Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 18

Ĩkanĩreni Inya Mĩcemanione ya Kĩũthũrano

Ĩkanĩreni Inya Mĩcemanione ya Kĩũthũrano

“Rekeni tũthũganagĩrie o muntũ na ũngĩ . . . , tũgĩkanagĩra inya.”—AHI. 10:24, 25.

RWĨMBO 88 Nijulishe Njia Zako

MUHTASARI a

1. Nĩkĩ tũritaga macookio mĩcemanione?

 KWA nini tunahudhuria mikutano ya kutaniko? Sababu ya msingi ni ili tumsifu Yehova. (Zab. 26:12; 111:1) Pia, tunahudhuria mikutano ili tutiane moyo katika nyakati hizi ngumu. (1 The. 5:11) Tunapoinua mkono na kutoa maelezo, tunachangia kutimiza mambo hayo mawili.

2. Nĩ twanya tũrĩkũ twĩthagĩrwa natu twa gũcookia mĩcemanione?

2 Kila juma, tuna fursa ya kutoa maelezo katika mikutano yetu. Kwa mfano, mwisho juma tunaweza kushiriki kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi la kutaniko. Kwenye mikutano ya katikati ya juma, tunaweza kutoa maelezo kwenye sehemu ya Hazina za Kiroho, Funzo la Biblia la Kutaniko, na sehemu nyingine za mazungumzo.

3. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ tũmba gũcemania nayo, na nĩatĩa Ahibirania 10:24, 25 yũmba gũtũtethia?

3 Sisi sote tunataka kumsifu Yehova na kuwatia moyo waabudu wenzetu. Lakini tunapotoa maelezo tunaweza kukabili changamoto. Tunaweza kuwa na wasiwasi kuhusu kutoa maelezo, au huenda tukatamani sana kushiriki lakini hatupati fursa za kushiriki mara nyingi kama tunavyotaka. Tunawezaje kukabiliana na changamoto hizo? Tutapata jibu la swali hilo katika barua ambayo mtume Paulo aliwaandikia Waebrania. Alipokuwa akizungumzia umuhimu wa kukutana pamoja alisema kwamba tunapaswa kukazia fikira ‘kutiana moyo.’ (Soma Waebrania 10:24, 25.) Tunapotambua kwamba wahudhuriaji wengine wanaweza kutiwa moyo na hata maneno rahisi yanayoonyesha imani yetu, hilo litapunguza wasiwasi kuhusu kujibu. Na ikiwa hatutachaguliwa mara nyingi kujibu, tunaweza kuwa na furaha kwamba wengine kutanikoni watapata fursa ya kujibu.—1 Pet. 3:8.

4. Nĩ mantũ jarĩkũ jathatũ jakarĩĩrua kĩthoomone gĩkĩ?

4 Katika makala hii, kwanza tutazungumzia jinsi tunavyoweza kutiana moyo katika kutaniko dogo ambalo lina watu wachache wanaotoa maelezo. Kisha, tutachunguza jinsi tunavyoweza kutiana moyo katika kutaniko kubwa ambalo watu wengi huinua mikono ili kutoa maelezo. Mwishowe, tutachunguza jinsi tunavyoweza kuwatia moyo wengine kupitia mambo tunayosema katika maelezo yetu.

ĨKANĨRENI INYA KĨŨTHURANONE GĨKĨNIINI

5. Nĩatĩa tũmba gwĩkanĩra inya rĩrĩa tũrĩ baakai mũcemanione?

5 Katika kutaniko dogo au kikundi, hakuna watu wengi wanaoinua mikono ili kutoa maelezo. Wakati mwingine, huenda yule anayeongoza akasubiri kwa muda mrefu kabla watu hawajainua mikono. Huenda ikaonekana kwamba mkutano unachosha—jambo ambalo halitii moyo. Unaweza kufanya nini? Uwe tayari kuinua mkono mara nyingi zaidi. Unapofanya hivyo, unaweza kuwachochea wengine washiriki mara nyingi zaidi.

6-7. Nĩatĩa tũmba kũthithia tũtĩgakĩre mono gũcookia mĩcemanione?

6 Namna gani ikiwa una wasiwasi wa kutoa maelezo? Watu wengi huhisi hivyo. Hata hivyo, ili uwatie moyo ndugu na dada zako, kwa nini usichunguze mapendekezo ya jinsi ya kupunguza wasiwasi kuhusu kutoa maelezo? Unawezaje kufanya hivyo?

7 Unaweza kuchunguza baadhi ya mapendekezo yaliyochapishwa katika magazeti ya zamani ya Mnara wa Mlinzi. b Kwa mfano, jitayarishe vizuri. (Met. 21:5) Kadiri unavyofahamu vizuri zaidi habari inayozungumziwa, ndivyo itakavyokuwa rahisi kwako kutoa maelezo. Pia, toa maelezo mafupi. (Met. 15:23; 17:27) Jibu fupi litakupunguzia wasiwasi. Jibu fupi, labda ambalo lina sentensi moja au mbili, linaweza kuwa rahisi zaidi kwa ndugu na dada zako kuelewa kuliko maelezo marefu yenye mawazo mengi. Unapotoa maelezo mafupi kwa maneno yako mwenyewe, utaonyesha kwamba umejitayarisha vizuri na kwamba unaelewa vizuri habari inayozungumziwa.

8. Nĩatĩa Jehova onaga gũciumia gwetũ?

8 Namna gani ikiwa utajaribu kutumia baadhi ya mapendekezo hayo, lakini bado uwe na wasiwasi kuhusu kutoa maelezo zaidi ya mara moja au mbili? Uwe na uhakika kwamba Yehova atathamini jitihada zako za kutoka moyoni za kufanya kile unachoweza. (Luka 21:1-4) Kutoa kilicho bora hakumaanishi kufanya jambo linalozidi uwezo wako. (Flp. 4:5) Amua jambo unaloweza kufanya, weka lengo la kulifanya, na usali ili uwe na moyo mtulivu. Mwanzoni, huenda lengo hilo likawa kutoa maelezo mafupi mara moja.

ĨKANĨRENI INYA KĨŨTHŨRANONE GĨKĨNENE

9. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ jomba kuumĩra biũthũranone bibinene?

9 Ikiwa kutaniko lenu lina wahubiri wengi, huenda ukakabili changamoto tofauti. Labda ndugu na dada wengi huinua mikono hivi kwamba mara nyingi hupati nafasi ya kutoa maelezo. Kwa mfano, sikuzote Danielle anafurahia kutoa maelezo kutanikoni. c Anaona kufanya hivyo kuwa sehemu ya ibada yake, njia ya kuwatia moyo wengine, na njia ya kukazia kweli za Biblia katika akili yake mwenyewe. Lakini alipohamia katika kutaniko kubwa, hakupata nafasi nyingi za kutoa maelezo—wakati mwingine hakuchaguliwa hata mara moja katika mkutano wote. Alisema hivi: “Nilivunjika moyo. Nilihisi ni kana kwamba nimekosa pendeleo. Hali hiyo inapotokea tena na tena, huenda ukafikiri jambo hilo linafanywa kimakusudi.”

10. Nĩatĩa tũmba kũthithia nĩkenda twĩthĩrwa na twanya tũtwingĩ twa gũcookia?

10 Je, umewahi kuhisi kama Danielle? Ikiwa ndivyo, huenda ukashawishiwa kutoinua mkono tena na badala yake, kusikiliza tu mkutano. Lakini usiache kujitahidi kutoa maelezo. Unaweza kufanya nini? Huenda ukaona inafaa kutayarisha maelezo kadhaa kwa kila mkutano. Kisha ikiwa hutachaguliwa kutoa maelezo mwanzoni mwa funzo, bado utakuwa na nafasi nyingine ya kutoa maelezo mkutano unapoendelea. Unapotayarisha Funzo la Mnara wa Mlinzi, fikiria jinsi kila fungu linavyohusiana na kichwa kikuu cha makala. Ukifanya hivyo, inaelekea kwamba utakuwa tayari kutoa maelezo wakati wowote wa funzo. Isitoshe, unaweza kujitayarisha kutoa maelezo katika mafungu ambayo yanazungumzia mafundisho mazito ya Biblia ambayo ni vigumu zaidi kuyaelezea. (1 Kor. 2:10) Kwa nini? Kwa sababu huenda si watu wengi watainua mkono katika sehemu hiyo. Namna gani ikiwa licha ya kutumia mapendekezo hayo, unatambua kwamba baada ya mikutano kadhaa bado hujapata nafasi ya kutoa maelezo? Kabla ya mkutano, unaweza kuzungumza na yule anayeongoza na kumwambia swali ambalo ungependa kujibu.

11. Nĩatĩa Afilipi 2:4 ĩgũtwĩkĩra inya kũthithia?

11 Soma Wafilipi 2:4. Akiongozwa na roho, mtume Paulo aliwatia moyo Wakristo waangalie faida za wengine. Tunaweza kutumiaje shauri hilo kwenye mikutano? Kwa kukumbuka kwamba kama sisi, wengine pia wanataka kutoka maelezo.

Kama vile unavyowaruhusu wengine washiriki katika mazungumzo, waruhusu wengine watoe maelezo kwenye mkutano (Tazama fungu la 12)

12. Njĩra ĩrĩa njega nĩ ĩrĩkũ ya gwĩkĩra bangĩ inya micemanione? (Tega kinya mbica.))

12 Fikiria jambo hili. Unapokuwa na mazungumzo pamoja na rafiki zako, je, unazungumza sana hivi kwamba wanakosa nafasi ya kuzungumza? La hasha! Unataka washiriki katika mazungumzo. Vivyo hivyo, kwenye mikutano, tungependa kuwapa wengi iwezekanavyo fursa ya kutoa maelezo. Kwa kweli, mojawapo ya njia bora zaidi ya kuwatia moyo ndugu na dada zetu, ni kuwapa nafasi ya kueleza imani yao. (1 Kor. 10:24) Acheni tuchunguze jinsi tunavyoweza kufanya hivyo.

13. Nĩatĩa tũmba kwaa babaingĩ nkũrũki kaanya ka gũcookia mĩcemanione?

13 Jambo moja tunaloweza kufanya ni kutoa maelezo mafupi, na hivyo kuwapa watu wengi zaidi muda wa kushiriki. Wazee na wahubiri wengine wenye uzoefu wanaweza kuweka mfano. Hata unapotoa maelezo mafupi, epuka kuzungumzia mambo mengi sana. Ukizungumzia kila jambo linalotajwa kwenye fungu, wengine watakosa jambo la kusema. Kwa mfano, katika fungu hili kuna mapendekezo mawili ambayo yametolewa—toa maelezo mafupi na uepuke kuzungumzia mambo mengi sana. Ikiwa utachaguliwa kwanza kutoa maelezo katika fungu hili, kwa nini usizungumzie jambo moja tu kati ya hayo?

Ni wakati gani ambao huenda tukaamua hatutainua mkono kwenye mkutano? (Tazama fungu la 14) f

14. Nĩmbi biũmba gũtũtethia kũthuura maita jarĩa tũgokĩĩria njara cietũ nĩkenda tũcookia? (Tega kinya mbica.)

14 Tumia utambuzi unapoamua mara ambazo utanyoosha mkono ili kutoa maelezo. Ikiwa tutainua mkono mara nyingi sana, huenda tukamfanya yule anayeongoza ahisi kwamba analazimika kutuchagua tena na tena hata ingawa wengine bado hawajapata nafasi. Hilo linaweza kuwafanya wengine wasiinue mkono.—Mhu. 3:7.

15. (a) Nĩatĩa tũbuĩrĩte kũthithia kethĩra tũtĩraewa kaanya ka gũcookia? (b) Nĩatĩa barĩa bagũtongeria bomba kũthũgaanĩria bonthe kĩũthũranone? (Tega kathandũkũ “ Kethĩra Nĩgwe Ũgũtongeria..”)

15 Ikiwa wahubiri wengi wanainua mkono wakati wa funzo, huenda tusitoe maelezo mara nyingi kama tunavyopenda. Wakati mwingine, huenda yule anayeongoza asituchague. Hilo linaweza kutuvunja moyo, lakini hatupaswi kukasirika tunapokosa kuchaguliwa.—Mhu. 7:9.

16. Nĩatĩa tũmba gwĩkĩra inya barĩa bacookia?

16 Ikiwa huwezi kutoa maelezo mara nyingi kama unavyopenda, kwa nini usiwasikilize wengine kwa makini wanaposhiriki kisha baada ya mkutano uwapongeze kwa maelezo yao? Huenda ndugu na dada zako wakatiwa moyo unapowapongeza kama vile ambavyo wangetiwa moyo ikiwa ungetoa maelezo. (Met. 10:21) Kuwapongeza wengine ni njia nyingine ambayo tunaweza kutiana moyo.

NJĨRA INGĨ CIA GWĨKANĨRA INYA

17. (a) Nĩatĩa aciari bomba gũtethia aana baao kũthuranĩra macookio jakwagĩra? (b) Kũringana na vidio, matagaaria jana ja kũthuranĩra macookio nĩ jarĩkũ? (Tega kinya nteto au gaiti.)

17 Ni njia gani nyingine ambazo tunaweza kutiana moyo katika mikutano yetu? Ikiwa wewe ni mzazi, wasaidie watoto wako watayarishe maelezo yanayolingana na umri wao. (Mt. 21:16) Nyakati nyingine, mambo mazito kama vile matatizo ya ndoa au masuala ya kiadili, huzungumziwa wakati wa funzo, lakini huenda kuna fungu moja au mawili ambayo mtoto anaweza kutoa maelezo. Pia, wasaidie watoto wako waelewe kwa nini huenda hawatachaguliwa kila mara wanapoinua mkono. Kufafanua jambo hilo kunaweza kuwasaidia wasivunjike moyo watu wengine wanapochaguliwa.—1 Tim. 6:18. d

18. Nĩatĩa tũmba kweba mantũ ja gwicwĩra ũkumio rĩrĩa tũgũcookia? (Njuno 27:2)

18 Sisi sote tunaweza kutayarisha maelezo yenye kujenga ambayo yatamletea Yehova heshima na kuwatia moyo Wakristo wenzetu. (Met.  25:11) Ingawa wakati mwingine tunaweza kutoa maelezo mafupi ya mambo tuliyojionea, tunapaswa kuepuka kuzungumza sana kujihusu. (Soma Methali 27:2; 2 Kor. 10:18) Badala yake, tunajitahidi kumkazia fikira Yehova, Neno lake, na watu wake kwa ujumla. (Ufu. 4:11) Hata hivyo, ikiwa swali kwenye fungu fulani linahusu kutoa maelezo ya kibinafsi, inafaa kufanya hivyo. Mfano wa swali hilo unapatikana kwenye fungu linalofuata kwenye makala hii.

19. (a) Gũkethĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ twathũgaanĩria bonthe barĩa barĩ mĩcemanione? (Aroma 1:11, 12) (b) Nĩmbi nabwaku ũgwĩragĩrua bwegie gũcookia mĩcemanione?

19 Ingawa hakuna sheria kali kuhusu jinsi ya kutoa maelezo, sisi sote tunaweza kujitahidi kutoa maelezo yenye kutia moyo. Huenda hilo likamaanisha kutoa maelezo mara nyingi zaidi. Au huenda likamaanisha kuridhika na nafasi tulizopata za kutoa maelezo, na kufurahi kwamba wengine wanapata nafasi ya kutoa maelezo. Tukikazia fikira faida za wengine kwenye mikutano ya kutaniko, sisi sote tutafurahia ‘kutiana moyo.’—Soma Waroma 1:11, 12.

RWĨMBO 93 Bariki Kukutana Kwetu

a Tunatiana moyo tunapotoa maelezo kwenye mikutano. Hata hivyo, wengine hupatwa na wasiwasi wanapotaka kutoa maelezo. Wengine hufurahia kutoa maelezo lakini wanatamani kujibu mara nyingi zaidi. Katika hali hizo mbili, tunawezaje kuonyeshana ufikirio ili sote tuhisi tumetiwa moyo? Na tunawezaje kutoa maelezo yanayowachochea ndugu na dada zetu katika upendo na matendo mazuri? Makala hii itaeleza.

b Ili kupata mapendekezo zaidi, chunguza gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 2019, uku. 8-13, na Septemba 1, 2003, uku. 19-22.

c Jina limebadilishwa.

d Tazama video kwenye jw.org Uwe Rafiki ya Yehova—Jitayarishe Kutoa Maelezo.

e Tazama gazeti Mnara wa Mlinzi la Julai 15, 2013, uku. 32, na la Septemba 1, 2003, uku. 21-22.

f MAELEZO YA PICHA: Katika kutaniko kubwa, ndugu ambaye tayari ametoa maelezo anawapatia wengine nafasi ya kushiriki kwenye mikutano.