Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 32

Rikia Wĩtĩkio Bwaku Kĩrĩ Mũũmbi

Rikia Wĩtĩkio Bwaku Kĩrĩ Mũũmbi

“Wĩtĩkio nĩ . . . kũmenya tũtĩ na nkaanja atĩ mantũ jau jatĩonekaga jarĩ o.”​—AHI. 11:1 KIMERU BIBLE, 2010.

RWĨMBO 11 Uumbaji Unamsifu Mungu

MUHTASARI *

1. Nĩmbi ũritanĩtwe biegie Mũũmbi wetũ?

IKIWA ulilelewa katika familia ya Mashahidi wa Yehova, inaelekea ulijifunza kumhusu Yehova tangu utotoni. Ulifundishwa kwamba Yehova ndiye Muumba, ana sifa zenye kuvutia, na kwamba ana kusudi lenye upendo kwa ajili ya wanadamu.—Mwa. 1:1; Mdo. 17:24-27.

2. Nĩatĩa antũ bamwe bonaga barĩa betĩkĩĩtie kũrĩ na mũũmbi?

2 Hata hivyo, watu wengi hawaamini Mungu yupo, sembuse kwamba yeye ni Muumba! Badala yake, wanaamini kwamba uhai ulijitokeza wenyewe, kisha viumbe hai sahili waligeuka polepole na kuwa viumbe tata zaidi. Baadhi ya watu hao wana elimu ya juu sana. Huenda wakadai kuwa sayansi imethibitisha kwamba Biblia si sahihi na kwamba watu walio na imani katika Muumba hawana elimu, ni dhaifu, au wanadanganyika kirahisi.

3. Nĩkĩ nĩ ũntũ bwa bata gwaka wĩtĩkio bwetũ?

3 Je, maoni ya watu fulani wenye elimu ya juu yatayumbisha imani yetu kwamba Yehova ni Muumba wetu mwenye upendo? Hilo linategemea sana kwa nini tunaamini kwamba Yehova ni Muumba wetu. Je, ni kwa sababu tuliambiwa tuamini hivyo au ni kwa sababu tumetumia muda kuchunguza wenyewe uthibitisho uliopo? (1 Kor. 3:12-15) Haidhuru tumekuwa Mashahidi wa Yehova kwa muda gani, sote tunahitaji kuendelea kujenga imani yetu. Tunapofanya hivyo, hatutapotoshwa na “falsafa na udanganyifu mtupu” unaofundishwa na watu wanaopinga Neno la Mungu. (Kol. 2:8; Ebr. 11:6) Ili kutusaidia, makala hii itazungumzia (1) kwa nini watu wengi hawana imani katika Muumba, (2) jinsi unavyoweza kujenga imani yako katika Yehova, Muumba wako, na (3) jinsi unavyoweza kuendelea kuimarisha imani yako.

NĨKĨ ANTŨ BABAINGĨ BATĨTĨKĨĨTIE KŨRĨ NA MUUMBI

4. Kũringana na Ahibirania 11:1 na nteto irĩa irĩgaiti, wĩtĩkio bwa mma bũrĩrĩgĩĩra mbi?

4 Baadhi ya watu wanafikiri kwamba kuwa na imani kunamaanisha kuamini kitu fulani bila uthibitisho. Lakini kulingana na Biblia, hiyo si imani ya kweli. (Soma Waebrania 11:1 na maelezo ya chini.) Ona kwamba kuwa na imani katika mambo halisi ambayo hayaonekani, kama vile Yehova, Yesu, na Ufalme wa mbinguni, kunategemea uthibitisho wenye kuridhisha. (Ebr. 11:3) Shahidi mmoja ambaye ni mtaalamu wa biolojia na kemia, anasema hivi: “Imani yetu si jambo lisilo na uthibitisho ambalo hupuuza mambo hakika ya kisayansi.”

5. Nĩkĩ antũ babaingĩ betĩkĩĩtie ũtũũro ka bwaciumĩĩrie bũtĩ na Mũũmbi?

5 Huenda tukajiuliza, ‘Ikiwa kuna uthibitisho wenye kuridhisha wa kuwepo kwa Muumba, kwa nini watu wengi wanaamini kwamba Mungu hakuhusika katika kutokeza uhai? ’ Baadhi ya watu hawajawahi kamwe kuchunguza uthibitisho uliopo wao wenyewe. Robert, ambaye sasa ni Shahidi wa Yehova, anasema hivi: “Kwa kuwa uumbaji haukutajwa kamwe shuleni, nilifikiri kwamba haukuwa kweli. Niliamini hivyo hadi nilipozungumza na Mashahidi wa Yehova nilipokuwa na umri wa miaka 22, na kusikia uthibitisho wenye kusadikisha na unaopatana na akili kutoka katika Biblia unaounga mkono uumbaji.” *—Tazama sanduku “Himizo kwa Wazazi.”

6. Nĩkĩ bamwe baregaga gwĩtĩkia kũrĩ na Mũrungu?

6 Baadhi ya watu hawana imani katika Muumba kwa sababu wanasema kwamba wanaamini tu kile wanachoweza kuona. Hata hivyo, kimsingi wanaamini kuwepo kwa vitu ambavyo hawawezi kuona, kama vile upepo, kwa sababu wana uthibitisho kwamba upepo ni kitu halisi. Aina ya imani inayotajwa katika Biblia inahusisha uthibitisho wa ‘mambo mengine halisi ambayo hayaonekani.’ (Ebr. 11:1) Inahitaji muda na jitihada ili sisi wenyewe tuchunguze uthibitisho uliopo, na watu wengi hawajasitawisha hamu inayohitajika ili kufanya hivyo. Mtu ambaye hatachunguza uthibitisho uliopo yeye mwenyewe, huenda akafikia mkataa kwamba hakuna Mungu.

7. Ka antũ bonthe barĩa athoomu baregaga atĩ Mũrungu noombĩre nthĩgũrũ? Tarĩĩria.

7 Baada ya kuchunguza uthibitisho uliopo, baadhi ya wanasayansi wamesadiki kwamba Mungu aliumba ulimwengu mzima. * Kama Robert, aliyetajwa awali, huenda baadhi ya watu walifikiri kwamba hakuna Muumba kwa sababu tu hawakufundishwa kuhusu uumbaji wakiwa chuo kikuu. Hata hivyo, wanasayansi wengi wamekuja kumjua na kumpenda Yehova. Kama ilivyo kwa wanasayansi hao, ni lazima sisi sote tujenge imani yetu katika Mungu, haidhuru tuna elimu kadiri gani. Hakuna anayeweza kufanya hivyo kwa niaba yetu.

ŨRĨA ŨŨMBA GWAKA WĨTĨKIO BWAKU KĨRĨ MŨŨMBI

8-9. (a) Tũgacunkũũna kĩũria kĩrĩku? (b) Nĩatĩa kwiritana mantũ jegie ũũmbi kũgakũguna?

8 Unaweza kujengaje imani yako katika Muumba? Acheni tuchunguze njia nne.

9 Jifunze kuhusu uumbaji. Unaweza kujenga imani yako katika Muumba kwa kuchunguza wanyama, mimea, na nyota. (Zab. 19:1; Isa. 40:26) Kadiri unavyojifunza kuhusu vitu hivyo, ndivyo utakavyosadiki kwamba Yehova ndiye Muumba. Mara nyingi machapisho yetu yanakuwa na makala zilizo na habari hususa kuhusu uumbaji. Usiruke makala hizo hata ikiwa unaona ni ngumu kuelewa. Jifunze mambo mengi kadiri unavyoweza. Na usisahau kutazama video maridadi zinazohusu uumbaji zilizoonyeshwa kwenye makusanyiko yetu ya eneo katika miaka ya karibuni, zinazopatikana kwenye tovuti yetu.

10. Ejana ngerekano ya ũrĩa ũũmbi bũrikithagia atĩ kũrĩ na Mũũmbi. (Aroma 1:20)

10 Unapojifunza kuhusu uumbaji, kazia uangalifu yale ambayo unafunua kumhusu Muumba wetu. (Soma Waroma 1:20.) Kwa mfano, huenda unajua kwamba jua letu halitoi tu joto linaloendeleza uhai, bali pia linatoa nishati yenye madhara katika mfumo wa miale ya urujuanimno (ultraviolet rays). Wanadamu wanahitaji kulindwa dhidi ya miale hiyo. Na tunalindwa! Jinsi gani? Dunia yetu ina tabaka la anga-hewa linalotukinga, yaani, tabaka la gesi ya ozoni linalochuja mionzi hiyo yenye madhara. Kadiri miale ya urujuanimno kutoka kwenye jua inavyoongezeka, ndivyo kiwango cha gesi ya ozoni kinavyoongezeka. Je, hukubali kwamba ni lazima kuwe na mtu fulani aliyebuni jambo hilo, na kwamba yeye ni Muumba mwenye akili na upendo?

11. Nĩkũ ũũmba kwona mantũ ja gwaka wĩtĩkio bwegie ũũmbi? (tega kathandũkũ “Gwa Kũrita Mantũ ja Gwaka Wĩtĩkio.”)

11 Unaweza kupata habari nyingi zenye kujenga imani kuhusu uumbaji kwa kutumia Fahirisi na kwa kufanya utafiti kwenye tovuti ya jw.org. Unaweza kuanza na makala na video kutoka kwenye mfululizo “Je, Ni Kazi ya Ubuni?” Makala na video hizo ni fupi na zina habari zenye kustaajabisha kuhusu wanyama na uumbaji mwingine. Pia, zina mifano ya jinsi wanasayansi wanavyojaribu kuiga vitu hivyo.

12. Rĩrĩa tũkwiritana Bibiria, nĩ jamwe ja mantũ jarĩkũ tũbuĩrĩte kũthũgaanĩria?

12 Jifunze Biblia. Mwanzoni, mtaalamu wa biolojia na kemia aliyetajwa awali, alikataa wazo la kwamba kuna Muumba. Hata hivyo, baada ya muda, alikuja kuamini kuwa kuna Muumba. Anasema hivi: “Imani yangu haikutegemea tu mambo niliyojifunza katika sayansi. Ilitegemea pia kujifunza kwa makini Biblia.” Labda tayari una ujuzi sahihi kuhusu mafundisho ya Biblia. Hata hivyo, ili kujenga imani yako katika Muumba, unahitaji kuendelea kujifunza Neno la Mungu. (Yos. 1:8; Zab. 119:97) Kwa mfano, fikiria jinsi ambavyo Biblia ni sahihi inapofafanua matukio ya kihistoria. Pia, fikiria kuhusu jinsi unabii wake ulivyotimizwa na upatano wake. Kufanya hivyo, kunaweza kuimarisha imani yako kwamba Muumba mwenye upendo na hekima alituumba na kwamba Biblia ni ujumbe kutoka kwake. *2 Tim. 3:14; 2 Pet. 1:21.

13. Nĩ ngerekano ĩrĩku ĩmwe ya ũũme ĩkwoneka Rũtetone rwa Mũrungu?

13 Unapojifunza Neno la Mungu, ona jinsi ushauri wake ulivyo na faida. Kwa mfano, miaka mingi iliyopita Biblia ilionya kwamba kupenda pesa kuna madhara na husababisha “maumivu mengi.” (1 Tim. 6:9, 10; Met. 28:20; Mt. 6:24) Je, bado onyo hilo linatufaa leo? Kitabu The Narcissism Epidemic, kinasema hivi: “Kwa ujumla watu wanaopenda mali hawana furaha sana na wameshuka moyo. Hata watu wanaotamani tu kuwa na pesa zaidi, huwa na afya mbaya ya akili; pia wana matatizo mengine ya kiafya.” Kwa kweli, onyo la Biblia kuhusu kupenda pesa ni lenye faida! Je, unaweza kufikiria kanuni nyingine za Biblia ambazo zimethibitika kuwa zenye manufaa? Kadiri tunavyothamini ushauri wa Biblia, ndivyo tutakavyotegemea zaidi hekima hiyo isiyopitwa na wakati kutoka kwa Muumba wetu anayetupenda. (Yak. 1:5) Matokeo ni kwamba tutakuwa na shangwe zaidi maishani.—Isa. 48:17, 18.

14. Nĩmbi wiritani bwa Bibiria bũkagwura bwegie Jehova?

14 Jifunze ukiwa na lengo linalofaa, yaani, kumjua Yehova. (Yoh. 17:3) Unapojifunza Biblia, utajifunza kuhusu utu na sifa za Yehova—ambazo zinaonekana pia katika uumbaji. Sifa hizo zinakuthibitishia kwamba Yehova ni Mtu halisi, na si wa kuwaziwa tu. (Kut. 34:6, 7; Zab. 145:8, 9) Kadiri unavyoendelea kumjua Yehova zaidi na zaidi, imani yako kwake itakua, upendo wako utaimarika, na urafiki wenu utakuwa wa karibu zaidi.

15. Nĩatĩa ũkagunĩka wera bangĩ bwegie wĩtĩkio bwaku?

15 Waeleze wengine kuhusu imani yako katika Mungu. Unapofanya hivyo, imani yako itaimarishwa. Lakini namna gani ikiwa mtu fulani uliyemhubiria atauliza swali kuhusu kuwepo kwa Mungu na huna uhakika wa jinsi ya kumjibu? Jitahidi kutafuta jibu la Kimaandiko kwenye mojawapo ya machapisho yetu, kisha zungumza naye kuhusu habari hiyo. (1 Pet. 3:15) Pia, unaweza kumwomba Shahidi mwenzako mwenye uzoefu akusaidie. Iwe mtu huyo atakubali au hatakubali majibu ya Biblia, utakuwa umenufaika kwa kufanya utafiti huo. Imani yako itaimarika. Matokeo ni kwamba hautashawishiwa kirahisi na madai ya uwongo ya wa wale wanaoonekana kuwa wenye hekima na elimu, ambao husema kwamba hakuna Muumba.

ĨTA NA MBERE KŨRIKIA WĨTĨKIO BWAKU!

16. Nĩmbi gĩgakarĩka kethĩra tũtĩĩta na mbere gwaka na kũrikia wĩtĩkio bwetũ?

16 Haidhuru tumekuwa tukimtumikia Yehova kwa muda mrefu kadiri gani, ni lazima tuendelee kujenga na kuimarisha imani yetu katika Yehova. Kwa nini? Kwa sababu ikiwa hatutakuwa makini, imani yetu inaweza kudhoofika. Kumbuka kwamba imani inahusisha uthibitisho wa mambo halisi yasiyoonekana. Ni rahisi kwetu kusahau mambo tusiyoyaona. Hivyo, Paulo alirejelea kukosa imani kuwa “dhambi inayotutatanisha kwa urahisi.” (Ebr. 12:1) Basi tunaweza kuepukaje mtego huo?—2 The. 1:3.

17. Nĩ ũtethio bũrĩkũ tũkũbatara kenda tũrikia wĩtĩkio bwetũ?

17 Kwanza, msihi Yehova akupatie roho yake takatifu, na ufanye hivyo mara kwa mara. Kwa nini? Kwa sababu imani ni sifa ya tunda la roho. (Gal. 5:22, 23) Hatuwezi kujenga na kuimarisha imani yetu katika Muumba wetu, bila msaada wa roho takatifu. Ikiwa tutaendelea kumwomba Yehova roho yake, atatupatia. (Luka 11:13) Tunaweza kusali hivi kihususa: “Tusaidie tuwe na imani zaidi.”—Luka 17:5.

18. Ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ Zaburi 1:2, 3, nĩ wendeeri bũrĩkũ tũũmba kũgwĩrĩrua?

18 Pia, jifunze kibinafsi na kwa ukawaida Neno la Mungu. (Soma Zaburi 1:2, 3.) Zaburi hiyo ilipotungwa, Waisraeli wachache walikuwa na nakala iliyokamilika ya Sheria ya Mungu. Hata hivyo, wafalme na makuhani wangeweza kupata nakala hizo, na kila baada ya miaka saba mpango ulifanywa ili “wanaume, wanawake, watoto” na wakaaji wageni wa Israeli wasikilize Sheria ya Mungu iliposomwa. (Kum. 31:10-12) Katika siku za Yesu, hati-kunjo za Maandiko zingepatikana miongoni mwa watu wachache na kwenye masinagogi. Tofauti na hilo, katika siku zetu, watu wengi wanaweza kupata Biblia ikiwa nzima au kwa sehemu. Hilo ni pendeleo kubwa. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunathamini pendeleo hilo?

19. Nĩmbi tũkũbatara kũthithia kenda tũtũũria wĩtĩkio bwetũ bũriki?

19 Tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini pendeleo la kuwa na Neno la Mungu kwa kulisoma kwa ukawaida. Funzo letu la kibinafsi halipaswi kuwa jambo la kivivi hivi tu tunalofanya tunapohisi tuna wakati wa ziada. Tunapodumisha ratiba yetu ya kujifunza, tunaweza kuendelea kuimarisha imani yetu.

20. Tũbuĩrĩte gũtua ĩtua rĩa kũthithia atĩa?

20 Tofauti na watu “wenye hekima na wenye elimu” wa ulimwengu huu, sisi tuna imani yenye nguvu inayotegemea Neno la Mungu. (Mt. 11:25, 26) Kupitia funzo letu la kitabu hicho kitakatifu, tunajua kwa nini hali za ulimwengu zinazorota na kile ambacho Yehova atafanya kuhusu hali hizo. Hivyo, acheni tuazimie kuimarisha imani yetu na kuwasaidia watu wengi kadiri inavyowezekana wawe na imani katika Muumba wetu. (1 Tim. 2:3, 4) Acheni tuendelee kutazamia kwa hamu wakati ambapo wote watakaokuwa hai duniani watamsifu Yehova na kusema maneno haya ya Ufunuo 4:11: “Unastahili, Ee Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu . . . kwa sababu uliumba vitu vyote.”

RWĨMBO 2 Jina Lako Ni Yehova

^ gic. 5 Maandiko yanafundisha wazi kwamba Yehova Mungu, ndiye Muumba. Lakini watu wengi hawaamini hilo. Wanasisitiza kwamba uhai ulijitokeza wenyewe. Ikiwa tutajitahidi kuimarisha imani yetu katika Mungu na Biblia, madai yao hayawezi kuyumbisha uhakika wetu. Makala hii itafafanua jinsi tunavyoweza kufanya hivyo.

^ gic. 5 Katika shule nyingi za umma, walimu hata hawafundishi kuwa kuna uwezekano kwamba Mungu aliumba vitu vyote. Baadhi ya walimu wanahisi ikiwa watafanya hivyo, watakuwa wakiwalazimisha wanafunzi waamini kwamba kuna Mungu na kuingilia uhuru wao wa kidini.

^ gic. 7 Maelezo ya watu zaidi ya 60 wenye elimu ya juu, kutia ndani wanasayansi, ambao wanaamini uumbaji yanaweza kupatikana kwenye Fahirisi ya karibuni. Chini ya kichwa “Sayansi,” tafuta kichwa kidogo “wanasayansi wanaoamini kuna uumbaji.” Baadhi ya maelezo hayo yanaweza pia kupatikana kwenye Mwongozo wa Utafiti wa Mashahidi wa Yehova. Chini ya habari “Sayansi na Teknolojia,” tafuta kichwa kidogo “‘Mahojiano’ (Mfululizo katika Amkeni!).”

^ gic. 12 Kwa mfano, tazama makala “Je, Sayansi Inapatana na Biblia?” katika gazeti la Amkeni! la Februari 2011, na makala “Yale Anayotabiri Yehova Yanatimia” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2008.