Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 49

RWĨMBO 147 Uzima wa Milele Umeahidiwa

Ũũmba Kũthithia Atĩa Nĩkenda Ũtũũra Kenya na Kenya?

Ũũmba Kũthithia Atĩa Nĩkenda Ũtũũra Kenya na Kenya?

“O muntu o muntu uria wonete Mutana na akamwitikia, agite mwoyo jwa kenya na kenya.”JOH. 6:40.

JAMBO KUU

Jinsi watiwa-mafuta na kondoo wengine wanavyonufaika na dhabihu ya Yesu Kristo.

1. Nĩatĩa bamwe baigagua bwegie gũtũũra kenya na kenya?

 WATU wengi wanakuwa makini kuhusu chakula wanachokula na wanajitahidi kufanya mazoezi kwa ukawaida ili wawe na afya nzuri. Hata hivyo, hawatarajii kuishi milele. Huenda wanafikiri kwamba haiwezekani kuishi milele na hawaoni hilo kuwa jambo lenye kutamanika kwa sababu ya matatizo yanayosababishwa na uzee. Hata hivyo, Yesu alizungumzia “uzima wa milele” kwa njia nzuri kama inavyoonyeshwa kwenye Yohana 3:16 na 5:24.

2. Nĩatĩa Johana mũrango jwa 6 jugaga bwegie mwoyo jwa kenya na kenya? (Johana 6:​39, 40)

2 Siku moja, Yesu aliulisha kimuujiza umati wa maelfu ya watu mikate na samaki. a Hilo lilikuwa jambo lenye kustaajabisha, lakini jambo alilosema siku iliyofuata lilikuwa lenye kustaajabisha hata zaidi. Umati huo ulikuwa umemfuata Kapernaumu, karibu na ufuo wa Bahari ya Galilaya, ambako Yesu aliwaambia watu kwamba wangeweza kufufuliwa na kufurahia uzima wa milele. (Soma Yohana 6:​39, 40.) Fikiria ahadi hiyo inamaanisha nini kwa marafiki na wapendwa wako ambao wamekufa. Maneno ya Yesu yanaonyesha kwamba watu wengi ambao wamekufa wanaweza kufufuliwa. Wewe pamoja na wapendwa wako mnaweza kufurahia uzima wa milele. Hata hivyo, imekuwa vigumu kwa wengi kuelewa maneno ambayo Yesu alisema kwenye mistari inayofuata katika Yohana sura ya 6. Acheni tuyachunguze kwa kina zaidi.

3. Kũringana na Johana 6:​51, nĩ ũntũ bũrĩkũ Jesũ aaguũrĩre bũmwegie?

3 Umati wa watu uliokuwa Kapernaumu waliona uhusiano kati ya mikate ambayo Yesu alikuwa ametoka kuwalisha watu na mana ambayo Yehova aliwaandalia mababu zao. Isitoshe, Maandiko yanaiita mana hiyo “mkate kutoka mbinguni.” (Zab. 105:40; Yoh. 6:31) Yesu alitumia mana kama msingi wa jambo ambalo angefundisha. Ingawa Mungu alikuwa amewaandalia mana hiyo kimuujiza, wale walioila mwishowe walikufa. (Yoh. 6:49) Kwa upande mwingine, Yesu alijiita “mkate wa kweli kutoka mbinguni,” “mkate wa Mungu,” na “mkate wa uzima.” (Yoh. 6:​32, 33, 35) Yesu alionyesha tofauti muhimu kati yake mwenyewe na mana. Alisema hivi: “Mimi ndio mkate ulio hai ambao ulishuka kutoka mbinguni. Yeyote akila mkate huu ataishi milele.” (Soma Yohana 6:51.) Wayahudi waliomsikiliza hawakumwelewa. Yesu angewezaje kudai kwamba alikuwa ameshuka kutoka mbinguni akiwa “mkate” ulio bora zaidi kuliko ule ambao Mungu aliwaandalia kimuujiza mababu zao? Yesu aliwaambia hivi: “Mkate nitakaotoa ni mwili wangu.” Alimaanisha nini? Ni muhimu kwetu kuelewa alichomaanisha kwa sababu jibu linaonyesha jinsi inavyowezekana kwetu na kwa wapendwa wetu waliokufa kupata uzima wa milele. Acheni tuone Yesu alimaanisha nini.

BIUGO MŨGATE JWA MWOYO NA MWĨRĨ JWAWE BIONANAGIA ATĨA

4. Nĩkĩ antũ bamwe baamakĩrue nĩ biugo bia Jesũ?

4 Baadhi ya watu waliokuwa wakimsikiliza Yesu walishtuka aliposema angetoa “mwili [wake] kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” Je, walifikiri kwamba angewapa mwili wake halisi ili wale? (Yoh. 6:52) Ona jambo hili lingine lenye kushtua ambalo Yesu aliwaambia: “Msipokula mwili wa Mwana wa binadamu na kunywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.”—Yoh. 6:53.

5. Nĩkĩ tũrĩna mma atĩ, Jesũ aatonanagia no mwanka antũ barĩngĩnyua tharĩke yaawe yongwa?

5 Katika siku za Noa, Mungu aliwakataza wanadamu kula damu. (Mwa. 9:​3, 4) Yehova alirudia tena amri hiyo alipowapa Waisraeli Sheria. Mtu yeyote ambaye angekula damu ‘angeuawa.’ (Law. 7:27) Yesu alishika Sheria hiyo. (Mt. 5:​17-19) Hivyo, ni jambo lisilowezekana kwamba angeuhimiza umati wa Wayahudi ule mwili wake halisi au kunywa damu yake. Lakini, kwa kusema maneno hayo yenye kushtua, Yesu alitaka kuwafundisha watu jinsi ya kupata “uzima wa milele.”—Yoh. 6:54.

6. Nĩkĩ tũũmba kuuga atĩ, biugo bia Jesũ biegie kũnyua tharike yaawe na kũrĩa mwĩrĩ jwawe biarĩ bia ngerekano?

6 Yesu alimaanisha nini? Ni wazi kwamba Yesu alikuwa akizungumza kwa njia ya mfano, kama alivyofanya mapema alipomwambia mwanamke Msamaria hivi: “Yeyote atakayekunywa maji nitakayompa hatakuwa na kiu kamwe, kwa sababu maji ambayo nitampa yatakuwa kama chemchemi ya maji ndani yake, inayobubujika ili kumpa uzima wa milele.” (Yoh. 4:​7, 14) b Yesu hakumaanisha kwamba mwanamke huyo angepata uzima wa milele kwa kunywa tu maji fulani halisi. Vivyo hivyo, hakumaanisha kwamba umati aliozungumza nao Kapernaumu ungeishi milele ikiwa ungekula mwili wake halisi na kunywa damu yake halisi.

MWANYA JWA BIATHO BIU BIO BIĨRĨ

7. Nĩatĩa antũ bamwe baugaga bwegie rwaria rwa Jesũ rũrĩa rũrĩ kĩrĩ Johana 6:53?

7 Baadhi ya watu wanadai kwamba maneno ya Yesu yanayopatikana kwenye Yohana 6:53 kuhusu kula mwili na kunywa damu yake yaliweka kielelezo cha kufuatwa wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana kwa sababu baadaye katika tukio hilo alitumia maneno yanayofanana. (Mt. 26:​26-28) Wanadai kwamba kila mtu anayehudhuria Mlo wa Jioni wa Bwana anapaswa kula mkate na kunywa divai inayopitishwa kwa wahudhuriaji. Je, hilo ni sahihi? Ni muhimu tutafute ukweli wa dai hilo kwa sababu kila mwaka mamilioni ya watu ulimwenguni kote hujiunga nasi kwa ajili ya tukio hilo. Tutaona tofauti kadhaa kati ya mambo yanayosemwa kwenye Yohana 6:53 na mambo ambayo Yesu alisema kwenye Mlo wa Jioni wa Bwana.

8. Nĩ mwanya jũrĩkũ jũrĩo gatĩgatĩ ka biatho biu bio biĩrĩ biarĩĩrĩtue nĩ Jesũ? (Tega kinya mbica.)

8 Acheni sasa tuchunguze tofauti kati ya matukio hayo mawili. Kwanza, Yesu alisema maneno yaliyo kwenye Yohana 6:​53-56 lini na wapi? Alizungumza akiwa mbele ya umati wa Wayahudi huko Galilaya mwaka wa 32 W.K. Huo ulikuwa mwaka mmoja kabla ya kuanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana jijini Yerusalemu. Pili, alikuwa akizungumza na nani? Wengi wa wasikilizaji wake huko Galilaya walikazia fikira zaidi kutosheleza mahitaji yao ya kimwili, kuliko kutosheleza mahitaji yao ya kiroho. (Yoh. 6:26) Isitoshe, Yesu aliposema jambo ambalo lilikuwa gumu kwao kuelewa, waliacha kumwamini. Hata baadhi ya wanafunzi wake waliacha kumfuata. (Yoh. 6:​14, 36, 42, 60, 64, 66) Linganisha tukio hilo na kile kilichotokea mwaka mmoja baadaye, mwaka wa 33 W.K., Yesu alipoanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana. Katika pindi hiyo, mitume wake washikamanifu 11 waliendelea kushirikiana naye hata ingawa hawakuelewa kikamili mambo yote ambayo Yesu alikuwa akifundisha. Tofauti na watu wengi huko Galilaya, mitume wake waaminifu walikuwa na uhakika kwamba Yesu alikuwa Mwana wa Mungu aliyekuja kutoka mbinguni. (Mt. 16:16) Yesu aliwapongeza wanafunzi wake hivi: “Ninyi ndio mmeshikamana nami katika majaribu yangu.” (Luka 22:28) Tofauti hizo mbili pekee zinaonyesha kuwa dai la kwamba maneno ya Yesu kwenye Yohana 6:53 yaliweka kielelezo cha kufuatwa wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana si la kweli. Lakini kuna uthibitisho mwingine zaidi.

Yohana sura ya 6 inasimulia kuhusu jambo ambalo Yesu aliuambia umati wa Wayahudi huko Galilaya (kushoto). Mwaka mmoja baadaye alizungumza na kikundi kidogo cha mitume wake waaminifu jijini Yerusalemu (kulia) (Tazama fungu la 8)


ŨNTŨ BŨU NĨ BŨKWEGIE

9. Nĩ gĩkundĩ kĩrĩkũ kĩa antũ Jesũ aaragĩĩria kĩrĩ Bĩakũrĩa bia Mwathani bĩa Ũgoro?

9 Katika Mlo wa Jioni wa Bwana, Yesu aliwapatia mitume wake mkate usiotiwa chachu na kuwaambia kwamba ulifananisha mwili wake. Kisha, akawapa divai na kuwaambia kwamba inamaanisha “damu . . . ya agano.” (Marko 14:​22-25; Luka 22:20; 1 Kor. 11:24) Hilo ni jambo muhimu sana. Agano jipya linafanyizwa na “nyumba ya Israeli [la kiroho]”—ambao watakuwa “katika Ufalme wa Mungu”—si pamoja na wanadamu kwa ujumla. (Ebr. 8:​6, 10; 9:15) Mitume hawakuelewa jambo hilo wakati huo, lakini baada ya muda mfupi wangetiwa mafuta kwa roho takatifu na kuingia katika agano jipya ili wawe na mahali pamoja na Yesu mbinguni.—Yoh. 14:​2, 3.

10. Nĩ mwanya jũrĩkũ jũrĩo kĩrĩ mantũ jarĩa Jesũ aarĩrie rĩrĩa aarĩ Galilaya, na jarĩa aarĩrie kĩrĩ Bĩakũrĩa bia Mwathani bĩa Ũgoro? (Tega kinya mbica.)

10 Ona kwamba wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana, Yesu alikazia fikira “kundi dogo.” Mitume wake waaminifu ambao walikuwa pamoja naye katika kile chumba, walikuwa washiriki wa kwanza katika kikundi hicho kidogo. (Luka 12:32) Wao pamoja na wengine ambao wangekuwa katika kikundi hicho walitarajiwa kushiriki ile mifano miwili—mkate na divai. Wao ndio watakaokuwa pamoja na Yesu mbinguni. Hivyo, hii ni tofauti nyingine kati ya Mlo wa Jioni wa Bwana na tukio lililotokea mapema huko Galilaya. Mambo ambayo Yesu alisema katika Mlo wa Jioni wa Bwana yalihusu tu kikundi kidogo cha watu. Lakini mambo ambayo aliuambia ule umati huko Galilaya yaliwahusu watu wengi.

Wale wanaokula mkate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho ni kikundi kidogo, lakini mtu yeyote anaweza kuonyesha imani katika Yesu na kupata uzima wa milele (Tazama fungu la 10)


11. Nĩ ũntũ bũrĩkũ Jesũ aaugĩre rĩrĩa aarĩ narĩa Galilaya, bũrĩa bũkwonania aataragĩĩria bwegie gĩkundi gĩkai kĩa antũ?

11 Yesu alipokuwa Galilaya mwaka wa 32 W.K., alikuwa akiwarejelea hasa Wayahudi waliotaka mkate kutoka kwake. Hata hivyo, Yesu alijaribu kuwasaidia watambue kwamba kuna jambo muhimu zaidi ya chakula. Jambo hilo lingeweza kuwasaidia kupata uzima wa milele. Na Yesu alisema kwamba wale waliokufa wangeweza kufufuliwa katika siku ya mwisho na kuishi milele. Hakuwa akiwarejelea watu wachache waliochaguliwa, kama alivyofanya baadaye wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana. Badala yake, akiwa Galilaya alizungumza kuhusu baraka ambayo watu wote watapata. Kwa kweli, alisema hivi: “Yeyote akila mkate huu ataishi milele . . . Mkate nitakaotoa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”Yoh. 6:51. c

12. Nĩmbĩ bikwendekana nĩkenda twona mwoyo jwa kenya na kenya?

12 Yesu hakuwaambia Wayahudi huko Galilaya kwamba kila mtu ambaye amewahi kuishi angepata baraka hiyo ya uzima wa milele. Ni wale tu ‘wanaokula mkate huu,’ yaani, wale wanaoonyesha imani watanufaika na baraka hiyo. Watu wengi leo katika dini za Kikristo wanasema kwamba wanamwamini Yesu, na wanamwita mwokozi wao. (Yoh. 6:29) Hata hivyo, baadhi ya watu huko Galilaya ambao mwanzoni walimwamini Yesu, waliacha kumwamini. Kwa nini?

13. Nĩmbĩ muntũ abuĩrĩte kũthithia nĩkenda atuĩka mũritwa wa mma wa Jesũ?

13 Watu wengi katika umati huo ambao Yesu alilisha walimfuata tu kwa sababu aliwapatia kile walichohitaji. Walipendezwa na kuponywa kimuujiza, kupata chakula cha bure, na walitaka awafundishe mambo waliyotaka kusikia. Hata hivyo, Yesu aliwaonyesha kwamba mambo mengi zaidi yalihitajika ili kuwa wanafunzi wake wa kweli. Hakuja ulimwenguni ili tu kutosheleza mahitaji ya kimwili ya watu. Walihitaji kukubali mwaliko wa ‘kwenda’ kwake, yaani, kwa kukubali na kutii kila kitu alichofundisha.—Yoh. 5:40; 6:44.

14. Tũbuĩrĩte kũthithia atĩa nĩkenda tũgunĩka kuumania na mwĩrĩ na tharike ya Jesũ?

14 Alipozungumza na umati huo wa watu, Yesu alikazia umuhimu wa kuonyesha imani. Katika nini? Uwezo wa kukomboa wa mwili na damu yake ambayo baada ya muda, angeitoa kama dhabihu. Imani hiyo ilikuwa muhimu kwa Wayahudi hao, na ni muhimu leo pia. (Yoh. 6:40) Naam, ili tunufaike kutokana na mwili na damu ya Yesu kama inavyoonyeshwa kwenye Yohana 6:​53, tunahitaji kuonyesha imani katika fidia. Watu wengi sana wanaweza kupata baraka hiyo.—Efe. 1:7.

15-16. Nĩ mantũ ja bata jarĩkũ twairitana kĩrĩ Johana mũrangõ jwa 6 jarĩa tũbuĩrĩte kũriikana?

15 Katika Yohana sura ya 6 tumejifunza mambo mengi muhimu ambayo yana thamani kubwa kwetu na kwa wapendwa wetu. Sura hiyo inaonyesha wazi jinsi Yesu anavyowajali watu. Alipokuwa Galilaya, aliwaponya wagonjwa, alifundisha kuhusu Ufalme, na alihakikisha alitosheleza uhitaji wa msingi wa wanadamu kwa kuwapa chakula. (Luka 9:11; Yoh. 6:​2, 11, 12) Jambo muhimu zaidi alifundisha kwamba yeye ndiye “mkate wa uzima.”—Yoh. 6:​35, 48.

16 Wale ambao aliwarejelea kuwa “kondoo wengine” hawashiriki na hawapaswi kushiriki mkate na divai wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana unaofanywa kila mwaka. (Yoh. 10:16) Hata hivyo, wananufaika kutokana na mwili na damu ya Yesu Kristo. Wanafanya hivyo kwa kuonyesha imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu na mambo mengi makubwa inayotimiza. (Yoh. 6:53) Tofauti na hilo, wale wanaopaswa kula mkate na kunywa divai, wanaonyesha kwamba wameingia katika agano jipya wakiwa na tarajio la kuwa warithi wa ufalme wa mbinguni. Kwa hiyo, iwe sisi ni watiwa-mafuta au kondoo wengine, simulizi katika Yohana sura ya 6 lina mambo muhimu sana kwetu tunayoweza kujifunza. Linakazia umuhimu wa kuonyesha imani na hivyo kupata uzima wa milele.

RWĨMBO 150 Mtafute Mungu Upate Ukombozi

a Yohana 6:​5-35 imezungumziwa katika makala iliyotangulia.

b Maji ambayo Yesu alitaja yanafananisha maandalizi ya Yehova ya uzima wa milele.

c Yohana sura ya 6 inatumia maneno “yeyote” na “kila mtu” yanayoweza kuwarejelea wale ambao wataishi milele.—Yoh. 6:​35, 40, 47, 54, 56-58.