Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 43

Ũũme bwa Mma Nĩbũkũgondoka na Kaajũ Gakanene

Ũũme bwa Mma Nĩbũkũgondoka na Kaajũ Gakanene

Uume ibugandukaga biigirone bia ntuura. Nibwaragia na mugambo jumunene marurine.”​—NJU. 1:20.

RWĨMBO 88 Nijulishe Njia Zako

MUHTASARI a

1. Nĩatĩa antũ babaingĩ betĩkagĩĩria ntukũne cietũ baewa kaanya ga kũgĩa na ũũme bwa mma? (Njuno 1:20, 21)

 KATIKA nchi nyingi, limekuwa jambo la kawaida kuona wahubiri wa Ufalme wenye furaha wakiwapa machapisho wapita-njia barabarani. Je, umewahi kushiriki katika kazi hiyo yenye kusisimua? Ikiwa umewahi kushiriki, bila shaka umefikiria kuhusu lugha ya mfano inayotumiwa kwenye kitabu cha Methali, yaani, hekima inayopaza sauti kubwa jijini ili watu wasikie ushauri wake. (Soma Methali 1:20, 21.) Biblia na machapisho yetu yana “hekima ya kweli,” yaani, hekima ya Yehova. Hii ndiyo habari ambayo watu wanahitaji kusikia ili waanze kutembea kwenye barabara inayoongoza kwenye uzima. Tunafurahi sana mtu anapochukua machapisho yetu. Lakini si wote wanaofanya hivyo. Baadhi ya watu hawataki kujua ujumbe ulio katika Biblia. Wengine hutucheka. Wanafikiri kwamba Biblia imepitwa na wakati. Na wengine hukosoa mafundisho ya Biblia kuhusu maadili, wakidai kwamba wale wanaofuata viwango hivyo hawana fadhili na wanajiona kuwa waadilifu kupita kiasi. Ingawa hivyo, kwa upendo Yehova anaendelea kuhakikisha kwamba watu wote wanaendelea kupata hekima ya kweli. Jinsi gani?

2. Nĩkũ ũũme bwa mma bwonekaga ntukũne cietũ, ĩndĩ babaingĩ bathuuraga kũthithia atĩa?

2 Njia moja ambayo Yehova anafanya hekima ya kweli ipatikane ni kupitia Neno lake, Biblia. Karibu kila mtu anaweza kupata kitabu hicho. Namna gani machapisho yetu yanayotegemea Biblia? Kwa baraka za Yehova, machapisho yetu yanapatikana katika lugha zaidi ya 1,000. Wale wanaosikiliza, yaani, wale wanaosoma na kufuata mambo wanayojifunza, watanufaika. Hata hivyo, watu wengi huamua kutosikiliza sauti ya hekima ya kweli. Wanapofanya maamuzi, wanategemea maoni yao wenyewe au kuwasikiliza wanadamu wenzao. Huenda hata wakatudharau kwa sababu tunaamua kufuata ushauri wa Biblia. Makala hii itazungumzia kwa nini watu hutenda kwa njia hiyo. Lakini kwanza, acheni tuchunguze jinsi tunavyoweza kupata hekima kutoka kwa Yehova.

KŨMENYA JEHOVA NĨGŨTONGAGĨĨRIA KĨRĨ ŨŨME BWA MMA

3. Nĩatĩa tũkũbatara kũthithia nĩkenda tũgĩĩa ũũme bwa mma?

3 Hekima inaweza kufafanuliwa kuwa uwezo wa kutumia mambo tunayojua ili kufanya maamuzi mazuri. Hata hivyo, hekima ya kweli inahusisha mengi zaidi. Biblia inasema hivi: “Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu Zaidi ni uelewaji.” (Met. 9:10) Basi, kabla ya kufanya uamuzi muhimu, tunapaswa kuongozwa na njia ya Yehova ya kufikiri, yaani, “kumjua Aliye Mtakatifu Zaidi,” huo ndio unaopaswa kuwa msingi wa maamuzi yetu. Tunaweza kufanya hivyo kwa kujifunza Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia. Tunapofanya hivyo, tunaonyesha hekima ya kweli.​—Met. 2:5-7.

4. Nĩkĩ tũũmba kuuga atĩ Jehova wenka, nĩwe ũũmba gũtwaa ũũme bwa mma?

4 Yehova peke yake ndiye anayeweza kutupatia hekima ya kweli. (Rom. 16:27) Kwa nini yeye ndiye Chanzo cha hekima? Kwanza, akiwa Muumba, ana ujuzi mwingi sana na uelewaji kuhusu uumbaji wake. (Zab. 104:24) Pili, matendo yote ya Yehova yanaonyesha kwamba ni mwenye hekima. (Rom. 11:33) Tatu, sikuzote ushauri wa Yehova wenye hekima huwanufaisha wale wanaoufuata. (Met. 2:10-12) Ili tupate hekima ya kweli, ni lazima tukubali kweli hizo za msingi na kuziruhusu ziongoze maamuzi na matendo yetu.

5. Kwĩthagĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ rĩrĩa antũ barega gwĩtĩkĩĩria Jehova arĩ Kaumo ka ũũme bwa mma?

5 Watu wengi tunaokutana nao katika huduma wanakubali kwamba kuna ubunifu wa kustaajabisha katika vitu vya asili; ingawa hivyo, wanakataa kukubali kwamba kuna Muumba na badala yake wanaamini fundisho la mageuzi. Wengine tunaokutana nao wanadai kwamba wanamwamini Mungu, lakini wanaona kwamba viwango vya Biblia vimepitwa na wakati, basi wanaamua kuishi kulingana na maoni yao wenyewe. Matokeo yamekuwaje? Je, hali zimekuwa bora ulimwenguni kwa sababu watu wameamua kutegemea hekima yao wenyewe, badala ya kutegemea hekima ya Mungu? Je, wamepata furaha ya kweli au tumaini linalotegemeka la wakati ujao? Mambo yanayotuzunguka yanathibitisha ukweli huu: “Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumpinga Yehova.” (Met. 21:30) Hilo linatuchochea tuendelee kumtegemea Yehova ili kupata hekima ya kweli! Inasikitisha kwamba wengi hawafanyi hivyo. Kwa nini?

GĨTŨMI ANTŨ BAREGAGA ŨŨME BWA MMA

6. Kũringana na Njuno 1:22-25, nĩ baaũ baregaga kũthikĩĩra kaajũ ka ũũme bwa mma?

6 Watu wengi hukataa kusikiliza hekima ya kweli ‘inapopaza sauti kubwa barabarani.’ Kulingana na Biblia, kuna vikundi vitatu vya watu wanaokataa hekima: “wajinga,” “wadhihaki,” na “wapumbavu.” (Soma Methali 1:22-25.) Acheni tuchunguze kwa undani tabia zinazowafanya watu hao wakatae hekima inayotoka kwa Mungu, na pia tutajifunza jinsi tunavyoweza kuepuka kusitawisha tabia hizo.

7. Nĩkĩ bamwe bathuuraga gwĩta na mbere gũkara na “waa bwao”?

7 “Wajinga” ni wale wasio na uzoefu, wanaoshawishiwa au kudanganywa kwa urahisi. (Met. 14:15, maelezo ya chini) Mara kwa mara tunakutana na watu hao katika huduma. Kwa mfano, fikiria kuhusu mamilioni ya watu wanaodanganywa na viongozi wa kidini au kisiasa. Baadhi yao hushtuka wanapojifunza kwamba wamedanganywa na viongozi hao. Lakini wale wanaotajwa kwenye Methali 1:22 huamua kuendelea kuwa wajinga kwa sababu wanapenda kuishi hivyo. (Yer. 5:31) Wanafurahia kufanya jinsi wanavyotaka na hawataki kujifunza mambo ambayo Biblia inasema au kuishi kulingana na viwango vya Biblia. Wengi wanahisi kama mwanamke fulani anayependa sana dini yake huko Quebec, Kanada, aliyemwambia hivi Shahidi aliyemtembelea, “Ikiwa kasisi wetu ametudanganya hilo ni kosa lake, si letu.” Bila shaka, hatungependa kuwaiga wale ambao wanakataa kujifunza kimakusudi!​—Met. 1:32; 27:12.

8. Nĩmbi bigatũtethia kwĩthĩrwa na ũmenyo bũrĩa bũkwagĩra?

8 Biblia ina sababu nzuri inapotutia moyo tusiendelee kuwa wajinga na badala yake ‘tuwe watu wazima katika uelewaji wetu.’ (1 Kor. 14:20) Tunajipatia uzoefu unaofaa kwa kutumia kanuni za Biblia maishani mwetu. Hatua kwa hatua, tunajionea kibinafsi jinsi kanuni hizo zinavyotusaidia kuepuka matatizo na kufanya maamuzi yenye hekima. Ni vizuri kuchunguza maendeleo ambayo tumefanya inapohusu kufanya maamuzi mazuri. Ikiwa tumekuwa tukijifunza Biblia na kuhudhuria mikutano kwa muda fulani, tunaweza kujiuliza kwa nini bado hatujachukua hatua ya kujiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa. Ikiwa tumebatizwa, je, tunafanya maendeleo tukiwa wahubiri na walimu wa habari njema? Je, maamuzi yetu yanaonyesha kwamba tunaongozwa na kanuni za Biblia? Je, tunaonyesha sifa za Kikristo tunaposhughulika na wengine? Tukitambua kwamba tunahitaji kufanya maendeleo, acheni tusikilize vikumbusho vya Yehova ambavyo “humfanya asiye na uzoefu awe na hekima.”​—Zab. 19:7.

9. Nĩatĩa barĩa ‘bamaragia’ mantũ ja Mũrungu bonanagia nĩ bakũrega ũũme bwa mma?

9 Kundi la pili la watu ambao wanapuuza hekima ya Mungu ni “wadhihaki.” Pindi fulani, tunakutana na watu hao tunapohubiri. Wanafurahia kuwadhihaki wengine. (Zab. 123:4) Biblia inaonya kwamba katika siku za mwisho, kungekuwa na wadhihaki wengi. (2 Pet. 3:3, 4) Kama wakwe wa Loti mwadilifu, leo, baadhi ya watu hawasikilizi maonyo yanayotoka kwa Mungu. (Mwa. 19:14) Wengi wanawacheka wale wanaoishi kulingana na kanuni za Biblia. Wadhihaki wanachochewa na “tamaa zao zisizompendeza Mungu.” (Yuda 7, 17, 18) Ufafanuzi wa Biblia kuhusu wadhihaki unapatana kabisa na mtazamo wa waasi-imani na wengine ambao wamemkataa Yehova!

10. O ta ũrĩa Zaburi 1:1 yonanĩtie, nĩatĩa tũũmba kũthithia tũtĩgakare ta barĩa bamaragia mantũ ja Mũrungu?

10 Tunawezaje kujilinda ili tusiwaige wadhihaki? Njia moja ni kuepuka kushirikiana na wale wenye mtazamo wa kukosoa-kosoa mambo. (Soma Zaburi 1:1.) Hilo linamaanisha kwamba hatusikilizi au kusoma habari zozote za waasi-imani. Tunatambua kwamba tusipokuwa waangalifu, tunaweza kusitawisha kwa urahisi roho ya kukosoa-kosoa mambo na kuanza kumtilia shaka Yehova na mwongozo tunaopokea kupitia tengenezo lake. Ili kuepuka mtego huo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, mimi nina mazoea ya kulalamika tunapopokea mwongozo au ufafanuzi mpya? Je, nina mwelekeo wa kuwachambua-chambua wale wanaoongoza?’ Ikiwa tutachukua hatua haraka ili kuondoa mielekeo kama hiyo ndani yetu, tutamfurahisha Yehova.​—Met. 3:34, 35.

11. Nĩatĩa barĩa ‘biaa’ bonaga ithimi bia Jehova biegie mĩtugo ya wagĩru?

11 Kundi la tatu la watu wanaokataa hekima ni “wapumbavu.” Ni wapumbavu kwa sababu wanakataa kuishi kulingana na sheria za Yehova kuhusu maadili. Wanafanya mambo wanayoona kuwa sawa machoni pao wenyewe. (Met. 12:15) Watu hao wanamkataa Yehova ambaye ndiye Chanzo cha hekima. (Zab. 53:1) Tunapokutana nao katika kazi ya kuhubiri, mara nyingi wao hutukosoa kwa ukali kwa sababu tunaheshimu viwango vya Biblia. Lakini hawawezi kutupatia mwongozo bora wa maisha. Biblia inasema hivi: “Mjinga hawezi kupata hekima ya kweli; hana lolote la kusema katika lango la jiji.” (Met. 24:7) Wapumbavu hawawezi kutupatia ushauri wowote wenye hekima ya kweli. Ndiyo sababu Yehova anatuonya ‘tukae mbali na mtu mpumbavu’!​—Met. 14:7.

12. Nĩmbi bigatũtethia kũregana na mĩĩtĩre ya barĩa biaa?

12 Tofauti na wale ambao wanachukia ushauri unaotoka kwa Mungu, sisi tunasitawisha upendo kuelekea njia za Mungu, kutia ndani viwango vyake vya maadili. Tunaweza kuimarisha upendo huo kwa kulinganisha matokeo ya kutii na matokeo ya kutotii. Tambua matatizo ambayo watu wanajiletea kwa sababu ya kukataa kwa upumbavu ushauri wa Yehova wenye hekima. Kisha ufikirie jinsi maisha yako yalivyo bora kwa sababu unamtii Mungu.​—Zab. 32:8, 10.

13. Rĩ, neka Jehova atũkinyagĩĩria kũthingata ũtaaro bwawe bwa ũũme?

13 Yehova anafanya iwezekane kwa watu wote kupata hekima, lakini hamlazimishi yeyote aikubali. Hata hivyo, anafafanua matokeo mabaya yanayowapata wale wanaokataa kusikiliza hekima. (Met. 1:29-32) Wale wanaoamua kutomtii Yehova “watapata matokeo ya njia yao.” Baada ya muda, njia yao ya maisha itawaongoza kwenye taabu, matatizo, na mwishowe uharibifu. Kinyume chake, wale wanaosikiliza ushauri wa Yehova wenye hekima na kuufuata wanapewa ahadi hii: “Yule anayenisikiliza ataishi kwa usalama naye hatahangaishwa na woga wa msiba.”​—Met. 1:33.

NĨTŨGUNĨKAGA KUUMANIA NA ŨŨME BWA MMA

Kushiriki katika mikutano huimarisha hali yetu ya kiroho (Tazama fungu la 15)

14-15. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na Njuno 4:23?

14 Tunapotumia hekima inayotoka kwa Mungu, sikuzote tunanufaika. Kama ambavyo tumejifunza, Yehova anafanya iwe rahisi kwa watu kupata ushauri wenye hekima. Kwa mfano, kotekote katika kitabu cha Methali ameandaa ushauri usiopitwa na wakati ambao utaboresha maisha yetu ikiwa tutaufuata. Acheni tuchunguze mifano minne ya ushauri huo wenye hekima.

15 Linda moyo wako wa mfano. Biblia inasema hivi: “Ulinde moyo wako kuliko vitu vyote unavyolinda, kwa maana humo ndimo zinamotoka chemchemi za uzima.” (Met. 4:23) Fikiria hatua tunazochukua ili kuulinda moyo wetu halisi. Tunahitaji kula chakula chenye lishe, kufanya mazoezi ya kutosha, na kuepuka mazoea mabaya. Tunachukua hatua kama hizo ili kuulinda moyo wetu wa mfano. Tunajilisha Neno la Mungu kila siku. Tunajitayarisha na kuhudhuria mikutano, pia tunashiriki katika mikutano hiyo. Tunaendelea kuwa wenye bidii kwa kushiriki kwenye huduma kwa ukawaida. Na tunaepuka kusitawisha mazoea yasiyofaa kwa kuendelea kujiepusha na kitu chochote kinachoweza kupotosha fikira zetu, kama vile burudani zenye ukosefu wa maadili na kushirikiana na watu wabaya.

Kuwa na maoni yenye usawaziko kuhusu pesa hutusaidia kuridhika na vitu tulivyo navyo (Tazama fungu la 16)

16. Nĩkĩ Njuno 23:4, 5 ĩgũtwagĩra mono naarua?

16 Ridhika na vitu ulivyo navyo. Biblia inatoa ushauri huu: “Usijichoshe kupata utajiri. . . . Ukiutupia jicho, haupo, kwa maana hakika utaota mabawa kama ya tai na kuruka mbali angani.” (Met. 23:4, 5) Mali za kimwili haziwezi kudumu. Ingawa hivyo, leo matajiri na maskini wanahangaikia kupita kiasi jinsi ya kupata pesa. Mara nyingi, mahangaiko hayo yanawafanya watende kwa njia ambayo inaharibu sifa zao, uhusiano wao na wengine, na hata afya yao. (Met. 28:20; 1 Tim. 6:9, 10) Kwa upande mwingine, hekima inatusaidia kuwa na maoni yenye usawaziko kuhusu pesa. Maoni hayo hutulinda dhidi ya pupa na kutusaidia kuwa wenye furaha na kuridhika.​—Mhu. 7:12.

Kufikiria kabla ya kuzungumza hutusaidia kuepuka kuwaumiza wengine kwa maneno yetu (Tazama fungu la 17)

17. Tũthithie atĩa nĩkenda tũgĩĩa “ruume rwa muntu umuume,” o ta ũrĩa kũgweti kĩrĩ Njuno 12:18?

17 Fikiria kabla ya kuzungumza. Tusipokuwa waangalifu, maneno yetu yanaweza kusababisha madhara makubwa. Biblia inasema hivi: “Maneno yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama upanga, lakini ulimi wa mwenye hekima huponya.” (Met. 12:18) Tunadumisha uhusiano mzuri na wengine tunapoepuka kupiga porojo kuhusu udhaifu wa wengine. (Met. 20:19) Ili maneno yetu yaponye badala ya kuumiza, ni lazima tujaze mioyo yetu ujuzi kutoka katika Neno la Mungu. (Luka 6:45) Tunapotafakari mambo ambayo Biblia inasema, maneno yetu yanaweza kuwa kama “chemchemi ya hekima” inayowaburudisha wengine.​—Met. 18:4.

Kufuata mwongozo kutoka kwa tengenezo hutusaidia kuboresha huduma yetu (Tazama fungu la 18)

18. Gũtumĩra ũtaaro bwa Njuno 24:6 kwomba gũtũtethia atĩa kũũmbana ũtangatĩrine?

18 Fuata mwongozo. Biblia inatoa ushauri huu unaotusaidia kupata mafanikio: “Kwa mwongozo wenye hekima utapigana vita vyako, na kupitia washauri wengi kuna ushindi.” (Met. 24:6, maelezo ya chini) Fikiria jinsi kufuata kanuni hiyo kunavyoweza kutusaidia kufanikiwa katika kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha. Badala ya kutimiza huduma yetu kwa njia yetu wenyewe, tunajitahidi kufuata mapendekezo tunayopewa. Tunapokea mwongozo wenye hekima kwenye mikutano yetu ya Kikristo, ambako washauri wenye uzoefu hutumia hotuba zinazotegemea Biblia na maonyesho ili kutuzoeza. Isitoshe, tengenezo la Yehova huandaa vifaa muhimu, yaani, machapisho na video ambazo huwasaidia watu kuelewa Biblia. Je, unajifunza jinsi ya kutumia vifaa hivyo ili kupata matokeo mazuri?

19. Nĩatĩa wigagua bwegie ũũme bũrĩa Jehova aejanaga? (Njuno 3:13-18)

19 Soma Methali 3:13-18. Tunashukuru sana kwa sababu ya ushauri mzuri unaopatikana katika Neno la Mungu! Maisha yetu yangekuwaje bila ushauri huo? Katika makala hii, tumechunguza mifano ya hekima inayotumika ambayo inapatikana kwenye kitabu cha Methali. Bila shaka, Yehova ametupatia ushauri wenye hekima katika Biblia nzima. Acheni tuazimie sikuzote kutenda kulingana na hekima ambayo Yehova anatuandalia. Hatuongozwi na maoni ya ulimwengu kuelekea hekima hiyo; tunasadiki kwamba wale “wanaoishika [hekima] kwa nguvu wataitwa wenye furaha.”

RWĨMBO 36 Tuulinde Moyo Wetu

a Hekima ambayo Yehova hutoa ni bora kuliko hekima yoyote ya ulimwengu. Katika makala hii, tutachunguza lugha ya mfano yenye kuchochea inayotajwa katika kitabu cha Methali, yaani, hekima inayopaza sauti kubwa katika viwanja vya jiji. Tutazungumzia jinsi tunavyoweza kupata hekima ya kweli, kwa nini baadhi ya watu hukataa kusikiliza maneno ya hekima, na jinsi tunavyonufaika tunaposikiliza hekima ya kweli.