Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 17

Jehova Agagũtethia Kũũmbana na Mantũ Jatĩrĩgĩĩri Ũtũũrone

Jehova Agagũtethia Kũũmbana na Mantũ Jatĩrĩgĩĩri Ũtũũrone

“Mithangiko ni imiingi iria itirimaga uria wagirite; indi mwathani namutunyukagia akamurita kiriyo yonthe.”—ZAB. 34:19.

RWĨMBO 44 Sala ya Mtu wa Hali ya Chini

MUHTASARI a

1. Nĩ ũmma bũrĩkũ tũrĩ nabu?

 TUKIWA watu wa Yehova, tunajua kwamba anatupenda na anataka tufurahie maisha bora kabisa. (Rom. 8:35-39) Pia, tunasadiki kwamba sikuzote tunanufaika tunapofuata kanuni za Biblia. (Isa. 48:17, 18) Hata hivyo, namna gani ikiwa tutakabili changamoto tusizotarajia?

2. Kwombĩka tũgacemania na mathĩĩna jarĩkũ, na jomba gũtũma tũgaciũria biũria birĩkũ?

2 Watumishi wote wa Yehova hukabili matatizo. Kwa mfano, huenda mtu wa familia akatuvunja moyo kwa njia fulani. Huenda tukakabili matatizo makubwa ya kiafya yanayotuzuia kufanya mengi katika utumishi wa Yehova. Huenda tukakabiliana na madhara yanayosababishwa na janga la asili. Au huenda tukateswa kwa sababu ya imani yetu. Tunapokabili majaribu kama hayo, tunaweza kujiuliza: ‘Kwa nini ninapatwa na jambo hili? Je, nimefanya kosa fulani? Je, jambo hili linamaanisha kwamba Yehova hanibariki?’ Je, umewahi kuhisi hivyo? Ikiwa ndivyo, usife moyo. Watumishi wengi washikamanifu wa Yehova wamepambana na hisia kama hizo.—Zab. 22:1, 2; Hab. 1:2, 3.

3. Nĩmbi tũmba kwiritana kuũmania na Zaburi 34:19?

3 Soma Zaburi 34:19. Ona mambo mawili muhimu katika Zaburi hiyo: (1) Watu waadilifu hukabili matatizo. (2) Yehova hutukomboa kutoka katika majaribu yetu. Yehova hutukomboa jinsi gani? Njia moja ni kwa kutusaidia kuona mambo kihalisi kwenye mfumo huu wa mambo. Ingawa Yehova anatuahidi kwamba tutapata shangwe tunapomtumikia, hajatuhakikishia kwamba hatutapatwa na matatizo sasa. (Isa. 66:14) Anatuhimiza tukazie fikira wakati ujao—wakati ambapo tutaishi maisha anayotaka tufurahie milele. (2 Kor. 4:16-18) Kwa sasa, anatusaidia kuendelea kumtumikia kila siku.—Omb. 3:22-24.

4. Nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

4 Acheni tuzungumzie mambo ambayo tunaweza kujifunza kutokana na mifano ya waabudu waaminifu wa Yehova wanaotajwa katika Biblia na wa nyakati zetu. Kama tutakavyoona, huenda tukakabili matatizo tusiyotarajia. Lakini tunapomtegemea Yehova, atatutegemeza sikuzote. (Zab. 55:22) Tunapochunguza mifano hiyo, jiulize hivi: ‘Mimi ningetendaje ikiwa ningekabili hali hiyo? Mifano hiyo inanisaidiaje kumtumaini Yehova hata zaidi? Ni masomo gani ninayoweza kutumia maishani mwangu?’

NGEREKANO KUUMA KĨRĨ BIBIRIA

Kwa miaka 20, Yehova alimbariki Yakobo alipomfanyia kazi kwa bidii Labani, mjomba wake aliyekuwa mdanganyifu (Tazama fungu la 5)

5. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ Jakubu aakũrũkĩrĩre kuumania na Labani? Tega mbica karatacine ka mbere.)

5 Watumishi wa Yehova wanaotajwa katika Biblia walikabili changamoto ambazo hawakutarajia. Mfikirie Yakobo. Baba yake alimwambia achukue mke kutoka kwa binti za Labani, mtu wao wa ukoo aliyemwabudu Yehova, na akamhakikishia kwamba Yehova angembariki sana. (Mwa. 28:1-4) Basi, Yakobo akafanya jambo linalofaa. Aliondoka nchi ya Kanaani na kusafiri kwenda nyumbani kwa Labani, ambaye alikuwa na mabinti wawili—Lea na Raheli. Yakobo alimpenda Raheli, binti mdogo wa Labani, na akakubali kumfanyia baba yake kazi kwa miaka saba kabla ya kumwoa Raheli. (Mwa. 29:18) Lakini mambo hayakwenda kama Yakobo alivyotarajia. Labani alimdanganya Yakobo na akamwoa Lea, binti yake mkubwa. Baada ya juma moja, Labani alimruhusu Yakobo amwoe Raheli, lakini ikiwa tu angefanya kazi kwa miaka mingine saba. (Mwa. 29:25-27) Pia, Labani alimtendea Yakobo isivyo haki katika makubaliano ya kazi. Kwa ujumla, Labani alimtendea Yakobo isivyo haki kwa miaka 20!—Mwa. 31:41, 42.

6. Nĩ mathĩĩna jangĩ jarĩkũ Jakubu oomĩrĩrie?

6 Yakobo alikabili matatizo mengine. Alikuwa na familia kubwa, lakini wanawe hawakuishi kwa amani kati yao. Hata walimuuza ndugu yao Yosefu utumwani. Wana wawili ya Yakobo, Simoni na Lawi, waliletea familia yao aibu, na kuliletea suto jina la Yehova. Isitoshe, Raheli, mke mpendwa wa Yakobo, alikufa alipokuwa akijifungua mtoto wao wa pili. Na kwa sababu ya njaa kali, Yakobo alilazimika kuhamia nchini Misri alipokuwa amezeeka.—Mwa. 34:30; 35:16-19; 37:28; 45:9-11, 28.

7. Nĩatĩa Jehova oonerie Jakubu atĩ naarĩ na wendeeri Bwawe?

7 Licha ya matatizo hayo yote, Yakobo hakupoteza imani yake katika Yehova na katika ahadi Zake. Naye Yehova, akamwonyesha Yakobo kwamba alikuwa na kibali chake. Kwa mfano, licha ya udanganyifu wa Labani, Yehova alimbariki Yakobo kwa kumpa mali nyingi. Na wazia jinsi Yakobo alivyomshukuru Yehova alipoungana tena na mwanaye Yosefu—mwana ambaye alidhani alikufa muda mrefu uliopita! Urafiki wa karibu kati ya Yakobo na Yehova, ulimsaidia kukabiliana na majaribu yake kwa mafanikio. (Mwa. 30:43; 32:9, 10; 46:28-30) Ikiwa tutadumisha urafiki wa karibu pamoja na Yehova, sisi pia tunaweza kukabiliana kwa mafanikio na majaribu tusiyotarajia.

8. Mũnene Daudi eerĩgĩrĩĩte kũthithia atĩa?

8 Mfalme Daudi hakuweza kutimiza kila jambo alilotarajia kufanya katika utumishi wa Yehova. Kwa mfano, Daudi alitamani sana kumjengea Mungu hekalu. Alimtajia nabii Nathani tamaa yake. Nathani akamjibu hivi: “Fanya jambo lolote lililo moyoni mwako, kwa sababu Mungu wa kweli yuko pamoja nawe.” (1 Nya. 17:1, 2) Tunaweza kuwazia jinsi maneno hayo yalivyomtia moyo Daudi. Huenda mara moja alianza kufanya mipango ya mradi huo mkubwa.

9. Nĩatĩa Daudi aathithĩrie arĩkwigua nteto cia kũmuuna nkoro?

9 Hata hivyo, baada ya muda mfupi, nabii wa Yehova alirudi na habari zenye kuvunja moyo. “Usiku huohuo” Yehova alimwambia Nathani kwamba Daudi hangejenga hekalu hilo, badala yake, lingejengwa na mmoja kati ya wanawe. (1 Nya. 17:3, 4, 11, 12) Daudi alitendaje alipopokea ujumbe huo? Alibadili lengo lake. Alikazia fikira kukusanya pesa na vifaa ambavyo mwanaye, Sulemani, angehitaji kwa ajili ya mradi huo.—1 Nya. 29:1-5.

10. Nĩatĩa Jehova aatharimĩre Daudi?

10 Mara tu baada ya kumjulisha Daudi kwamba si yeye ambaye angejenga hekalu, Yehova alifanya agano pamoja naye. Yehova alimwahidi Daudi kwamba mmoja wa wazao wake angetawala milele. (2 Sam. 7:16) Katika ulimwengu mpya, wazia jinsi Daudi atakavyofurahi kujua kwamba anafurahia maisha chini ya Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Yesu, Mfalme aliyetokana na familia yake! Simulizi hili linatusaidia kuona kwamba hata ikiwa hatuwezi kutimiza yote tuliyotarajia kufanya katika utumishi wa Yehova, huenda Mungu wetu akatubariki kwa njia nyingine ambazo hatungetarajia kamwe.

11. Akristũ ba karine ya mbere baatharimĩrwe atĩa kinya kethĩra Ũnene bũteejĩre ĩgiita rĩrĩa beerĩgĩrĩĩte? (Mathithio 6:7)

11 Wakristo wa karne ya kwanza walikabiliana na changamoto zisizotarajiwa. Kwa mfano, walitazamia kwa hamu Ufalme wa Mungu uje, lakini hawakujua wakati ambapo ungefika. (Mdo. 1:6, 7) Basi, walifanya nini? Waliendelea kuhubiri kwa bidii. Habari njema ilipoendelea kuenea, waliona jinsi Yehova alivyokuwa akibariki jitihada zao.—Soma Matendo 6:7.

12. Nĩatĩa Akristũ ba karine ya mbere baathithĩrie rĩrĩa kwagĩĩre mpara?

12 Pindi fulani, njaa kubwa ilitokea “juu ya dunia yote inayokaliwa.” (Mdo. 11:28) Wakristo wa karne ya kwanza waliathiriwa pia. Je, unaweza kuwazia jinsi njaa hiyo kubwa ilivyowaathiri? Bila shaka, vichwa vya familia walihangaika kuhusu jinsi ambavyo wangeziandalia chakula familia zao. Namna gani vijana ambao walikuwa na malengo ya kupanua huduma yao? Je, huenda walifikiri kwamba walipaswa kuahirisha malengo yao? Licha ya hali zao, Wakristo hao walibadilikana kulingana na hali. Waliendelea kuhubiri kwa njia yoyote waliyoweza na wakashiriki kwa furaha vitu vyao vya kimwili pamoja na waabudu wenzao huko Yudea.—Mdo. 11:29, 30.

13. Nĩ itharimo birĩkũ Akristũ bau boonere ĩgiita rĩu rĩa mpara?

13 Wakristo walipata baraka gani wakati wa njaa hiyo? Wale waliopokea msaada waliona jinsi Yehova alivyowasaidia moja kwa moja. (Mt. 6:31-33) Bila shaka, walihisi wakiwa karibu zaidi na waabudu wenzao ambao waliwasaidia. Na wale waliotoa michango au kushiriki kwa njia nyingine katika kazi ya kutoa msaada, walipata furaha inayotokana na kutoa. (Mdo. 20:35) Yehova aliwabariki wote walipobadilikana kulingana na hali.

14. Gwakarĩkĩre atĩa kĩrĩ Baranaba na mũtũmwa Paũlũ, na maumĩra jaarĩ jarĩkũ? (Mathithio 14:21, 22)

14 Wakristo wa karne ya kwanza waliteswa mara nyingi, pindi nyingine huenda wakati ambao hawakutarajia. Fikiria jambo lililompata Barnaba na mtume Paulo walipokuwa wakihubiri katika eneo la Listra. Mwanzoni, walikaribishwa kwa uchangamfu na watu waliowasikiliza. Lakini baadaye, wapinzani “wakaushawishi umati,” na baadhi ya watu haohao wakampiga mawe Paulo na kumwacha wakiwazia kwamba amekufa. (Mdo. 14:19) Lakini Barnaba na Paulo waliendelea kuhubiri sehemu nyingine. Matokeo yalikuwaje? Waliwafanya “watu wengi kuwa wanafunzi,” na maneno na mfano wao uliwaimarisha waabudu wenzao. (Soma Matendo 14:21, 22.) Watu wengi walinufaika kwa sababu Barnaba na Paulo hawakuvunjika moyo hata walipokabili mateso yasiyotarajiwa. Ikiwa hatutavunjika moyo katika kazi ambayo Yehova ametupatia, sisi pia tutabarikiwa.

NTUKŨNE CIETŨ

15. Nĩmbi ũkwiritana kuumania na ngerekano ya Mũtana wa Baaba A. H. Macmillan?

15 Katika miaka iliyotangulia mwaka wa 1914, watu wa Yehova walikuwa na matarajio makubwa. Kwa mfano, mfikirie Ndugu A. H. Macmillan. Kama wengi wakati huo, Ndugu Macmillan alifikiri kwamba angeenda mbinguni baada ya muda mfupi. Katika hotuba aliyotoa Septemba, 1914, alisema hivi: “Inawezekana kwamba hii ndiyo hotuba yangu ya mwisho ya watu wote ambayo nitatoa.” Bila shaka, hiyo haikuwa hotuba yake ya mwisho. Baadaye Ndugu Macmillan aliandika hivi: “Labda baadhi yetu tulifikiri haraka-haraka kwamba tungeenda mbinguni mara moja.” Aliongezea hivi: “Jambo tunalopaswa kufanya ni kuendelea kuwa na bidii katika utumishi wa Bwana.” Ndugu Macmillian aliendelea kuwa na bidii. Alikuwa na bidii katika huduma. Alipata pendeleo la kuwatia moyo ndugu wengi waliokuwa wamefungwa gerezani kwa sababu ya kutounga mkono upande wowote. Na aliendelea kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa uaminifu hata alipozeeka. Ndugu Macmillian alinufaikaje kwa kutumia wakati wake vizuri alipokuwa akisubiri thawabu yake? Muda mfupi kabla ya kifo chake mwaka wa 1966, aliandika hivi: “Imani yangu ni yenye nguvu leo, kama ambavyo imekuwa sikuzote.” Huo ni mtazamo mzuri sana ambao sote tunapaswa kuiga—hasa ikiwa tumekuwa tukivumilia kwa muda mrefu kuliko tulivyotarajia!—Ebr. 13:7.

16. Nĩ ũntũ bũrĩkũ bũtĩĩrĩgĩĩri bwagwatĩre Herbert Jennings na mwekũrũ waawe? (Jakubu 4:14)

16 Wengi kati ya watumishi wa Yehova wanapambana na matatizo ya afya yasiyotarajiwa. Kwa mfano, katika simulizi lake la maisha, Ndugu Herbert Jennings b alieleza jinsi yeye na mke wake walivyofurahia mgawo wao wa umishonari huku Ghana. Hata hivyo, baada ya muda, alipatikana na ugonjwa mbaya sana wa kihisia. Kwa kutegemea andiko la Yakobo 4:14, Ndugu Jennings alisema hali hiyo ilikuwa “‘kesho’ ambayo hatukutarajia.” (Soma.) Aliandika hivi: “Ilibidi tuone mambo kihalisi, tukafanya mpango wa kuondoka nchini Ghana na kuacha marafiki wetu wengi wa karibu, tukarudi nchini Kanada [kwa ajili ya matibabu].” Yehova alimsaidia Ndugu Jennings na mke wake waendelee kumtumikia kwa uaminifu licha ya changamoto walizokuwa wakikabili.

17. Nĩatĩa ngerekano ya Mũtana wa Baaba Jennings ĩgunĩte Akristũ bangĩ?

17 Maelezo ya unyoofu ya Ndugu Jennings katika simulizi lake la maisha, yamewasaidia sana watu wengine. Dada mmoja aliandika hivi: “Sijawahi kuchochewa kama nilivyochochewa niliposoma makala hiyo. . . . Kusoma jinsi Ndugu Jennings alivyolazimika kuacha mgawo ili kushugulikia ugonjwa wake kulinisaidia kuona hali yangu kwa njia yenye usawaziko.” Vivyo hivyo, ndugu mwingine aliandika hivi: “Baada ya kutumikia nikiwa mzee wa kutaniko kwa miaka kumi, nililazimika kuacha pendeleo hilo kwa sababu ya ugonjwa wa kiakili. Nililemewa sana na hisia za kushindwa hivi kwamba nilivunjika moyo niliposoma makala za masimulizi ya maisha. . . . Lakini uvumilivu wa Ndugu Jennings ulinitia moyo.” Hilo linatukumbusha kwamba tunapovumilia matatizo yasiyotarajiwa, hilo linaweza kuwatia moyo wengine. Hata mambo yasipoenda kama tulivyotarajia maishani, bado tunaweza kuwa mfano mzuri wa imani na uvumilivu.—1 Pet. 5:9.

Ikiwa tutamtegemea Yehova tunapopatwa na matatizo tusiyotarajia, hilo litatusaidia kumkaribia hata zaidi (Tazama fungu la 18)

18. O ta ũrĩa kwonanĩtue mbicene, nĩmbi ũkwiritana kuumania na ngerekano ya mwekũrũ ntigwa kuuma Nigeria?

18 Watumishi wengi wa Yehova wameathiriwa na majanga kama vile janga la COVID-19. Kwa mfano, mjane mmoja nchini Nigeria alikuwa na kiasi kidogo sana cha pesa na chakula. Asubuhi moja, binti yake alimuuliza wangekula nini baada ya kupika kikombe chao cha mwisho cha mchele. Dada yetu alimwambia binti yake kwamba hawakuwa na pesa au chakula kingine lakini wanapaswa kumwiga mjane wa Sarefathi—kwa kutayarisha chakula chao cha mwisho na kumtumaini Yehova kabisa. (1 Fal. 17:8-16) Hata kabla hawajaanza kufikiria kuhusu chakula chao cha mchana siku hiyo, walipokea kifurushi cha msaada kutoka kwa waabudu wenzao. Kifurushi hicho kilikuwa na chakula ambacho kingewatosha kwa zaidi ya majuma mawili. Dada huyo alisema kwamba hakutambua jinsi ambavyo Yehova alikuwa akisikiliza kwa makini mambo aliyomwambia binti yake. Kwa kweli, ikiwa tutamtegemea Yehova tunapopatwa na matatizo tusiyotarajia, hilo litatusaidia kumkaribia hata zaidi.—1 Pet. 5:6, 7.

19. Nĩ mĩthangĩko ĩrĩkũ Aleksey Yershov oomĩrĩĩrie?

19 Katika miaka ya hivi karibuni, wengi kati ya ndugu na dada zetu wamevumilia mateso ambayo hawakutarajia. Fikiria mfano wa Ndugu Aleksey Yershov, anayeishi nchini Urusi. Watu wa Yehova walifurahia uhuru wa kadiri fulani Ndugu Yershov alipobatizwa mwaka wa 1994. Hata hivyo, baada ya miaka kupita hali ilibadilika nchi Urusi. Mwaka wa 2020, askari walivamia nyumba ya Ndugu Yershov na kufanya msako, na mali zake nyingi zikachukuliwa. Miezi kadhaa baadaye, serikali ilimfungulia mashtaka ya uhalifu. Jambo baya hata zaidi, mashtaka hayo yalitegemea rekodi za video zilizotengenezwa na mtu ambaye kwa zaidi ya mwaka mmoja alijifanya anapendezwa na kujifunza Biblia. Huo ulikuwa usaliti mkubwa!

20. Nĩatĩa Mũtana wa Baaba Yershov eekĩĩre inya ngwatanĩro yaawe amwe na Jehova?

20 Je, mateso ya Ndugu Yershov yamekuwa na matokeo mazuri? Ndiyo. Uhusiano wake na Yehova umeimarika zaidi. Anasema hivi: “Mimi na mke wangu tunasali pamoja mara nyingi zaidi. Ninatambua kwamba singeweza kuvumilia hali hii bila msaada wa Yehova.” Anaongezea hivi: “Funzo la kibinafsi linanisaidia kukabiliana na hali zinazonivunja moyo. Mimi hutafakari mifano ya watumishi waaminifu walioishi zamani. Kuna masimulizi mengi yaliyoandikwa katika Biblia ambayo yanaonyesha umuhimu wa kuendelea kuwa mtulivu na kumtumaini Yehova.”

21. Nĩmbi twairitana kĩthoomone gĩkĩ?

21 Tumejifunza nini katika makala hii? Wakati mwingine tunakabili matatizo tusiyotarajia katika ulimwengu huu. Ingawa hivyo, sikuzote Yehova huwasaidia watumishi wake wanapomtegemea. Kama andiko letu la msingi linavyosema, “mwadilifu ana matatizo mengi, lakini Yehova humwokoa kutoka katika matatizo hayo yote.” (Zab. 34:19) Na tuendelee kukazia fikira, si matatizo tunayopata, bali nguvu ambazo Yehova anatupatia. Kisha kama mtume Paulo, tutaweza kusema: “Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yule anayenipa nguvu.”—Flp. 4:13.

RWĨMBO 38 Atakupa Nguvu

a Ingawa tunaweza kukabili changamoto tusizotarajia katika mfumo huu, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atawategemeza waabudu wake waaminifu. Yehova aliwasaidiaje watumishi wake wakati uliopita? Anatusaidiaje leo? Kuchunguza mifano ya watu wanaotajwa katika Biblia na mifano ya nyakati zetu, kutaimarisha usadikisho wetu kwamba ikiwa tutamtegemea Yehova, atatusaidia pia.