayefaa.—1 Kor. 6:18.

7. Nĩatĩa ũũmbi bwa kĩmathũgaanio bũgatethia mũtana wa baaba ũmwĩthĩ rĩrĩa akũthuura birĩa agekĩra na kwigemia?

7 Njia nyingine ambayo mwanamume kijana huonyesha kwamba amesitawisha uwezo wa kufikiri ni kwa kufanya maamuzi mazuri kuhusu mavazi na mapambo. Mara nyingi, mitindo inayopendwa ya mavazi imebuniwa na kutangazwa na watu ambao hawamheshimu Yehova au wanaoishi maisha yasiyo na maadili. Njia yao ya kufikiri iliyopotoka kimaadili inaonekana kupitia mitindo ya mavazi yanayobana sana au yanayofanya mwanamume aonekane kama mwanamke. Anapochagua mavazi, mwanamume kijana anayetaka kuwa Mkristo mkomavu ataongozwa na kanuni za Biblia na mifano mizuri kutanikoni. Anaweza kujiuliza hivi: ‘Je, maamuzi yangu yanaonyesha kwamba nina utimamu wa akili na ninawafikiria wengine? Je, jinsi ninavyovalia inafanya iwe rahisi kwa wengine kuamini kwamba mimi ni mtumishi wa Mungu mwenye bidii?’ (1 Kor. 10:​31-33; Tito 2:6) Mwanamume kijana mwenye uwezo wa kufikiri ataheshimiwa, si na ndugu na dada tu, bali pia na Baba yake wa mbinguni.

8. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ omba kwiritana kwaa muntũ ũkwĩrĩgĩrĩka?

8 Uwe mwenye kutegemeka. Mwanamume kijana anayetegemeka, anatimiza majukumu yake yote kwa bidii. (Luka 16:10) Fikiria mfano mkamilifu wa Yesu. Hakuwahi kamwe kuwa mzembe au kutotimiza majukumu yake. Badala yake, alitimiza migawo ambayo Yehova alimpa, hata ilipokuwa vigumu kufanya hivyo. Aliwapenda watu—hasa wanafunzi wake—na alikuwa tayari kutoa uhai wake kwa ajili yao. (Yoh. 13:1) Mwige Yesu, kwa kutimiza kwa bidii mgawo wowote unaopewa. Ikiwa hujui jinsi ya kutimiza mgawo huo, uwe mnyenyekevu na uwaombe msaada ndugu wakomavu. Usiridhike kamwe na kutimiza mambo machache. (Rom. 12:11) Badala yake, kamilisha mgawo wako, na kuufanya “kama kwa Yehova, na si kwa wanadamu.” (Kol. 3:23) Bila shaka, wewe si mkamilifu, hivyo, uwe mwenye kiasi na ukubali makosa yoyote unayofanya.—Met. 11:2.

IRITANE ŨTEA BWA GŨTUMĨRA ŨTŨŨRONE

9. Nĩkĩ no mwanka mũtana wa baaba ũmwĩthĩ airitane ũtea bwa gũtumĩra ũtũũrone?

9 Ili uwe mwanamume Mkristo mkomavu, utahitaji kujifunza stadi zinazofaa. Stadi hizo zitakusaidia kutimiza majukumu yako kutanikoni, kupata kazi itakayokutegemeza wewe au familia yako, na zitakusaidia kuwa na uhusiano mzuri na wengine. Fikiria stadi muhimu zifuatazo.

Kusoma na kuandika vizuri kutakusaidia wewe mwenyewe na kutaniko (Tazama fungu la 10-11)

10-11. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ agatetheka o amwe na kĩũthũrano tontũ bwa kwiritana kwandĩka na kũthooma bwega? (Zaburi 1:​1-3) (Tega kinya mbica.)

10 Jifunze kusoma na kuandika vizuri. Biblia inasema kwamba mwanamume mwenye furaha na mwenye mafanikio hutumia muda kila siku kusoma Neno la Mungu na kulitafakari. (Soma Zaburi 1:​1-3.) Kwa kusoma Biblia kila siku, atajua njia ya Yehova ya kufikiri ambayo itamsaidia kufikiria mambo kwa njia nzuri, na kujifunza jinsi ya kutumia Maandiko vizuri. (Met. 1:​3, 4) Wanaume kama hao wanahitajika kutanikoni. Kwa nini?

11 Ndugu na dada zetu wanahitaji msaada wa wanaume wenye uwezo wa kufundisha na kuwapa ushauri unaotegemea Biblia. (Tito 1:9) Ikiwa unajua kusoma na kuandika vizuri, utaweza kuandaa hotuba na maelezo yenye habari zenye kujenga na kuimarisha imani. Pia, utaweza kuandika mambo makuu kwa njia nzuri unapojifunza na unaposikiliza hotuba kwenye mikutano ya kutaniko, makusanyiko ya mzunguko na ya eneo. Mambo hayo yatakusaidia kujenga imani yako na kuwatia moyo wengine.

12. Nĩmbi bigagũtethia kwĩthĩrwa na ũtea bũbwega bwa kwaria?

12 Sitawisha ustadi wa kuwasiliana vizuri. Ni lazima mwanamume Mkristo ajifunze kuwasiliana vizuri. Mwanamume anayewasiliana vizuri anasikiliza na kutambua mawazo na hisia za wengine. (Met. 20:5) Anaweza kutambua mabadiliko ya sauti ya mtu, ishara za uso, na za mwili. Huwezi kujifunza kufanya mambo hayo bila kutumia muda pamoja na watu. Ikiwa una mazoea ya kutumia tu vifaa vya kielektroni ili kuwasiliana, kama vile kutuma barua-pepe na jumbe za simu, uwezo wako wa kuwasiliana ana kwa ana na watu unaweza kupungua. Hivyo, tafuta fursa za kuzungumza na watu wengine ana kwa ana.—2 Yoh. 12.

Ni vizuri kujifunza ustadi utakaokusaidia kupata kazi (Tazama fungu la 13)

13. No mwanka mũtana ũmwĩthĩ airitane ũntũ bũrĩkũ bũngĩ? (1 Timotheo 5:8) (Tega kinya mbica.)

13 Jifunze kujitegemeza. Ni lazima mwanamume Mkristo mkomavu awe na uwezo wa kujitegemeza na kuwategemeza watu wa nyumba yake. (Soma 1 Timotheo 5:8.) Katika baadhi ya nchi, huenda ndugu vijana wakajifunza ustadi fulani kutoka kwa baba yao au mtu mwingine wa ukoo. Katika nchi nyingine, mwanamume kijana anaweza kujifunza ufundi au kazi nyingine akiwa shule ya sekondari. Vyovyote vile, ni vizuri kujifunza ustadi utakaokusaidia kupata kazi. (Mdo. 18:​2, 3; 20:34; Efe. 4:28) Fanya kazi kwa bidii na uhakikishe unakamilisha kazi unayoanza. Wengine watatambua hilo na watathamini kazi yako. Hivyo, kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kupata kazi na kuidumisha. Sifa na stadi tulizozungumzia ni za muhimu pia kwa mwanamume Mkristo ili aweze kutimiza majukumu yake ya wakati ujao. Acheni tuzungumzie baadhi ya majukumu hayo.

ITHURANĨRE TONTŨ BWA TWANYA TWA ĨGIITA RĨĨJĨTE

14. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ omba kwithuranĩra kwaa mũtungatĩri wa ĩgiita rĩonthe?

14 Mtumishi wa wakati wote. Wanaume wengi Wakristo wakomavu walianza utumishi wa wakati wote wakiwa na umri mdogo. Upainia unamsaidia mwanamume kijana kujifunza jinsi ya kufanya kazi vizuri pamoja na watu mbalimbali. Pia, unamsaidia kupanga bajeti vizuri na kushikamana nayo. (Flp. 4:​11-13) Njia nzuri ya kuanza utumishi wa wakati wote ni kufanya upainia msaidizi. Wengi hutumikia wakiwa mapainia wasaidizi kwa muda fulani, jambo linalowasaidia kuwa tayari kuanza upainia wa kawaida. Upainia unaweza kufungua mlango unaoongoza kwenye aina nyingine za utumishi wa wakati wote, kutia ndani kutumikia ukiwa mjenzi au Mwanabetheli.

15-16. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ omba kwagĩra gũtumĩka kĩũthũranone?

15 Mtumishi wa huduma au mzee. Wanaume Wakristo wanapaswa kuwa na lengo la kustahili kuwatumikia ndugu na dada zao wakiwa wazee wa kutaniko. Biblia inasema kwamba wanaume wanaojitahidi kufikia jukumu hilo ‘wanatamani kazi njema.’ (1 Tim. 3:1) Kabla ya kutumikia akiwa mzee, ni lazima ndugu astahili kutumikia akiwa mtumishi wa huduma. Watumishi wa huduma wanawasaidia wazee kwa njia nyingi hususa. Wazee na watumishi wa huduma wanawatumikia kwa unyenyekevu ndugu na dada zao na kushiriki kwa bidii katika huduma. Ndugu vijana wanaweza kustahili kutumikia wakiwa watumishi wa huduma hata wanapokuwa katika miaka ya mwishoni ya utineja. Na mtumishi wa huduma mwenye sifa za kustahili anaweza kuwekwa rasmi kuwa mzee hata akiwa na umri wa miaka 20.

16 Unawezaje kustahili kupata majukumu hayo? Biblia inataja tu orodha ya sifa unazohitaji kuwa nazo. Hata hivyo, kumbuka kwamba sifa hizo zote zinategemea Biblia na upendo wako kwa Yehova, familia yako, na kutaniko. (1 Tim. 3:​1-13; Tito 1:​6-9; 1 Pet. 5:​2, 3) Jitahidi kuelewa kila sifa. Sali kwa Yehova akusaidie kufikia sifa hizo. c

Yehova anataka mume ampende mke na watoto wake na kuwatunza kimwili, kihisia, na zaidi ya ote kiroho (Tazama fungu la 17)

17. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ omba kwithuranĩra kwaa mũkũrũ ũgũrene na kĩongo kĩa nja? (Tega kinya mbica.)

17 Mume na kichwa cha familia. Kama Yesu alivyoonyesha, baadhi ya wanaume Wakristo wakomavu wanaendelea kuwa waseja. (Mt. 19:12) Hata hivyo, ikiwa utaamua kufunga ndoa, utakuwa na jukumu la ziada la kuwa mume na kichwa cha familia. (1 Kor. 11:3) Yehova anatarajia mume ampende mke wake na kumtunza kimwili, kihisia, na kiroho. (Efe. 5:​28, 29) Sifa na stadi tulizozungumzia mwanzoni mwa makala hii, kama vile, kusitawisha uwezo wa kufikiri, kuwaheshimu wanawake, na kuwa mwenye kutegemeka, zitakusaidia ukiwa mwenzi wa ndoa. Utakuwa umejitayarisha vizuri kutimiza majukumu yako ukiwa mume na kichwa cha familia.

18. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ omba kwithuranĩra kwaa mũciari?

18 Baba. Baada ya kufunga ndoa, unaweza kuwa baba. Unaweza kujifunza nini kutoka kwa Yehova kuhusu kuwa baba mzuri? Unaweza kujifunza mambo mengi. (Efe. 6:4) Yehova alimwambia waziwazi Mwana wake, Yesu, kwamba anampenda na kumkubali. (Mt. 3:17) Ikiwa utakuwa baba, hakikisha kuwa unawahakikishia kwa ukawaida watoto wako kwamba unawapenda. Wapongeze mara kwa mara kwa mambo mazuri wanayofanya. Akina baba wanaoiga mfano wa Yehova wanawasaidia watoto wao kuwa wanaume na wanawake Wakristo wakomavu. Unaweza kujitayarisha sasa kwa ajili ya jukumu hilo kwa kuwajali kwa upendo watu katika familia yenu na katika kutaniko na kwa kujifunza kuwaambia kwamba unawapenda na unawathamini. (Yoh. 15:9) Hilo litakusaidia kutimiza majukumu ambayo huenda ukawa nayo wakati ujao ukiwa mume na baba. Kwa wakati huu, utakuwa mwenye thamani kubwa kwa Yehova na msaada mkubwa kwa familia yenu, na kutanikoni.

NĨATĨA ŨKATHITHIA NANDĨ?

Wanaume wengi vijana ambao wamefundishwa kupitia Maandiko na wanatumia mambo waliyojifunza, wamekuwa Wakristo wakomavu (Tazama fungu la 19-​20)

19-20. Nĩmbi bigatethia atana ba baaba babeethĩ kwaa akũrũ Akristũ bagimaru? (Tega kinya mbica karatacine ka mbere.)

19 Ndugu vijana, hamwezi kuwa wanaume Wakristo wakomavu bila jitihada zozote. Mnahitaji kuchagua mifano mizuri ya kuiga, kusitawisha uwezo wa kufikiri, kutegemeka, kujifunza stadi zitakazowasaidia maishani, na kujitayarisha kwa ajili ya majukumu ya wakati ujao.

20 Wakati mwingine huenda ukahisi umelemewa unapotafakari mambo unayohitaji kufanyia kazi. Lakini unaweza kufanikiwa. Kumbuka kwamba Yehova anatamani kukusaidia. (Isa. 41:​10, 13) Bila shaka, akina ndugu na dada kutanikoni watakusaidia pia. Utakapofikia hatua ya kuwa mwanamume Mkristo Mkomavu, maisha yako yatakuwa yenye kufurahisha na yenye kuridhisha. Tunawapenda, enyi ndugu vijana! Yehova na awabariki mnapojitahidi kuwa wanaume Wakristo wakomavu.—Met. 22:4.

RWĨMBO 65 Songa Mbele!

a Wanaume wakomavu wanahitajika katika kutaniko la Kikristo. Katika makala hii, tutachunguza jinsi ninyi ndugu vijana mnavyoweza kuwa wanaume Wakristo wakomavu.

b Tazama “Ufafanuzi wa Maneno” katika makala iliyotangulia.

c Tazama Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, sura ya 5-6.