Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 38

RWĨMBO 25 Mali ya Pekee

Gwe Rĩ, Nũkũthingatĩĩra Mĩkaana?

Gwe Rĩ, Nũkũthingatĩĩra Mĩkaana?

“Umwe akajukua, na ungi atigwe.”MAT. 24:40.

JAMBO KUU

Tutachunguza mifano mitatu ya Yesu na kuzungumzia jinsi inavyohusiana na kipindi cha hukumu kitakachotukia mwishoni mwa mfumo huu wa mambo.

1. Nĩ kũgambithua kũrĩkũ gũgaakarĩka ĩgiita rĩtĩ kũraaja?

 TUNAISHI katika kipindi chenye kusisimua! Hivi karibuni, Yesu atamhukumu kila mtu aliye hai. Yesu alieleza kuhusu mambo ambayo yangetukia kabla ya hukumu hiyo kwa kuwapa wanafunzi wake “ishara” ya kinabii ya kuwapo kwake kusikoonekana na ya “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mt. 24:3) Unabii huo umerekodiwa kwenye sura ya 24 na 25 ya kitabu cha Mathayo na kwenye masimulizi yanayolingana kwenye Marko sura ya 13 na Luka sura ya 21.

2. Nĩ mantũ jarĩkũ tũkaarĩĩria, na kũthithia ũu gũgatũtethia atĩa?

2 Kupitia mifano mitatu, Yesu alitupatia maonyo yanayotusaidia. Mifano hiyo ni ile ya kondoo na mbuzi, mabikira wenye busara na mabikira wapumbavu, na mfano wa talanta. Kila mfano unatusaidia kuelewa jinsi matendo ya mtu yanavyoathiri hukumu atakayopata. Tunapochunguza mifano hiyo, acheni tutambue mambo tunayojifunza na jinsi tunavyoweza kuyatumia. Mfano wa kwanza tutakaozungumzia ni wa kondoo na mbuzi.

NGʼONDU NA MBŨRI

3. Nĩ ĩgiita rĩrĩkũ Jesũ akagambithia antũ?

3 Katika mfano wa kondoo na mbuzi, Yesu alizungumzia hukumu ya watu ambao wana fursa ya kuitikia vizuri wanapohubiriwa habari njema na kuwaunga mkono ndugu zake waliotiwa mafuta. (Mt. 25:​31-46) Wakati wa “dhiki kuu,” atatoa hukumu hiyo kabla tu ya Har–​Magedoni. (Mt. 24:21) Kama tu ambavyo mchungaji anawatenganisha kondoo na mbuzi, ndivyo ambavyo Yesu atawatenganisha wale wanaowaunga mkono kwa ushikamanifu wafuasi wake waliotiwa mafuta na wale ambao hawafanyi hivyo.

4. Kũringana na Isaya 11:​3, 4, nĩkĩ tũbuĩrĩte kwĩthĩrwa na mma atĩ Jesũ akagambithia antũ na ĩota? (Tega kinya mbica karatacine ka mbere.)

4 Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba Yesu, akiwa Mwamuzi aliyechaguliwa na Yehova, atahukumu kwa uadilifu. (Soma Isaya 11:3, 4.) Atachunguza matendo, mitazamo, na mambo ambayo watu wanasema—kutia ndani jinsi wanavyowatendea ndugu zake waliotiwa mafuta. (Mt. 12:​36, 37; 25:40) Yesu atawajua wale ambao waliwaunga mkono ndugu zake watiwa-mafuta na kuunga mkono kazi yao. a Njia moja kuu ambayo wale walio kama kondoo wanawaunga mkono ndugu za Kristo ni kwa kuwasaidia katika kazi ya kuhubiri. Wale wanaowaunga mkono watahukumiwa kuwa “waadilifu”na watakuwa na tumaini la kupata “uzima wa milele” duniani. (Mt. 25:46; Ufu. 7:​16, 17) Hiyo ni thawabu kubwa sana kwa wale wanaodumisha utimilifu wao! Kwa kubaki kuwa waaminifu wakati na baada ya dhiki kuu, majina yao yataendelea kuwa katika “kitabu cha uzima.”—Ufu. 20:15.

Hivi karibuni, Yesu atawahukumu watu kuwa kondoo au mbuzi (Tazama fungu la 4)


5. Nĩ kĩthoomo kĩrĩkũ tũkwiritana kuumania na njuno ya ngʼondu na mbũri, na nĩ baũ babuĩrĩte gũkucĩĩrua nĩyo?

5 Uwe mwaminifu na mshikamanifu. Mfano wa Yesu wa kondoo na mbuzi unawakazia hasa wale ambao wana tumaini la kuishi milele duniani. Wanaonyesha imani yao kwa kuwaunga mkono ndugu za Kristo katika kazi ya kuhubiri na pia kwa kukubali kwa ushikamanifu mwongozo wa kikundi kidogo cha ndugu waliotiwa mafuta ambao Yesu amewachagua. (Mt. 24:45) Lakini wale walio na tumaini la kuishi mbinguni wanahitaji pia kutii onyo lililo kwenye mfano huo. Kwa nini? Kwa sababu Yesu anachunguza matendo, mitazamo, na mambo wanayosema. Ni lazima wao pia wajithibitishe kuwa waaminifu. Isitoshe, Yesu alisimulia mifano mingine miwili ambayo ina maonyo hususa kwa watiwa-mafuta. Mifano hiyo inapatikana pia kwenye sura ya 25 ya kitabu cha Mathayo. Acheni sasa tuchunguze mfano wa mabikira wenye busara na mabikira wapumbavu.

AARĨ BABOOME NA BANGĨ BIAA

6. Nĩatĩa aarĩ batano kĩrĩ barĩa ĩkũmi boonanĩrie atĩ nĩbaarĩ na ũũme? (Mathayo 25:​6-10)

6 Katika mfano wa mabikira, Yesu alizungumza kuhusu mabikira kumi ambao walienda kumpokea bwana harusi. (Mt. 25:​1-4) Wote walitazamia kuandamana na bwana harusi kwenye karamu yake ya ndoa. Yesu alisema kwamba mabikira watano walikuwa “wenye busara” na wale wengine watano walikuwa “wapumbavu.” Wale mabikira wenye busara walikuwa tayari na walikaa macho. Walikuwa tayari kumsubiri bwana harusi kwa muda wowote uliohitajika, hata ikiwa angefika usiku sana. Hivyo, walibeba taa za mafuta ili zitoe mwangaza. Hata walibeba mafuta ya ziada ikiwa bwana harusi angechelewa. Hivyo, walihakikisha kwamba taa zao zingeendelea kuwaka. (Soma Mathayo 25:​6-10.) Bwana harusi alipofika, wale mabikira wenye busara waliingia ndani pamoja naye kwenye karamu ya ndoa. Vivyo hivyo, Wakristo watiwa-mafuta ambao wamethibitika kuwa tayari kwa kuendelea kukaa macho na kuwa waaminifu hadi kuja kwa Kristo, watahukumiwa kuwa wenye kustahili kujiunga pamoja na Bwana Harusi, Yesu, katika Ufalme wake wa mbinguni. b (Ufu. 7:​1-3) Namna gani wale mabikira watano wapumbavu?

7. Nĩmbi biakarĩkĩĩre aarĩ barĩa batano biaa, na nĩkĩ?

7 Tofauti na wale mabikira wenye busara, wale mabikira watano wapumbavu hawakuwa tayari bwana harusi alipofika. Taa zao zilikuwa karibu kuzimika, na hawakuwa wamebeba mafuta ya ziada. Waliposikia kwamba bwana harusi alikuwa karibu kufika, walihitaji kwenda kununua mafuta. Hawakuwa wamerudi bwana harusi alipowasili. Wakati huo, “mabikira waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye kwenye karamu ya ndoa, na mlango ukafungwa.” (Mt. 25:10) Baadaye, wale mabikira wapumbavu waliporudi na kutaka kuingia, bwana harusi aliwaambia hivi: “Siwajui ninyi.” (Mt. 25:​11, 12) Mabikira hao hawakuwa wamejitayarisha kumsubiri bwana harusi kwa muda wowote ambao ungehitajika. Watiwa-mafuta wanajifunza nini?

8-9. Nĩ kĩthoomo kĩrĩkũ etũrĩrua maguta bakwiritana kuumania na njuno ya aarĩ ĩkũmi? (Tega kinya mbica.)

8 Uwe tayari na ukae macho. Yesu hakuwa akitabiri kwamba kungekuwa na vikundi viwili vya watiwa-mafuta—kikundi kimoja kilichokuwa tayari kusubiri hadi mwisho wa mfumo huu wa mambo na kikundi kingine ambacho hakikuwa tayari. Badala yake, alikuwa akifafanua jambo ambalo lingewapata watiwa-mafuta ikiwa hawangekuwa tayari kuvumilia kwa uaminifu hadi mwisho. Hawangepokea thawabu yao. (Yoh. 14:​3, 4) Hilo ni jambo zito sana! Iwe tumaini letu ni la kuishi mbinguni au duniani, sisi sote tunapaswa kufikiria kwa uzito onyo linalopatikana kwenye mfano wa mabikira. Ni lazima kila mmoja wetu aendelee kuwa macho na kujitayarisha, akiwa tayari kuvumilia mpaka mwisho.—Mt. 24:13.

9 Baada ya kusimulia mfano wa mabikira ili kukazia umuhimu wa kuwa tayari na kukaa macho, Yesu alisimulia mfano wa talanta. Mfano huo unakazia umuhimu wa kuwa na bidii.

Itafaa kila mmoja wetu achukulie kwa uzito onyo katika mfano wa mabikira kwa kujitayarisha na kukaa macho, akiwa tayari kuvumilia mpaka mwisho (Tazama fungu la 8-9)


TALANTA

10. Nĩatĩa nkombo ijĩrĩ cionanĩrie nkuma ya wĩtĩkua? (Mathayo 25:​19-23)

10 Katika mfano wa talanta, Yesu alizungumza kuhusu watumwa wawili ambao walikuwa waaminifu kwa bwana wao na mmoja ambaye hakuwa mwaminifu. (Mt. 25:​14-18) Watumwa hao wawili walithibitika kuwa waaminifu kwa kufanya kazi kwa bidii ili kuongeza faida ya bwana wao. Kabla ya kusafiri ng’ambo, aliwakabidhi talanta—kiasi kikubwa cha pesa. Wale watumwa wawili waaminifu walikuwa na bidii na walitumia pesa kwa hekima. Matokeo yalikuwaje? Bwana wao aliporudi walikuwa wamepata mara mbili ya kile alichowapatia. Bwana wao aliwapongeza—wakaingia “katika shangwe ya bwana [wao].” (Soma Mathayo 25:​19-23.) Lakini namna gani kuhusu mtumwa wa tatu? Alitumiaje pesa ambazo bwana wake alimpatia?

11. Nĩmbi biakarĩkĩĩre nkombo ĩrĩa yaarĩ na ‘ũthao,’ na nĩkĩ?

11 Mtumwa wa tatu alipokea talanta moja lakini alikuwa “mvivu.” Bwana wake alitarajia atumie talanta hiyo kwa hekima. Badala yake, aliificha ardhini. Bwana wake aliporudi, mtumwa huyo hakuwa na kitu chochote cha ziada cha kumpatia bwana wake. Mtumwa huyo hakuwa na mtazamo mzuri. Badala ya kuomba msamaha kwa sababu alishindwa kuongeza mali za bwana wake, mtumwa huyo alimhukumu bwana wake isivyo haki na kumwita “mtu mgumu.” Mtumwa huyo hakupata kibali cha bwana wake. Zaidi ya hilo, alinyang’anywa talanta yake na kutupwa nje ya nyumba ya bwana wake.—Mt. 25:​24, 26-30.

12. Nkombo irĩa ijĩrĩ mbĩtĩkua irĩrũngamĩĩra baaũ ntukũne cietũ?

12 Wale watumwa wawili waaminifu wanafananisha Wakristo watiwa-mafuta walio waaminifu. Bwana wao, Yesu, anawaalika waingie “katika shangwe ya bwana [wao].” Wanapokea thawabu yao ya kimbingu, ufufuo wa kwanza. (Mt. 25:​21, 23; Ufu. 20:5b) Kwa upande mwingine, mfano mbaya wa mtumwa mvivu unawapatia onyo watiwa-mafuta. Jinsi gani?

13-14. Nĩ ithoomo birĩkũ etũrĩrua maguta bakwiritana kuumania na njuno ya talanta? (Tega kinya mbica.)

13 Uwe mwenye bidii. Katika mfano wa talanta, kama ilivyokuwa tu katika mfano wa mabikira, Yesu hakuwa akitabiri kwamba watiwa-mafuta wangekuwa wavivu. Badala yake, alikuwa akieleza mambo ambayo yangetukia ikiwa wangepoteza bidii yao. Wangeshindwa kufanya “mwito na kuchaguliwa [kwao] kuwe hakika kwa ajili [yao],” na hawangeruhusiwa kuingia katika Ufalme wa mbinguni.—2 Pet. 1:10.

14 Mfano wa Yesu wa mabikira na wa talanta unaonyesha wazi kwamba Wakristo watiwa-mafuta wote wanahitaji kuwa tayari na kukaa macho pamoja na kuwa na bidii. Lakini je, Yesu alisema jambo lingine lolote ambalo ni onyo kwa watiwa-mafuta? Ndiyo! Maneno ya Yesu yanayopatikana kwenye Mathayo 24:​40, 41 yanahusiana pia na hukumu ya mwisho ya watiwa-mafuta.

Yesu anapendezwa kuwaona watiwa-mafuta wakijithibitisha kuwa wenye bidii (Tazama fungu la 13-14) d


NĨ BAAŨ ‘BAKAJŨKUA’?

15-16. Nĩatĩa ĩandĩko rĩa Mathayo 24:​40, 41, rĩkwonania ũbatu bwa etũrĩrua maguta gũkara baimenyeerete?

15 Kabla ya kusimulia mifano hiyo mitatu, Yesu alizungumzia hukumu ya mwisho ya watiwa-mafuta ambayo ingefunua ni nani ambao wangepata kibali. Alizungumzia wanaume wawili waliofanya kazi shambani na wanawake wawili waliokuwa wakisaga kwenye jiwe la kusagia. Katika kila kisa, wote wawili wanaonekana wakifanya kazi ileile, lakini Yesu alisema kwamba ‘mmoja angechukuliwa na mwingine angeachwa.’ (Soma Mathayo 24:​40, 41.) Kisha aliwahimiza wafuasi wake hivi: “Endeleeni kukesha kwa sababu hamjui Bwana wenu atakuja siku gani.” (Mt. 24:42) Yesu alisema jambo linalofanana na hilo katika mfano wa mabikira. (Mt. 25:13) Je, maneno hayo yanahusiana? Inaonekana hivyo. Watiwa-mafuta waaminifu na wanyoofu pekee ndio ‘watakaochukuliwa,’ na kupokelewa na Yesu katika Ufalme wa mbinguni.—Yoh.14:3.

16 Endelea kukesha. Mtiwa-mafuta yeyote ambaye haendelei kuwa macho kiroho hatakusanywa pamoja na wale “waliochaguliwa.” (Mt. 24:31) Na watu wote wenye tumaini la kuishi milele duniani pia wanapaswa kuyaona maneno ya Yesu kuwa onyo la kuendelea kukesha na kuwa waaminifu.

17. Nĩkĩ tũtĩbuĩrĩte gũcumbũka rĩrĩa Jehova athuura gwĩtũũrĩria bamwe maguta na kĩrundu kĩawe gĩkĩtheru?

17 Kwa kuwa tumemjua Yehova vizuri, tunatumaini hukumu zake. Hivyo, hatuhangaishwi ikiwa Yehova amechagua kuwatia mafuta baadhi ya watu waaminifu katika miaka ya karibuni. c Tunakumbuka mambo ambayo Yesu alisema katika mfano wake wa shamba la mizabibu kuhusu wafanyakazi waliofika saa kumi na moja. (Mt. 20:​1-16) Wale ambao walialikwa kufanya kazi katika shamba la mizabibu baadaye siku hiyo, walipokea mshahara uleule ambao wale walioanza kazi mapema walilipwa. Vivyo hivyo, haidhuru wakati ambao watiwa-mafuta wanachaguliwa, watapokea thawabu yao mbinguni ikiwa watahukumiwa kuwa waaminifu.

ATHĨKĨRA MĨKAANA

18-19. Nĩ ithoomo na mĩkaana ĩrĩkũ tũgacũnkũũna?

18 Tumechunguza nini? Kwa wale wenye tumaini la kuishi milele duniani, mfano wa kondoo na mbuzi unakazia umuhimu wa kuendelea kuwa waaminifu na washikamanifu kwa Yehova—sasa na wakati wa dhiki kuu inayokuja. Wakati huo ujao, Yesu atawahukumu wale walio waaminifu kuwa wanastahili kupata “uzima wa milele.”—Mt. 25:46.

19 Pia, tulichunguza mifano miwili inayowapatia maonyo watiwa-mafuta. Katika mfano wa Yesu wa mabikira wenye busara na mabikira wapumbavu, watano kati yao walithibitika kuwa wenye hekima. Walijitayarisha na walikaa macho, wakiwa tayari kumsubiri bwana harusi kwa muda wowote uliohitajika. Lakini mabikira wapumbavu hawakujitayarisha. Hivyo, bwana harusi hakuwaruhusu waingie katika karamu yake ya ndoa. Ni lazima sisi pia tuwe tayari kusubiri kwa muda wowote unaohitajika hadi Yesu atakapoleta mwisho wa mfumo huu wa mambo. Pia, katika mfano wa Yesu wa talanta, tulichunguza watumwa wawili waaminifu ambao walikuwa na bidii. Walifanya kazi kwa bidii kwa ajili ya bwana wao na wakapata kibali chake. Hata hivyo, mtumwa mvivu alikataliwa. Tumejifunza nini? Ni lazima tuwe na mengi ya kufanya katika utumishi wa Yehova hadi mwisho utakapofika. Na hatimaye, tulichunguza jinsi watiwa-mafuta wanavyopaswa kuendelea kukesha ili ‘wachukuliwe’ na Yesu na kupata thawabu yao mbinguni. Wakiwa na hamu kubwa, watiwa-mafuta hao wanatazamia ‘kukusanywa pamoja’ kwa Yesu mbinguni. Baada ya vita vya Har–​Magedoni, watakuwa bibi harusi wa Yesu katika ndoa ya Mwanakondoo.—2 The. 2:1; Ufu. 19:9.

20. Nĩatĩa Jehova akathithĩria barĩa bathikagĩĩra mĩkaana yaawe?

20 Ingawa saa ya hukumu inakaribia sana, hatuna sababu ya kuogopa. Ikiwa tutaendelea kuwa waaminifu, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo atatupatia “nguvu zinazopita zile za kawaida” ili “[tufanikiwe] . . . kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.” (2 Kor. 4:7; Luka 21:36) Iwe tumaini letu ni la kuishi mbinguni au duniani, tutamfurahisha Baba yetu ikiwa tutatii maonyo yanayopatikana katika mifano ya Yesu. Kupitia fadhili zisizostahiliwa za Yehova, majina yetu yatapatikana ‘yakiwa yameandikwa katika kile kitabu’ cha uzima.—Dan. 12:1; Ufu. 3:5.

RWĨMBO 26 Mlinitendea Mimi

a Tazama makala “Tunajua Nini Kuhusu Hukumu za Yehova za Wakati Ujao?” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Mei 2024.

b Kwa habari zaidi, tazama makala “Je, ‘Utaendelea Kukesha’?” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 2015.

d MAELEZO YA PICHA: Dada mtiwa-mafuta anaongoza funzo la Biblia pamoja na mwanamke kijana ambaye amempata katika huduma.