Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 27

RWĨMBO 73 Tupe Ujasiri

Ĩthĩrwa na Ũcamba ta Zadoki

Ĩthĩrwa na Ũcamba ta Zadoki

“Zadoki aarĩ muntũ ũmwĩthĩ na ncamba ya ndwaa.”1 KAR. 12:28.

JAMBO KUU

Jinsi mfano wa Sadoki unavyoweza kutusaidia kuwa jasiri.

1-2. Zadoki aarĩ ũũ? (1 Mantu ja Karaja 12:​22, 26-28)

 WAZIA tukio hili. Umati wa wanaume zaidi ya 340,000 umekusanyika ili kumweka Daudi kuwa mfalme wa Israeli yote. Kwa siku tatu, wanaume hao walikaa kwenye milima yenye miamba karibu na Hebroni, walizungumza kwa uchangamfu, walicheka, na kuimba kwa shangwe nyimbo za kumsifu Yehova. (1 Nya. 12:39) Katika umati huo, kulikuwa na mwanamume kijana anayeitwa Sadoki ambaye inaelekea watu wengi wasingemtambua. Hata hivyo, Yehova alihakikisha tunajua kwamba Sadoki alikuwepo kwenye tukio hilo. (Soma 1 Nyakati 12:​22, 26-28.) Sadoki alikuwa nani?

2 Sadoki alikuwa kuhani aliyefanya kazi kwa ukaribu na Kuhani Mkuu Abiathari. Pia, Sadoki alikuwa mwonaji na Yehova alimpatia hekima nyingi sana na uwezo wa kutambua mapenzi Yake. (2 Sam. 15:27) Watu walimfuata Sadoki walipohitaji ushauri wenye hekima. Pia, alikuwa mwanamume mwenye ujasiri. Katika makala hii, tutajifunza jinsi Sadoki alivyoonyesha ujasiri.

3. (a) Nĩkĩ athathaayia ba Jehova bakũbatara kwĩthĩrwa na ũcamba? (b) Nĩmbi tũkaarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

3 Katika siku hizi za mwisho, Shetani ameongeza mashambulizi yake dhidi ya watu wa Mungu. (1 Pet. 5:8) Tunahitaji sifa ya ujasiri tunapomngojea Yehova amwondoe Shetani na mfumo wake mwovu. (Zab. 31:24) Acheni tuchunguze njia tatu ambazo tunaweza kuiga ujasiri wa Sadoki.

GWATA MBARU ŨNENE BWA MŨRUNGU

4. Nĩkĩ antũ ba Jehova bakũbatara kwĩthĩrwa na ũcamba nĩkenda bagwata mbaru Ũnene bwa Mũrungu? (Tega kinya mbica.)

4 Tukiwa watu wa Yehova, tunaunga mkono Ufalme wa Mungu kwa moyo wetu wote, lakini mara nyingi tunahitaji ujasiri ili kufanya hivyo. (Mt. 6:33) Kwa mfano, katika ulimwengu huu mwovu, tunahitaji ujasiri ili kuishi kulingana na viwango vya Yehova na kuhubiri habari njema ya Ufalme. (1 The. 2:2) Pia, mara nyingi tunahitaji ujasiri ili kutounga mkono upande wowote katika masuala ya kisiasa yanayozidi kuleta migawanyiko katika mfumo huu wa mambo. (Yoh. 18:36) Watumishi wengi wa Yehova wamepoteza mali zao, wameteswa, au wamefungwa kwa sababu ya kukataa kujihusisha katika masuala ya kisiasa au kukataa kujiunga na jeshi.

Wengine wanapounga mkono upande fulani katika masuala ya kisiasa, wewe utafanya nini? (Tazama fungu la 4)


5. Nĩkĩ Zadoki aabataraga ũcamba nĩkenda agwata mbaru Daudi?

5 Sadoki hakwenda Hebroni ili tu kusherehekea tukio la Daudi kuwekwa kuwa Mfalme. Alienda na silaha akiwa tayari kwa ajili ya vita. (1 Nya. 12:38) Alikuwa tayari kumfuata Daudi vitani na kuwalinda Waisraeli dhidi ya adui zao. Ingawa huenda Sadoki hakuwa na uzoefu mwingi wa kupigana katika vita, alikuwa mwanamume jasiri sana.

6. Nĩatĩa Daudi eekĩre ngerekano ĩnjega ya kwĩthĩrwa na ũcamba nĩkenda Zadoki amĩthingata? (Zaburi 138:3)

6 Sadoki aliyekuwa kuhani, alijifunzaje kuwa jasiri hivyo? Alizungukwa na wanaume wenye nguvu na waliokuwa jasiri. Bila shaka, alinufaika kutokana na mfano wao. Kwa mfano, ujasiri alioonyesha Daudi ‘alipowaongoza Waisraeli vitani’ uliwachochea Waisraeli wote kumuunga mkono kwa moyo wote. (1 Nya. 11:​1, 2) Sikuzote Daudi alimtegemea Yehova amsaidie alipopambana na adui zake. (Zab. 28:7; soma Zaburi 138:3.) Sadoki alijifunza kutokana na wanaume wengine wenye ujasiri—kama vile, Yehoyada na Benaya, mwana wake aliyekuwa shujaa, pamoja na wakuu wengine 22 ambao walimuunga mkono Daudi. (1 Nya. 11:​22-25; 12:​26-28) Wanaume hao wote waliazimia kuunga mkono ufalme wa Daudi.

7. (a) Nĩ ngerekano irĩkũ ntukũne cietũ ciegie ũcamba tũũmba kũthingata? (b) Nĩmbi ũkwiritana kuumania na ngerekano ya Mũtana wa Baaba Nsilu, o ta ũrĩa kwonanĩtue vidione?

7 Tunapata nguvu na ujasiri tunapofikiria mifano ya wale ambao kwa ujasiri wameunga mkono utawala wa Yehova. Mfalme wetu, Yesu Kristo, alikataa kwa uthabiti kujihusisha katika siasa za mfumo huu wa mambo wa Shetani. (Mt. 4:​8-11; Yoh. 6:​14, 15) Sikuzote alimtegemea Yehova ampe nguvu. Pia, tuna mifano mingi ya wanaume vijana katika siku zetu ambao wamekataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya dhamiri au wamekataa kushiriki katika masuala ya kisiasa. Tunakutia moyo usome masimulizi yao kwenye tovuti ya jw.org. a

TETHEERIA ATANA BA BAABA BANGĨ

8. Nĩ magiita ta jarĩkũ akũrũ ba kĩũthũrano bomba kũbatara ũcamba nĩkenda batethia atana na aarĩ ba baaba?

8 Watu wa Yehova wanapenda kusaidiana. (2 Kor. 8:4) Hata hivyo, nyakati nyingine tunahitaji ujasiri ili kufanya hivyo. Kwa mfano, vita vinapotokea, wazee wa kutaniko wanatambua kwamba ndugu na dada zao wanahitaji kutiwa moyo, kutegemezwa, na labda kupewa Biblia na machapisho yetu au mahitaji ya kimwili. Kwa sababu wanawapenda kondoo, wazee wanahatarisha uhai wao ili kuwaandalia ndugu na dada mahitaji yao. (Yoh. 15:​12, 13) Wanapofanya hivyo, wanaiga ujasiri wa Sadoki.

9. O ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ 2 Samweli 15:​27-29, nĩatĩa Daudi eerĩre Zadoki athithie? (Tega kinya mbica.)

9 Uhai wa Daudi ulikuwa hatarini. Absalomu, mwana wake, alikuwa ameazimia kuunyakua ufalme kutoka kwa Daudi. (2 Sam. 15:​12, 13) Daudi alihitaji kuondoka Yerusalemu mara moja! Aliwaambia watumishi wake hivi: “Tuondoke, tukimbie, kwa maana hakuna yeyote kati yetu atakayemkwepa Absalomu!” (2 Sam. 15:14) Watumishi wake walipokuwa wakiondoka, Daudi alitambua kwamba mtu fulani alihitaji kubaki ili aendelee kumpatia habari kuhusu mipango ya Absalomu. Hivyo, aliwatuma jijini Sadoki na makuhani wengine ili wamletee habari. (Soma 2 Samweli 15:​27-29.) Walihitaji kuwa waangalifu sana. Jambo ambalo Daudi aliwaambia makuhani hao wafanye lilikuwa hatari na hata wangeweza kupoteza uhai wao. Wazia jambo ambalo Absalomu—mwanamume mwenye majivuno, mwenye kulipiza kisasi, na mwenye hila—angewafanyia Sadoki na makuhani wengine ikiwa angetambua kwamba walikuwa wakimpeleleza ili kumlinda Daudi!

Daudi alimtuma Sadoki akatimize mgawo hatari (Tazama fungu la 9)


10. Nĩatĩa Zadoki na barĩa baarĩ amwe nawe baakarĩrie Daudi?

10 Daudi alimwomba Sadoki na Hushai, rafiki mwingine mshikamanifu wa Daudi, wamsaidie kutekeleza mpango fulani. (2 Sam. 15:​32-37) Akifuata mpango huo, Hushai aliweza kuaminiwa na Absalomu na akampendekezea mbinu ya kivita ambayo ingempa Daudi muda wa kujitayarisha kwa ajili ya shambulizi. Kisha, Hushai akamjulisha Sadoki na Abiathari kuhusu mpango huo. (2 Sam. 17:​8-16) Na wanaume hao wawili walifanikiwa kupeleka ujumbe kwa Daudi. (2 Sam. 17:17) Kwa msaada wa Yehova, Sadoki na makuhani wenzake walifanikiwa kutimiza jukumu muhimu katika kulinda uhai wa Daudi.—2 Sam. 17:​21, 22.

11. Nĩatĩa tũũmba kwigerekania na ũcamba bwa Zadoki rĩrĩa tũgũtethia atana na aarĩ ba baaba?

11 Ikiwa tunaombwa kuwasaidia ndugu zetu wanapokabili hatari fulani, tunawezaje kuonyesha ujasiri kama ule wa Sadoki? (1) Fuata mwongozo. Katika hali kama hizo, ni muhimu tudumishe umoja. Unga mkono mwongozo unaotoka kwenye ofisi yenu ya tawi. (Ebr. 13:17) Wazee wanapaswa kupitia kwa ukawaida mipango ya kutaniko lao ya kujitayarisha kwa ajili ya majanga, pamoja na miongozo ya tengenezo kuhusu mambo ya kufanya majanga yanapotokea. (1 Kor. 14:​33, 40) (2) Uwe jasiri lakini mwenye tahadhari. (Met. 22:3) Fikiri kabla ya kutenda. Usihatarishe uhai wako isivyo lazima. (3) Mtegemee Yehova. Kumbuka kwamba Yehova anataka wewe na ndugu zako muwe salama. Anaweza kukusaidia ili uwapatie ndugu zako msaada kwa njia iliyo salama.

12-13. Nĩmbi ũkwiritana kuumania na ngerekano ya Viktor na Vitalii? (Tega kinya mbica.)

12 Fikiria mfano wa Viktor na Vitalii, wazee wawili wa kutaniko waliofanya kazi ya kupeleka chakula na maji kwa waabudu wenzao nchini Ukrainia. Viktor anasema hivi: “Tulitafuta chakula kila mahali. Mara nyingi tulisikia watu wakitupiana risasi karibu na eneo tulilokuwa. Ndugu mmoja alitoa msaada wa chakula kutoka kwenye duka lake. Mchango huo uliwasaidia wahubiri wengi kupata mahitaji yao ya lazima kwa kipindi fulani. Tulipokuwa tukipakia bidhaa hizo kwenye lori letu, bomu lilianguka mita 20 kutoka mahali tulipokuwa. Nilimsihi Yehova siku nzima ili anipatie ujasiri wa kuendelea kuwasaidia wahubiri.”

13 Vitalii anasema hivi: “Tulihitaji ujasiri mwingi sana. Safari yangu ya kwanza ilichukua saa 12. Nilisali kwa Yehova muda wote nilipokuwa safarini.” Vitalii alikuwa jasiri, lakini pia alichukua tahadhari. Anaendelea kusema hivi: “Niliendelea kusali kwa Yehova anipe hekima na niwe mwenye kiasi. Niliendesha gari kwenye barabara zilizoruhusiwa na wenye mamlaka. Nimenufaika kwa kujionea kibinafsi jinsi ndugu na dada walivyofanya kazi pamoja. Waliondoa vitu vilivyozuia njia, walikusanya vitu vilivyotolewa kama msaada na kuvipakia kwenye gari, na walitupatia chakula na mahali pa kulala tulipokuwa njiani.”

Katika nyakati za hatari, uwe jasiri lakini mwenye tahadhari unapowasaidia ndugu zako (Tazama fungu la 12-13)


GWATĨĨRA WĨTĨKĨKUA BWAKU KĨRĨ JEHOVA

14. Nĩatĩa tũũmba kũringithua rĩrĩa muntũ twendete atiga kwaa mwĩtĩkĩkua kĩrĩ Jehova?

14 Mojawapo kati ya majaribu magumu zaidi tunayoweza kukabili ni wakati mtu wa familia au rafiki wa karibu anapomwacha Yehova. (Zab. 78:40; Met. 24:10) Kadiri tunavyokuwa na uhusiano wa karibu na mtu huyo, ndivyo inavyoweza kuwa vigumu zaidi kuvumilia hali hiyo. Ikiwa umepitia hali hiyo yenye kuumiza, mfano wa Sadoki unaweza kukuimarisha.

15. Nĩkĩ Zadoki aabataraga ũcamba nĩkenda agwatĩĩra wĩtĩkĩkua bwawe kĩrĩ Jehova? (1 Anene 1:​5-8)

15 Sadoki aliendelea kuwa mshikamanifu kwa Yehova ingawa Abiathari, rafiki yake, aliamua kutokuwa mshikamanifu. Jambo hilo lilitukia mwishoni mwa utawala wa Daudi. Daudi alipokuwa anakaribia kufa, Adoniya, mwana wake, alijaribu kunyakua ufalme ambao Yehova alikuwa ameahidi kumpatia Sulemani. (1 Nya. 22:​9, 10) Abiathari aliamua kumuunga mkono Adoniya. (Soma 1 Wafalme 1:​5-8.) Alipofanya hivyo, Abiathari hakuwa mshikamanifu kwa Daudi na pia kwa Yehova! Je, unaweza kuwazia jinsi Sadoki alivyohuzunika na kuvunjika moyo? Kwa zaidi ya miaka 40, yeye na Abiathari walikuwa wamefanya kazi pamoja wakiwa makuhani. (2 Sam. 8:17) Walikuwa wakilitunza pamoja “Sanduku la Mungu wa kweli.” (2 Sam. 15:29) Mwanzoni, wanaume hao wawili waliunga mkono ufalme wa Daudi—na walifanya mambo mengine mengi katika utumishi wa Yehova.—2 Sam. 19:​11-14.

16. Kwombĩka nĩmbi biatetherie Zadoki kũgwatĩĩra wĩtĩkĩkua bwawe?

16 Sadoki aliendelea kuwa mshikamanifu kwa Yehova licha ya uamuzi wa Abiathari. Daudi hakutilia shaka kamwe ushikamanifu wa Sadoki. Njama ya Adoniya ilipogundulika, Daudi aliwachagua Sadoki, Nathani, na Benaya ili wamtie mafuta Sulemani kuwa mfalme. (1 Fal. 1:​32-34) Bila shaka, kushirikiana na waabudu washikamanifu wa Yehova, kama vile Nathani na watu wengine waliomuunga mkono Mfalme Daudi, kulimwimarisha na kumtia moyo Sadoki. (1 Fal. 1:​38, 39) Sulemani alipokuwa mfalme, “akamweka Sadoki kuwa kuhani badala ya Abiathari.”—1 Fal. 2:35.

17. Nĩatĩa ũũmba kwigerekania na Zadoki rĩrĩa muntũ wendete atiga kwa mwĩtĩkĩkua kĩrĩ Jehova?

17 Unawezaje kumwiga Sadoki? Ikiwa mtu fulani unayempenda anaamua kumwacha Yehova, mwonyeshe Yehova kwamba umechagua kuwa mshikamanifu kwake. (Yos. 24:15) Yehova atakupa nguvu na ujasiri unaohitaji. Mtegemee Yehova na kusali kwake na uendelee kushirikiana kwa ukaribu na waabudu wenzako walio washikamanifu. Yehova anathamini ushikamanifu wako, na atakuthawabisha.—2 Sam. 22:26.

18. Nĩmbi ũkwiritana kuumania na ngerekano ya Marco na Sidse?

18 Fikiria mfano wa Marco na Sidse, mke wake, ambao binti zao wawili, walio watu wazima, waliiacha kweli. Marco anasema hivi: “Tangu siku ambayo watoto wako wanazaliwa, unawapenda sana. Na utafanya jambo lolote ili kuwalinda dhidi ya hatari. Hivyo, inavunja moyo sana wanapoamua kumwacha Yehova.” Anaongezea hivi: “Lakini Yehova amekuwa pamoja nasi. Amehakikisha kwamba ninapokuwa dhaifu, mke wangu anakuwa na nguvu, na anapokuwa dhaifu, mimi ninakuwa na nguvu.” Sidse anasema hivi: “Hatungeweza kuvumilia ikiwa Yehova hangetupatia nguvu tulizohitaji. Nilikuwa nikijilaumu kwa sababu binti zangu waliacha kumtumikia Yehova, hivyo nilimwambia Yehova jinsi nilivyohisi. Baada ya muda mfupi, dada ambaye hatukuwa tumeonana kwa miaka mingi, alinifuata na kuweka mikono yake juu ya mabega yangu, na kunitazama usoni, kisha akaniambia hivi, ‘Sidse, kumbuka kwamba hupaswi kujilaumu!’ Kwa msaada wa Yehova, nimefaulu kudumisha shangwe yangu ninapoendelea kumtumikia.”

19. Nĩatĩa ũthuurĩte kũthithia?

19 Yehova anataka waabudu wake wote wawe na ujasiri kama Sadoki. (2 Tim. 1:7) Hata hivyo, hataki tutegemee nguvu zetu wenyewe. Anataka tumtegemee yeye. Hivyo, unapokabili hali inayohitaji uwe jasiri, sali kwa Yehova. Unaweza kuwa na uhakika kwamba atakupa ujasiri kama aliokuwa nao Sadoki!—1 Pet. 5:10.

RWĨMBO 126 Uwe Macho, Simama Imara, Uwe na Nguvu