Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 31

Rĩ, Nũkwenda Gweteera Jehova?

Rĩ, Nũkwenda Gweteera Jehova?

“Nkonania mwerekera jwa gweteera.”​—MIK. 7:7 NWT.

RWĨMBO 128 Kuvumilia Mpaka Mwisho

MUHTASARI *

1-2. Nĩmbi tũgacũnkũũna kĩthoomone gĩkĩ?

UNAHISIJE wakati mzigo unaouhitaji sana unapokosa kufika kwa wakati uliotarajia? Je, unavunjika moyo? Methali 13:12 inaeleza ukweli huu: “Matarajio yaliyoahirishwa hufanya moyo uwe mgonjwa.” Lakini namna gani ikiwa utagundua kwamba kuna sababu nzuri zilizofanya mzigo usiwasili wakati ulipoutarajia? Inaelekea katika kisa hicho, utakuwa tayari kungojea kwa subira.

2 Katika makala hii, tutachunguza kanuni kadhaa za Biblia zinazoweza kutusaidia kusitawisha na kudumisha ‘mtazamo wa kungojea.’ (Mika 7:7) Kisha, tutachunguza maeneo mawili ambayo ni lazima tumngojee Yehova kwa subira ili atende. Mwishowe, tutachunguza baraka watakazopata wale walio tayari kumngojea Yehova.

MORITANI JA BIBIRIA JARĨA JAGŨTŨRITANA WETEERI

3. Nĩatĩa ũritani bũrĩa bũgweti kĩrĩ Njuno 13:11 bũkwonania?

3 Mfano unaoonyesha umuhimu wa kuwa na subira unapatikana kwenye Methali 13:11. Inasema: “Mali inayopatikana haraka itapungua, lakini mali ya yule anayeikusanya kidogo kidogo itaongezeka.” Je, umeiona kanuni? Ni jambo la hekima kufanya mambo kwa subira, hatua moja baada ya nyingine.

4. Nĩatĩa ũritani bũrĩa bũkwoneka kĩrĩ Njuno 4:18 bũkwonania?

4 Andiko la Methali 4:18 linatuambia kwamba “kijia cha waadilifu ni kama nuru nyangavu ya asubuhi inayong’aa zaidi na zaidi mpaka mchana kamili.” Maneno hayo yanafafanua kwa usahihi njia ambayo Yehova anafunua kusudi lake kwa watu wake, yaani, hatua kwa hatua. Hata hivyo, kwa njia pana zaidi, mstari huo unaweza kutumiwa inapohusu maendeleo ya kiroho ambayo Mkristo anafanya maishani. Ukuzi wa kiroho hauwezi kuharakishwa. Unachukua muda. Ikiwa tutajifunza na kutumia kwa bidii ushauri tunaopata kupitia Neno la Mungu na tengenezo lake, hatua kwa hatua tutasitawisha utu na sifa kama za Kristo. Pia, tutaongeza ujuzi wetu kumhusu Mungu. Ona jinsi Yesu alivyofafanua jambo hilo.

Kama tu mmea unavyokua kidogo-kidogo, ndivyo mtu anayesikia na kukubali ujumbe wa Ufalme anavyokua kiroho hatua kwa hatua (Tazama fungu la 5)

5. Nĩatĩa Jesũ atarĩrĩrie ũkũri bwa ĩtagaaria kwa ĩtagaaria bwa gĩkĩrudu?

5 Yesu alitumia mfano kufafanua jinsi ujumbe wa Ufalme tunaohubiri ulivyo kama mbegu ndogo, ambayo hatua kwa hatua inasitawi kwenye mioyo ya watu wanyoofu. Alisema hivi: “Nazo mbegu huota na kuwa ndefu—naye [mpandaji] hajui jinsi zinavyokua. Udongo wenyewe hutokeza mazao hatua kwa hatua, kwanza jani, kisha suke, mwishowe nafaka iliyokomaa ndani ya suke.” (Marko 4:27, 28) Yesu alimaanisha nini? Alikuwa akifafanua kwamba kama tu ambavyo mmea unakua hatua kwa hatua, ndivyo mtu anayekubali ujumbe wa Ufalme anavyokua kiroho hatua kwa hatua. Kwa mfano, kadiri wanafunzi wetu wa Biblia wenye mioyo minyoofu wanavyomkaribia zaidi Yehova, ndivyo tunavyoanza kuona mabadiliko mengi mazuri wanayofanya. (Efe. 4:22-24) Lakini ni lazima tukumbuke kwamba ni Yehova anayeifanya mbegu hiyo ndogo ikue.—1 Kor. 3:7.

6-7. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na ũrĩa Jehova oombĩre nthĩgũrũ?

6 Katika mambo yote ambayo anafanya, kwa subira Yehova hutumia muda mwingi kadiri anavyohitaji ili kukamilisha kazi yake. Anafanya hivyo kwa utukufu wa jina lake na kwa faida ya wengine. Kwa mfano, fikiria jinsi Yehova alivyotayarisha dunia hatua kwa hatua kwa ajili ya wanadamu.

7 Inapofafanua jinsi Yehova alivyoiumba dunia, Biblia inataja kwamba ‘aliweka vipimo vyake,’ alizamisha “nguzo zake” ndani, na ‘aliweka jiwe lake la pembeni.’ (Ayu. 38:5, 6) Hata alitumia muda kutafakari kazi yake. (Mwa. 1:10, 12) Je, unaweza kuwazia jinsi malaika walivyohisi walipoona uumbaji wa Yehova ukifanyizwa hatua kwa hatua? Hapana shaka walisisimka sana! Hata pindi moja ‘walianza kushangilia kwa sauti.’ (Ayu. 38:7) Tunajifunza nini? Kazi ya Yehova ya uumbaji ilichukua maelfu ya miaka ili kukamilika, lakini alipochunguza kila kitu alichoumba kwa ufikirio mwingi, alitangaza kwamba kilikuwa “chema sana.”—Mwa. 1:31

8. Nandĩ nĩmbi tũkaarĩĩria?

8 Kama tulivyoona katika mifano iliyotajwa awali, tunaweza kupata kanuni nyingi katika Neno la Mungu zinazokazia kwa nini tunahitaji kuwa na subira. Sasa tutachunguza maeneo mawili hususa ambayo ni lazima tuwe tayari kumngojea Yehova.

NĨRĨ TŨKŨBATARA GWETEERA JEHOVA?

9. Nĩ ta ĩgiita rĩrĩkũ tũkũbatara gweteera Jehova?

9 Huenda tukahitaji kungojea sala zetu zijibiwe. Tunaposali ili tupate nguvu za kukabiliana na jaribu au ili kupata msaada wa kushinda udhaifu fulani, huenda tukahisi kwamba msaada tunaohitaji hauji haraka kama tulivyotarajia. Kwa nini Yehova hajibu sala zetu zote papo hapo?

10. Bwegie maromba jeetũ, nĩkĩ weteeri bũkwendeka?

10 Yehova husikiliza kwa makini sala zetu. (Zab. 65:2) Anaziona sala zetu za kutoka moyoni kuwa uthibitisho wa imani yetu. (Ebr. 11:6) Yehova anapendezwa pia kuona ni kwa kadiri gani tumeazimia kuishi kulingana na sala zetu na kufanya mapenzi yake. (1 Yoh. 3:22) Hivyo, huenda tukahitaji kuwa na subira na kutenda kulingana na sala zetu, pindi tunapojitahidi kushinda zoea fulani baya au udhaifu wetu. Yesu alionyesha kwamba baadhi ya sala zetu huenda zisijibiwe papo hapo. Alituhimiza hivi: “Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila mtu anayeomba hupokea, na kila mtu anayetafuta hupata, na kila mtu anayepiga hodi, atafunguliwa.”(Mt. 7:7, 8) Tunapofuata ushauri huo na ‘kudumu katika sala,’ tunaweza kuwa na uhakika kwamba Baba yetu wa mbinguni anatusikia na atajibu sala zetu.—Kol. 4:2.

Tunapokuwa tukimngojea Yehova, tunaendelea kusali kwake tukiwa na imani (Tazama fungu la 11) *

11. Nĩatĩa Ahibirania 4:16 yũmba gũtũtethia rĩrĩa macookio ja maromba jeetũ gwakara ta jacereerwa?

11 Ingawa huenda ikaonekana kana kwamba sala yetu inachelewa kujibiwa, Yehova anaahidi kwamba atajibu sala yetu kwa “wakati unaofaa.” (Soma Waebrania 4:16, maelezo ya chini.) Hiyo ndiyo sababu hatupaswi kamwe kumlaumu Yehova, ikiwa inaonekana kana kwamba sala yetu haijibiwi haraka kama tulivyotarajia. Kwa mfano, watu wengi wamekuwa wakisali kwa miaka mingi waone Ufalme wa Mungu ukikomesha mfumo huu wa mambo. Hata Yesu alisema kwamba tunapaswa kusali kuhusu jambo hilo. (Mt. 6:10) Lisingekuwa jambo la hekima ikiwa mtu angeruhusu imani yake kwa Mungu idhoofike kwa sababu mwisho haukuja kwa wakati ambao wanadamu walitarajia! (Hab. 2:3; Mt. 24:44) Ni jambo la hekima kuendelea kumngojea Yehova na kusali kwake tukiwa na imani. Mwisho utakuja kwa wakati unaofaa kabisa, kwa kuwa tayari Yehova amechagua ‘siku na saa’ ya kuja kwa siku hiyo. Na siku hiyo itathibitika kuwa wakati unaofaa kabisa kwa watu wote.—Mt. 24:36; 2 Pet. 3:15.

Tunaweza kujifunza somo gani kuhusu subira kutoka kwa Yosefu? (Tazama fungu la 12 hadi 14)

12. Nĩ mantũne jarĩkũ weteeri bwetũ bũũmba kũgerua?

12 Huenda tukahitaji kuwa na subira tunapongojea haki itendeke. Mara nyingi watu katika ulimwengu huu wanawatendea isivyo haki watu wa jinsia tofauti, rangi, kabila, utamaduni, au taifa tofauti. Wengine wanatendewa isivyo haki kwa sababu wana ulemavu fulani au matatizo ya akili. Watu wengi wa Yehova wamekabili ukosefu wa haki kwa sababu ya imani yao inayotegemea Biblia. Tunapokosewa kwa njia hizo, tunapaswa kukumbuka maneno ya Yesu. Alisema hivi: “Yule atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.” (Mt. 24:13) Lakini namna gani ikiwa unajua kuhusu dhambi nzito ambayo mtu fulani kutanikoni amefanya? Baada ya wazee wa kutaniko kujulishwa jambo hilo, je, utaliacha mikononi mwao, na kwa subira kungojea walishughulikie kwa njia ya Yehova? Huenda wazee wakahitaji kufanya nini?

13. Nĩmbi bikwendeka kenda tũthithia mantũ na njĩra ya Jehova?

13 Wazee wa kutaniko wanapojulishwa kuhusu dhambi nzito kutanikoni, wanasali na kutafuta hekima “inayotoka juu” ili wapate maoni ya Yehova kuhusu hali hiyo. (Yak. 3:17) Lengo lao ni ‘kumrudisha mtenda dhambi kutoka kwenye kosa la njia yake’ ikiwa inawezekana. (Yak. 5:19, 20) Pia, wanataka kufanya yote wanayoweza ili kulilinda kutaniko na kuwafariji wale walioumizwa. (2 Kor. 1:3, 4) Wanaposhughulikia visa vya dhambi nzito, ni lazima kwanza wapate habari zote, jambo linaloweza kuchukua muda. Kisha, kwa sala na uangalifu wanatoa shauri la Kimaandiko na kumrekebisha mtenda dhambi “kwa kiwango kinachofaa.” (Yer. 30:11) Ingawa hawachukui muda mrefu sana, wazee pia hawafanyi uamuzi haraka-haraka. Mambo yanaposhughulikiwa kwa njia inayofaa, kutaniko lote litanufaika. Ingawa matatizo yanaweza kushughulikiwa kwa njia hiyo nzuri, huenda bado mtu aliyekosewa akahisi maumivu. Ikiwa unakabili hali hiyo, unaweza kufanya nini ili kupunguza maumivu unayohisi?

14. Nĩ ngerekano ĩrĩku ya Bibiria yũũmba gũgũtethia kũũmbana na ũrũrũ bwa gwatĩrua nĩ Mũkristũ ũngĩ?

14 Je, umewahi kukosewa sana na mtu fulani, labda hata mwabudu mwenzako? Unaweza kupata mifano ya pekee katika Neno la Mungu ambayo inatufundisha jinsi ya kumngojea Yehova arekebishe mambo. Kwa mfano, ingawa Yosefu alitendewa isivyo haki na ndugu zake mwenyewe, hakuruhusu dhambi zao zimfanye awe mwenye uchungu. Badala yake, aliendelea kukazia fikira utumishi wake kwa Yehova, ambaye alimthawabisha sana kwa kuvumilia kwa subira. (Mwa. 39:21) Baada ya muda, Yosefu aliweza kuwasamehe wale waliomuumiza na kuona jinsi Yehova alivyokuwa amembariki. (Mwa. 45:5) Kama Yosefu, tunafarijika tunapomkaribia Yehova na kuacha mambo mikononi mwake.—Zab. 7:17; 73:28.

15. Nĩmbi gĩatethererie mwarĩ-o-baaba ũmwe kũũmbana rĩrĩa athithĩĩrue na njĩra ĩtĩ ya ĩota?

15 Ni kweli kwamba si ukosefu wote wa haki ni mzito kama aliotendewa Yosefu, lakini sote tunaumia tunapotendewa isivyo haki kwa njia moja au nyingine. Tunapokuwa na tatizo na mtu, kutia ndani mtu ambaye si mwabudu wa Yehova, tutanufaika ikiwa tutatumia kanuni za Biblia. (Flp. 2:3, 4) Fikiria kisa kimoja. Dada fulani aliumia sana alipogundua kwamba mfanyakazi mwenzake alikuwa akiwaeleza watu mambo mabaya na yasiyo ya kweli kumhusu. Badala ya kuchukua hatua haraka-haraka, dada huyo alichukua wakati kutafakari mfano wa Yesu. Alipokuwa akitukanwa, hakujibu kwa kutukana. (1 Pet. 2:21, 23) Akiwa na hilo akilini, aliamua kutofanya jambo lolote. Baadaye, alisikia kwamba mfanyakazi mwenzake alikuwa anakabiliana na tatizo zito la afya na alikuwa na mkazo sana. Dada huyo aliamua kwamba huenda mfanyakazi mwenzake hakumaanisha alichosema. Hivyo, alifurahi sana kwamba alivumilia kwa subira ukosefu huo wa haki, na alipata amani.

16. Nĩmbi kĩũmba gũkũboreria kwethĩrwa nũkũũmĩĩria wagi bwa ĩota? (1 Petero 3:12)

16 Ikiwa unavumilia ukosefu wa haki au jambo lingine linalokusababishia maumivu, kumbuka kwamba Yehova huwakaribia wale “waliovunjika moyo.” (Zab. 34:18) Anakupenda kwa sababu ya subira yako na kwa kumtupia mzigo wako. (Zab. 55:22) Yeye ndiye mwamuzi wa dunia yote. Hakuna jambo asiloliona. (Soma 1 Petro 3:12.) Unapopitia hali ngumu ambazo huwezi kusuluhisha, je, utakuwa tayari kumngojea?

ITHARIMO BĨTĨ NA MŨTHIA KĨRĨ BARĨA BETAGĨĨRA JEHOVA

17. Ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ Isaya 30:18, nĩ ũrikithia bũrĩkũ Jehova agũtwa?

17 Hivi karibuni, Baba yetu wa mbinguni atatubariki sana kupitia Ufalme wake. Andiko la Isaya 30:18 linasema: “Yehova anangoja kwa subira ili kuwaonyesha kibali, naye atainuka ili kuwaonyesha rehema. Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki. Wenye furaha ni wote wanaoendelea kumtarajia.” Wale wote wanaoendelea kumtarajia Yehova watapata baraka nyingi sasa na pia katika ulimwengu mpya unaokuja.

18. Nĩ itharimo birĩkũ twetereete?

18 Watu wa Mungu watakapoingia katika ulimwengu mpya, hawatahitaji tena kuvumilia mahangaiko na changamoto ambazo ni lazima wakabili leo. Hakutakuwa na ukosefu wa haki, na maumivu hayatakuwepo tena. (Ufu. 21:4) Hatutahitaji kungojea kwa wasiwasi mambo tunayohitaji kwa sababu yatapatikana kwa wingi. (Zab. 72:16; Isa. 54:13) Hiyo ni baraka kubwa sana!

19. Nandĩ Jehova arĩtũthuranĩra tontũ bwa ũntũ bũrĩkũ ĩtagaaria kwa ĩtagaaria?

19 Kwa sasa, kila tunaposhinda zoea fulani baya na kusitawisha sifa fulani nzuri, Yehova anatutayarisha kwa ajili ya maisha chini ya utawala wake. Usivunjike moyo au kukata tamaa. Maisha bora zaidi yako mbele yetu! Kwa kuwa tuna wakati ujao mzuri tunaoutarajia, acheni tuendelee kuwa tayari kumngojea Yehova kwa subira anapokamilisha kazi yake!

RWĨMBO 118 “Tupe Imani Zaidi”

^ gic. 5 Je, umewahi kumsikia mtumishi wa Yehova wa miaka mingi akisema, ‘Sikuwahi kutarajia kwamba katika umri wangu bado ningekuwa ninaishi katika mfumo huu wa mambo’? Sote tunatamani kuona Yehova akikomesha mfumo huu wa mambo, hasa katika nyakati hizi ngumu. Hata hivyo, ni lazima tujifunze kuwa na subira. Katika makala hii, tutachunguza kanuni za Biblia zitakazotusaidia kuwa na mtazamo wa kungojea. Pia, tutachunguza maeneo mawili ambayo ni lazima tumngojee Yehova kwa subira. Mwishowe tutachunguza baraka watakazopata wale walio tayari kumngojea Yehova.

^ gic. 56 MAELEZO YA PICHA: Tangu utotoni, dada huyu amekuwa akisali kwa ukawaida kwa Yehova. Alipokuwa mtoto, wazazi wake walimfundisha jinsi ya kusali. Alipokuwa kijana, alianza kutumikia akiwa painia na mara kwa mara alimwomba Yehova ambariki katika huduma. Miaka mingi baadaye, mume wake alipokuwa mgonjwa sana, alitoa dua kwa Yehova ili ampe nguvu alizohitaji kuvumilia jaribu hilo. Leo, akiwa mjane anadumu katika sala akiwa na uhakika kwamba Baba yake wa mbinguni atajibu sala zake—kama tu alivyofanya katika maisha yake yote.