Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 51

Gwĩrĩrua Wĩrĩgĩĩro Bũtĩna Mantũ ja Gũkuuna Nkoro

Gwĩrĩrua Wĩrĩgĩĩro Bũtĩna Mantũ ja Gũkuuna Nkoro

“Wirigiriiro nabu butiikirithagia nthao.”—AR. 5:5.

RWĨMBO 142 Kushikilia Tumaini Letu

MUHTASARI a

1. Nĩkĩ tũũmba kuuga Iburahimu naarĩ na wĩrĩgĩĩro bũũriku?

 YEHOVA alimwahidi Abrahamu, rafiki yake, kwamba mataifa yote duniani yangebarikiwa kupitia uzao wake. (Mwa. 15:5; 22:18) Kwa sababu Abrahamu alikuwa na imani yenye nguvu katika Mungu, alikuwa na uhakika kwamba ahadi ya Mungu ingetimia. Hata hivyo, Abrahamu alipokuwa na umri wa miaka 100 na mke wake miaka 90, wenzi hao waaminifu bado hawakuwa na mwana. (Mwa. 21:​1-7) Ingawa hivyo, Biblia inasema hivi: “Kwa kutegemea tumaini, [Abrahamu] alikuwa na imani kwamba angekuwa baba ya mataifa mengi kulingana na yale yaliyokuwa yamesemwa.” (Rom. 4:18) Unajua kwamba tumaini la Abrahamu lilitimizwa. Alikuja kuwa baba ya mwana ambaye alimsubiri kwa muda mrefu, Isaka. Kwa nini Abrahamu alikuwa na uhakika kwamba Yehova angetimiza ahadi yake?

2. Nĩkĩ Iburahimu ataarĩ na nkanja atĩ wĩrane bwa Jehova bũrĩngĩũjũra?

2 Kwa sababu alikuwa na uhusiano wa kibinafsi pamoja na Yehova, Abrahamu alikuwa na ‘uhakika kamili kwamba kile alichoahidi Mungu’ kingetimia. (Rom. 4:21) Yehova alimkubali Abrahamu na kumtangaza kuwa mwadilifu kwa sababu ya imani yake. (Yak. 2:23) Kama inavyoonyeshwa kwenye Waroma 4:​18, Abrahamu alikuwa na imani na pia tumaini. Acheni sasa tuchunguze maneno aliyosema mtume Paulo kuhusu tumaini, kama yanavyoonyeshwa kwenye Waroma sura ya 5.

3. Nĩmbi Paũlũ ataarĩrĩĩtie bwegie wĩrĩgĩĩro?

3 Paulo anaeleza kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba “tumaini [letu] halikatishi tamaa.” (Rom. 5:5) Pia, anatusaidia kuelewa jinsi tumaini letu la Kikristo linavyoweza kuwa imara. Tunapochunguza hatua ambazo Paulo ameorodhesha kwenye Waroma 5:​1-5, tufikirie hali yetu wenyewe. Unapofanya hivyo, inaelekea utatambua kwamba kadiri muda unavyopita, ndivyo tumaini lako la Kikristo linavyokuwa imara zaidi. Pia, mazungumzo yetu yatakusaidia kutambua jinsi unavyoweza kufanya tumaini lako liwe imara zaidi kuliko lilivyo sasa. Acheni kwanza tuchunguze tumaini lenye utukufu ambalo Paulo anasema halikatishi tamaa.

WĨRĨGĨĨRO BWETŨ BŨRĨ NA MWAGO

4. Nĩmbi biarĩĩrĩtue kĩrĩ Aroma 5:​1, 2?

4 Soma Waroma 5:​1, 2. Paulo aliliandikia kutaniko la Roma maneno hayo. Ndugu na dada kwenye kutaniko hilo walikuwa wamejifunza kumhusu Yehova na Yesu, walikuwa wamesitawisha imani, na kuwa Wakristo. Hivyo Mungu “[aliwatangaza] kuwa waadilifu kutokana na imani,” na kuwatia mafuta kwa roho takatifu. Naam, walipata tumaini lenye uhakika na zuri ajabu.

5. Nĩ wĩrĩgĩĩro bũrĩkũ etũrĩrua maguta barĩ nabu?

5 Baadaye, Paulo aliwaandikia Wakristo watiwa-mafuta jijini Efeso kuhusu tumaini ambalo Mungu alikuwa amewapatia. Tumaini hilo linatia ndani kupokea ‘urithi wa watakatifu.’ (Efe. 1:18) Pia, Paulo aliwaeleza Wakolosai mahali ambapo tumaini lao lingetimizwa. Aliliita “tumaini [walilowekewa] akiba mbinguni.” (Kol. 1:​4, 5) Hivyo, tumaini la Wakristo watiwa-mafuta ni kwamba watafufuliwa ili wapate uzima wa milele mbinguni, ambapo watatawala pamoja na Kristo.—1 The. 4:​13-17; Ufu. 20:6.

Ndugu F. W. Franz alifafanua vizuri uhakika ambao Wakristo watiwa-mafuta wanao kuhusu tumaini lao (Tazama fungu la 6)

6. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwe mwĩtũrĩrua maguta augĩre bwegie wĩrĩgĩĩro bwawe?

6 Wakristo watiwa-mafuta wanalithamini sana tumaini hilo. Mmoja wao ni Ndugu Frederick Franz, ambaye alisema hivi kutoka moyoni: “Tumaini letu ni jambo la hakika, na litatimizwa kikamili kwa kila mmoja wa wale washiriki 144,000 wa kundi dogo kwa kadiri inayopita hata yale ambayo tumeweza kuwazia.” Baada ya kumtumikia Mungu kwa uaminifu kwa miaka mingi, mwaka wa 1991 Ndugu Franz alisema hivi kwa uhakika: “Hatujapoteza maoni yetu ya thamani ya tumaini hilo. . . . Tunalithamini hata zaidi tunapozidi kulingojea. Ni jambo linalostahili kungojewa, hata ikiwa lingehitaji miaka milioni moja. Ninaliona tumaini letu kuwa lenye thamani kubwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote.”

7-8. Nĩ wĩrĩgĩĩro bũrĩkũ babaingĩ barĩ nabu? (Aroma 8:20, 21)

7 Waabudu wengi wa Yehova leo wana tumaini tofauti. Ni tumaini ambalo Abrahamu alikuwa nalo—uzima wa milele duniani chini ya Ufalme wa Mungu. (Ebr. 11:​8-10, 13) Paulo aliandika kuhusu matokeo yenye utukufu yanayowasubiri wale walio na tumaini hilo. (Soma Waroma 8:​20, 21.) Ulipojifunza kwa mara ya kwanza kuhusu ahadi ya Biblia ya wakati ujao, ni jambo gani lililokuvutia zaidi? Je, ni kwamba siku moja utakuwa mkamilifu, bila mwelekeo wa kutenda dhambi? Au je, ulisisimka ulipojifunza kwamba wapendwa wako waliokufa wataishi tena katika paradiso duniani? Kwa sababu ya hayo, unatazamia mambo mengi “kwa msingi wa tumaini.”

8 Iwe tunatarajia kufurahia uzima wa milele mbinguni au duniani, tuna tumaini lenye utukufu linalotupa sababu ya kushangilia. Na tumaini letu lenye shangwe linaweza kuwa imara hata zaidi. Maneno ya Paulo yanayofuata yanaonyesha jinsi hilo linavyowezekana. Acheni tuchunguze mambo aliyoandika kuhusu tumaini letu. Maneno aliyoandika yatatusaidia kuwa na uhakika zaidi kwamba tumaini letu litaendelea kuwa imara na halitatukatisha tamaa kamwe.

ŨRĨA WĨRĨGĨĨRO BŨKŨRAGA

Wakristo wote wanaweza kutarajia aina fulani ya dhiki (Tazama fungu la 9-10)

9-10. O ta ũrĩa ngerekano ya Paũlũ ĩkwonania, nĩmbi Akristũ boomba kwĩrĩgĩĩra? (Aroma 5:3) (Tega kinya mbica.)

9 Soma Waroma 5:3. Paulo anataja kwamba dhiki inaweza kuhusika katika kuimarisha zaidi tumaini letu. Huenda hilo likatushangaza. Ukweli ni kwamba wafuasi wote wa Kristo wanaweza kutazamia kupata dhiki. Fikiria mfano wa Paulo. Aliwaambia hivi Wathesalonike: “Tulipokuwa pamoja nanyi, tulikuwa tukiwaambia mapema kwamba tutapatwa na dhiki, na imekuwa hivyo.” (1 The. 3:4) Na aliwaandikia hivi Wakorintho: “Hatutaki mkose kujua, akina ndugu, kuhusu dhiki tuliyopata . . . Hatukuwa na uhakika hata kuhusu uhai wetu.”—2 Kor. 1:8; 11:​23-27.

10 Leo pia, Wakristo wanaweza kutazamia kupatwa na dhiki ya aina fulani. (2 Tim. 3:12) Namna gani wewe? Je, umepatwa na dhiki kwa sababu ya kumwamini Yesu na kumfuata? Huenda marafiki na watu wa ukoo wamekudhihaki. Huenda hata wamekutendea kwa ukatili. Je, unapata matatizo kazini kwa sababu ya azimio lako la kuendelea kuwa mnyoofu katika mambo yote? (Ebr. 13:18) Je, umekabili upinzani kutoka kwa serikali kwa sababu ya kuwaambia wengine tumaini lako? Hata tukabili dhiki ya aina gani, Paulo anasema tunapaswa kushangilia. Kwa nini?

11. Nĩkĩ tũbuĩrĩte kũthuura kũmĩĩria magerio jonthe jarĩa tũgacemania najo?

11 Tunaweza kushangilia tunapopatwa na dhiki kwa sababu ya sifa ambayo dhiki inatokeza. Kama Waroma 5:3 inavyosema, “dhiki hutokeza uvumilivu.” Wakristo wote watapatwa na dhiki, hivyo ni lazima Wakristo wote wawe na sifa ya uvumilivu. Tunahitaji kuazimia kuvumilia majaribu yoyote ambayo huenda tukakabili. Tutakapofanya hivyo, ndipo tu tutaona utimizo wa tumaini letu. Hatutaki kuwa kama wale ambao Yesu aliwafikiria alipozungumzia mbegu zilizoanguka kwenye miamba. Mwanzoni walilipokea neno kwa shangwe, hata hivyo “dhiki au mateso” yalipotokea, walikwazika. (Mt. 13:​5, 6, 20, 21) Ni kweli kwamba si rahisi kukabili upinzani au dhiki na hatufurahii mambo hayo, lakini tunapovumilia tunapata manufaa. Kwa njia gani?

12. Nĩatĩa tũgunĩkaga rĩrĩa twomĩĩria magerio?

12 Mwanafunzi Yakobo alieleza manufaa ya kuvumilia majaribu. Aliandika hivi: “Acheni uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili muwe kamili na timamu katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.” (Yak. 1:​2-4) Yakobo anauzungumzia uvumilivu kana kwamba una kazi ya kufanya. Ni kazi gani ambayo inapaswa kukamilishwa na uvumilivu? Unaweza kukusaidia kusitawisha kwa kadiri kubwa zaidi sifa nyingine kama vile subira, imani, na kumtegemea Mungu. Hata hivyo, tunaweza kupata faida nyingine muhimu kupitia uvumilivu.

13-14. Kũmĩĩria kwĩthagĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ, na nĩatĩa bũu bũkũgwatanĩra na wĩrĩgĩĩro? (Aroma 5:4)

13 Soma Waroma 5:4. Paulo anataja kwamba uvumilivu hutokeza “hali yenye kukubaliwa.” Uvumilivu wako hukupatia kibali cha Yehova. Hilo halimaanishi kwamba Yehova anafurahi unapokabili majaribu au matatizo. Wewe ndiye anayekukubali. Uvumilivu wako hutokeza hali yenye kukubaliwa. Baraka bora sana!—Zab. 5:12.

14 Kumbuka kwamba Abrahamu alivumilia majaribu na kufurahia kibali cha Mungu. Yehova alimwona Abrahamu kuwa rafiki Yake na akahesabiwa kuwa mwadilifu. (Mwa. 15:6; Rom. 4:​13, 22) Inaweza kuwa hivyo kwetu pia. Mungu hatoi kibali chake kwa msingi wa kiasi cha kazi tunachofanya katika utumishi wake au mapendeleo tunayofurahia. Anatupatia kibali chake kwa sababu ya kuvumilia kwa uaminifu. Sisi sote tunaweza kuvumilia, licha ya umri, hali, au uwezo wetu. Je, kwa sasa unavumilia kwa uaminifu jaribu fulani? Ikiwa ndivyo, kumbuka kwamba una kibali cha Mungu. Kutambua kwamba tuna kibali cha Mungu kunaweza kuwa na matokeo makubwa sana kwetu. Kunaweza kuimarisha tumaini letu.

WĨRĨGĨĨRO BŨŨRIKU

15. Nĩ ũntũ bũrĩkũ bũngĩ Paũlũ aagwetere, na nĩkĩ bũũmba kũrigaria antũ bamwe?

15 Kama Paulo alivyoeleza, tunapata kibali cha Yehova kwa kuvumilia majaribu kwa mafanikio. Ona jinsi Paulo anavyoendeleza mazungumzo yake: “Nayo hali yenye kukubaliwa, [hutokeza] tumaini, nalo tumaini halikatishi tamaa.” (Rom. 5:​4, 5) Huenda jambo hilo likawachanganya baadhi ya watu. Kwa nini? Kwa sababu kama ilivyoonyeshwa mwanzoni, katika Waroma 5:​2, Paulo alitaja kwamba tayari Wakristo jijini Roma walikuwa na tumaini, “tumaini la utukufu wa Mungu.” Hivyo, huenda mtu akauliza, ‘Ikiwa tayari Wakristo hao walikuwa na tumaini, kwa nini Paulo anaorodhesha tumaini kwenye mazungumzo yake yaliyofuata?’

Tumaini lako la mwanzoni lililokuvutia sana, sasa limekuwa tumaini lenye nguvu zaidi, tumaini la Kikristo lililo imara (Tazama fungu la 16-17)

16. Nĩatĩa muntũ ambagia gũkũria wĩrĩgĩĩro? (Tega kinya mbica.)

16 Tunaweza kuelewa Paulo alimaanisha nini kwa kukumbuka kwamba tumaini ni kitu kinachokua. Kwa mfano: Je, unakumbuka mara ya kwanza uliposikia kuhusu tumaini zuri linalopatikana katika Neno la Mungu? Wakati huo, huenda ulifikiri kwamba wazo la kuishi milele katika dunia paradiso ni jambo la kuwaziwa tu. Hata hivyo, kadiri ulivyomjua vizuri zaidi Yehova na ahadi zilizo katika Biblia, ndivyo ulivyokuwa na uhakika zaidi kwamba tumaini hilo litatimia.

17. Nĩatĩa wĩrĩgĩĩro bwaku bwĩtaga na mbere gũkũra nyuma ya kwirita kĩrĩ Jehova na kũbatithua?

17 Hata baada ya kujiweka wakfu na kubatizwa, tumaini lako liliendelea kukua kadiri ulivyoendelea kujifunza mengi na kukomaa kiroho. (Ebr. 5:13–6:1) Inaelekea umejionea mambo yanayotajwa kwenye Waroma 5:​2-4. Ulikabili dhiki mbalimbali, lakini ulivumilia na kuhisi kibali cha Mungu. Ukiwa na uhakika kwamba una kibali cha Mungu, sasa una sababu kubwa hata zaidi ya kutarajia kupokea mambo aliyoahidi. Tumaini lako limekuwa imara zaidi kuliko mwanzoni. Limekuwa halisi zaidi kwako, linakugusa kibinafsi. Linakuchochea zaidi, linakuongoza katika kila sehemu ya maisha yako na kubadili jinsi unavyowatendea watu wa familia yako, jinsi unavyofanya maamuzi, na hata jinsi unavyotumia wakati wako.

18. Nĩ ũrikithia bũrĩkũ Jehova aejanĩte?

18 Mtume Paulo anataja jambo lingine muhimu sana kuhusu tumaini tunalokuwa nalo baada ya kupata kibali cha Mungu. Anakuhakikishia kwamba tumaini lako litatimizwa. Kwa nini unaweza kuwa na uhakika huo? Paulo anawatajia Wakristo uhakikisho huu kutoka kwa Mungu: “Tumaini halikatishi tamaa; kwa sababu upendo wa Mungu umemiminwa ndani ya mioyo yetu kupitia roho takatifu, ambayo tulipewa.” (Rom. 5:5) Una kila sababu ya kuwa na uhakika na tumaini hilo, yaani, tumaini lako.

19. Nĩ ũmma bũrĩkũ ũũmba kwĩthĩrwa nabu bwegie wĩrĩgĩĩro bwaku?

19 Tafakari kuhusu ahadi ya Yehova kwa Abrahamu na jinsi alivyokubaliwa naye, na alivyomwona kuwa rafiki Yake. Tumaini la Abrahamu lilitimia. Biblia inasema hivi: “Baada ya Abrahamu kuonyesha subira, aliipata ahadi hiyo.” (Ebr. 6:15; 11:​9, 18; Rom. 4:​20-22) Kwa hakika hakukatishwa tamaa. Unaweza kuwa na uhakika huohuo kwamba ikiwa utaendelea kuwa mwaminifu, tumaini lako litathawabishwa. Tumaini lako ni halisi; ni sababu ya kushangilia, si ya kukatishwa tamaa! (Rom. 12:12) Paulo aliandika hivi: “Mungu anayetoa tumaini na awajaze ninyi shangwe yote na amani kwa kumtegemea, ili tumaini lenu liongezeke kwa nguvu za roho takatifu.”—Rom. 15:13.

RWĨMBO 139 Wazia Wakati Vitu Vyote Vitakuwa Vipya

a Katika makala hii, tutachunguza tumaini letu la Kikristo linatia ndani mambo gani na kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba litatimia. Waroma sura ya 5 itatusaidia kuona jinsi tumaini tulilo nalo sasa linavyotofautiana na tumaini tulilokuwa nalo tulipoanza kujifunza kweli.