Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 14

‘Thingata Makinya Jaawe’

‘Thingata Makinya Jaawe’

“Kristo kinya we naanyamaarirue ni untu bwenu nawe arabutigira mungˈuanano jumwega, nikenda bukathingataga makinya jawe.”—1 PET. 2:21.

RWĨMBO 13 Kristo, Kielelezo Chetu

MUHTASARI *

Yesu ametuachia hatua zake ili tuzifuate kwa ukaribu (Tazama fungu la 1 na 2)

1-2. Nĩatĩa tũũmba kũthingata makinya ja Jesũ? Ejana ngerekano.

WAZIA kwamba wewe ni miongoni mwa kikundi cha watu wanaotembea katika nyika hatari, iliyofunikwa na theluji. Mnamfuata mwongozaji mwenye uzoefu. Anapotembea anaacha nyuma alama za viatu, au hatua zake kwenye theluji. Pindi moja huwezi kumwona mwongozaji huyo! Lakini hushikwi na wasiwasi. Badala yake, wewe pamoja na watu wengine unaotembea nao, mnafuata kwa ukaribu na kadiri mwezavyo hatua za mwongozaji huyo!

2 Tukiwa Wakristo wa kweli, kwa njia ya mfano tunatembea katika nyika hatari, yaani, ulimwengu huu mwovu. Inapendeza kwamba Yehova ametupatia Mwongozaji mkamilifu—Yesu Kristo, Mwana wake ambaye tunaweza kufuata hatua zake kwa ukaribu. (1 Pet. 2:21) Kulingana na kitabu kimoja cha marejeo ya Biblia, Petro anatumia lugha ya mfano kumlinganisha Yesu na mwongozaji. Kama mwongozaji anavyoacha nyuma alama za viatu vyake, Yesu ametuachia alama za viatu, au hatua ambazo tunaweza kufuata. Acheni tuchunguze maswali matatu kuhusu kufuata hatua za Yesu: Inamaanisha nini kufuata hatua za Yesu? Kwa nini tunapaswa kufanya hivyo? Na tunaweza kufanya hivyo jinsi gani?

KŨTHINGATA MAKINYA JA JESŨ NĨ KUUGA ATĨA?

3. Kũthingata makinya ja muntũ ũngĩ nĩ kuuga atĩa?

3 Inamaanisha nini kufuata hatua za mtu fulani? Katika Biblia, nyakati nyingine maneno ‘tembea’ na “miguu” yanarejelea njia ya maisha ya mtu. (Mwa. 6:9; Met. 4:26) Kielelezo ambacho mtu huacha maishani mwake, kinaweza kulinganishwa na alama za viatu, au hatua anazoacha nyuma anapotembea. Hivyo, kufuata hatua za mtu fulani kunamaanisha kufuata mfano wake, yaani, kumwiga.

4. Kũthingata makinya ja Jesũ nĩ kuuga atĩa?

4 Hivyo basi, inamaanisha ni kufuata hatua za Yesu? Kwa ufupi, inamaanisha kuiga mfano wake. Katika andiko letu la msingi, mtume Petro anazungumzia kihususa mfano mzuri ambao Yesu alituwekea wa kuvumilia mateso; hata hivyo, tunaweza kumwiga Yesu kwa njia nyingine nyingi. (1 Pet. 2:18-25) Kwa kweli, njia yote ya maisha ya Yesu, yaani, kila kitu alichosema na kutenda, ni mfano mzuri ambao tunaweza kufuata.

5. Antũ batĩũjũri rĩ, no boombe kũthingata ngerekano ĩmbũjũru ya Jesũ? Taarĩĩria.

5 Tukiwa wanadamu wasio wakamilifu, je, kweli tunaweza kufuata mfano wa Yesu? Ndiyo, tunaweza. Kumbuka kwamba Petro anatuhimiza ‘tufuate hatua za Yesu kwa ukaribu’—si kwa ukamilifu. Ikiwa tunafuata hatua zake kwa makini, yaani, tunafanya yote tuwezayo tukiwa wanadamu wasio wakamilifu, tutakuwa tukitii maneno haya ya mtume Yohana kwamba tuendelee “kutembea kama huyo [Yesu] alivyotembea.”—1 Yoh. 2:6

NĨKĨ TŨTHINGATE MAKINYA JA JESŨ?

6-7. Nĩkĩ tũũmba kuuga kũthingata makinya ja Jesũ gũgatũma tũkuĩrĩĩria Jehova?

6 Tunapofuata hatua za Yesu tutamkaribia zaidi Yehova. Kwa nini tunaweza kusema hivyo? Kwanza, Yesu alituwekea mfano wa pekee sana wa jinsi ya kuishi kwa njia ambayo inampendeza Mungu. (Yoh. 8:29) Hivyo, tunapofuata hatua za Yesu, tutampendeza Yehova. Na tunaweza kuwa na hakika kwamba Baba yetu wa mbinguni atawakaribia wale wanaojitahidi kuwa rafiki zake.—Yak. 4:8

7 Pili, Yesu alimwiga Baba yake kikamilifu. Hiyo ndiyo sababu Yesu angeweza kusema hivi: “Yeyote ambaye ameniona mimi amemwona Baba pia.” (Yoh. 14:9) Tunapoiga sifa nzuri za Yesu na jinsi alivyoshughulika na wengine—kwa mfano, jinsi alivyomsikitikia mtu mwenye ukoma, alivyomwonyesha hisia-mwenzi mwanamke mwenye ugonjwa mbaya, na alivyowaonyesha huruma wanaoomboleza—tunakuwa tukimwiga Yehova pia. (Marko 1:40, 41; 5:25-34; Yoh. 11:33-35) Kadiri tunavyokuwa na sifa kama za Yehova, ndivyo tunavyomkaribia zaidi.

8. Taarĩĩria nĩkĩ kũthingata makinya ja Jesũ gũgatũteethia ‘kũũmba’ nthĩgũrũ.

8 Kufuata hatua za Yesu kunatusaidia tusikengeushwe na ulimwengu huu mwovu. Katika usiku wa mwisho wa maisha yake hapa duniani, Yesu aliweza kusema hivi: “Mimi nimeushinda ulimwengu.” (Yoh. 16:33) Alimaanisha kwamba alikuwa amekataa kuruhusu njia ya kufikiri, malengo, na matendo ya watu wa ulimwengu huu yamwathiri. Kamwe Yesu hakujiruhusu aache kukazia fikira sababu iliyomfanya atumwe duniani, yaani, kumtetea Yehova. Namna gani sisi? Katika ulimwengu huu, kuna mambo mengi yanayoweza kutukengeusha. Lakini kama Yesu, ikiwa tutaendelea kukazia fikira kufanya mapenzi ya Yehova, sisi pia ‘tutaushinda’ ulimwengu.—1 Yoh. 5:5.

9. No mwanka tũthithie atĩa nĩkenda twĩta na mbere gũkara njĩrene ya mwoyo?

9 Kufuata hatua za Yesu huongoza kwenye uzima wa milele. Mwanamume kijana tajiri alipomuuliza Yesu alihitaji kufanya nini ili apate uzima wa milele, Yesu alimjibu hivi: ‘Njoo uwe mfuasi wangu.’ (Mt. 19:16-21) Yesu aliwaambia hivi baadhi ya Wayahudi ambao hawakuamini kwamba alikuwa Kristo: “Kondoo wangu . . . hunifuata. Mimi ninawapa uzima wa milele.” (Yoh. 10:24-29) Yesu alimwambia Nikodemo, mshiriki wa Sanhedrini aliyependezwa na mafundisho ya Yesu kwamba wale ‘wanaomwamini’ wangepata “uzima wa milele.” (Yoh. 3:16) Tunaonyesha kwamba tunamwamini Yesu kwa kutumia mambo aliyofundisha na kwa kuiga mfano wake. Ikiwa tutafanya hivyo, tutabaki katika barabara inayoongoza kwenye uzima wa milele.—Mt. 7:14.

NĨATĨA TŨŨMBA KŨTHINGATA MAKINYA JA JESŨ BWEGA?

10. Nĩmbi biendekaga kĩrĩ ‘kũmenya’ Jesũ bwega? (Johana 17:3)

10 Ili tufaulu kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu, ni lazima tumjue. (Soma Yohana 17:3.) ‘Kumjua’ Yesu ni jambo tunalopaswa kuendelea kufanya. Ni lazima tumjue vizuri zaidi na zaidi, yaani, tujifunze kuhusu sifa zake, njia yake ya kufikiri, na viwango vyake. Haidhuru tumekuwa katika kweli kwa muda mrefu kadiri gani, ni lazima tuendelee kujitahidi kumjua Yehova na Mwana wake.

11. Nĩmbi biarĩĩragua kĩrĩ mauku jana ja Injli?

11 Ili kutusaidia tumjue Mwana wake, kwa upendo Yehova alitia ndani ya Neno lake vile vitabu vinne vya Injili. Vitabu hivyo vya Injili vina masimulizi ya maisha na huduma ya Yesu. Masimulizi hayo yanatuambia kuhusu mambo ambayo Yesu alisema, yanatuonyesha mambo ambayo alifanya, na kutufunulia jinsi alivyohisi. Vitabu hivyo vinne vinatusaidia ‘kufikiria sana’ mfano wa Yesu. (Ebr. 12:3) Tunaweza kusema kwamba vitabu hivyo vina hatua ambazo Yesu alituachia. Hivyo, kwa kujifunza vitabu vya Injili, tunaweza kumjua Yesu zaidi na zaidi. Matokeo ni kwamba tutaweza kufuata hatua zake kwa ukaribu.

12. Nĩatĩa tũũmba kũgunĩka buru kuumania na mauku ja Injili?

12 Ili tunufaike kikamili na vitabu vya Injili, ni lazima tufanye mengi zaidi ya kuvisoma tu. Tunahitaji kutenga wakati ili kujifunza vitabu hivyo kwa makini na kuvitafakari kwa kina. (Linganisha Yoshua 1:8, maelezo ya chini.) Acheni tuchunguze mapendekezo mawili yanayoweza kutusaidia kutafakari na kutumia mambo tunayosoma kwenye vitabu hivyo vya Injili.

13. Nĩatĩa tũũmba kũgwĩrĩrua mantũ jarĩa jarĩ kĩrĩ mauku ja Injili?

13 Kwanza, yafanye masimulizi ya vitabu vya Injili yawe halisi zaidi kwako. Tumia uwezo wako wa kuwazia mambo ili kuona, kusikia, na kuhisi mambo yaliyokuwa yakitukia. Ili kukusaidia kufanya hivyo, fanya utafiti kwa kutumia vifaa vya kujifunzia vilivyoandaliwa na tengenezo la Yehova. Chunguza muktadha, yaani, matukio yanayotangulia au kufuata habari unayojifunza. Tafuta habari zaidi kuhusu watu na maeneo yanayotajwa katika simulizi hilo. Linganisha simulizi unalojifunza na simulizi hilohilo kwenye kitabu kingine cha Injili. Nyakati nyingine, mwandikaji mmoja wa Injili anatia ndani habari muhimu ambazo mwandikaji mwingine aliziacha.

14-15. Nĩatĩa tũũmba gũtumĩra ũtũũrone bwetũ mantũ jarĩa jaandĩki kĩrĩ mauku ja Injili?

14 Pili, tumia masimulizi ya Injili katika maisha yako. (Yoh. 13:17) Baada ya kujifunza kwa makini simulizi fulani la Injili jiulize: ‘Je, kuna jambo lolote katika simulizi hili ninaloweza kutumia maishani mwangu? Ninaweza kutumiaje simulizi hili ili kumsaidia mtu mwingine?’ Jaribu kumfikiria mtu hususa, kisha kwa wakati unaofaa, kwa upendo na busara shiriki naye jambo ulilojifunza.

15 Acheni tuchunguze mfano wa jinsi tunavyoweza kutumia mapendekezo hayo mawili. Tutachunguza simulizi la mjane maskini ambaye Yesu alikuwa akimtazama hekaluni.

MWEKŨRŨ NTIGWA KĨŨRŨNE

16. Taarĩĩria ũntũ bũrĩa bwandĩki kĩrĩ Mariko 12:41.

16 Lifanye simulizi liwe halisi zaidi kwako. (Soma Marko 12:41.) Wazia tukio lifuatalo. Ni siku ya Nisani 11, 33 W.K.—siku chache kabla ya kifo cha Yesu. Yesu ametumia muda mwingi siku hiyo kufundisha hekaluni. Lakini viongozi wa kidini wamekuwa wakimpinga. Awali, baadhi yao walitilia shaka mamlaka yake. Wengine walijaribu kumuuliza maswali ambayo walidhani hangeweza kujibu. (Marko 11:27-33; 12:13-34) Sasa Yesu ameenda upande mwingine wa hekalu. Akiwa hapo—huenda kwenye eneo lililoitwa Ua wa Wanawake—anaweza kuona masanduku ya hazina kando ya kuta za ua huo. Anaketi hapo na kuanza kuwatazama watu wanaotumbukiza michango yao kwenye masanduku. Anaona matajiri wengi wakitumbukiza sarafu nyingi. Huenda yuko karibu sana hivi kwamba anasikia sauti za sarafu zinapotumbukizwa kwenye masanduku.

17. Nĩatĩa mwekũrũ ntigwa ũrĩa ũgweti kĩrĩ Mariko 12:42 aathithĩrie?

17 Soma Marko 12:42. Baada ya muda, Yesu anamwona mwanamke fulani. Ni mwanamke ‘mjane maskini.’ (Luka 21:2) Maisha ni magumu sana kwake; inaelekea si rahisi kwake kupata mahitaji ya msingi ya maisha. Hata hivyo, ameenda kwenye sanduku mojawapo na bila kujionyesha anatumbukiza sarafu mbili ndogo, ambazo labda hata hazitoi sauti zinapotumbukizwa kwenye sanduku. Yesu anajua alichotumbukiza—sarafu mbili za leptoni, ambazo ni sarafu ndogo zaidi zilizotumiwa wakati huo. Hazitoshi hata kununua shore mmoja, ambaye ni miongoni mwa ndege wa bei rahisi zaidi waliouzwa kwa ajili ya chakula.

18. Kũringana na Mariko 12:43, 44, nĩatĩa Jesũ augĩre bwegie mũũthi jwa mwekũrũ ntigwa?

18 Soma Marko 12:43, 44. Yesu anavutiwa sana na mjane huyo. Hivyo, anawaita wanafunzi wake, anawaonyesha mjane huyo, na kusema hivi: “Mjane huyu maskini ametumbukiza zaidi ya wote.” Kisha anafafanua hivi: “Wote [hasa matajiri] walitumbukiza kutokana na ziada yao, lakini yeye, ingawa ni maskini, alitumbukiza kila kitu alichokuwa nacho, riziki yake yote.” Mjane huyo mwaminifu alipotoa pesa zake za mwisho siku hiyo, alikuwa akiyaweka maisha yake mikononi mwa Yehova, Mungu mwenye kujali.—Zab. 26:3.

Kama Yesu, wapongeze wale ambao wanampa Yehova kilicho bora kulingana uwezo wao (Tazama fungu la 19 na 20) *

19. Nĩ ũntũ bũrĩkũ bwa gĩtũmi tũũmba kwiritana kuumania na biugo bia Jesũ biegie mwekũrũ ntigwa?

19 Tumia simulizi hilo katika maisha yako. Jiulize, ‘Ninaweza kujifunza somo gani kutokana na maneno ya Yesu kuhusu mjane maskini?’ Mfikirie mjane huyo. Bila shaka alitamani angeweza kumtolea Yehova zaidi. Hata hivyo, alifanya kile alichoweza; alimpa Yehova kilichokuwa bora kabisa kulingana na uwezo wake. Na Yesu alijua kwamba mchango wake ulikuwa wenye thamani machoni pa Baba yake. Hapa tunajifunza somo muhimu: Yehova anapendezwa tunapompa kilicho bora, yaani, utumishi wetu wa moyo na nafsi yote. (Mt. 22:37; Kol. 3:23) Yehova anafurahi anapoona tunafanya yote tunayoweza! Tunaweza kutumia kanuni hiyo inapohusu kiasi cha muda na nguvu tunazotumia katika ibada yetu, kutia ndani katika huduma na mikutano.

20. Nĩatĩa ũũmba gũtumĩra jarĩa wairitana kuumania na rũgono rwegie mwekũrũ ntigwa? Ejana ngerekano.

20 Unaweza kutumiaje maishani somo ulilojifunza kutokana na simulizi la yule mjane? Jaribu kuwafikiria watu hususa ambao huenda wakahitaji kuhakikishiwa kwamba jitihada zao zinampendeza Yehova. Kwa mfano, je, unamjua dada fulani mwenye umri mkubwa ambaye labda anahisi hatia au kuwa hafai, kwa sababu kwa sasa hana nguvu au afya inayomruhusu kufanya mengi katika huduma kama alivyokuwa akifanya zamani? Au je, unaweza kumfikiria ndugu mwenye ugonjwa wa kudumu unaomsababishia maumivu, ambaye anavunjika moyo kwa sababu hawezi kufika Jumba la Ufalme kwa ajili ya kila mkutano? Wasaidie ndugu na dada kama hao kwa kumwambia maneno ‘mema kwa ajili ya kujenga.’ (Efe. 4:29) Shiriki pamoja nao somo lenye kutia moyo ambalo tumejifunza kutokana na simulizi la mjane maskini. Maneno yako yenye kutia moyo yanaweza kuwahakikishia kwamba Yehova anafurahi tunapomtolea kilicho bora kulingana na uwezo wetu. (Met. 15:23; 1 The. 5:11) Unapowapongeza wengine kwa kumtolea Yehova kilicho bora kulingana na uwezo wao, haidhuru kinaonekana kuwa ni kidogo kadiri gani, unafuata hatua za Yesu kwa ukaribu.

21. Nĩatĩa ũthuurĩte kũthithia?

21 Tunathamini sana kwamba masimulizi ya Injili yanatupatia habari nyingi hususa kuhusu maisha ya Yesu, ambazo zinatusaidia kumwiga, yaani, kufuata hatua zake kwa ukaribu! Kwa nini usianze mradi wa kujifunza vitabu vya Injili kwenye funzo lako la kibinafsi au kwenye Ibada ya Familia? Acheni tukumbuke kwamba ili tunufaike kikamili kutokana na funzo hilo, tunahitaji kuyafanya masimulizi tunayosoma yawe halisi zaidi kwetu na tuyatumie maishani. Zaidi ya kuiga mambo ambayo Yesu alifanya, tunahitaji pia kusikiliza yale aliyosema. Katika makala inayofuata, tutazungumzia mambo tunayoweza kujifunza kutokana na maneno ya mwisho ya Yesu akiwa mwanadamu.

RWĨMBO 15 Msifuni Mzaliwa wa Kwanza wa Yehova!

^ gic. 5 Tukiwa Wakristo wa kweli, tunahitaji ‘kufuata hatua [za Yesu] kwa ukaribu.’ Ni “hatua” gani hizo? Makala hii itajibu swali hilo. Pia, itazungumzia kwa nini tunahitaji kufuata hatua zake kwa ukaribu na jinsi tunavyoweza kufanya hivyo.

^ gic. 60 MAELEZO YA PICHA: Baada ya kutafakari kuhusu mambo ambayo Yesu alisema kuhusu yule mjane maskini, dada fulani anampongeza dada mwenye umri mkubwa kwa utumishi wake wa nafsi yote.