Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 16

‘Mutana wa Nyakwe Akariuka’!

‘Mutana wa Nyakwe Akariuka’!

‘Jesu areera [Martha]: ‘Mutana wa nyakwe akariuka.’’—JOHANA 11:23.

RWĨMBO 151 Ataita

MUHTASARI a

1. Mũtana ũmwe ũmũniini atarĩĩrie atĩa wĩrĩgĩĩro bwawe bwegiĩ kũriũkua?

 MVULANA anayeitwa Matthew ana ugonjwa mbaya sana na amelazimika kufanyiwa upasuaji mara nyingi. Alipokuwa na umri wa miaka saba, yeye na familia yake walikuwa wakitazama programu ya kila mwezi kwenye JW Broadcasting®. Karibu na mwisho wa programu hiyo, waliona video ya muziki kuhusu kukaribisha wapendwa wetu wakati wa ufufuo. b Baada ya programu hiyo, Matthew alienda kuwashika wazazi wake mkono na akawaambia hivi: “Mama na Baba mmeona? Hata nikifa, nitafufuliwa. Mnaweza kunisubiri, mambo yatakuwa sawa.” Je, unaweza kuwazia jinsi wazazi hao walivyohisi walipotambua kwamba tumaini la ufufuo ni halisi sana kwa mtoto wao?

2-3. Nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi kũthũgaanĩria wĩrane bwa kũriũkua?

2 Mara kwa mara, ni vizuri sisi sote tutafakari ahadi ya Biblia kuhusu ufufuo wa wakati ujao. (Yoh. 5:28, 29) Kwa nini? Kwa sababu hatujui wakati ambapo huenda tukakabili ugonjwa unaohatarisha uhai au kufiwa na mtu tunayempenda. (Mhu. 9:11; Yak. 4:13, 14) Tumaini letu la ufufuo linaweza kutusaidia kuvumilia changamoto kama hizo. (1 The. 4:13) Maandiko yanatuhakikishia kwamba Baba yetu wa mbinguni anatujua vizuri na anatupenda sana. (Luka 12:7) Yehova Mungu anatujua vizuri sana hivi kwamba anaweza kutufufua tukiwa na utu na kumbukumbu zilezile. Yehova anatupenda sana hivi kwamba ametupatia nafasi ya kuishi milele, hata ikiwa itamaanisha kutufufua!

3 Katika makala hii, kwanza tutazungumzia kwa nini tunaweza kuamini ahadi ya ufufuo. Kisha tutachunguza simulizi la Biblia linaloimarisha imani, ambalo lina maneno ya andiko letu la msingi: “Ndugu yako atafufuka.” (Yoh. 11:23) Mwishowe, tutajifunza jinsi tunavyoweza kufanya tumaini la ufufuo liwe halisi zaidi kwetu.

NĨKĨ TŨMBA GWĨTĨKIA WĨRĨGĨĨRO BWA KŨRIŨKUA

4. Nĩkenda twĩtĩkia wĩrane bũnna, tũbuĩrĩte kwĩthĩrwa na ũrikithia bũrĩkũ? Ejana ngerekano.

4 Ili tuamini ahadi, ni lazima tusadiki kwamba yule anayetoa ahadi hiyo anatamani na ana nguvu, au uwezo, wa kuitimiza. Wazia kwamba nyumba yako imeharibiwa sana na dhoruba. Rafiki yako anakuja na kukuahidi, ‘Nitakusaidia kurekebisha nyumba yako.’ Ni mnyoofu na unasadiki kwamba anatamani kukusaidia. Ikiwa yeye ni mjenzi mwenye ustadi na ana vifaa vinavyohitajika, unajua kwamba pia ana uwezo wa kukusaidia. Basi unaamini ahadi yake. Namna gani kuhusu ahadi ya Mungu ya ufufuo? Je, kweli anatamani na ana nguvu za kuitimiza?

5-6. Nĩkĩ tũmba kwĩthĩrwa na ũmma atĩ Jehova arĩna wirirĩĩria bwa kũriũkia akuũ?

5 Je, Yehova anatamani kuwafufua wafu? Bila shaka, anatamani kuwafufua. Aliwaongoza baadhi ya waandikaji wa Biblia kuandika kuhusu ahadi ya ufufuo wa wakati ujao. (Isa. 26:19; Hos. 13:14; Ufu. 20:11-13) Na Yehova anapotoa ahadi sikuzote yeye huitimiza. (Yos. 23:14) Kwa kweli, Yehova anatamani kuwafufua waliokufa. Kwa nini tunaweza kusema hivyo?

6 Fikiria maneno ambayo Ayubu alisema. Alikuwa na uhakika kwamba hata akifa, Yehova angekuwa na hamu kubwa ya kumwona akiishi tena. (Ayu. 14:14, 15, maelezo ya chini) Bado Yehova anahisi hivyo kuelekea waabudu wake wote waliokufa. Anatamani kuwafufua, wakiwa na afya nzuri na furaha. Namna gani mabilioni ya watu ambao walikufa bila kupata nafasi ya kujifunza ukweli kumhusu Yehova? Mungu wetu mwenye upendo anataka kuwafufua pia. (Mdo. 24:15) Anataka wawe na nafasi ya kuwa rafiki zake na kuishi milele duniani. (Yoh. 3:16) Ni wazi kwamba Yehova anatamani kuwafufua wafu.

7-8. Nĩkĩ tũmba kwĩthĩrwa na ũmma atĩ Jehova arĩna inya ya kũriũkia akuũ?

7 Je, Yehova ana nguvu pia za kuwafufua waliokufa? Bila shaka! Yeye ni “Mweza-Yote.” (Ufu. 1:8) Basi ana nguvu za kutosha kumshinda adui yeyote, kutia ndani kifo. (1 Kor. 15:26) Tunaimarishwa na kufarijiwa kwa kujua jambo hilo. Fikiria jambo ambalo Dada Emma Arnold alijionea. Yeye na familia yake walikabili majaribu makali ya imani wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu. Walipofiwa na wapendwa wao katika kambi za mateso za Wanazi, Emma alisema hivi ili kumfariji binti yake: “Ikiwa kifo kingewaweka wanadamu katika kifungo milele, basi kingekuwa na nguvu kuliko Mungu, sivyo?” Kwa kweli, Yehova ana nguvu kuliko vitu vyote! Mungu Mweza-Yote aliyeumba uhai ana uwezo wa kuwarudishia uhai wale waliokufa.

8 Sababu nyingine inayotusaidia kujua kwamba Yehova ana uwezo wa kuwafufua waliokufa ni kwamba kumbukumbu yake haina mipaka. Anaita kila nyota kwa jina. (Isa. 40:26) Pia, anawakumbuka wale waliokufa. (Ayu. 14:13; Luka 20:37, 38) Anaweza kukumbuka habari zote kuhusu wale atakaowafufua, kutia ndani mwonekano wao, utu wao, mambo waliyojionea maishani, na kumbukumbu zao.

9. Nĩkĩ wĩtĩkĩtie wĩrane bwa Jehova bwa ĩgiita rĩĩjĩte bwegie kũriũkia antũ?

9 Ni wazi kwamba tunaweza kuamini ahadi ya Yehova kuhusu ufufuo wa wakati ujao kwa sababu tunajua anatamani na ana nguvu za kuitimiza. Fikiria sababu nyingine ya kuamini ahadi ya Mungu ya ufufuo: Tayari Yehova amefanya hivyo. Katika nyakati za Biblia, aliwawezesha wanaume wachache waaminifu, kutia ndani Yesu, wawafufue wafu. Acheni tuchunguze simulizi moja la ufufuo ambao Yesu alifanya, linalopatikana kwenye Yohana sura ya 11.

JESŨ GŨKUĨRWA NĨ MŨCOORE ENDETE

10. Nĩ ũntũ bũrĩkũ bwaumĩĩre rĩrĩa Jesũ aatũmagĩĩria rwongo rwa Bethania, na aathithĩrie atĩa? (Johana 11:1-3)

10 Soma Yohana 11:1-3. Wazia hali ilivyokuwa huko Bethania mwishoni mwa mwaka wa 32 W.K. Yesu alikuwa na marafiki wa karibu katika kijiji hicho—Lazaro na dada zake wawili, Maria na Martha. (Luka 10:38-42) Lakini Lazaro akapatwa na ugonjwa, na dada zake wakawa na wasiwasi. Walituma ujumbe kwa Yesu, ambaye alikuwa ng’ambo ya Yordani, mwendo wa siku mbili hivi kutoka Bethania. (Yoh. 10:40) Kwa kusikitisha, Lazaro alikufa karibu na wakati ambao wajumbe walifika mahali ambako Yesu alikuwa. Ingawa Yesu alijua kwamba rafiki yake amekufa, alibaki mahali alipokuwa kwa siku mbili zaidi, kisha akaanza safari ya kwenda Bethania. Basi, wakati ambao Yesu aliwasili, Lazaro alikuwa amekufa kwa siku nne. Yesu alikusudia kufanya jambo ambalo lingewanufaisha rafiki zake na kumtukuza Mungu.—Yoh. 11:4, 6, 11, 17.

11. Nĩ kĩthoomo kĩrĩkũ kĩegie ũcoore tũmba kwiritana kuumania na rũgono rũrũ?

11 Tunajifunza somo kuhusu urafiki kutokana na simulizi hilo. Fikiria jambo hili: Maria na Martha walipotuma ujumbe kwa Yesu, hawakumwomba aje Bethania. Walisema tu kwamba rafiki yake mpendwa alikuwa mgonjwa. (Yoh. 11:3) Lazaro alipokufa, Yesu angeweza kumfufua hata akiwa mbali. Ingawa hivyo, Yesu aliamua kwenda Bethania ili awe pamoja na rafiki zake, Maria na Martha. Je, una rafiki anayeweza kukusaidia bila kumwomba msaada? Basi, unajua kwamba unaweza kumtegemea akusaidie “nyakati za taabu.” (Met. 17:17) Kama Yesu, acheni tuwe rafiki kama huyo kwa wengine! Sasa turudi kwenye simulizi hilo na tuone jambo lililofuata.

12. Nĩ wĩrane bũrĩkũ Jesũ aaere Martha, na nĩkĩ bwarĩ bwa kwĩrĩgĩrĩka? (Johana 11:23-26)

12 Soma Yohana 11:23-26. Martha anapata habari kwamba Yesu anakaribia Bethania. Anaenda haraka kukutana naye na anamwambia hivi: “Bwana, kama ungekuwa hapa ndugu yangu hangekufa.” (Yoh. 11:21) Ukweli ni kwamba angeweza kumponya Lazaro. Lakini Yesu alikusudia kufanya jambo lenye kustaajabisha hata zaidi. Alimwahidi hivi: “Ndugu yako atafufuka.” Pia, alimpa Martha sababu nyingine ya kuamini ahadi yake, kwa kusema: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.” Naam, Mungu alikuwa amempa Yesu nguvu za kuwafufua wafu. Hapo awali, alikuwa amemfufua msichana mdogo muda mfupi baada ya kufa na pia alikuwa amemfufua mwanamume kijana, inaelekea siku ileile ambayo kijana huyo alikufa. (Luka 7:11-15; 8:49-55) Lakini je, angeweza kumfufua mtu ambaye alikuwa amekufa kwa siku nne na ambaye mwili wake ulikuwa umeanza kuharibika?

“LAZARO, UMA!”

Yesu aliwahurumia sana rafiki zake waliokuwa wakiomboleza (Tazama fungu la 13 na 14)

13. O ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ Johana 11:32-35, Jesũ aathithĩrie atĩa arĩkwona Maria na antũ bangĩ bakĩrĩra? (Tega kinya mbica.)

13 Soma Yohana 11:32-35. Wazia jambo lililofuata. Maria, yule dada mwingine wa Lazaro, alienda kukutana na Yesu. Alirudia maneno ambayo dada yake alikuwa amesema: “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.” Yeye na watu wengine waliokuwa pamoja naye walikuwa wamehuzunika sana. Yesu alipoona na kusikia wakilia, naye pia alihuzunika sana. Akichochewa na huruma nyororo kuelekea rafiki zake, Yesu alitokwa na machozi. Anaelewa jinsi tunavyoumia sana tunapofiwa na mpendwa wetu. Kwa kweli, alitamani kuwaondolea jambo lililowaletea machozi!

14. Nĩmbi tũmba kwiritana biegie Jehova, kuumania na ũrĩa Jesũ aathithĩĩrie Maria arĩkwona akĩrĩra?

14 Kutokana na jinsi Yesu alivyotenda alipomwona Maria akilia tunajifunza kwamba Mungu ni mwenye huruma nyororo. Kwa nini tunaweza kusema hivyo? Kama tulivyoona kwenye makala iliyotangulia, Yesu anaonyesha kikamilifu njia ya kufikiri na hisia za Baba yake. (Yoh. 12:45) Basi, tunaposoma kwamba Yesu alihisi huruma nyingi sana kuelekea rafiki zake waliokuwa wakiomboleza hivi kwamba akalia, tunaweza kufikia mkataa kwamba Yehova pia anatusikitikia sana anapoona machozi yetu ya huzuni. (Zab. 56:8) Je, hilo halikuchochei utamani kumkaribia zaidi Mungu wetu mwenye huruma nyororo?

Yesu alionyesha kwamba ana nguvu za kuwafufua wafu (Tazama fungu la 15 na 16)

15. O ta ũrĩa gũtarĩrĩĩtue kĩrĩ Johana 11:41-44, nĩatĩa gwakarĩkĩre mbĩrĩrene ya Lazaro? (Tega kinya mbica.)

15 Soma Yohana 11:41-44. Yesu alipofika kwenye kaburi la Lazaro aliagiza jiwe liondolewe. Martha alipinga jambo hilo, akisema kwamba kufikia wakati huo lazima mwili ulikuwa unanuka. Yesu akajibu hivi: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?” (Yoh. 11:39, 40) Kisha Yesu akatazama mbinguni na kusali hadharani. Alitaka kumpa Yehova utukufu kwa jambo ambalo lingefuata. Yesu akaita hivi kwa sauti kubwa: “Lazaro, njoo huku nje!” Na Lazaro akatoka kwenye kaburi! Yesu alifanya jambo ambalo wengine walifikiri haliwezekani.—Tazama makala “Kwa nini ilimchukua Yesu siku nne ili kufika kwenye kaburi la Lazaro?” kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2008.

16. Nĩatĩa rũgono rũrĩa rũrĩ kĩrĩ Johana Mũrango jwa 11 rũgwĩkĩra wĩtĩkio bwetũ inya kĩrĩ wĩrĩgĩĩro bwa kũriũkua?

16 Simulizi lililo kwenye Yohana sura ya 11 linaimarisha imani yetu katika tumaini la ufufuo. Jinsi gani? Kumbuka ahadi ambayo Yesu alimpa Martha: “Ndugu yako atafufuka.” (Yoh. 11:23) Kama Baba yake, Yesu anatamani na ana nguvu za kutimiza ahadi hiyo. Machozi yake yanafunua kwamba anatamani sana kuondoa kifo na huzuni inayosababishwa na kifo. Na Lazaro alipotoka kwenye kaburi, Yesu alithibitisha tena kwamba ana nguvu za kuwafufua wafu. Pia, fikiria jambo ambalo Yesu alimkumbusha Martha: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?” (Yoh. 11:40) Tuna sababu nzuri za kuamini kwamba ahadi ya Mungu ya ufufuo itatimia. Hata hivyo, tunaweza kufanya nini ili tumaini hilo liwe halisi zaidi kwetu?

ŨRĨA TŨMBA KWONANIA BURU TŨTĨNA NKANJA ATĨ ANTŨ BAKARIŨKUA

17. Nĩmbi tũbuĩrĩte kũriikana rĩrĩa tũkũthooma ngono cia Bibiria ciegie kũriũka?

17 Soma na utafakari kuhusu ufufuo wa wakati uliopita. Katika Biblia kuna masimulizi ya watu wanane waliofufuliwa. c Kwa nini usichunguze kwa makini kila simulizi? Unapofanya hivyo, kumbuka kwamba walikuwa watu halisi—wanaume, wanawake, na watoto. Tafuta masomo unayoweza kujifunza. Fikiria jinsi kila mfano unavyoonyesha kwamba Mungu anatamani na ana nguvu za kuwafufua wafu. Zaidi ya yote, tafakari kuhusu ufufuo muhimu zaidi—ufufuo wa Yesu. Kumbuka kwamba ufufuo wake ulithibitishwa na mamia ya watu na unatupatia msingi thabiti wa imani yetu.—1 Kor. 15:3-6, 20-22.

18. Nĩatĩa ũũmba gũtumĩra bwega ndwĩmbo cietũ ciegie wĩrĩgĩĩro bwa kũriũkua? (Tega kinya nteto gaiti.)

18 Sikiliza “nyimbo za kiroho” zinazotaja tumaini la ufufuo. d (Efe. 5:19) Nyimbo hizo zinafanya ufufuo uwe halisi zaidi kwetu na zinaimarisha imani yetu katika tumaini hilo lenye thamani. Sikiliza nyimbo hizo, fanyeni mazoezi ya kuimba, na mzungumzie maana ya maneno yake wakati wa ibada yenu ya familia. Kariri maneno ya nyimbo hizo katika akili na moyo wako. Kisha utakapokabili jaribu linalohatarisha uhai au kufiwa na mpendwa wako, roho ya Yehova itakusaidia kukumbuka nyimbo hizo, nawe utapata faraja na nguvu kutokana nazo.

19. Nĩmbi tũmba kũthũgaanĩria biegie kũrĩũkua? (Tega kathanduku “ Wenda Kũbooria Atĩa?”)

19 Tumia uwezo wako wa kuwazia. Yehova ametupatia uwezo wa kujiwazia tukiwa kwenye ulimwengu mpya. Dada mmoja anaeleza hivi: “Nimetumia muda mwingi sana kujiwazia nikiwa kwenye ulimwengu mpya hivi kwamba ni kama ninanusa harufu ya maua ya waridi yakichanua katika paradiso.” Wazia ukikutana na wanaume na wanawake waaminifu wanaotajwa katika Biblia. Unatazamia kukutana na nani? Utamuuliza maswali gani mtu huyo? Pia, wazia ukikutana na wapendwa wako waliokufa. Fikiria mambo yatakavyokuwa mtakapokutana—maneno ya kwanza mtakayozungumza, jinsi mtakavyokumbatiana kwa uchangamfu, na machozi yenu ya shangwe.

20. Ĩtua rĩetũ rĩbuĩrĩte kwĩthĩrwa rĩrĩ rĩrĩkũ?

20 Tunamshukuru sana Yehova kwa ahadi ya ufufuo. Tunaweza kuwa na uhakika kwamba ahadi hiyo itatimizwa, kwa kuwa Yehova anatamani na ana nguvu za kuitimiza. Acheni tuendelee kuimarisha imani yetu katika tumaini hilo lenye thamani. Tukifanya hivyo, tutaendelea kumkaribia zaidi Mungu ambaye ni kana kwamba anamwahidi kila mmoja wetu hivi, ‘Wapendwa wako watafufuka!’

RWĨMBO 147 Uzima wa Milele Umeahidiwa

a Ikiwa umempoteza mpendwa wako katika kifo, bila shaka ahadi ya ufufuo inakufariji sana. Hata hivyo, unawezaje kuwaeleza wengine sababu ya kuamini ahadi hiyo? Na unawezaje kufanya tumaini la ufufuo liwe halisi zaidi kwako? Kusudi la makala hii ni kutusaidia sisi sote tuimarishe imani yetu katika tumaini la ufufuo.

b Video hiyo ya muziki yenye kichwa Paradiso Ipo Karibu Sana ilikuwa katika programu ya Novemba 2016 kwenye JW Broadcasting.

c Tazama sanduku “Masimulizi Nane ya Ufufuo Yanayotajwa Katika Biblia” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1, 2015, uku. 4)

d Tazama nyimbo zifuatazo katika kitabu ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’: “Wazia Wakati Vitu Vyote Vitakuwa Vipya” (Wimbo 139), “Kaza Macho Kwenye Zawadi!” (Wimbo 144), na “Ataita” (Wimbo 151). Pia, tazama kwenye jw.org nyimbo zilizotungwa “Paradiso Ipo Karibu Sana,” “Ulimwengu Mpya,” na “Utaona.”