Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 41

Womba Kwona Kũgwĩrua kwa Mma

Womba Kwona Kũgwĩrua kwa Mma

“KITHARIMO-RI, ni kiri muntu wonthe uria ukiraga Mwathani, O uria witaga na njira ciawe.”​—ZAB. 128:1.

RWĨMBO 110 “Shangwe ya Yehova”

MUHTASARI a

1. “Ũbatu bwetũ bwa gĩkĩrundu” nĩmbi, na nĩatĩa bũtũtethagia kwĩthĩrwa na kũgwĩrua?

 FURAHA ya kweli si hisia za kijuu-juu tu zinazokuja na kwenda. Furaha ya kweli inaweza kudumu katika maisha yote ya mtu. Jinsi gani? Yesu alieleza jambo hilo katika Mahubiri yake ya Mlimani: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.” (Mt. 5:3) Yesu alijua kwamba wanadamu wameumbwa wakiwa na tamaa kubwa ya kumjua na kumwabudu Muumba wao, Yehova Mungu. Huo ndio ‘uhitaji wetu wa kiroho.’ Na kwa kuwa Yehova ni “Mungu mwenye furaha,” wale wanaomwabudu wanaweza kuwa na furaha pia.​—1 Tim. 1:11.

“Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu.”​—Mt. 5:10 (Tazama fungu la 2 na 3) d

2-3. (a) Kũringana na Jesũ, nĩ baaũ bangĩ bomba kwĩthĩrwa na kũgwĩrua? (b) Nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ, na nĩkĩ ũntũ bũbũ bũkũbatarĩka?

2 Je, tunaweza kuwa na furaha ikiwa tu hatuna matatizo maishani? Hapana. Katika mahubiri yake, Yesu alisema jambo la kushangaza. “Wale wanaoomboleza,” iwe ni kwa sababu ya kupondwa na dhambi zao au kwa sababu wanakabili matatizo maishani, wanaweza kuwa na furaha. Yesu alisema hivyo pia kuhusu “wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu” au wale wanaopatwa na ‘shutuma’ kwa sababu ya kuwa wafuasi wa Kristo. (Mt. 5:4, 10, 11) Lakini inawezekanaje kuwa na furaha ya kweli katika hali hizo?

3 Yesu alikuwa akitufundisha kwamba furaha ya kweli haitokani na kutokuwa na matatizo maishani, bali inatokana na kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho na kumkaribia Mungu. (Yak. 4:8) Tunawezaje kufanya hivyo? Katika makala hii, tutazungumzia hatua tatu za msingi zinazoongoza kwenye furaha ya kweli.

RĨA BIAKŨRĨA BIA GĨKĨRUNDU

4. Ĩtagaaria rĩa mbere nĩ rĩrĩkũ rĩrĩa rĩtongagĩĩria kĩrĩ kũgwĩrua kwa mma? (Zaburi 1:1-3)

4 HATUA YA 1: Ili tuwe na furaha ya kweli, ni lazima tule chakula cha kiroho. Wanadamu na wanyama wanahitaji chakula cha kimwili ili waendelee kuishi. Lakini ni wanadamu tu wanaoweza kula chakula cha kiroho. Na tunahitaji chakula hicho. Ndiyo sababu Yesu alisema: “Mwanadamu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.” (Mt. 4:4) Kwa hiyo hatupaswi kuruhusu siku ipite bila kula chakula cha kiroho kinachopatikana katika Neno la Mungu lenye thamani, Biblia. Mtunga zaburi alisema hivi: ‘Mwenye furaha ni mtu ambaye anapendezwa na sheria ya Yehova, naye huisoma mchana na usiku.’​—Soma Zaburi 1:1-3.

5-6. (a) Nĩmbi tũũmba kwiritana kuumania na Bibiria? (b) Kũthooma Bibiria kũũmba gũtũtethia na njĩra irĩkũ?

5 Kwa upendo, Yehova ametupatia habari muhimu katika Biblia kuhusu jinsi ya kuishi maisha yenye furaha. Tunajifunza kuhusu kusudi lake kutuelekea. Tunajifunza kuhusu jinsi tunavyoweza kumkaribia na kupata msamaha wa dhambi zetu. Na tunajifunza kuhusu tumaini zuri ajabu analoahidi kuhusu wakati ujao. (Yer. 29:11) Kweli hizo ambazo tunazipata kwa kujifunza Biblia, zinafanya mioyo yetu ijae shangwe!

6 Kama tunavyojua, Biblia pia ina ushauri mwingi unaoweza kutumika katika maisha yetu ya kila siku. Tunapofuata ushauri huo, tunaweza kupata furaha. Kila mara unapovunjwa moyo na matatizo maishani, tumia muda mwingi zaidi kusoma Neno la Yehova na kulitafakari. Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”​—Luka 11:28.

7. Nĩatĩa ũũmba kũgunĩka nkũrũki rĩrĩa ũkũthooma Rũteto rwa Mũrungu?

7 Unaposoma Neno la Mungu, tumia muda kufurahia mambo unayosoma. Kwa mfano, je, umewahi kujionea jambo hili? Mtu fulani anakuandalia chakula unachokipenda sana. Lakini labda kwa sababu ulikuwa na haraka au ulikuwa na mambo mengine akilini, unakula chakula hicho haraka-haraka bila kufurahia ladha yake. Baada ya kumaliza kula, unatambua kwamba umekula haraka-haraka na unatamani kwamba afadhali ungekula polepole na kufurahia kabisa chakula hicho. Je, umewahi kusoma Biblia haraka-haraka hivi kwamba ukakosa kufurahia kikamili ujumbe wake? Tumia muda kufurahia usomaji wa Neno la Mungu; yaone matukio, wazia sauti, na ufikirie kuhusu mambo unayosoma. Ukifanya hivyo, utaongeza furaha yako.

8. Nĩatĩa “nthũmba mbĩtĩkua na ĩnjume” ĩkwingia ngũgĩ yaayo? (Tega kinya Nteto Gaiti.)

8 Yesu alimweka rasmi “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ili aandae chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa, nasi tunalishwa vizuri sana kiroho. b (Mt. 24:45) Maandiko yaliyoongozwa na roho takatifu ndicho kiungo muhimu katika chakula chote kinachoandaliwa na mtumwa mwaminifu. (1 The. 2:13) Chakula hicho cha kiroho kinatusaidia kujua njia ya Yehova ya kufikiri, kama inavyofunuliwa katika Biblia. Hiyo ndiyo sababu tunasoma magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na makala zilizo kwenye jw.org. Tunajitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kutaniko inayofanywa katikati ya juma na mwisho juma. Na tunatazama kila programu ya mwezi ya JW Broadcasting® ikiwa inapatikana. Kula chakula kingi cha kiroho kutatusaidia kuchukua hatua ya pili inayoongoza kwenye furaha ya kweli.

TŨŨRA KŨRINGANA NA ITHIMI BIA JEHOVA

9. Ĩtagaaria rĩa jaĩrĩ rĩrĩa rĩtongagĩĩria kĩrĩ kũgwĩrua kwa mma nĩ rĩrĩkũ?

9 HATUA YA 2: Ili tuwe na furaha ya kweli tunahitaji kuishi kulingana na viwango vya Yehova. Mtunga zaburi aliandika hivi: “Mwenye furaha ni kila mtu anayemwogopa Yehova, anayetembea katika njia Zake.” (Zab. 128:1) Kumwogopa Yehova kunamaanisha kwamba tunamheshimu sana hivi kwamba tunaogopa kufanya jambo lolote ambalo hapendi. (Met. 16:6) Basi, tunaendelea kujitahidi kuishi kulingana na viwango vya Mungu vya yaliyo sawa na yasiyo sawa kama vinavyofafanuliwa katika Biblia. (2 Kor. 7:1) Tutakuwa wenye furaha ikiwa tutafanya mambo anayopenda na kuepuka mambo anayochukia.​—Zab. 37:27; 97:10; Rom. 12:9.

10. Kũringana na Aroma 12:2, kaanya geetũ nĩ karĩkũ?

10 Soma Waroma 12:2. Huenda mtu akajua kwamba Yehova ana mamlaka ya kuamua mambo yaliyo sawa na yasiyo sawa, lakini pia ni lazima akubali kufuata viwango vya Mungu. Kwa mfano, huenda mtu akajua kwamba serikali ina haki ya kuweka kiwango cha kasi ya kuendesha magari barabarani. Lakini huenda asikubali kufuata viwango hivyo. Matokeo ni kwamba anaendesha gari kwa mwendo kasi kuliko inavyokubaliwa. Tunaonyesha kupitia matendo yetu kwamba kwa kweli kuishi kulingana na viwango vya Yehova ndiyo njia bora ya maisha. (Met. 12:28) Daudi alihisi hivyo, kwa maana alisema hivi kumhusu Yehova: “Unanijulisha njia ya uzima. Shangwe tele iko mbele zako; kuna furaha kwenye mkono wako wa kuume milele.”​—Zab. 16:11.

11-12. (a) Rĩrĩa twinyĩrĩkĩte kana tuunĩki nkoro, tũbuĩrĩte kwimenyera tũtĩkathithie ũntũ bũrĩkũ? (b) Nĩatĩa biugo birĩa birĩ kĩrĩ Afilipi 4:8 biumba gũtũtethia rĩrĩa tũkũthuura mantũ ja kwigwĩria?

11 Tunapopatwa na wasiwasi au kuvunjika moyo, huenda tukahisi kwamba tunahitaji kufanya jambo ambalo litatusaidia kusahau matatizo yetu. Hilo linaeleweka, lakini tunapaswa kuwa waangalifu ili tusishawishiwe kufanya jambo ambalo Yehova anachukia.​—Efe. 5:10-12, 15-17.

12 Katika barua yake kwa Wafilipi, mtume Paulo aliwahimiza Wakristo waendelee kufikiria mambo yaliyo ya “uadilifu, . . . safi kiadili, . . . Yanayopendeka, [na] ya wema wa adili.” (Soma Wafilipi 4:8.) Ingawa Paulo hakuwa akiandika kihususa kuhusiana na burudani, mambo aliyoandika yanapaswa kutuongoza tunapochagua burudani. Jaribu kufanya hivi: Kila mahali ambapo neno “mambo” linapatikana kwenye mstari huo, badilisha na uweke neno “nyimbo,” “sinema,” “vitabu,” au “michezo ya video.” Kufanya hivyo kutakusaidia utambue burudani inayokubalika machoni pa Mungu na ile ambayo haikubaliki. Tunataka kupatanisha maisha yetu na viwango vya juu vya Yehova. (Zab. 119:1-3) Kisha tukiwa na dhamiri safi, tunaweza kuchukua hatua inayofuata inayoongoza kwenye furaha ya kweli.​—Mdo. 23:1.

ĨĨKA ŨTHATHAYIA BWA JEHOVA MBERE

13. Ĩtagaaria rĩa jathatũ nĩ rĩrĩkũ rĩrĩa rĩtongagĩĩria kĩrĩ kũgwĩrua kwa mma? (Johana 4:23, 24)

13 HATUA YA 3: Hakikisha kwamba unatanguliza ibada ya Yehova maishani mwako. Akiwa Muumba wetu, Yehova anastahili kabisa kupokea ibada yetu. (Ufu. 4:11; 14:6, 7) Basi, jambo muhimu zaidi maishani mwetu linapaswa kuwa kumwabudu Yehova kwa njia anayoikubali, yaani, “kwa roho na kweli.” (Soma Yohana 4:23, 24.) Tungependa roho takatifu ya Mungu iongoze ibada yetu ili ipatane na kweli zilizo katika Neno lake. Tunapaswa kutanguliza ibada yetu hata kama tunaishi katika nchi ambayo kazi yetu imewekewa vizuizi au kupigwa marufuku. Kufikia sasa, zaidi ya ndugu na dada 100 wamefungwa gerezani kwa sababu wao ni Mashahidi wa Yehova. c Ingawa hivyo, kwa furaha wanafanya yote wanayoweza ili kusali, kujifunza, na kuwaambia wengine kumhusu Mungu na Ufalme wake. Tunaposhutumiwa au kuteswa tunaweza kuwa na furaha kwa kujua kwamba Yehova yuko pamoja nasi, naye atatuthawabisha.​—Yak. 1:12; 1 Pet. 4:14.

NGEREKANO YA KĨNANDĨ

14. Nĩatĩa gwakarĩkĩre kĩrĩ mũtana-wa-baaba ũmwe ũmwĩthĩ kuuma Tajikistan, na nĩkĩ?

14 Masimulizi halisi ya maisha ya watu yanathibitisha kwamba hatua tatu ambazo tumetoka kuzungumzia zinaongoza kwenye furaha ya kweli, hata tuwe tunakabili hali gani. Fikiria jambo lililompata Jovidon Bobojonov mwenye umri wa miaka 19, anayeishi nchini Tajikistan, ambaye alikataa utumishi wa kijeshi. Oktoba 4, 2019, alitekwa nyara kutoka nyumbani kwake, akawekwa kizuizini kwa miezi kadhaa, na kutendewa kama mhalifu. Ukosefu huo wa haki uliripotiwa katika vyombo vya habari vya nchi mbalimbali. Ilitangazwa kwamba alipigwa ili kujaribu kumshinikiza akubali kula kiapo cha kuwa mwaminifu kwa jeshi na kuvaa sare zao. Baada ya hapo, alipatwa na hatia na kupelekwa katika kambi ya kazi ngumu mpaka wakati ambapo rais wa nchi hiyo alimsamehe na kuagiza aachiliwe huru. Katika kipindi hicho chote kigumu, Jovidon aliendelea kudumisha utimilifu na furaha yake. Jinsi gani? Kwa kutambua sikuzote uhitaji wake wa kiroho.

Jovidon alikula chakula cha kiroho, aliishi kulingana na viwango vya Mungu, na kutanguliza ibada ya Yehova maishani mwake (Tazama fungu la 15 hadi 17)

15. Nĩatĩa Jovidon aarĩjaga biakũrĩa bia gĩkĩrundu rĩrĩa aarĩ nceera?

15 Alipokuwa gerezani, Jovidon alikula chakula cha kiroho hata wakati ambapo hakuwa na Biblia wala machapisho yetu. Hilo liliwezekanaje? Ndugu na dada katika eneo hilo walimpelekea chakula cha kimwili na wakaandika andiko la siku kwenye mfuko wa kubebea bidhaa. Hivyo, alifaulu kusoma Biblia na kuitafakari kila siku. Baada ya kuachiliwa huru kutoka gerezani, alitoa ushauri huu kwa wale ambao bado hawajakabili majaribu makali: “Ni jambo muhimu sana utumie uhuru wako kikamili kwa kuongeza ujuzi wako kumhusu Yehova kupitia kusoma Neno lake na machapisho yetu.”

16. Nĩmbi Jovidon eekaga mathũgaanione jaawe?

16 Ndugu yetu aliishi kulingana na viwango vya Yehova. Badala ya kukazia fikira tamaa zisizofaa na kujihusisha na mwenendo mbaya, alimkazia fikira Yehova na mambo anayothamini. Jovidon alistaajabishwa na umaridadi wa uumbaji wa Yehova. Kila asubuhi alipoamka, alisikia sauti za ndege wakiimba. Usiku alitazama mwezi na nyota. Alisema: “Zawadi hizo kutoka kwa Yehova zilinifanya nihisi furaha na kunitia moyo.” Tunapothamini maandalizi ya Yehova ya kiroho na ya kimwili, tunapata shangwe moyoni, na shangwe hiyo inaweza kuimarisha uwezo wetu wa kuvumilia.

17. Nĩatĩa biugo bia 1 Petero 1:6, 7 biũmba gũtethia muntũ ũrĩa ũgũkũrũkĩĩra ũntũ ta bwa Jovidon?

17 Pia, Jovidon alitanguliza ibada ya Yehova maishani mwake. Alijua umuhimu wa kudumisha utimilifu wake kumwelekea Mungu wa kweli. Yesu alisema hivi: “Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.” (Luka 4:8) Makamanda wa jeshi na wanajeshi walitaka Jovidon akane dini yake. Badala yake, alisali kwa bidii kila siku, mchana na usiku, akimwomba Yehova amsaidie asikate tamaa na aendelee kuwa mwaminifu. Licha ya kutendewa kwa njia isiyo ya haki, Jovidon hakulegeza msimamo wake kamwe. Matokeo ni kwamba anashangilia kwa kuwa ana kitu ambacho hakuwa nacho kabla ya kutekwa nyara, kupigwa, na kufungwa gerezani, yaani, imani iliyojaribiwa.​—Soma 1 Petro 1:6, 7.

18. Nĩatĩa tũũmba gũtũũria kũgwĩrua gwetũ?

18 Yehova anajua kile tunachohitaji ili tuwe na furaha ya kweli. Ikiwa utafuata hatua tatu zinazoongoza kwenye furaha ya kweli, unaweza kudumisha furaha yako licha ya kukabili hali ngumu. Kisha wewe pia utaweza kusema hivi: “Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!”​—Zab. 144:15.

RWĨMBO 89 Sikiliza, Tii, Upate Baraka

a Kwa watu wengi, ni vigumu kupata furaha ya kweli kwa sababu wanatafuta furaha kwa njia isiyofaa kwa kufuatia anasa, mali, umashuhuri, au mamlaka. Ingawa hivyo, Yesu alipokuwa duniani aliwafundisha watu jinsi ya kupata furaha. Katika makala hii, tutachunguza hatua tatu zinazoweza kutusaidia kupata furaha ya kweli.

b Soma pia makala “Je, Unapata ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’? ” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 2014.

c Kwa habari zaidi, tafuta maneno “Wamefungwa kwa Sababu ya Imani Yao” kwenye jw.org.

d MAELEZO YA PICHA: Katika igizo hili, Mashahidi wanamuunga mkono ndugu ambaye anakamatwa na kupelekwa mahakamani ili kushtakiwa.