Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 50

Wĩtĩkio na Mathithio Biomba Gũtongeeria Kĩrĩ Wagĩru

Wĩtĩkio na Mathithio Biomba Gũtongeeria Kĩrĩ Wagĩru

‘Rũmagĩĩra wĩtĩkio bũrĩa Iburahimu [ĩthe wetũ] aarĩ nabu.’—AR. 4:12.

RWĨMBO 119 Lazima Tuwe na Imani

MUHTASARI a

1. Rĩrĩa tũkũthũgaanĩria wĩtĩkio bwa Iburahimu, nĩ biũria birĩkũ tũũmba gũciũria?

 INGAWA watu wengi wamesikia kuhusu Abrahamu, hawajui mengi kumhusu. Hata hivyo, unajua mambo mengi kumhusu Abrahamu. Kwa mfano, unajua kwamba Biblia inasema Abrahamu alikuwa “baba ya wale wote walio na imani.” (Rom. 4:11) Hata hivyo, huenda ukajiuliza, ‘Je, ninaweza kutembea katika hatua za Abrahamu na kuwa na imani kama ile aliyokuwa nayo?’ Ndiyo, unaweza.

2. Nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi gũcũnkũũna ngerekano ya Iburahimu? (Jakubu 2:​22, 23)

2 Njia moja tunayoweza kusitawisha imani kama ya Abrahamu ni kwa kujifunza kuhusu mfano wake. Sikuzote Abrahamu alifanya mambo ambayo Mungu alimwagiza. Alihamia nchi ya mbali na nyumbani kwake, aliishi kwenye mahema kwa miaka mingi, na alikuwa tayari kumtoa dhabihu mwana wake mpendwa, Isaka. Matendo hayo yalionyesha ana imani yenye nguvu. Imani na matendo ya Abrahamu yalifanya apate kibali cha Mungu na kuwa rafiki yake. (Soma Yakobo 2:​22, 23.) Yehova anataka—wewe pia—ufurahie baraka hizo. Kwa sababu hiyo, aliwaongoza waandikaji wa Biblia Paulo na Yakobo, warejelee mfano wa Abrahamu. Acheni tuchunguze mfano wake, kama ulivyozungumziwa kwenye Waroma sura ya 4 na Yakobo sura ya 2. Sura hizo mbili zinazungumzia jambo muhimu kumhusu Abrahamu.

3. Nĩ maandĩko jarĩkũ Paũlũ na Jakubu baagwetere?

3 Paulo na Yakobo walinukuu andiko la Mwanzo 15:​6, linalosema: “[Abrahamu] akawa na imani katika Yehova, Naye akamhesabu kuwa mwadilifu.” Uadilifu unarejelea hali ambayo mtu anaonwa na Mungu kuwa mwenye kukubalika, na hata asiye na hatia. Inastaajabisha sana kwamba mwanadamu mwenye dhambi na asiye mkamilifu anaweza kuonwa na Mungu kuwa hana hatia! Bila shaka, ungependa iwe hivyo kwako pia, na hilo linawezekana. Sasa tutajifunza kwa nini Yehova alimwita Abrahamu mwadilifu, na mambo tunayopaswa kufanya ili tuitwe waadilifu.

WĨTĨKIO NĨBWENDEKAGA KĨRĨ KWĨTHĨRWA NA WAGĨRU

4. Nĩmbi birigagĩĩria antũ kwaa babagĩru?

4 Katika barua yake kwa Waroma, Paulo alisema kwamba wanadamu wote ni watenda dhambi. (Rom. 3:23) Basi, inawezekanaje kwa mtu kuonwa kuwa mwadilifu au asiye na hatia na hivyo kupata kibali cha Mungu? Ili kuwasaidia Wakristo wote wanyoofu kujibu swali hilo, Paulo alitumia mfano wa Abrahamu.

5. Nĩ mũsingi jũrĩkũ Jehova aatumĩĩre kuuga Iburahimu nĩ aarĩ ũmwagĩru? (Aroma 4:​2-4)

5 Yehova alimtangaza Abrahamu kuwa mwadilifu alipokuwa akiishi katika nchi ya Kanaani. Kwa nini Yehova aliweza kumtangaza Abrahamu kuwa mwadilifu? Je, ni kwa sababu Abrahamu alishika kikamili Sheria ya Musa? La hasha. (Rom. 4:13) Taifa la Israeli lilipewa Sheria hiyo zaidi ya miaka 400 baada ya Mungu kumtangaza Abrahamu kuwa mwadilifu. Basi, ni kwa msingi gani Mungu alimtangaza Abrahamu kuwa mwadilifu? Kupitia fadhili Zake zisizostahiliwa, Yehova alimtangaza Abrahamu kuwa mwadilifu kwa sababu ya imani yake.—Soma Waroma 4:​2-4.

6. Nĩatĩa Jehova aethagia muntũ mwĩyia ũmwagĩru?

6 Paulo alifafanua zaidi kwamba mtu anapoweka imani katika Mungu, “imani yake inahesabiwa kuwa ni uadilifu.” (Rom. 4:5) Paulo aliongeza hivi: “Kama vile Daudi pia anavyosema kuhusu furaha ya mtu ambaye Mungu humhesabu kuwa mwadilifu bila matendo: ‘Wenye furaha ni wale ambao matendo yao ya kuasi sheria yamesamehewa na ambao dhambi zao zimefunikwa; mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hatahesabu dhambi yake kamwe.’” (Rom. 4:​6-8; Zab. 32:​1, 2) Mungu anasamehe au kufunika dhambi za wale wanaoweka imani kwake. Anawasamehe kabisa na hatahesabu dhambi zao kamwe. Yehova anawaona watu hao kuwa hawana hatia na waadilifu kwa msingi wa imani yao.

7. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ antũ etĩkua barĩa baathathayia Mũrungu baarĩ babagĩru?

7 Ingawa Abrahamu, Daudi, na waabudu wengine waaminifu wa Mungu walitangazwa kuwa waadilifu, bado walikuwa watenda dhambi wasio wakamilifu. Lakini kwa sababu ya imani yao, Mungu aliwaona kuwa wasio na hatia hasa alipowalinganisha na wale ambao hawakuwa na imani kwake. (Efe. 2:12) Kama Paulo anavyoeleza waziwazi kwenye barua yake, ni lazima mtu awe na imani ili kuwa na uhusiano wa kibinafsi pamoja na Mungu. Ndivyo ilivyokuwa kwa Abrahamu na Daudi, na ni hivyo kwetu pia.

KŨRĨNA NGWATANĨRO ĨRĨKŨ YA WĨTĨKIO NA MATHITHIO?

8-9. Nĩ mantũ jarĩkũ antũ bamwe batĩciũkagĩrwa nĩjo bwega jegie mantũ jarĩa jaandĩki nĩ Paũlũ na Jakubu, na nĩkĩ?

8 Kwa karne nyingi, uhusiano kati ya imani na matendo umekuwa ukijadiliwa sana katika dini zinazodai kuwa za Kikristo. Baadhi ya viongozi wa kidini wanafundisha kwamba jambo pekee unalohitaji kufanya ili uokolewe ni kumwamini Bwana Yesu Kristo. Huenda umewasikia wakisema, “Mkubali Yesu na uokolewe.” Huenda viongozi hao wa kidini wakanukuu maneno haya ya Paulo: “Mungu humhesabu [mtu] kuwa mwadilifu bila matendo.” (Rom. 4:6) Hata hivyo, wengine wanasema kwamba unaweza “kujiokoa mwenyewe” kwa kutembelea maeneo yanayoonwa na kanisa kuwa matakatifu na kufanya matendo mema. Huenda wakanukuu maneno ya Yakobo 2:24 ambayo yanasema: “Mtu hutangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo, na si kwa imani peke yake.”

9 Kwa sababu ya maoni hayo tofauti, baadhi ya waandishi wa kidini wamefikia mkataa kwamba Paulo na Yakobo hawakukubaliana kuhusu suala la imani na matendo. Huenda viongozi wa kidini wakadai kuwa Paulo aliamini kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu kwa imani bila matendo, lakini Yakobo alifundisha kwamba matendo ni muhimu ili kuwa na kibali cha Mungu. Profesa wa elimu ya kidini anasema hivi: “Yakobo hakuelewa nia ya Paulo ya kusisitiza kwamba [kutangazwa kuwa mwadilifu] ni kupitia imani na si kupitia matendo.” Lakini Yehova alimwongoza Paulo na Yakobo kuandika mambo hayo. (2 Tim. 3:16) Hivyo, lazima kuna njia rahisi ya kupatanisha maneno yao. Njia hiyo ni kwa kuchunguza muktadha wa maneno yao.

Paulo alikazia kwa Wakristo Wayahudi walio Roma kwamba imani ilikuwa muhimu, si matendo ya Sheria (Tazama fungu la 10) b

10. Nĩ ‘mathithio’ jarĩkũ Paũlũ monomono aarĩĩragia? (Aroma 3:​21, 28) (Tega kinya mbica.)

10 Paulo alizungumzia “matendo” gani katika Waroma sura ya 3 na 4? Kimsingi alikuwa akirejelea “matendo ya sheria,” yaani, sheria ya Musa, iliyotolewa kwenye Mlima Sinai. (Soma Waroma 3:​21, 28.) Inaonekana kwamba katika siku za Paulo, haikuwa rahisi kwa baadhi ya Wakristo Wayahudi, kuamini kwamba Sheria ya Musa na matendo yaliyopaswa kufanywa kulingana na Sheria hiyo yalikuwa yameondolewa. Hivyo, Paulo alitumia mfano wa Abrahamu kuthibitisha kwamba msimamo wa uadilifu mbele za Mungu hautokani na “matendo ya sheria.” Unatokana na kuwa na imani. Kujua jambo hilo kunatia moyo kwa sababu kunatupatia uhakika kwamba tunaweza kuwa na msimamo mzuri mbele za Mungu. Kunamaanisha kwamba tunaweza kusitawisha imani katika Mungu na Kristo, jambo ambalo linaweza kutupatia kibali cha Mungu.

Yakobo aliwahimiza Wakristo kuonyesha imani yao kwa “matendo,” kama vile kufanya matendo ya fadhili bila ubaguzi (Tazama fungu la 11-12) c

11. Nĩ ‘mathithio’ jarĩkũ Jakubu aagwetaga?

11 Kwa upande mwingine, “matendo” yanayozungumziwa kwenye Yakobo sura ya 2 si “matendo ya sheria” yaliyotajwa na Paulo. Yakobo anarejelea matendo, au mambo, ambayo Wakristo hufanya kila siku maishani. Matendo hayo yanaonyesha ikiwa Mkristo ana imani ya kweli katika Mungu au la. Fikiria mifano miwili ambayo Yakobo alitumia.

12. Nĩatĩa Jakubu aatarĩĩrie ngwatanĩro yegie wĩtĩkio na mathithio? (Tega kinya mbica.)

12 Katika mfano wa kwanza, Yakobo anazungumzia umuhimu wa Wakristo kutokuwa na ubaguzi wanaposhughulika na wengine. Alifafanua jambo hilo kwa kutumia kisa cha mwanamume aliyemwonyesha upendeleo mtu tajiri, lakini alimdharau mtu maskini. Yakobo alionyesha kwamba huenda mtu huyo akadai kwamba ana imani, lakini matendo yake hayathibitishi hilo. (Yak. 2:​1-5, 9) Katika mfano wake wa pili, Yakobo anamtaja mtu aliyemwona ‘ndugu au dada asiye na nguo au chakula’ lakini hakumsaidia. Hata ikiwa mtu huyo alidai kwamba ana imani, hakuionyesha kwa matendo; hivyo, imani yake ni bure. Kama Yakobo alivyoandika, “imani bila matendo imekufa.”—Yak. 2:​14-17.

13. Nĩatĩa Jakubu aataarĩĩrie ũntũ bwegie wĩtĩkio bũrĩna mathithio? (Jakubu 2:​25, 26)

13 Yakobo alimrejelea Rahabu kuwa mfano mzuri wa mtu aliyeonyesha imani kwa matendo. (Soma Yakobo 2:​25, 26.) Rahabu alikuwa amesikia kumhusu Yehova na alitambua kwamba alikuwa akiwategemeza Waisraeli. (Yos. 2:​9-11) Rahabu alionyesha imani yake kwa matendo—aliwalinda wapelelezi wawili Waisraeli, maisha yao yalipokuwa hatarini. Kwa sababu hiyo, mwanamke huyo asiye Mwisraeli ambaye hakuwa mkamilifu, alitangazwa kuwa mwadilifu kama Abrahamu. Mfano alioweka unakazia umuhimu wa kuonyesha imani kwa matendo.

14. Nĩatĩa mantũ jarĩa Paũlũ na Jakubu baandĩkĩre jakũgwatanĩra?

14 Waandikaji hao wawili wa Biblia, Paulo na Yakobo, walikuwa wakielezea suala la imani na matendo kwa njia mbili tofauti. Paulo alikuwa akiwaambia Wakristo Wayahudi kwamba hawangeweza kupata kibali cha Yehova kwa kufanya tu matendo ya Sheria ya Musa. Yakobo alikuwa akikazia uhitaji wa Wakristo wote wa kuonyesha imani yao kwa kuwafanyia wengine mema.

Je, imani yako inakuchochea kufanya matendo ambayo Yehova anayakubali? (Tazama fungu la 15)

15. Nĩ na njĩra irĩkũ imwe tũũmba kwonania wĩtĩkio gũkũrũkĩĩra mathithio jeetũ? (Tega kinya mbica.)

15 Yehova hasemi kwamba ikiwa tunataka kutangazwa kuwa waadilifu ni lazima tufanye mambo yaleyale ambayo Abrahamu alifanya. Kwa kweli, kuna njia nyingi ambazo tunaweza kuonyesha imani kwa matendo yetu. Tunaweza kuwakaribisha wapya kutanikoni, kuwasaidia ndugu na dada ambao kwa kweli wana uhitaji, na kuwafanyia mema watu wa familia yetu; mambo hayo yote Mungu atayakubali na kuyabariki. (Rom. 15:7; 1 Tim. 5:​4, 8; 1 Yoh. 3:18) Kuhubiri kwa bidii habari njema ni mojawapo ya matendo mema muhimu zaidi yanayoonyesha kwamba tuna imani. (1 Tim. 4:16) Sisi sote tunaweza kuonyesha kwa matendo yetu kuwa tuna imani kwamba ahadi za Yehova zitatimia na kwamba njia zake ni bora. Na tukifanya hivyo, tunaweza kuwa na uhakika kabisa kwamba Mungu atatuona kuwa waadilifu, na atatuita rafiki zake.

NĨTŨKŨBATARA WĨRĨGĨĨRO NĨKENDA TWĨTHĨRWA NA WĨTĨKIO

16. Kwarĩ na ngwatanĩro ĩrĩkũ kĩrĩ wĩrĩgĩĩro na wĩtĩkio bwa Iburahimu?

16 Waroma sura ya 4 inaonyesha somo lingine muhimu tunaloweza kujifunza kutoka kwa Abrahamu: umuhimu wa tumaini. Yehova aliahidi kwamba kupitia Abrahamu “mataifa mengi” yangebarikiwa. Abrahamu alikuwa na tumaini zuri sana! (Mwa. 12:3; 15:5; 17:4; Rom. 4:17) Lakini hata Abrahamu alipokuwa na umri wa miaka 100 na Sara miaka 90, mwana aliyeahidiwa hakuwa amezaliwa. Kwa maoni ya wanadamu, ilionekana kwamba haiwezekani kwa Abrahamu na Sara kuwa na mwana. Hilo lilikuwa jaribu kubwa kwa Abrahamu. “Lakini kwa kutegemea tumaini, alikuwa na imani kwamba angekuwa baba ya mataifa mengi.” (Rom. 4:​18, 19) Na hatimaye, tumaini la Abrahamu lilitimia. Alikuja kuwa baba ya Isaka, mwana aliyemsubiri kwa muda mrefu.—Rom. 4:​20-22.

17. Ta acoore ba Mũrungu, nĩatĩa tũmenyaga atĩ kwombĩka tũkoonwa tũrĩ babagĩru?

17 Tunaweza kuwa na kibali cha Mungu, kuhesabiwa kuwa waadilifu, na kuwa rafiki za Mungu kama Abrahamu. Hilo ndilo jambo ambalo Paulo alikazia alipoandika hivi: “Maneno ‘ilihesabiwa kwake’ hayakuandikwa kwa ajili [ya Abrahamu] tu, bali pia kwa ajili yetu ambao itahesabiwa, kwa sababu tunamwamini Yeye aliyemfufua Yesu.” (Rom. 4:​23, 24) Kama Abrahamu, tunahitaji kuwa na imani, matendo pamoja na tumaini. Paulo anaendelea kuzungumzia tumaini letu katika Waroma sura ya 5, jambo ambalo tutazungumzia katika makala inayofuata.

RWĨMBO 28 Kuwa Rafiki ya Yehova

a Tunataka kupata kibali cha Mungu na atuone kuwa waadilifu. Kwa kutumia maneno ya Paulo na Yakobo, makala hii itazungumzia jinsi hilo linavyowezekana na kwa nini tunahitaji kuwa na imani na pia matendo ili tupate kibali cha Yehova.

b MAELEZO YA PICHA: Paulo aliwahimiza Wakristo Wayahudi wakazie imani, si “matendo ya sheria,” kama vile kuvaa vazi lenye uzi wa bluu, kusherehekea Pasaka, na desturi za kunawa mikono.

c MAELEZO YA PICHA: Yakobo aliwatia moyo Wakristo waonyeshe imani kwa kuwafanyia wengine mema, kama vile kuwasaidia maskini.