Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 41

RWĨMBO 13 Kristo, Kielelezo Chetu

Jarĩa Tũũmba Kwiritana Kuumania na Ntukũ 40 cia Mũthia cia Jesũ aja Nthĩgũrũne

Jarĩa Tũũmba Kwiritana Kuumania na Ntukũ 40 cia Mũthia cia Jesũ aja Nthĩgũrũne

‘Nawe aroonwa nĩbo ĩgiita rĩa ntukũ mĩrongo ĩna akiaragia mantũ ja Ũnene bwa Mũrungu.’—ATUM. 1:3.

JAMBO KUU

Jinsi ya kuiga mfano wa Yesu ambao alituwekea katika zile siku 40 za mwisho akiwa duniani.

1-2. Nĩatĩa gwakarĩkĩre rĩrĩa aritwa baĩrĩ ba Jesũ beetĩte Emaũ?

 NI NISANI 16, 33 W.K. Wanafunzi wa Yesu wana huzuni na wanaogopa sana. Wanafunzi wawili wanaondoka Yerusalemu na kuelekea Emau, kijiji kilicho kilomita 11 kutoka Yerusalemu. Wanaume hao wamevunjika moyo sana kwa sababu Yesu, mwanamume ambaye wamekuwa wakimfuata, alikuwa ametoka tu kuuawa. Tumaini lao la kwamba Masihi angefanya mambo yenye kustaajabisha lilionekana halingetimia. Lakini jambo ambalo hawakutarajia likatokea.

2 Wakiwa njiani wanakutana na mwanamume wasiyemfahamu. Wanafunzi hao wanamweleza jinsi walivyovunjika moyo kwa sababu ya mambo yaliyompata Yesu. Kisha, mwanamume huyo wasiyemfahamu anaanza kuzungumzia mambo ambayo hawatasahau kamwe maishani. Akiwafafanulia “kuanzia Musa na Manabii wote,” anawaeleza kwa nini ilikuwa lazima Masihi ateswe na kufa. Wanaume hao watatu wanapofika katika kijiji cha Emau, yule mwanamume anajitambulisha kwamba yeye ndiye Yesu aliyefufuliwa! Wazia shangwe ambayo wanafunzi hao walikuwa nayo walipojua kwamba Masihi alikuwa hai!—Luka 24:​13-35.

3-4. Nĩmbi biakarĩkĩĩre aritwa ba Jesũ, na nĩmbi tũkairitana kĩthoomone gĩkĩ? (Mathithio 1:3)

3 Yesu aliwatokea wanafunzi wake mara kadhaa katika zile siku 40 za mwisho akiwa duniani. (Soma Matendo 1:3.) Katika kipindi hicho, wafuasi wa Yesu waliokuwa na huzuni na woga, walibadilika na kuwa walimu na wahubiri wa Ufalme wenye shangwe, uhakika, na ujasiri. a

4 Tunaweza kunufaika kwa kujifunza kuhusu kipindi hicho chenye kusisimua cha maisha ya Yesu. Katika makala hii, tutajifunza kuhusu jinsi Yesu alivyotumia kipindi hicho (1) kuwatia moyo wanafunzi wake, (2) kuwasaidia waongeze uelewaji wao wa Maandiko, na (3) kuwazoeza ili watimize majukumu makubwa zaidi. Tutajifunza jinsi tunavyoweza kuiga mfano wa Yesu katika njia hizo.

ĨKĨRA BANGĨ INYA

5. Nĩkĩ aritwa ba Jesũ baabataraga gwĩkĩrwa inya?

5 Wanafunzi wa Yesu walihitaji kutiwa moyo. Kwa nini? Kwa sababu baadhi yao walikuwa wameacha nyumba, familia, na biashara ili wamfuate Yesu wakati wote. (Mt. 19:27) Wengine walitengwa na jamii kwa sababu ya kuwa wanafunzi wake. (Yoh. 9:22) Walikuwa tayari kujidhabihu kwa njia hizo kwa sababu waliamini kwamba Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa. (Mt. 16:16) Lakini Yesu alipouawa, walivunjika moyo kwa sababu walidhani kwamba mambo ambayo walitumaini hayangetimia.

6. Nĩmbi Jesũ aathithĩrie nyuma ya kũriũkua?

6 Bila shaka, Yesu alijua kwamba huzuni ya wanafunzi wake haikuwa ishara ya udhaifu wa kiroho, bali zilikuwa hisia za kawaida baada ya kufiwa na mpendwa wao. Hivyo, siku ileile aliyofufuliwa, alianza kuwatia moyo rafiki zake. Kwa mfano, alimtokea Maria Magdalene alipokuwa akilia kwenye kaburi lake. (Yoh. 20:​11, 16) Pia, aliwatokea wale wanafunzi wawili waliotajwa awali. Na alimtokea mtume Petro. (Luka 24:34) Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Yesu? Fikiria jambo lililotokea baada ya Yesu kufufuliwa na kumtokea kwanza Maria Magdalene.

7. O ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ Johana 20:​11-16, nĩatĩa Jesũ oonere Mariamu akĩthithagia rũũkĩrĩ rwa Nisani 16, na ũntũ bũu bwatũmĩre athithia atĩa? (Tega kinya mbica.)

7 Soma Yohana 20:​11-16. Mapema asubuhi ya Nisani 16, wanawake kadhaa washikamanifu walienda mahali ambapo kaburi la Yesu lilikuwa. (Luka 24:​1, 10) Acheni tuchunguze kisa cha mmoja wa wanawake hao, Maria Magdalene. Maria alipofika kwenye kaburi, lilikuwa tupu. Alikimbia na kwenda kumwambia Petro na Yohana, kisha akawafuata walipokuwa wakielekea kwenye kaburi. Baada ya wanaume hao kuthibitisha kwamba kaburi lilikuwa tupu, walirudi nyumbani. Lakini Maria hakurudi. Alibaki hapo akilia. Yesu alikuwa akimtazama, ingawa Maria hakujua. Aliyaona machozi ya mwanamke huyo mwaminifu, naye aliguswa moyo sana. Hivyo, alimtokea Maria, kisha akafanya jambo rahisi ambalo lilimtia moyo sana. Yesu alizungumza naye na kumpatia mgawo muhimu—wa kuwaambia ndugu zake kwamba amefufuliwa.—Yoh. 20:​17, 18.

Mwige Yesu kwa kuwa mwenye utambuzi na kwa kuwaonyesha hisia mwenzi wale waliovunjika moyo (Tazama fungu la 7)


8. Nĩatĩa tũũmba kwigerekania na Jesũ?

8 Tunawezaje kumwiga Yesu? Kama Yesu, tunaweza kuwachochea ndugu na dada zetu waendelee kumtumikia Yehova, ikiwa tutatambua mambo yanayowahangaisha na kuzungumza nao kwa hisia mwenzi. Fikiria mfano wa dada anayeitwa Jocelyn, ambaye dada yake alikufa katika aksidenti mbaya. Anasema hivi: “Kwa miezi mingi, muda wote nilikuwa na huzuni kubwa sana.” Hata hivyo, ndugu mmoja na mke wake walimwalika nyumbani kwao, wakamsikiliza kwa makini, na kumhakikishia kwamba ana thamani machoni pa Yehova. Jocelyn anasema hivi: “Nilihisi ni kana kwamba Yehova alikuwa amewatumia ili kunitoa kwenye bahari yenye dhoruba kali na kuniweka kwenye mashua ya kuokoa uhai. Walinisaidia kupata tena hamu ya kuendelea kumtumikia Yehova.” Sisi pia tunaweza kuwatia moyo wengine kwa kuwasikiliza kwa makini wanapotumiminia mioyo yao na kuzungumza nao kwa fadhili, tukiwa na lengo la kuwaimarisha ili waendelee kumtumikia Yehova.—Rom. 12:15.

TETHERIA BANGĨ BACIŨKĨRWE NĨ MAANDĨKO

9. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ aritwa ba Jesũ baacemanĩrie najo, na nĩatĩa Jesũ aabatetherie?

9 Wanafunzi wa Yesu walilikubali Neno la Mungu na walijitahidi kulitumia katika maisha yao. (Yoh. 17:6) Hata hivyo, hawakuelewa kwa nini Yesu alikufa kwenye mti wa mateso kama mhalifu. Yesu alitambua kwamba walikuwa na shaka, si kwa sababu ya kuwa na mioyo mibaya, lakini kwa sababu ya kukosa uelewaji. (Luka 9:​44, 45; Yoh. 20:9) Hivyo, aliwasaidia waelewe maana ya Maandiko. Fikiria jinsi alivyofanya hivyo alipowatokea wale wanafunzi wawili waliokuwa wakielekea Emau.

10. Nĩatĩa Jesũ arikĩthĩĩrie aritwa baawe atĩ kamma nĩwe aarĩ Mesiya? (Luka 24:​18-27)

10 Soma Luka 24:​18-27. Ona kwamba Yesu hakuwajulisha mara moja yeye alikuwa nani. Badala yake, aliwauliza maswali. Kwa nini? Huenda alitaka wamweleze mambo yaliyokuwa akilini na moyoni mwao. Nao walifanya hivyo. Walimwambia kwamba walitarajia Yesu angewakomboa Waisraeli kutoka katika ukandamizaji wa Waroma. Baada ya kueleza waziwazi mambo yaliyowahangaisha, Yesu alitumia Maandiko kuwasaidia wanaume hao waelewe kwamba kuna unabii mwingi uliokuwa umetimizwa. b Baadaye jioni hiyo, Yesu alitumia wakati kuwahakikishia wanafunzi wengine mambo hayo. (Luka 24:​33-48) Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi hilo?

11-12. (a) Nĩmbi tũkwiritana kuumania na njĩra ĩrĩa Jesũ aatumĩre kũritana mma cia Bibiria? (Tega kinya mbica.) (b) Nĩatĩa mwarimũ wa Bibiria wa Nortey aamũtetherie?

11 Tunawezaje kumwiga Yesu? Kwanza, unapowafundisha wanafunzi wa Biblia, kwa busara waulize maswali yatakayokusaidia kujua kilicho akilini na moyoni mwao. (Met. 20:5) Unapoelewa hisia zao, waonyeshe jinsi ya kutafuta maandiko hususa wanayoweza kutumia katika hali zao. Kisha, epuka mwelekeo wa kuwaambia cha kufanya. Badala yake, wasaidie kuelewa maana ya Maandiko na kutambua jinsi wanavyoweza kutumia kanuni za Biblia maishani mwao. Fikiria kisa cha ndugu nchini Ghana anayeitwa Nortey.

12 Nortey alipokuwa na umri wa miaka 16, alianza kujifunza Biblia. Hata hivyo, baada ya muda mfupi, familia yake ilianza kumpinga. Nini kilichomsaidia kubaki imara? Mwalimu wake wa Biblia alikuwa ametumia kitabu cha Mathayo, sura ya 10, kumweleza kwamba Wakristo wa kweli wangeteswa. Nortey anasema hivi: “Hivyo, nilipoanza kuteswa, nilisadiki kwamba nilikuwa nimeipata kweli.” Pia, mwalimu wake alimsaidia kuelewa andiko la Mathayo 10:​16, ili awe mwangalifu na mwenye heshima anapozungumzia mambo yanayohusu dini akiwa nyumbani. Baada ya kubatizwa, Nortey alitaka kuanza upainia, lakini baba yake alitaka aende chuo kikuu. Badala ya kumwambia Nortey jambo la kufanya, mwalimu wake alimuuliza maswali ambayo yangeweza kumsaidia kutafakari kuhusu kanuni za Kimaandiko. Matokeo yalikuwa nini? Nortey aliamua kuanza utumishi wa wakati wote. Baba yake alimwambia aondoke nyumbani. Nortey anahisije kuhusu jambo hilo? Anasema hivi: “Ninasadiki kwamba nilifanya uamuzi sahihi.” Ikiwa sisi pia tutatumia wakati kuwasaidia wengine waelewe maana ya Maandiko, tutawasaidia kuwa Wakristo walio imara.—Efe. 3:​16-19.

Mwige Yesu kwa kuwasaidia wengine waelewe maana ya Maandiko (Tazama fungu la 11) e


TETHIA ANTŨ ARŨME KWAGĨRA KWAA “BIEWA” KĨRĨ ANTŨ

13. Nĩatĩa Jesũ aathithĩrie nĩkenda atigĩĩra ngũgĩ ya Ĩthe nĩgwĩta na mbere kũritwa? (Aefeso 4:8)

13 Alipokuwa duniani, Yesu alifanya kikamilifu kazi ambayo Baba yake alikuwa amempatia. (Yoh. 17:4) Lakini Yesu hakuwa na mtazamo wa kwamba ‘Ikiwa unataka jambo lifanywe kwa njia sahihi, ni lazima wewe mwenyewe ulifanye.’ Wakati wa miaka mitatu na nusu ya huduma yake, aliwazoeza wengine kufanya kazi hiyo. Kabla ya kurudi mbinguni, Yesu aliwakabidhi wanafunzi wake—ambao baadhi yao walikuwa katika miaka yao ya ishirini—jukumu la kuwatunza kondoo wenye thamani wa Yehova na kuongoza katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. (Soma Waefeso 4:8.) Yesu alitumiaje siku zake 40 za mwisho akiwa duniani kuwasaidia wanaume hao waliojitoa, washikamanifu, na wenye bidii wastahili ‘kuwa wanaume walio zawadi’?

14. Nĩatĩa Jesũ aatetherie aritwa baawe gũkũra gĩkĩrundu, ĩgiita rĩa ntukũ 40 ciawe cia mũthia aja nthĩgũrũne? (Tega kinya mbica.)

14 Yesu aliwapatia wanafunzi wake ushauri wa moja kwa moja lakini kwa upendo. Kwa mfano, alitambua kwamba baadhi yao walikuwa na mwelekeo wa kuwa na shaka, hivyo aliwapa shauri. (Luka 24:​25-27; Yoh. 20:27) Aliwaonyesha umuhimu wa kukazia zaidi kazi ya kulichunga kundi kuliko kazi zao za kimwili. (Yoh. 21:15) Aliwakumbusha kwamba wasihangaike kupita kiasi kuhusu mapendeleo ambayo huenda wengine wangepata katika utumishi wa Yehova. (Yoh. 21:​20-22) Na alirekebisha baadhi ya mawazo yasiyo sahihi waliyokuwa nayo kuhusu Ufalme na kuwasaidia kukazia fikira kazi ya kuhubiri habari njema. (Mdo. 1:​6-8) Wazee wa kutaniko wanaweza kujifunza nini kutoka kwa Yesu?

Mwige Yesu kwa kuwasaidia akina ndugu wastahili mapendeleo zaidi (Tazama fungu la 14)


15-16. (a) Nĩ na njĩra irĩkũ akũrũ ba kĩũthũrano bomba kwigerekania na Jesũ? Taarĩĩria. (b) Nĩatĩa Patrick aagunĩkĩre kuumania na ũtaaro bũrĩa aaerwe?

15 Wazee wa kutaniko wanawezaje kumwiga Yesu? Ni lazima wawazoeze na kuwasaidia wanaume, kutia ndani wale ambao wana umri mdogo, wastahili kutimiza majukumu makubwa zaidi. c Wazee wa kutaniko hawatarajii kwamba wale wanaowazoeza wawe wakamilifu. Wanapaswa kuwapatia ushauri wenye upendo ili akina ndugu vijana wapate uzoefu na waone uhitaji wa kuwa wanyenyekevu, waaminifu, na wawe tayari kuwatumikia wengine.—1 Tim. 3:1; 2 Tim. 2:2; 1 Pet. 5:5.

16 Fikiria jinsi ndugu anayeitwa Patrick alivyonufaika aliposhauriwa. Akiwa kijana, alikuwa na mwelekeo wa kuzungumza kwa ukali na kutenda kwa njia isiyo ya fadhili, hata kwa akina dada. Mzee wa kutaniko alitambua udhaifu wa Patrick na akampatia shauri la moja kwa moja, lakini kwa njia yenye fadhili. Patrick anasema hivi: “Ninafurahi kwamba alifanya hivyo. Nilikuwa ninavunjika moyo nilipokuwa nikiona akina ndugu wengine wakipata mapendeleo ya utumishi ambayo nilitamani. Lakini shauri la mzee huyo lilinisaidia kuona umuhimu wa kukazia fikira kuwatumikia ndugu na dada zangu kwa unyenyekevu, badala ya kukazia fikira mgawo au pendeleo fulani kutanikoni.” Matokeo ni kwamba Patrick aliwekwa rasmi kuwa mzee alipokuwa na umri wa miaka 23.—Met. 27:9.

17. Nĩatĩa Jesũ oonanĩrie atĩ neetĩkagia aritwa baawe?

17 Yesu aliwapa wanafunzi wake jukumu la kuhubiri na pia kufundisha. Huenda wanafunzi hao walihisi kwamba hawastahili kupewa mgawo huo. Hata hivyo, Yesu hakuwa na shaka kwamba wangeweza kutimiza kazi hiyo, na aliwaambia hivyo. Akionyesha kwamba anawatumaini kabisa, Yesu alisema: “Kama vile ambavyo Baba amenituma, mimi pia ninawatuma ninyi.”—Yoh. 20:21.

18. Nĩatĩa akũrũ ba kĩũthũrano bomba kwigerekania na Jesũ?

18 Wazee wa kutaniko wanawezaje kumwiga Yesu? Wazee wenye uzoefu huwapa wengine majukumu. (Flp. 2:​19-22) Kwa mfano, wazee wanaweza kuwahusisha vijana katika usafi na udumishaji wa Jumba la Ufalme. Baada ya kuwapatia kazi fulani, wazee wanaweza kuonyesha kwamba wanawatumaini wale ambao wamewapa kazi hiyo kwa kuwazoeza na kutumaini kwamba watafanya kazi hiyo kwa usahihi. Mzee mpya ambaye anaitwa Matthew anasema kwamba anathamini sana wakati wazee wenye uzoefu wanapomzoeza kikamili kufanya mgawo fulani na kutumaini kwamba atautimiza. Anasema hivi: “Nimenufaika walipoyaona makosa yangu kuwa sehemu ya hatua za kujifunza na kunisaidia kuboresha njia yangu ya kufanya kazi.” d

19. Tũbuĩrĩte gũtua ĩtua rĩa kũthithia atĩa?

19 Yesu alitumia zile siku 40 za mwisho akiwa duniani kuwatia moyo, kuwafundisha, na kuwazoeza wengine. Acheni tuazimie kufuata mfano wake kwa ukaribu. (1 Pet. 2:21) Atatusaidia kufanya hivyo. Isitoshe, aliahidi hivi: “Mimi nipo pamoja nanyi sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”—Mt. 28:20.

RWĨMBO 15 Msifuni Mzaliwa wa Kwanza wa Yehova!

a Vitabu vya Injili na vitabu vingine vya Biblia vina rekodi ya pindi nyingi ambazo Yesu aliyefufuliwa aliwatokea watu wengine, kama vile Maria Magdalene (Yoh. 20:​11-18); wale wanawake wengine (Mt. 28:​8-10; Luka 24:​8-11); wale wanafunzi wawili (Luka 24:​13-15); Petro (Luka 24:34); mitume isipokuwa Tomasi (Yoh. 20:​19-24); mitume, pamoja na Tomasi (Yoh. 20:26); wanafunzi 7 (Yoh. 21:​1, 2); zaidi ya wanafunzi 500 (Mt. 28:16; 1 Kor. 15:6); Yakobo, ndugu yake (1 Kor. 15:7); mitume wote (Mdo. 1:4); na mitume karibu na Bethania. (Luka 24:​50-52) Huenda pindi nyingine ambazo Yesu aliwatokea watu hazikurekodiwa.—Yoh. 21:25.

b Ili kupata orodha ya unabii mbalimbali wa Kimasihi, tazama makala yenye kichwa “Je, Unabii wa Kimasihi Unathibitisha Kwamba Yesu Alikuwa Ndiye Masihi?” kwenye jw.org.

c Katika visa fulani, wanaume wenye kustahili walio na umri wa miaka 25 hadi 30 wanaweza kuwekwa rasmi kuwa waangalizi wa mzunguko. Hata hivyo, ni lazima kwanza wanaume hao wapate uzoefu wa kutumikia wakiwa wazee wa kutaniko.

d Ili kupata mapendekezo zaidi kuhusu jinsi ya kuwasaidia akina ndugu vijana wastahili kupata mapendeleo, soma gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 2018, ukurasa wa 11-12, fungu la 15-17, na la Aprili 15, 2015, ukurasa wa 3-13.

e MAELEZO YA PICHA: Baada ya kusaidiwa kuelewa maana ya Maandiko, mwanafunzi wa Biblia anaamua kutupa mapambo yake ya Krismasi.