Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 8

RWĨMBO 123 Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi kwa Ushikamanifu

Ĩta na Mbere Kũthingata Ũtongeeria bwa Jehova

Ĩta na Mbere Kũthingata Ũtongeeria bwa Jehova

[Ni Jehova], nĩni . . . ngũtongagĩĩria.’ISA. 48:17.

JAMBO KUU

Makala hii itatusaidia kuona jinsi Yehova anavyowaongoza watu wake leo na baraka tunazofurahia tunapofuata mwongozo wake.

1. Tarĩĩria nĩkĩ tũbuĩrĩte kũthingata Jehova arĩ mũtongeeria weetũ.

 WAZIA kwamba umepotea kwenye msitu. Uko katika hali hatari: kuna wanyama pori, wadudu wanaoambukiza magonjwa, mimea yenye sumu, na maeneo yenye mawemawe. Utathamini sana kuwa na mwongozaji mwenye uzoefu anayejua maeneo yenye hatari na jinsi ya kukuepusha nayo! Ulimwengu huu ni kama msitu huo. Umejaa hatari ambazo hasa zinahatarisha hali yetu ya kiroho. Lakini tuna mwongozaji mkamilifu—Yehova. Anatuondoa mbali na hatari na kutuongoza ili tufike mwisho wa safari yetu, yaani, kwenye uzima wa milele katika ulimwengu mpya.

2. Nĩatĩa Jehova atũtongagĩĩria?

2 Yehova anatuongozaje? Kwanza kabisa, anatumia Neno lake, Biblia. Pia, anatumia wawakilishi wake duniani. Kwa mfano, anamtumia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ili kuandaa chakula cha kiroho kinachotusaidia kufanya maamuzi kwa hekima. (Mt. 24:45) Yehova pia anatumia wanaume wengine wenye uwezo kutuongoza. Kwa mfano, waangalizi wa mzunguko na wazee wa kutaniko wanatutia moyo na kutupatia mwongozo unaotusaidia kukabiliana na nyakati ngumu. Tunashukuru sana kwa mwongozo wenye kutegemeka tunaopata katika siku hizi za mwisho zilizo hatari! Mwongozo huo unatusaidia kuendelea kuwa na kibali cha Yehova na kubaki katika barabara ya uzima.

3. Nĩmbi tũkaarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

3 Ingawa hivyo, huenda pindi fulani tukaona ni vigumu kufuata mwongozo wa Yehova, hasa ikiwa tunaupata kupitia wanaume wasio wakamilifu. Kwa nini? Kwa sababu ushauri wao huenda usifaane na mapendezi yetu. Au huenda tukahisi kwamba mwongozo tunaopokea si wa hekima na kufikia mkataa kwamba haukutoka kwa Yehova. Katika pindi hizo, tunahitaji kuwa na uhakika kwamba Yehova anawaongoza watu wake na kwamba kufuata mwongozo wake huleta baraka. Ili kutusaidia kuimarisha uhakika wetu, tutachunguza katika makala hii (1) jinsi Yehova alivyowaongoza watu wake katika nyakati za Biblia, (2) jinsi anavyotuongoza leo, na (3) jinsi tunavyonufaika tunapoendelea kufuata mwongozo wake.

Tangu nyakati za kale hadi leo, Yehova ametumia wawakilishi wake duniani kuwaongoza watu wake (Tazama fungu la 3)



ŨRĨA JEHOVA AATONGERERIE MŨGONGO JWA ISIRAELI

4-5. Nĩatĩa Jehova oonanĩrie atĩ naatumagĩra Musa gũtongeeria Aisiraeli? (Tega mbica karatacine ka mbere.)

4 Yehova alimweka rasmi Musa awaongoze Waisraeli walipokuwa wakiondoka Misri. Naye aliwapatia Waisraeli uthibitisho ulioonekana wazi kwamba alikuwa akiwaongoza kupitia Musa. Kwa mfano, Yehova aliwapatia nguzo ya wingu mchana na nguzo ya moto usiku. (Kut. 13:21) Musa alifuata nguzo hiyo ambayo ilimwongoza yeye na Waisraeli hadi kwenye Bahari Nyekundu. Watu waliingiwa na hofu walipofikiri kwamba hawana pa kukimbilia, wakiwa kati ya bahari na jeshi la Wamisri lililokuwa likiwafuatilia. Walifikia mkataa kwamba Musa alikuwa amekosea alipowaleta kwenye Bahari Nyekundu. Lakini halikuwa kosa. Kupitia Musa, Yehova alikuwa amewaongoza kimakusudi watu wake wafike mahali hapo. (Kut. 14:2) Kisha Mungu akawakomboa kwa njia yenye kustaajabisha sana.—Kut. 14:​26-28.

Musa alitegemea nguzo ya wingu kuwaongoza watu wa Mungu nyikani (Tazama fungu la 4-5)



5 Kwa miaka 40 baada ya hapo, Musa aliendelea kuitegemea nguzo ya wingu ili kuwaongoza watu wa Mungu nyikani. a Kwa kipindi fulani, Yehova aliiweka nguzo hiyo juu ya hema la Musa, ambapo Waisraeli wote wangeiona. (Kut. 33:​7, 9, 10) Yehova alizungumza na Musa kutoka katika nguzo hiyo, naye Musa aliwasilisha maagizo ya Yehova kwa watu. (Zab. 99:7) Waisraeli walikuwa na uthibitisho wa kutosha kwamba Yehova alikuwa akimtumia Musa ili kuwaongoza.

Musa akiwa na Yoshua ambaye angemkabidhi majukumu yake (Tazama fungu la 5, 7)



6. Nĩatĩa Aisiraeli beetĩkĩrĩĩrie ũtongeeria bwa Jehova? (Gutara 14:​2, 10, 11)

6 Kwa kusikitisha, Waisraeli wengi walikataa uthibitisho ulio wazi kwamba Yehova alikuwa akimtumia Musa akiwa mwakilishi Wake. (Soma Hesabu 14:​2, 10, 11.) Tena na tena, walikataa kukubali kwamba Yehova alikuwa akimtumia Musa kuwaongoza. Matokeo ni kwamba kizazi hicho cha Waisraeli kilizuiliwa kuingia katika Nchi ya Ahadi.—Hes. 14:30.

7. Gweta ngerekano cia barĩa baathingatĩre ũtongeeria bwa Jehova. (Gutara 14:24) (Tega kinya mbica.)

7 Hata hivyo, baadhi ya Waisraeli walifuata mwongozo wa Yehova. Kwa mfano, Yehova alisema hivi: “Kalebu . . . aliendelea kunifuata kwa moyo wote.” (Soma Hesabu 14:24.) Mungu alimthawabisha Kalebu, na hata alimpatia eneo alilochagua Kalebu mwenyewe katika nchi ya Kanaani. (Yos. 14:​12-14) Pia, Waisraeli walioruhusiwa kuingia katika Nchi ya Ahadi waliweka mfano mzuri wa kufuata mwongozo wa Yehova. Yoshua alipochukua nafasi ya Musa akiwa kiongozi aliyewekwa rasmi, Waisraeli “wakamheshimu sana sikuzote za maisha yake.” (Yos. 4:14) Matokeo ni kwamba Yehova aliwabariki kwa kuwaingiza katika nchi aliyowaahidi.—Yos. 21:​43, 44.

8. Tarĩĩria ũrĩa Jehova aatongagĩĩria antũ baawe ĩgiitene rĩa anene ba Isiraeli. (Tega kinya mbica.)

8 Miaka mingi baadaye, Yehova aliwainua waamuzi ili wawaongoze watu wake. Kisha katika nyakati za wafalme, Yehova aliwaweka rasmi manabii ili wawaongoze watu wake. Wafalme waliokuwa waaminifu walitii ushauri wa manabii. Kwa mfano, kwa unyenyekevu Mfalme Daudi alikubali kurekebishwa na nabii Nathani. (2 Sam. 12:​7, 13; 1 Nya. 17:​3, 4) Mfalme Yehoshafati alimtegemea nabii Yahazieli ili kupata mwongozo na aliwatia moyo watu wa Yuda wawe “na imani katika manabii [wa Mungu].” (2 Nya. 20:​14, 15, 20) Mfalme Hezekia alipokabili taabu, alimwomba msaada nabii Isaya. (Isa. 37:​1-6) Kila mara wafalme walipofuata mwongozo wa Yehova, walibarikiwa na taifa lililindwa. (2 Nya. 20:​29, 30; 32:22) Watu wote walipaswa kuona wazi kwamba Yehova alikuwa akitumia manabii ili kuongoza watu wake. Hata hivyo, wafalme wengi, kutia ndani watu waliwakataa manabii wa Yehova.—Yer. 35:​12-15.

Mfalme Hezekia na nabii Isaya (Tazama fungu la 8)



ŨRĨA JEHOVA AATONGERERIE AKRISTŨ BA KARINE YA MBERE

9. Nĩ baaũ Jehova aatumagĩra gũtongeeria Akristũ ba karine ya mbere? (Tega kinya mbica.)

9 Katika karne ya kwanza W.K., Yehova alianzisha kutaniko la Kikristo. Aliwaongozaje Wakristo hao wa mapema? Alimweka rasmi Yesu kuwa kichwa cha kutaniko. (Efe. 5:23) Lakini Yesu hakumwongoza kila mwanafunzi kibinafsi. Aliwatumia mitume na wanaume wazee huko Yerusalemu kuongoza. (Mdo. 15:​1, 2) Pia, wazee waliwekwa rasmi kuyaongoza makutaniko.—1 The. 5:12; Tito 1:5.

Mitume na wanaume wazee huko Yerusalemu (Tazama fungu la 9)



10. (a) Akristũ bamwe ba karine ya mbere beetĩkĩrĩĩrie atĩa ũtongeeria bũrĩa baaerwe? (Mathithio 15:​30, 31) (b) Nĩkĩ antũ bamwe karaaja baareganaga na barĩa Jehova aathuurĩte? (Tega kathandũkũ “ Kwa Nini Baadhi ya Watu Wamekataa Uthibitisho Ulio Wazi?”)

10 Wakristo wa karne ya kwanza waliitikiaje? Wengi wao walifurahi kufuata maagizo waliyopokea. Isitoshe, “wakashangilia kwa sababu ya kutiwa moyo.” (Soma Matendo 15:​30, 31.) Hata hivyo, Yehova amekuwa akiwaongoza jinsi gani watu wake katika nyakati za karibuni zaidi?

ŨRĨA JEHOVA ATŨTONGAGĨĨRIA NTUKŨNE CIETŨ

11. Ejana ngerekano ĩkwonania ũrĩa Jehova ethĩrĩtwe agĩtongeeria antũ baawe ntukũne cietũ.

11 Yehova anaendelea kuwaongoza watu wake leo. Amekuwa akifanya hivyo kupitia Neno lake na Mwana wake, ambaye ni kichwa cha kutaniko. Je, tunajionea uthibitisho kwamba katika nyakati zetu Mungu ameendelea kutumia wawakilishi wake hapa duniani? Ndiyo. Kwa mfano, fikiria mambo fulani yaliyotukia mwishoni mwa miaka ya 1800. Charles Taze Russell na wenzake walianza kuelewa kwamba mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka muhimu inapohusu kusimamishwa kwa Ufalme wa Mungu. (Dan. 4:​25, 26) Walitegemea unabii wa Biblia, ili kufikia mkataa huo. Je, Yehova alikuwa akiongoza utafiti wao katika Biblia? Ni wazi alikuwa akifanya hivyo. Mambo yaliyotukia ulimwenguni mwaka wa 1914 yalithibitisha kwamba Ufalme wa Mungu ulikuwa umeanza kutawala. Vita vya Kwanza vya Ulimwengu vilianza, na kufuatiwa na magonjwa, matetemeko ya ardhi, na upungufu wa chakula. (Luka 21:​10, 11) Kwa kweli Yehova alikuwa akiwatumia wanaume hao wanyoofu ili kuwasaidia watu wake.

12-13. Nĩ mĩbango ĩrĩkũ yaathithĩrue ngũgĩ ya gũtũmĩĩria na kũritana ĩrĩ kwongereka ĩgiita rĩa Ndũa ya Ijĩrĩ ya Kĩmanthĩgũrũ?

12 Pia, fikiria mambo yaliyotukia wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu. Baada ya kuchunguza Ufunuo 17:​8, akina ndugu wanaoongoza walio kwenye makao makuu ya ulimwenguni pote walitambua kwamba vita hivyo visingeongoza kwenye Har–​Magedoni, badala yake kungekuwa na kipindi cha amani ya kadiri ambacho kingetokeza fursa za kupanua kazi yetu ya kuhubiri. Hivyo, ingawa wakati huo uamuzi huo haukuonekana kuwa wenye hekima, shule iliyoitwa Chuo cha Biblia cha Gileadi cha Watchtower ilianzishwa na tengenezo la Yehova ili kuwazoeza wamishonari kuhubiri na kufundisha katika nchi mbalimbali kotekote duniani. Wamishonari walitumwa hata wakati wa kipindi cha vita. Pia, mtumwa mwaminifu alipanga kuwe na Mafunzo ya Huduma ya Kitheokrasi b ili kuwazoeza wote kutanikoni kuwa wahubiri na walimu wazuri zaidi. Kwa njia hizo, watu wa Mungu walikuwa wakitayarishwa kwa ajili ya kazi ambayo bado ilihitaji kufanywa.

13 Leo, tunaona wazi kwamba Yehova alikuwa akiwaongoza watu wake katika kipindi hicho kigumu. Tangu Vita vya Pili vya Ulimwengu, watu wa Yehova katika nchi nyingi wamefurahia amani ya kadiri na uhuru wanapoendelea na kazi ya kuhubiri. Isitoshe, kazi hiyo imekuwa na matokeo makubwa.

14.Nĩkĩ tũũmba gwĩtĩkia ũtongeeria bũrĩa buumaga kĩrĩ ũthuranĩri bwa Jehova na kĩrĩ akũrũ ba biũthũrano? (Kugwurirwa 2:1) (Tega kinya mbica.)

14 Leo, washiriki wa Baraza Linaloongoza wanaendelea kuutegemea mwongozo wa Kristo. Wangependa maagizo wanayowapatia akina ndugu yapatane na maoni ya Yehova na Yesu. Na wanawatumia waangalizi wa mzunguko na wazee ili kuyapatia makutaniko mwongozo. c Wazee watiwa-mafuta wako kwenye ‘mkono wa kuume’ wa Kristo. (Soma Ufunuo 2:1.) Bila shaka, wazee hao si wakamilifu na wanafanya makosa. Pindi fulani Musa na Yoshua walifanya makosa, kama ilivyokuwa kwa mitume pia. (Hes. 20:12; Yos. 9:​14, 15; Rom. 3:23) Bado Kristo anamwongoza kwa makini mtumwa mwaminifu na wazee waliowekwa rasmi, na ataendelea kufanya hivyo “sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mt. 28:20) Hivyo, tuna kila sababu ya kutumaini mwongozo ambao anatupatia kupitia wale aliowaweka rasmi ili kuongoza.

Baraza Linaloongoza leo (Tazama fungu la 14)



NĨ TŨGUNĨKAGA RĨRĨA TWETA NA MBERE KŨTHINGATA ŨTONGEERIA BWA JEHOVA

15-16. Nĩmbi ũũmba kwiritana kuumania na ngerekano cia barĩa baathingatĩre ũtongeeria bwa Jehova?

15 Tunapoendelea kufuata mwongozo wa Yehova, tunapata baraka hata sasa. Kwa mfano, Andy na Robyn walitumia ushauri wa mtumwa mwaminifu wa kurahisisha maisha yao. (Mt. 6:22) Matokeo ni kwamba waliweza kujitolea kufanya kazi kwenye miradi ya ujenzi ya kitheokrasi. Robyn anasema hivi: “Tumeishi kwenye nyumba ndogo sana, mara nyingi hazikuwa na eneo la kupikia. Pia, nilihitaji kuuza vifaa vyangu vingi vya kupigia picha, kazi ambayo niliipenda sana. Nililia nilipoviuza. Lakini kama Sara, mke wa Abrahamu, niliazimia kutazama mbele, si nyuma.” (Ebr. 11:15) Wenzi hao walinufaikaje? Robyn anasema hivi: “Tumeridhika sana kwa sababu tunajua kwamba tunampa Yehova kila kitu tulicho nacho. Tunapofanya kazi kwenye migawo ya kitheokrasi, tunapata kionjo cha jinsi maisha yatakavyokuwa kwenye ulimwengu mpya.” Andy anakubaliana na maneno hayo, anasema: “Tuna furaha kwa sababu tunatumia wakati na nguvu zetu zote kuunga mkono Ufalme.”

16 Tunanufaika kwa njia gani nyingine tunapoendelea kufuata mwongozo wa Yehova? Baada ya kumaliza shule ya sekondari, Marcia alifuata ushauri wa kuingia katika utumishi wa Yehova akiwa painia. (Mt. 6:33; Rom. 12:11) Anasema hivi: “Nilipata ufadhili wa kulipiwa ada ya chuo kikuu kwa miaka minne. Lakini nilitaka kufuatia malengo ya kiroho. Hivyo, nilichagua kwenda kwenye shule ya ufundi ili kujifunza kazi ambayo ingenitegemeza ninapofanya huduma yangu. Huo ulikuwa mojawapo ya uamuzi bora zaidi niliowahi kufanya. Sasa ninafurahia kuwa painia wa kawaida, na ratiba yangu ya kazi inaniruhusu kufanya kazi Betheli nikiwa mjitoleaji anayetoka nyumbani na kufurahia mapendeleo mengine ya pekee.”

17. Nĩ itharimo bingĩ birĩkũ twonaga rĩrĩa tweta na mbere kũthingata ũtongeeria bwa Jehova? (Isaya 48:​17, 18)

17 Nyakati nyingine, tunapata ushauri unaotulinda kutokana na mambo kama vile kupenda mali na mambo mengine ambayo yanaweza kutufanya tuvunje sheria za Mungu. Katika hali hizo pia, tunanufaika tunapofuata mwongozo ambao Yehova huandaa. Tunakuwa na dhamiri safi na kuepuka mahangaiko yasiyo ya lazima. (1 Tim. 6:​9, 10) Matokeo ni kwamba tunaweza kumwabudu Yehova kwa moyo wote, jambo ambalo linatuletea shangwe nyingi, amani, na tunaridhika sana.—Soma Isaya 48:​17, 18.

18. Nĩkĩ ũthuurĩte gwĩta na mbere kũthingata ũtongeeria bwa Jehova?

18 Bila shaka, Yehova ataendelea kutumia wawakilishi wake hapa duniani ili kutupatia mwongozo wakati wa dhiki kuu na tutakapokuwa kwenye ule Utawala wa Miaka Elfu Moja. (Zab. 45:16) Je, tutaendelea kufuata mwongozo huo hata ikiwa kufanya hivyo kutahitaji tudhabihu mambo ambayo tunapenda? Itakuwa rahisi kufanya hivyo ikiwa tunafuata mwongozo ambao Yehova anatupatia sasa. Hivyo, acheni sikuzote tuendelee kufuata mwongozo wa Yehova, kutia ndani mwongozo ambao unatolewa na wanaume ambao wamewekwa rasmi ili kutulinda. (Isa. 32:​1, 2; Ebr. 13:17) Na tunapofanya hivyo, tuna kila sababu ya kumtumaini Yule anayetuongoza, Yehova, ambaye atatuondoa mbali na hatari za kiroho na kutuongoza ili tufike mwisho wa safari yetu, yaani, kwenye uzima wa milele katika ulimwengu mpya.

ŨŨMBA GŨCOOKIA ATĨA?

  • Nĩatĩa Jehova aatongererie mũgongo jwa Isiraeli?

  • Nĩatĩa Jehova aatongererie Akristũ ba karine ya mbere?

  • Nĩatĩa tũgunĩkaga rĩrĩa twathingata ũtongeeria bwa Jehova ntukũne cietũ?

RWĨMBO 48 Kutembea na Yehova Kila Siku

a Yehova alimweka rasmi malaika “aliyekuwa akitangulia kambi,” na kuliongoza taifa ili liingie katika Nchi ya Ahadi. Ni wazi kwamba malaika huyo alikuwa Mikaeli—Yesu kabla ya kuwa mwanadamu.—Kut. 14:19; 32:34.

b Baadaye iliitwa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Leo, mazoezi hayo ni sehemu ya mkutano wetu wa katikati ya juma.