Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 50

RWĨMBO 135 Mwaliko Wenye Upendo wa Yehova: “Uwe na Hekima, Mwanangu”

Ũrĩa Aciari Bomba Gũtetheeria Aana Kũrikia Wĩtĩkio Bwao

Ũrĩa Aciari Bomba Gũtetheeria Aana Kũrikia Wĩtĩkio Bwao

“Nikenda buumbaga kumenyera mantu jaria meega, jaria jeetikirika, na jaria jari jamoojuru jaria Murungu eendaga jathithua.”ARO. 12:2.

JAMBO KUU

Madokezo hususa yatakayowasaidia wazazi kudumisha mawasiliano mazuri pamoja na watoto wao na kuwasaidia kuimarisha imani yao katika Mungu na Biblia.

1-2. Nĩatĩa aciari bomba gũcookeria mwana wao biũria biegie mantũ jarĩa twĩtĩkĩtie kuuma Bibiriene?

 WATU wengi wanakubali kwamba kuwalea watoto kunahusisha kazi nyingi sana. Ikiwa wewe ni mzazi mwenye mtoto mdogo, tunakupongeza kwa kujitahidi kwa bidii kujenga imani ya mtoto wako. (Kum. 6:​6, 7) Kadiri mtoto wako anavyokuwa, huenda akaanza kuuliza maswali mazito kuhusu mambo tunayoamini yanayotegemea Biblia, kutia ndani viwango vya Biblia kuhusu maadili.

2 Mwanzoni, huenda maswali ya mtoto wako yakafanya uwe na wasiwasi. Huenda hata ukaona kwamba imani yake inaanza kudhoofika. Hata hivyo, ukweli ni kwamba kadiri watoto wanavyokua wanahitaji kuuliza maswali ili waimarishe imani yao. (1 Kor. 13:11) Hivyo, huhitaji kuogopa. Unaweza kuona maswali ya unyoofu ambayo mtoto wako anauliza kuhusu imani yetu kuwa nafasi ya kumsaidia asitawishe uwezo wake wa kufikiri.

3. Nĩmbi tũgacũnkũũna kĩthoomone gĩkĩ?

3 Katika makala hii, tutazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kuwasaidia watoto wao (1) kusitawisha imani yao wenyewe, (2) kuongeza uthamini wao kuelekea viwango vya Biblia kuhusu maadili, na (3) kutetea mambo wanayoamini. Pia, tutazungumzia kwa nini ni vizuri watoto wako waulize maswali, na tutapendekeza baadhi ya mambo mnayoweza kufanya mkiwa familia ambayo huenda yakawapatia wazazi fursa ya kuzungumzia imani yetu ya Kikristo.

TETHEERIA MWANA WAAKU GŨKŨRIA WĨTĨKIO BWAWE

4. Nĩ bĩũria birĩkũ bĩmwe mwana waaku oomba kwĩthĩrwa arĩ nabio, na nĩkĩ?

4 Wazazi Wakristo wanatambua kwamba imani katika Mungu si jambo ambalo mtoto anarithi. Hukuzaliwa ukiwa na imani katika Yehova. Hivyo ndivyo ilivyo kwa mtoto wako pia. Hivyo, huenda mtoto wako akaanza kujiuliza maswali kama vile: ‘Ninawezaje kujua kwamba kuna Mungu? Je, kweli ninaweza kuamini kile ambacho Biblia inasema?’ Katika Biblia tunatiwa moyo tutumie ‘nguvu zetu za kufikiri’ na ‘kuhakikisha mambo yote.’ (Rom. 12:1; 1 The. 5:21) Hata hivyo, unawezaje kumsaidia mtoto wako aimarishe imani yake?

5. Nĩatĩa aciari bomba kũthithia nĩkenda batetheeria mwana waao gũkũria wĩtĩkio bwawe kwerekera jarĩa jarĩ Bibiriene? (Aroma 12:2)

5 Mtie moyo mtoto wako ajithibitishie kwamba kile ambacho Biblia inafundisha ni kweli. (Soma Waroma 12:2.) Mtoto wako anapouliza maswali, tumia nafasi hiyo kumwonyesha jinsi ya kutafuta majibu kwa kutumia vifaa vya utafiti, kama vile Fahirisi na Mwongozo wa Utafiti wa Mashahidi wa Yehova. Katika Mwongozo wa Utafiti, chini ya habari “Biblia,” anaweza kutafuta kichwa “Iliongozwa na Roho ya Mungu” ili kupata uthibitisho kwamba Biblia si kitabu kizuri tu kilichoandikwa na wanadamu. Badala yake, ni “neno la Mungu.” (1 The. 2:13) Kwa mfano, anaweza kufanya utafiti kuhusu jiji la kale la Waashuru la Ninawi. Wakati uliopita, baadhi ya wachambuzi wa Biblia walidai kwamba jiji la Ninawi halikuwahi kuwepo. Lakini katika miaka ya 1850, magofu ya jiji hilo yalichimbuliwa, na kuthibitisha kwamba simulizi hilo la Biblia ni sahihi. (Sef. 2:​13-15) Ili kupata habari zaidi kuhusu jinsi kuharibiwa kwa jiji la Ninawi kulivyotimiza unabii wa Biblia, anaweza kusoma makala “Je, Wajua?” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Novemba 2021. Kwa kulinganisha mambo anayojifunza kutoka katika machapisho yetu na mambo anayojifunza katika ensaiklopedia na vyanzo vingine vinavyotegemeka, mtoto wako ataweza kuimarisha imani yake katika mambo ambayo Biblia inasema.

6. Nĩatĩa aciari bomba gũtetheeria aana gũkũria ũũmbi bwao bwa kũthũgaania? Ejana ngerekano. (Tega kinya mbica.)

6 Chochea uwezo wa kufikiri wa mtoto wako. Wazazi wana fursa mbalimbali za kuwahusisha watoto wao katika mazungumzo yenye kusisimua kuhusu Biblia au imani katika Mungu. Huenda fursa hizo zikajitokeza mnapotembelea jumba la makumbusho, bustani, au sehemu ya maonyesho kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova. Kwa mfano, mnapotembelea jumba la makumbusho, iwe ni kupitia mtandao au kihalisi, unaweza kumsaidia mtoto wako kukazia fikira matukio ya kihistoria na vitu vya kale ambavyo vinaweza kuimarisha uhakika wake kwamba Biblia ni sahihi. Je, mtoto wako anajua kwamba jina la kibinafsi la Mungu linapatikana kwenye Jiwe la Moabu la miaka 3,000 iliyopita? Jiwe halisi la Moabu linaonyeshwa kwenye Jumba la Makumbusho la Louvre jijini Paris, Ufaransa. Pia, mfano wa Jiwe la Moabu unapatikana kwenye maonyesho ya “Biblia na Jina la Mungu” yaliyopo katika Makao Makuu ya Ulimwenguni Pote ya Mashahidi wa Yehova huko Warwick, New York. Jiwe la Moabu linaonyesha kwamba Mfalme Mesha wa Moabu alimwasi mfalme wa Israeli. Hilo ni kulingana na kile ambacho Biblia inasema. (2 Fal. 3:​4, 5) Mtoto wako anapojionea kwa macho yake mwenyewe uthibitisho wa kwamba Biblia ni sahihi na ya kweli, imani yake itakuwa yenye nguvu zaidi—Linganisha 2 Mambo ya Nyakati 9:6.

Je, unaweza kuchochea uwezo wa kufikiri wa mtoto wako kwa kumwonyesha mambo ambayo yanapatikana katika majumba ya makumbusho? (Tazama fungu la 6)


7-8. (a) Nĩmbi tũũmba kwiritana kuumania na ũthongi bwa into birĩa biũmbi? Ejana ngerekano. (Tega kinya mbica.) (b) Nĩ biũria birĩkũ biũmba gũtetheeria mwana kũrikia wĩtĩkio bwawe kwerekera Mũũmbi?

7 Mtie moyo mtoto wako atafakari kuhusu uumbaji. Mnapotembelea maeneo ya mashambani au bustani, msaidie mtoto wako achunguze uumbaji na kutambua vitu vyenye maumbo yanayojirudia-rudia. Kwa nini? Maumbo hayo yanathibitisha kwamba uumbaji ulitokezwa na mbuni mwenye akili na hekima nyingi. Kwa mfano, maumbo yanayojiviringa yamefanyiwa utafiti na wanasayansi kwa miaka mingi. Mtaalamu wa biolojia na fizikia, Nicola Fameli, anaeleza kwamba unapohesabu idadi ya maumbo yanayojiviringa, unatambua kwamba yanatokeza mfuatano fulani wa namba. Mfuatano huo wa namba unaitwa Fibonacci. Maumbo yanayojiviringa yanaweza kuonwa kwenye vitu vingi, kama vile katika baadhi ya makundi ya nyota, kombe la konokono, majani ya mimea, na ua la alizeti. a

8 Kadiri mtoto wako anavyojifunza mengi zaidi katika somo la sayansi akiwa shuleni, ndivyo atakavyogundua kwamba kuna sheria zinazoongoza maumbo ya vitu vingi. Kwa mfano, miti mingi ina maumbo yanayojirudia-rudia (fractal patterns). Shina linajigawanya katika matawi na matawi yanajigawanya katika vitawi. Maumbo hayo yanapatikana pia katika vitu vingine. Lakini ni nani aliyeweka sheria zinazotokeza maumbo hayo? Ni nani aliyebuni maumbo hayo yenye mpangilio maridadi? Kadiri mtoto wako anavyotafakari kuhusu maswali hayo, inaelekea ndivyo atakavyoweza kusitawisha imani yenye nguvu kwamba Mungu aliumba vitu vyote. (Ebr. 3:4) Mtoto wako anapoendelea kukua, unaweza kumuuliza swali hili, “Ikiwa Mungu alituumba, je, inapatana na akili kufikia mkataa kwamba ametupatia pia mwongozo wa maadili ili tuwe na furaha?” Kisha, unaweza kumweleza kwamba mwongozo huo wenye thamani unapatikana katika Biblia.

NASA, ESA, and the Hubble Heritage (STScl/AURA)-ESA/Hubble Collaboration

Ni nani aliyetokeza umaridadi na ubuni ulio katika uumbaji? (Tazama fungu la 7-8)


TETHEERIA MWANA WAAKU ATĨĨE ITHIMI BIA MŨRUNGU BIA WAGĨRU

9. Nĩmbi biũmba gũtũma mwana ethĩrwa na nkanja kwerekera moritani ja Bibiria jegie ithimi bia Mũrungu bia wagĩru?

9 Ikiwa mtoto wako anatilia shaka thamani ya viwango vya Biblia kuhusu maadili, jaribu kutambua sababu zinazomfanya ahisi hivyo. Je, ni kweli kwamba hakubaliani na viwango vya Biblia kuhusu maadili, au tatizo ni kwamba anapozungumza na wengine anashindwa kutetea mambo anayoamini? Vyovyote vile, unaweza kumsaidia mtoto wako athamini zaidi viwango vya Biblia kwa kujifunza naye kitabu Furahia Maisha Milele! b

10. Nĩatĩa ũũmba gũtethia mwana waakũ kũthũgaanĩria ngwatanĩro yaawe amwe na Jehova?

10 Mtie moyo mtoto wako athamini uhusiano wake wa kibinafsi pamoja na Yehova. Unapojifunza Biblia pamoja na mtoto wako, jitahidi kujua maoni yake kwa kumuuliza maswali ya maoni na kutumia mifano inayopatikana kwenye kitabu Furahia Maisha Milele! (Met. 20:5) Kwa mfano, somo la 8 linamlinganisha Yehova na rafiki anayejali ambaye hutupatia vikumbusha vinavyoweza kutulinda na kutunufaisha. Baada ya kuzungumzia andiko la 1 Yohana 5:​3, unaweza kumuuliza hivi: “Kwa kuwa unajua kwamba Yehova ni rafiki mzuri, unapaswa kuwa na maoni gani kuhusu mambo anayotuambia tufanye?” Huenda hilo likaonekana kuwa swali rahisi, lakini unapomuuliza swali hilo unaweza kumsaidia mtoto wako aone sheria za Mungu kuwa uthibitisho wa upendo Wake.—Isa. 48:​17, 18.

11. Nĩatĩa ũũmba gũtetheeria mwana waakũ gũtĩĩa moritani ja Bibiria? (Njuno 2:​10, 11)

11 Zungumzia manufaa ya kutumia kanuni za Biblia. Mnaposoma pamoja Biblia au andiko la siku, zungumzieni jinsi ambavyo kanuni za Biblia zimeisaidia familia yenu. Kwa mfano, je, mtoto wako anaona manufaa ya kuwa mwenye bidii na mnyoofu? (Ebr. 13:18) Pia, unaweza kukazia jinsi kutumia kanuni za Biblia kunavyoweza kutulinda kimwili na kihisia. (Met. 14:​29, 30) Kuzungumzia kanuni kama hizo, kutamsaidia mtoto wako athamini hata zaidi ushauri unaopatikana katika Biblia.—Soma Methali 2:​10, 11.

12. Nĩatĩa mũciari ũmwe atethetie mũtana waawe gũtĩĩa moritani ja Bibiria?

12 Steve, baba anayeishi nchini Ufaransa, anaeleza jinsi ambavyo yeye na mke wake wanamsaidia Ethan, mwana wao ambaye ni tineja, atambue kwamba Yehova ametuwekea sheria kwa sababu anatupenda. Steve anasema hivi: “Tunamuuliza maswali kama vile, ‘Kwa nini Yehova anataka tuheshimu kanuni hii? Kanuni hii inaonyeshaje kwamba anatupenda? Ni nini kinachoweza kutokea ikiwa hutatumia kanuni hii?’” Mazungumzo kama hayo yamemsaidia Ethan kusitawisha imani yenye nguvu na kutumia kanuni za Yehova katika maisha yake. Steve anaongezea hivi: “Lengo letu ni kumsaidia Ethan atambue kwamba hekima iliyo katika Biblia inazidi kwa mbali hekima ya wanadamu.”

13. Nĩatĩa aciari bomba kũmenyerithia aana baao gũtumĩra moritani ja Bibiria? Ejana ngerekano.

13 Mzoeze mtoto wako kutumia kanuni za Biblia. Fursa moja ya kufanya hivyo ni wakati kunapokuwa na mradi wa kusoma kitabu fulani shuleni. Huenda kitabu hicho kikatokeza wazo la kwamba wahusika wanaojihusisha katika maadili mapotovu au walio na milipuko ya hasira wanafaa kuigwa. Unaweza kumtia moyo mtoto wako atumie kanuni za Biblia anapotafakari kuhusu matendo ya wahusika wanaotajwa katika kitabu hicho. (Met. 22:​24, 25; 1 Kor. 15:33; Flp. 4:8) Huenda jambo hilo likamsaidia kuwa tayari kutoa ushahidi kwa mwalimu wake na wanafunzi wenzake wanapozungumzia kitabu hicho darasani.

TETHEERIA MWANA WAAKU KWĨTHĨRWA NA ŨCAMBA BWA GŨTETEERA WĨTĨKIO BWAWE

14. Nĩ ũntũ bũrĩkũ bũũmba gwĩkĩra Mũkristũ ũmwĩthĩ ũgũũa, na nĩkĩ?

14 Nyakati nyingine, huenda vijana Wakristo wakakosa ujasiri wa kutetea imani yao. Huenda wakaogopa wanapohitaji kueleza kwa nini hawaamini nadharia ya mageuzi. Kwa nini? Kwa sababu walimu wao wanaweza kudai kwamba nadharia ya mageuzi ni jambo hakika. Ikiwa wewe ni mzazi, unawezaje kumsaidia mtoto wako awe na ujasiri wa kutetea imani yake?

15. Nĩmbi biũmba gũtethia Mũkristũ ũmwĩthĩ kwĩthĩrwa na mma nkũrũki kwerekera jarĩa etĩkĩtie?

15 Msaidie mtoto wako awe na uhakika zaidi katika mambo anayoamini. Mtoto wako hapaswi kuaibika kwa sababu anajua ukweli kuhusu uumbaji. (2 Tim. 1:8) Kwa nini? Ukweli ni kwamba wanasayansi wengi pia wanaelewa kwamba uhai haukujitokeza wenyewe tu. Wanasayansi hao wamejionea uthibitisho kwamba ni lazima uhai uliumbwa na mbuni mwenye akili nyingi. Matokeo ni kwamba hawakubaliani na nadharia ya mageuzi ambayo inafundishwa katika shule nyingi duniani kote. Mtoto wako anaweza kuimarisha uhakika wake kwa kutafakari sababu zilizowachochea ndugu na dada wengine kuamini kwamba uhai uliumbwa. c

16. Nĩatĩa aciari bomba gũtetheeria aana gũteteera wĩtĩkio bwao kwerekera Mũũmbi? (1 Petero 3:15) (Tega kinya mbica.)

16 Msaidie mtoto wako awe tayari kutetea imani yake kwamba kuna Muumba. (Soma 1 Petro 3:15.) Mnaweza kupitia pamoja mfululizo wa makala kwenye jw.org wenye kichwa “Vijana Huuliza—Uumbaji au Mageuzi?” Kisha, mzungumzie jambo ambalo mtoto wako anahisi litamsaidia awathibitishie vizuri zaidi wengine ukweli kumhusu Muumba. Mkumbushe kwamba hahitaji kubishana na wanafunzi wenzake. Mtie moyo atumie hoja rahisi na inayoeleweka anapojadiliana na wale ambao wako tayari kuzungumzia jambo hilo. Kwa mfano, huenda mwanafunzi mwenzake akasema hivi: “Ninaamini tu kile ninachoona, na sijawahi kumwona Mungu.” Kijana Mkristo anaweza kujibu hivi: “Wazia unatembea katikati ya msitu ulio mbali sana na makazi ya watu, kisha unaona kisima kilichojengwa kwa mawe? Ungefikia mkataa gani? Ikiwa kuwepo kwa kisima ni uthibitisho ulio wazi kwamba mtu fulani mwenye akili alikijenga, basi kuwepo kwa ulimwengu ni uthibitisho ulio wazi hata zaidi kwamba kuna Muumba!”

Tumia hoja rahisi na inayoeleweka unapozungumza na wanafunzi wenzako (Tazama fungu la 16-17) d


17. Nĩatĩa aciari bomba gwĩkĩra aana baao inya gũcwaa twanya twa kwarĩĩria mma cia Bibiria amwe na antũ bangĩ? Taarĩria.

17 Mtie moyo mtoto wako atafute fursa za kuwaeleza wengine kweli za Biblia. (Rom. 10:10) Huenda ukalinganisha jitihada zake za kuzungumza kuhusu imani yake na jitihada za kujifunza jinsi ya kucheza ala fulani ya muziki. Mwanzoni, mtu anayejifunza atafanya mazoezi kwa kujifunza nyimbo rahisi. Baada ya muda, ataona ikiwa rahisi zaidi kucheza ala hiyo ya muziki. Vivyo hivyo, huenda kijana Mkristo akatumia utangulizi ulio rahisi anapowaeleza wengine kuhusu imani yake. Kwa mfano, huenda akamuuliza mwanafunzi mwenzake hivi: “Je, ulijua kwamba wahandisi huiga vitu vya asili wanapotengeneza kitu fulani? Ningependa nikuonyeshe video moja nzuri.” Baada ya kumwonyesha video hiyo kutoka kwenye mfululizo wenye kichwa, Je, Ni Kazi ya Ubuni? anaweza kusema hivi: “Ikiwa wanasayansi wanasifiwa kwa sababu ya kuiga vitu vya asili, je, ni nani anayestahili kusifiwa tunapoona vitu hivyo vya asili?” Utangulizi huo rahisi unaweza kutosha kumchochea mwanafunzi mwenzake apendezwe zaidi na habari hiyo na awe tayari kujifunza zaidi.

ĨTA NA MBERE GŨTETHEERIA MWANA WAAKU GWĨKĨRA INYA WĨTĨKIO BWAWE

18. Nĩatĩa aciari bomba gwĩta na mbere gwĩkĩra inya wĩtĩkio bwa aana baao kwerekera Mũrungu?

18 Tunaishi katika ulimwengu uliojaa watu ambao hawana imani katika Yehova. (2 Pet. 3:3) Hivyo, wazazi mnapojifunza Biblia na watoto wenu, watie moyo wachunguze habari zitakazowasaidia kuliheshimu zaidi Neno la Mungu na viwango vyake vya maadili. Chochea uwezo wake wa kufikiri kwa kumsaidia kutafakari kwa kina kuhusu mambo maridadi katika uumbaji wa Yehova. Msaidie athamini zaidi unabii wa Biblia wenye kustaajabisha ambao tayari umetimia. Na zaidi ya yote, sali pamoja na mtoto wako na usali kwa ajili yake. Unapofanya hivyo, unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atakuthawabisha kwa jitihada zako za kumsaidia mtoto wako aimarishe imani yake.—2 Nya. 15:7.

RWĨMBO 133 Mwabudu Yehova Ujanani

b Ikiwa mtoto wako tayari amemaliza kujifunza kitabu Furahia Maisha Milele!, unaweza kupitia tena pamoja naye masomo katika sehemu ya 3 na 4, ambayo yanazungumzia viwango vya Biblia kuhusu maadili.

c Tazama makala “Kwa Nini Tunaamini Kuna Muumba?” katika gazeti la Amkeni! la Septemba 2006, na broshua Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai. Ili kupata mifano zaidi, tazama mfululizo wa video wenye kichwa Maoni Kuhusu Chanzo cha Uhai kwenye jw.org.

d MAELEZO YA PICHA: Shahidi wa Yehova kijana akimwonyesha mwanafunzi mwenzake ambaye anapendezwa na ndege ndogo aina ya drone, video katika mfululizo wenye kichwa Je, Ni Kazi ya Ubuni?