Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 48

RWĨMBO 97 Uhai Unategemea Neno la Mungu

Mantũ Jarĩa Tũkwiritana Kuumania na Kĩama kĩa Jesũ kĩa Mĩgate

Mantũ Jarĩa Tũkwiritana Kuumania na Kĩama kĩa Jesũ kĩa Mĩgate

“Nini mugate jwa mwoyo; muntu uria wijaga kirini atikaigua mpara.”JOH. 6:35.

JAMBO KUU

Kuchunguza simulizi linalopatikana kwenye Yohana sura ya 6, linaloonyesha jinsi Yesu alivyotokeza kimuujiza mikate na samaki kwa ajili ya umati mkubwa, na mambo tunayojifunza kutokana na simulizi hilo.

1. Nĩatĩa mũgate jwonagwa tene Bibiriene?

 MKATE ulikuwa chakula kikuu cha watu wengi katika nyakati za Biblia. (Mwa. 14:18; Luka 4:4) Isitoshe, mkate ulikuwa muhimu sana hivi kwamba mara nyingine Biblia inatumia neno “mkate” kumaanisha chakula kwa ujumla. (Mt. 6:11) Pia, mkate ulikuwa sehemu muhimu katika miujiza miwili ya Yesu inayojulikana sana. (Mt. 16:​9, 10) Simulizi moja kati ya hayo, linapatikana kwenye Yohana sura ya 6. Tunapochunguza simulizi hilo, tutaona mambo tunayojifunza ambayo tunaweza kuyatumia leo.

2. Nĩ kagiita karĩkũ ũbatu bwa biakũrĩa bwaumĩĩre?

2 Baada ya safari ndefu ya kuhubiri pamoja na mitume wake, Yesu alisafiri nao kwenye mashua na kuvuka Bahari ya Galilaya ili wakapumzike. (Marko 6:​7, 30-32; Luka 9:10) Walifika mahali pasipo na watu kwenye eneo la Bethsaida. Hata hivyo, baada ya muda mfupi, maelfu ya watu walifika hapo ili kumwona. Yesu hakuwapuuza. Kwa fadhili, alitumia wakati ili kuwafundisha kuhusu Ufalme na kuwaponya wagonjwa. Kwa kuwa muda ulikuwa umesonga sana, wanafunzi walijiuliza watu hao wote wangepata wapi chakula. Huenda baadhi yao walikuwa na chakula kidogo, lakini wengi wao wangehitaji kwenda vijijini wakajinunulie chakula. (Mt. 14:15; Yoh. 6:​4, 5) Yesu angefanya nini?

KĨAMA KĨA MŨGATE

3. Nĩatĩa Jesũ aathithĩrie kwerekera mobatu ja kĩrĩndĩ? (Tega kinya mbica karatacine ka mbere.)

3 Yesu aliwaambia mitume wake hivi: “Si lazima waondoke; ninyi wapeni chakula.” (Mt. 14:16) Hilo lilikuwa tatizo kwa sababu kulikuwa na wanaume 5,000 hivi. Na ukijumlisha wanawake na watoto, huenda kulikuwa na watu 15,000 waliohitaji kulishwa. (Mt. 14:21) Andrea akasema hivi: “Hapa kuna mvulana mdogo aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Je, hivi vitawatosha watu wengi hivi?” (Yoh. 6:9) Mikate ya shayiri ilikuwa chakula ambacho watu walikula kwa ukawaida, na huenda samaki hao wadogo walikuwa wamewekwa chumvi na kukaushwa. Hata hivyo, chakula ambacho mvulana huyo alikuwa nacho hakingetosha kuwalisha watu wengi hivyo—au je, kingetosha?

Yesu alishughulikia mahitaji ya kiroho na ya kimwili ya watu (Tazama fungu la 3)


4. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na Johana 6:​11-13? (Tega kinya mbica.)

4 Yesu alitaka kuuonyesha ukarimu umati huo wa watu, hivyo aliwaagiza wote waketi katika vikundi kwenye nyasi. (Marko 6:​39, 40; soma Yohana 6:​11-13.) Tunasoma kwamba Yesu alitoa shukrani kwa Baba yake kwa ajili ya mikate na samaki hao. Ilifaa kabisa kumshukuru Mungu, ambaye kihalisi ndiye Chanzo cha chakula. Hicho ni kikumbusho kizuri kwetu cha kufuata mfano wa Yesu wa kusali kabla ya kula, iwe tuko peke yetu au pamoja na watu wengine. Kisha, Yesu akaagiza chakula kigawanywe, na watu wakala na kushiba. Hata kulikuwa na chakula kilichobaki, ambacho Yesu hakutaka kitupwe. Hivyo, aliagiza chakula hicho kilichobaki kikusanywe, huenda ili kitumiwe baadaye. Yesu alituwekea mfano mzuri wa jinsi ya kutumia vitu tulivyo navyo kwa hekima. Ikiwa wewe ni mzazi, unaweza kuchunguza simulizi hilo pamoja na watoto wako na kuzungumzia mambo mnayoweza kujifunza kuhusu sala, ukaribishaji wageni, na ukarimu.

Jiulize hivi, ‘Je, mimi ninafuata mfano wa Yesu wa kusali kabla ya kula?’ (Tazama fungu la 4)


5. Nĩatĩa antũ beendaga kũthithia nyũma ya Jesũ kũringa kĩama, nawe nĩ ĩtagaaria rĩrĩkũ aajũkĩrie?

5 Watu walivutiwa na njia ya Yesu ya kufundisha na miujiza yake. Wakijua kwamba Musa alikuwa ameahidi kwamba Mungu angewainulia nabii wa pekee, huenda watu hao walijiuliza hivi: ‘Je, inawezekana kwamba Yesu ndiye nabii huyo?’ (Kum. 18:​15-18) Ikiwa ndivyo, ilionekana kwamba angekuwa mtawala wa pekee sana, ambaye huenda angeweza kuandaa chakula kwa ajili ya taifa zima. Hivyo, watu hao “walitaka kuja kumkamata [Yesu] wamfanye awe mfalme.” (Yoh. 6:​14, 15) Ikiwa Yesu angeruhusu jambo hilo, angekuwa akishiriki katika siasa za Wayahudi, ambao walikuwa chini ya utawala wa Waroma. Je, alifanya hivyo? Hapana. Tunasoma kwamba kwa uthabiti Yesu ‘alienda mlimani.’ Hivyo, licha ya kushinikizwa na wengine, Yesu hakujihusisha na siasa. Hilo ni somo zuri sana kwetu!

6. Nĩatĩa tũũmba kwonania nĩtũkũthingata ngerekano ya Jesũ? (Tega kinya mbica.)

6 Ni wazi kwamba hatutaombwa tufanye muujiza wa kuandaa mkate au kuwaponya wagonjwa; wala watu hawatajaribu kutushinikiza tuwe wafalme au watawala wa taifa. Lakini huenda wakatushinikiza tujihusishe katika siasa kwa kupiga kura au kuonyesha kwamba tunamuunga mkono mtu ambaye wanahisi anaweza kuboresha mambo. Hata hivyo, mfano wa Yesu uko wazi. Alikataa kujihusisha na masuala ya kisiasa, na hata baadaye alisema hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.” (Yoh. 17:14; 18:36) Wakristo leo wanahitaji kuiga njia ya Yesu ya kufikiri na matendo yake. Tunauunga mkono Ufalme, tunatoa ushahidi kuuhusu, na kusali uje. (Mt. 6:10) Acheni sasa turudi kwenye simulizi kuhusu jinsi Yesu alivyoandaa mkate kimuujiza na tuchunguze mambo mengine tunayoweza kujifunza.

Akiwawekea wafuasi wake kielelezo cha kufuata, Yesu hakujihusisha katika siasa za Wayahudi au Waroma (Tazama fungu la 6)


KĨAMA KĨA ‘MĨGATE’ KĨONANAGIA ATĨA

7. Nĩatĩa Jesũ aathithĩrie, na atũmwa baawe beetĩkĩrĩrie atĩa mantũ jau? (Johana 6:​16-20)

7 Baada ya Yesu kulisha umati wa watu, aliwaagiza mitume wake waondoke eneo hilo na kurudi Kapernaumu kwa mashua, naye akaenda mlimani, hivyo akaepuka jitihada za umati huo za kumfanya kuwa mfalme. (Soma Yohana 6:​16-20.) Mitume hao walipokuwa wakisafiri kwenye mashua, dhoruba kubwa ikatokea, iliyosababisha upepo mkali na mawimbi makubwa. Kisha, Yesu akafika mahali mitume walipokuwa, akiwa anatembea juu ya maji. Naye alimwalika mtume Petro atembee pia juu ya maji. (Mt. 14:​22-31) Mara tu Yesu alipoingia kwenye mashua, dhoruba ikatulia. Wanafunzi wake walichochewa kusema hivi: “Kwa kweli wewe ni Mwana wa Mungu.” a (Mt. 14:33) Ingawa hivyo, bado hawakuona uhusiano uliokuwepo kati ya muujiza huo na ule mwingine wa kuulisha umati wa watu. Marko anaongezea habari hii: “[Mitume] wakashangaa sana, kwa maana hawakuwa wamefahamu maana ya ule muujiza wa mikate, bado mioyo yao ilikuwa mizito isiweze kuelewa.” (Marko 6:​50-52) Mitume walishindwa kuelewa kwamba Yehova alikuwa amempa Yesu nguvu nyingi sana za kufanya miujiza. Hata hivyo, muda mfupi baadaye, Yesu mwenyewe alizungumzia kuhusu ule muujiza wa mikate, na hivyo kutufundisha somo lingine.

8-9. Nĩkĩ kĩrĩndĩ kĩathingatĩre Jesũ? (Johana 6:​26, 27)

8 Umati wa watu ambao Yesu aliwalisha ulikazia fikira tu kutosheleza mahitaji yao ya kimwili na tamaa zao. Jinsi gani? Siku iliyofuata, walitambua kwamba Yesu na mitume wake walikuwa wameondoka. Hivyo, umati huo ulipanda mashua kadhaa zilizokuwa zimewasili kutoka Tiberia na wakasafiri kuelekea Kapernaumu ili kumtafuta Yesu. (Yoh. 6:​22-24) Je, sababu yao kuu ya kwenda huko ilikuwa kusikia mengi zaidi kuhusu Ufalme? Hapana. Sababu yao kuu ilikuwa kutosheleza mahitaji yao ya kimwili. Tunajuaje hilo?

9 Ona jambo lililotukia umati wa watu ulipokutana na Yesu karibu na Kapernaumu. Yesu alisema waziwazi kwamba hangaiko lao kuu lilikuwa kutosheleza mahitaji yao ya kimwili. Ingawa ‘walikula mikate na kushiba,’ Yesu alisema kwamba hicho kilikuwa “chakula kinachoharibika.” Badala yake, aliwahimiza wafanye kazi kwa ajili ya “chakula kinachodumu kufikia uzima wa milele.” (Soma Yohana 6:​26, 27.) Yesu alisema kwamba Baba yake angewaandalia chakula hicho. Ni lazima wazo la kwamba chakula kingeweza kuwapatia uzima wa milele liliwashangaza! Ni chakula gani ambacho kingeweza kufanya hivyo, na wasikilizaji wa Yesu wangewezaje kukipata?

10. Nĩ mantũ jarĩkũ jegĩe “ngugi cia Murungu” antũ baabataraga kwiritana?

10 Inaelekea Wayahudi hao walihisi kwamba wangehitaji kufanya mambo au kazi fulani ili wastahili kupata chakula hicho. Huenda walikuwa wakifikiria “kazi” au matendo yanayotajwa kwenye Sheria ya Musa. Hata hivyo, Yesu aliwaambia hivi: “Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba mwonyeshe imani katika yule aliyemtuma.” (Yoh. 6:​28, 29; maelezo ya chini) Kuonyesha imani katika mwakilishi wa Mungu ni muhimu ili kupata “uzima wa milele.” Isitoshe, tayari Yesu alikuwa amezungumza kuhusu jambo hilo mapema. (Yoh. 3:​16-18, 36) Na baadaye angekuwa na mengi zaidi ya kusema kuhusu jinsi tunavyoweza kupata uzima wa milele.—Yoh. 17:3.

11. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ Ayahudi boonanĩrie atĩ, baamakagĩra akĩ kũnyirua na mũgate? (Zaburi 78:​24, 25)

11 Wayahudi hao hawakukubali fundisho la Yesu kuhusu ‘kazi mpya ya Mungu.’ Walimuuliza hivi: “Utafanya ishara gani, ili tuone na kukuamini?” (Yoh. 6:30) Walisema kwamba mababu zao katika siku za Musa walipokea mana ambayo ingeweza kulinganishwa na mkate. (Neh. 9:15; soma Zaburi 78:​24, 25.) Ni wazi kwamba akilini bado walikuwa wakifikiria kutoshelezwa na mkate halisi. Hata walishindwa kumwomba Yesu ufafanuzi zaidi alipozungumza kuhusu “mkate wa kweli kutoka mbinguni,” ambao ulikuwa kama mana kutoka mbinguni ambayo ingewapa uzima wa milele. (Yoh. 6:32) Walikazia sana mahitaji yao ya kimwili hivi kwamba walipuuza kweli za kiroho ambazo Yesu alikuwa akijaribu kuwaeleza. Tunajifunza nini kutokana na simulizi hilo?

MWOROTO JWETŨ JŨMŨNENE NĨ JŨRĨKŨ

12. Jesũ oonanĩrie nĩ ũntũ bũrĩkũ bũrĩ bwa gĩtũmi nkũrũki?

12 Tunapata somo muhimu kwenye Yohana sura ya 6. Hangaiko letu kuu linapaswa kuwa mahitaji yetu ya kiroho. Kumbuka kwamba Yesu alisema jambo hilo alipokuwa akipinga kishawishi cha Shetani. (Mt. 4:​3, 4) Na kwenye Mahubiri ya Mlimani, Yesu alikazia umuhimu wa kutambua uhitaji wetu wa kiroho. (Mt. 5:3) Hivyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, njia yangu ya maisha inaonyesha kwamba ninakazia fikira zaidi kutosheleza mahitaji yangu ya kiroho au ya kimwili?’

13. (a) Nĩkĩ nĩ ũntũ bũbwega kũgwĩrĩrua bĩakũrĩa? (b) Nĩ mũkaana jũrĩkũ tũkũbatara kũjũkia na ũrĩto? (1 Akorintho 10:​6, 7, 11)

13 Ni jambo linalofaa kusali kuhusu mahitaji yetu ya kimwili na kuyafurahia. (Luka 11:3) Kazi ngumu inayotuwezesha “kula na kunywa” inatuletea shangwe na inatoka “mkononi mwa Mungu wa kweli.” (Mhu. 2:24; 8:15; Yak. 1:17) Hata hivyo, tunahitaji kuhakikisha kwamba hatutangulizi mambo ya kimwili maishani. Mtume Paulo alikazia jambo hilo alipowaandikia Wakristo waliokuwa wakiishi karibu na mwisho wa mfumo wa mambo wa Kiyahudi. Aliwakumbusha matukio katika historia ya Israeli, kutia ndani mambo yaliyotukia karibu na Mlima Sinai. Aliwaonya Wakristo ‘wasitamani mambo mabaya, kama Waisraeli walivyotamani.’ (Soma 1 Wakorintho 10:​6, 7, 11.) Waisraeli waliruhusu tamaa yao ya chakula ifanye hata maandalizi ya kimuujiza ya Yehova yawe “mambo mabaya.” (Hes. 11:​4-6, 31-34) Na walipoabudu ndama wa dhahabu walionyesha kwamba walijali zaidi kula, kunywa, na kujifurahisha, badala ya kumtii Yehova. (Kut. 32:​4-6) Paulo alitaja mfano wao kama onyo kwa Wakristo walioishi kabla ya mwisho wa mfumo wa mambo wa Kiyahudi mwaka wa 70 W.K. Leo, tunaishi karibu na mwisho wa mfumo huu wa mambo, hivyo ni muhimu kwetu kuchukua kwa uzito shauri la Paulo.

14. Mantũne jegĩe biakũrĩa, nĩmbi tũkwĩrĩgĩĩra nthĩngũrũne ĩnjerũ?

14 Alipozungumza kuhusu “mkate wetu kwa ajili ya siku hii,” Yesu alitufundisha pia kwamba tusali mapenzi ya Mungu yatendeke “duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mt. 6:​9-11) Unafikiri ulimwengu utakuwaje wakati huo? Biblia inaonyesha kwamba mapenzi ya Mungu kwa dunia yanatia ndani kuwa na chakula kizuri. Kulingana na Isaya 25:​6-8, kutakuwa na vyakula vingi tutakavyofurahia chini ya Ufalme wa Yehova. Zaburi 72:16 inatabiri hivi: “Kutakuwa na nafaka nyingi duniani; itafurika juu ya milima.” Je, unatazamia kwa hamu kutumia nafaka hizo kutayarisha mkate unaoupenda au kujaribu mapishi mapya? Pia, unaweza kutazamia kupanda mashamba ya mizabibu na kufurahia matunda yake. (Isa. 65:​21, 22) Na kila mtu duniani atafurahia mambo hayo mazuri.

15. Nĩ mantũ jarĩkũ barĩa bakariũkua ĩgiita rĩjĩĩte bakaritanwa? (Johana 6:35)

15 Soma Yohana 6:35. Fikiria tena kuhusu wale waliokula mikate na samaki ambao Yesu aliandaa? Inawezekana utakutana na baadhi yao katika ufufuo unaokuja. Hata ingawa hawakuonyesha imani wakati huo, huenda watafufuliwa. (Yoh. 5:​28, 29) Watu hao watahitaji kujifunza maana ya maneno haya ya Yesu: “Mimi ndio mkate wa uzima. Yeyote anayekuja kwangu hatapata njaa kamwe.” Watahitaji kusitawisha imani katika dhabihu ya Yesu, ambaye alitoa uhai wake kwa ajili yao. Wakati huo, kutakuwa na programu ya elimu ya kiroho kwa ajili ya watakaofufuliwa na watoto wowote watakaozaliwa. Itakuwa shangwe kubwa sana kushiriki katika programu hiyo ya kufundisha! Kufanya kazi hiyo kutakuletea shangwe zaidi kuliko kula mkate halisi. Naam, mambo ya kiroho ndiyo yatakuwa mambo muhimu zaidi.

16. Nĩ mantũ jarĩkũ tũgacũnkũũna kĩthoomone kĩu kĩthingatĩte?

16 Tumechunguza sehemu ya simulizi la Yohana sura ya 6, lakini Yesu alikuwa na mengi zaidi ya kufundisha kuhusu “uzima wa milele.” Wayahudi walipaswa kumsikiliza kwa makini Yesu, nasi tunapaswa kufanya hivyo. Tutaendelea kuchunguza Yohana sura ya 6 katika makala inayofuata.

RWĨMBO 20 Ulimtoa Mwana Wako Mpendwa

a Ili kupata habari zaidi kuhusu simulizi hilo lenye kusisimua, soma kitabu Yesu—Njia, Kweli, na Uzima, uku. 131, na Igeni Imani Yao, uku. 185.