Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 1

Borera na Wĩrĩgĩĩre Jehova

Borera na Wĩrĩgĩĩre Jehova

ĨANDĨKO RĨETU RĨA MWAKA JWA 2021: “Bwaborera na bwatua kwirigagiira, nirio bukagita inya.”​—ISA. 30:15.

RWĨMBO 3 Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

MUHTASARI *

1. O ta Mũnene Daudi, nĩatĩa bamwe beetũ boomba kũũria?

SOTE tungependa kuwa na maisha matulivu na yenye amani. Hakuna yeyote kati yetu anayefurahia kuwa na mahangaiko au wasiwasi. Hata hivyo, huenda nyakati nyingine tukahangaishwa na wasiwasi. Isitoshe, huenda baadhi ya watumishi wa Yehova wakauliza swali ambalo Mfalme Daudi alimuuliza Yehova: “Nitahangaika kwa wasiwasi mpaka lini, nikiwa na huzuni moyoni mwangu kila siku?”—Zab. 13:2.

2. Kĩthoomone gĩkĩ nĩmbi tũkaarĩĩria?

2 Ingawa hatuwezi kuepuka kabisa kuishi bila kuwa na mahangaiko au wasiwasi wowote, kuna mengi tunayoweza kufanya ili kudhibiti hisia hizo. Katika makala hii, kwanza, tutazungumzia baadhi ya mambo yanayoweza kutusababishia mahangaiko. Kisha, tutazungumzia njia sita hususa zinazoweza kutusaidia kuendelea kuwa watulivu tunapokabiliana na matatizo yetu.

MANTŨ JATANTATŨ JARĨA JAGATŨTETHIA KWĨTHĨRWA NA ŨBORERU

3. Nĩ mantũ jarĩkũ joomba gũtũnogia, na twomba kũjathiria?

3 Huenda tusiweze kudhibiti au kuzuia baadhi ya mambo yanayoweza kutusababishia mahangaiko. Kwa mfano, hatuwezi kudhibiti ni kwa kiwango gani bei ya chakula, mavazi, na malazi itapanda kila mwaka; wala hatuwezi kudhibiti ni kwa kadiri gani wafanyakazi au wanafunzi wenzetu watajaribu kutushawishi ili tusiwe waaminifu au tufanye uasherati. Na hatuwezi kuzuia uhalifu katika ujirani wetu. Tunakabili changamoto hizo kwa sababu tunaishi katika ulimwengu ambao njia ya kufikiri ya watu wengi haitegemei kanuni za Biblia. Shetani, mungu wa ulimwengu huu, anajua kwamba baadhi ya watu wataruhusu “mahangaiko ya mfumo huu wa mambo” yawazuie kumtumikia Yehova. (Mt. 13:22; 1 Yoh. 5:19) Haishangazi kwamba ulimwengu umejaa matatizo yanayofanya watu wawe na mahangaiko!

4. Tũũmba kũthithia atĩa rĩrĩa tũrĩ na mĩnoga ĩmĩritũ?

4 Tunapokabiliana na matatizo makubwa maishani, huenda tukalemewa sana na mahangaiko hivi kwamba tukashindwa kufikiria jambo lingine lolote. Kwa mfano, huenda tukawa na wasiwasi kwamba hatutafanikiwa kupata pesa za kutosha kwa ajili ya mahitaji yetu, au kwamba tutakuwa wagonjwa na kushindwa kufika kazini, au hata kupoteza kazi yetu. Huenda pia tukawa na wasiwasi kwamba tutakosa kuwa waaminifu tunaposhawishiwa kuvunja sheria ya Mungu. Hivi karibuni, Shetani atawachochea wale anaowaongoza wawashambulie watu wa Mungu, hivyo huenda tukawa na wasiwasi kuhusu jinsi tutakavyotenda tutakaposhambuliwa. Huenda tukajiuliza hivi: ‘Je, ni vibaya kuwa na mahangaiko kwa kadiri fulani kuhusu mambo hayo?’

5. Nĩatĩa Jesũ augaga rĩrĩa augĩre: “Tigageni kwithangikia”?

5 Tunajua kwamba Yesu aliwaambia hivi wafuasi wake: ‘Acheni kuhangaika.’ (Mt. 6:25) Je, hilo linamaanisha kwamba anatarajia tusiwe na mahangaiko yoyote? La hasha! Isitoshe, nyakati zilizopita baadhi ya watumishi washikamanifu wa Yehova walihangaishwa na wasiwasi, lakini hawakupoteza kibali cha Yehova. * (1 Fal. 19:4; Zab. 6:3) Ukweli ni kwamba Yesu alikuwa akitutia moyo. Asingependa tulemewe sana na mahangaiko ya maisha hivi kwamba utumishi wetu kwa Mungu uathiriwe. Basi, ni mambo gani yanayoweza kutusaidia kudhibiti hisia zinazosababishwa na mahangaiko?—Tazama sanduku “Mambo ya Kufanya.”

MANTŨ JATANTATŨ JARĨA JAGATŨTETHIA KWĨTHĨRWA NA ŨBORERU

Tazama fungu la 6 *

6. Nĩmbi yũmba kũboreeria mĩthangĩko yetũ kũringana na Afilipi 4:6, 7?

6 (1) Sali mara kwa mara. Wakristo walio chini ya mkazo wanaweza kupata utulivu wanaposali kwa Yehova kutoka moyoni. (1 Pet. 5:7) Yehova anaweza kujibu sala zako kwa kukupa “amani ya Mungu inayozidi uelewaji wote” wa mwanadamu. (Soma Wafilipi 4:6, 7.) Yehova hutuliza mawazo yetu yanayotuhangaisha kupitia roho yake takatifu yenye nguvu.—Gal. 5:22.

7. Nĩ ũntũ bũrĩkũ tũbuĩrĩte kũmenya rĩrĩa tũkũromba Mũrungu?

7 Unaposali kwa Yehova mmiminie moyo wako. Mweleze mambo hususa. Mweleze tatizo ulilo nalo, na mfafanulie jinsi unavyohisi kulihusu. Ikiwa tatizo lako linaweza kusuluhishwa, mwombe hekima ya kupata suluhisho hilo na nguvu za kulitekeleza. Ikiwa huwezi kutatua tatizo hilo, mwombe Yehova akusaidie usiwe na mahangaiko kupita kiasi kuhusu tatizo lako. Unapotaja mambo hususa kwenye sala zako, mwishowe utaweza kuona waziwazi jinsi Yehova anavyozijibu. Ikiwa sala yako haitajibiwa mara tu baada ya kusali, usife moyo. Yehova hataki tu utaje mambo hususa katika sala, bali pia anataka uendelee kusali bila kuacha.—Luka 11:8-10.

8. Nĩ mantũ jarĩkũ tũbuĩrĩte kũgweta marombene jeetũ?

8 Unapomtupia Yehova mahangaiko yako katika sala, hakikisha pia unatia ndani maneno ya shukrani. Ni vema kuhesabu baraka zetu, hata tunapokuwa tukipitia hali ngumu sana. Ikiwa nyakati nyingine unashindwa kupata maneno yanayofaa ya kuelezea hisia zako za ndani, kumbuka kwamba Yehova anaweza kujibu hata sala fupi kama vile, “Tafadhali nisaidie!”—2 Nya. 18:31; Rom. 8:26.

Tazama fungu la 9 *

9. Ũkaria bwa mma bũũmba kwonekana atĩa?

9 (2) Tegemea hekima ya Yehova, si ya kwako. Katika karne ya nane K.W.K., watu wa Yuda walikuwa na wasiwasi kwamba wangeshambuliwa na Waashuru. Hivyo, waliomba msaada kutoka kwa taifa la kipagani la Misri ili waepuke kuwa chini ya utawala wa Waashuru. (Isa. 30:1, 2) Yehova aliwaonya kwamba kuwategemea Wamisri kungewaletea matatizo makubwa. (Isa. 30:7, 12, 13) Kupitia nabii Isaya, Yehova aliwaambia watu hao jinsi ambavyo wangeweza kupata usalama wa kweli. Alisema hivi: “Mtakuwa na nguvu mkiendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini” katika Yehova.—Isa. 30:15b.

10. Nĩ ta magiitene jarĩkũ tũũmba kwonania nĩtũkwĩrĩgĩĩra Jehova?

10 Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunamtumaini Yehova? Fikiria mifano ifuatayo. Tuseme umepata kazi yenye mshahara mkubwa zaidi ambayo itachukua muda wako mwingi na kuingilia ratiba yako ya kiroho. Au tuseme mfanyakazi mwenzako anakuonyesha kwamba anavutiwa na wewe kimahaba, lakini mtu huyo si mtumishi wa Mungu aliyebatizwa. Au wazia kwamba mtu wa familia yako unayempenda anakuambia hivi: “Chagua moja, mimi au huyo Mungu wako.” Katika kila moja ya visa hivyo, utakuwa na uamuzi mgumu wa kufanya, lakini Yehova atakupatia mwongozo unaohitaji kushughulikia kila moja ya hali hizo. (Mt. 6:33; 10:37; 1 Kor. 7:39) Swali ni; Je, utautumaini mwongozo huo hivi kwamba utakuwa tayari kuutumia?

Tazama fungu la 11 *

11. Nĩ Maandĩko jarĩkũ tũũmba kũthooma kenda tũboreera rĩrĩa tũkũthangĩkua?

11 (3) Jifunze kutokana na mifano mizuri na mibaya. Biblia ina mifano mingi inayokazia umuhimu wa kuendelea kuwa watulivu na kumtumaini Yehova. Unapochunguza masimulizi hayo, jitahidi kutambua kile kilichowasaidia watumishi wa Mungu waendelee kuwa watulivu walipokabili upinzani mkali. Kwa mfano, mahakama kuu ya Wayahudi ilipowaamuru mitume waache kuhubiri, mitume hao hawakuogopa. Badala yake, walisema hivi kwa ujasiri: “Lazima tumtii Mungu kuwa mtawala badala ya wanadamu.” (Mdo. 5:29) Hata baada ya kupigwa viboko, mitume hawakuogopa. Kwa nini? Kwa sababu walijua kwamba Yehova alikuwa upande wao. Alipendezwa nao. Hivyo, waliendelea kuhubiri habari njema. (Mdo. 5:40-42) Vivyo hivyo, mwanafunzi Stefano alipokabili kifo, aliendelea kuwa mwenye amani na mtulivu sana hivi kwamba uso wake ulionekana “kama uso wa malaika.” (Mdo. 6:12-15) Kwa nini? Kwa sababu alikuwa na uhakika kwamba alikuwa na kibali cha Yehova.

12. Kũringana na 1 Petero 3:14 na 4:14, nĩkĩ tũũmba kwĩthĩrwa na kũgwĩrua rĩrĩa tũkũtha- ngĩkua?

12 Mitume walikuwa na uthibitisho ulio wazi kwamba Yehova alikuwa pamoja nao. Alikuwa amewapa nguvu za kufanya miujiza. (Mdo. 5:12-16; 6:8) Leo, hatuna uwezo wa kufanya miujiza. Hata hivyo, kupitia Neno lake, Yehova anatuhakikishia kwa upendo kwamba tunapoteseka kwa ajili ya uadilifu, anapendezwa nasi na roho yake iko pamoja nasi. (Soma 1 Petro 3:14; 4:14.) Hivyo, badala ya kukazia fikira jinsi tutakavyotenda tutakapoteswa vikali wakati ujao, tunahitaji kukazia fikira mambo tunayoweza kufanya sasa ili kuimarisha uhakika wetu katika uwezo wa Yehova wa kututegemeza na kutuokoa. Kama tu wanafunzi hao wa mapema walivyofanya, ni lazima sisi pia tutumaini ahadi hii ya Yesu: “Nitawapa maneno na hekima, ambayo wapinzani wenu wote kwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.” Yesu anatupatia uhakika huu: “Mkivumilia, mtauokoa uhai wenu.” (Luka 21:12-19) Na usisahau kamwe kwamba Yehova anakumbuka hata jambo dogo zaidi kuhusu watumishi wake wanaokufa wakiwa waaminifu kwake. Naye atatumia ujuzi huo kuwafufua.

13. Tũũmba kũgunĩka atĩa twathooma mantũ jarĩa joonetwe ja barĩa baaremerwe nĩ kũboreera na kwĩrĩgĩĩra Jehova?

13 Pia, tunaweza kujifunza kutokana na mifano ya wale ambao walishindwa kuendelea kuwa watulivu na kumtumaini Yehova. Kuchunguza mifano hiyo mibaya kutatusaidia tuepuke kufanya makosa yaleyale waliyofanya. Kwa mfano, mwanzoni mwa utawala wake, Mfalme Asa wa Yuda alimtegemea Yehova wakati jeshi kubwa lilipokuja kupigana naye, na Yehova alimbariki kwa kumpa ushindi. (2 Nya. 14:9-12) Hata hivyo, baadaye, wakati jeshi dogo zaidi la Mfalme Baasha wa Israeli lilipokuja dhiki yake, Asa aliwalipa Wasiria ili kupata msaada wa kijeshi badala ya kutegemea ukombozi wa Yehova, kama alivyokuwa amefanya wakati uliopita. (2 Nya. 16:1-3) Na alipopata ugonjwa mbaya sana karibu na mwishoni mwa maisha yake, hakumtegemea Yehova ili amsaidie.—2 Nya. 16:12.

14. Nĩ ũntũ bũrĩkũ tũũmba kwiritana kũmania na maatia ja Asa?

14 Mwanzoni, Asa alimtegemea Yehova alipopata matatizo. Lakini baadaye hakumgeukia Mungu ili kupata msaada, akajaribu kushughulikia matatizo aliyokabili kwa njia yake mwenyewe. Kwa mtazamo wa kijuu-juu, mpango wa Asa wa kuwageukia Wasiria ili kupata msaada dhidi ya Waisraeli huenda ulionekana unafaa. Lakini mafanikio ya Asa yalikuwa ya muda mfupi. Yehova alimwambia hivi kupitia nabii fulani: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Siria nawe hukumtegemea Yehova Mungu wako, jeshi la mfalme wa Siria limeponyoka kutoka mikononi mwako.” (2 Nya. 16:7) Ni lazima tuwe waangalifu tusijiamini kupita kiasi na kushughulikia mambo kwa njia yetu wenyewe hivi kwamba tunashindwa kutafuta mwongozo wa Yehova kupitia Neno lake. Hata tunapokabili hali ya dharura, tunapaswa kuwa watulivu na kumtegemea Yehova, naye atatusaidia ili tufanikiwe.

Tazama fungu la 15 *

15. Nĩ atĩa tũũmba kũthithia rĩrĩa tũkũthooma Bibiria?

15 (4) Kariri mistari ya Biblia. Unapopata mistari ya Biblia inayoonyesha kwamba tunaweza kupata nguvu kwa kuendelea kuwa watulivu na kumtumaini Yehova, jitahidi kukariri mistari hiyo. Ili uweze kukumbuka mistari hiyo, huenda ikafaa kuisoma kwa sauti au kuiandika na kuipitia mara kwa mara. Yoshua aliagizwa asome kitabu cha Sheria kwa ukawaida kwa sauti ya chini ili aweze kutenda kwa hekima. Pia, vikumbusho hivyo vingemsaidia kushinda woga ambao huenda angehisi alipokuwa akiwaongoza watu wa Mungu. (Yos. 1:8, 9) Mistari mingi inayopatikana katika Neno la Mungu inaweza kukupatia amani ya akili na moyoni katika hali ambazo kwa kawaida zingesababisha uwe na wasiwasi au hofu.—Zab. 27:1-3; Met. 3:25, 26.

Tazama fungu la 16 *

16. Jehova oomba gũtumĩra atĩa kĩũthũrano gũtũtetheeria kũborera na kũmwĩrĩgĩĩra?

16 (5) Shirikiana na watu wa Mungu. Yehova anawatumia ndugu na dada zetu ili kutusaidia tuendelee kuwa watulivu na kumtumaini yeye. Tunapokuwa kwenye mikutano, tunanufaika na mafundisho yanayotolewa jukwaani, maelezo yanayotolewa na waliohudhuria, na mazungumzo yenye kujenga pamoja na ndugu na dada zetu. (Ebr. 10:24, 25) Pia, tunaweza kutiwa moyo sana tunapowaeleza hisia zetu marafiki tunaowatumaini kutanikoni. “Neno jema” kutoka kwa rafiki linaweza kupunguza sana mahangaiko tuliyo nayo.—Met. 12:25.

Tazama fungu la 17 *

17. Kũringana na Ahibirania 6:19, nĩ atĩa wĩrĩgĩĩro bwetũ kĩrĩ ũnene bũtũejaga kũũmĩĩria kinya rĩrĩa kũrĩ na mathĩĩna?

17 (6) Imarisha tumaini lako. Tumaini letu la Ufalme ni “kama nanga ya nafsi,” inayotusaidia kuendelea kuwa imara licha ya changamoto tunazokabiliana nazo au mawazo yenye kuhangaisha. (Soma Waebrania 6:19.) Tafakari kuhusu ahadi za Yehova za wakati ujao ambapo hatutakuwa na mawazo yenye kuhangaisha. (Isa. 65:17) Jiwazie ukiwa katika ulimwengu mpya wenye amani ambamo hali zenye kusababisha mkazo hazitakuwapo tena. (Mika 4:4) Pia, unaweza kuimarisha tumaini lako kadiri unavyowaeleza wengine kuhusu tumaini hilo. Fanya yote uwezayo katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Ukifanya hivyo, unaweza “kuwa na uhakikisho kamili wa tumaini mpaka mwisho.”—Ebr. 6:11.

18. Nĩ mathĩĩna jarĩkũ tũũmba kwĩrĩgĩĩra magita jejĩĩte, na tũũmba kũũmbana atĩa?

18 Kadiri mfumo huu wa mambo unavyofikia mwisho wake, tutakabili changamoto nyingi hata zaidi zinazoweza kutuletea mawazo yenye kuhangaisha. Andiko letu la mwaka wa 2021 linaweza kutusaidia kukabiliana na changamoto hizo na kuendelea kuwa watulivu, si kwa nguvu zetu wenyewe, bali kwa kumtumaini Yehova. Hivyo, katika mwaka huu, acheni tuonyeshe kwa matendo yetu kwamba tuna imani katika ahadi hii ya Yehova: “Mtakuwa na nguvu mkiendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”Isa. 30:15.

RWĨMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Letu

^ gic. 5 Andiko la mwaka wa 2021 linakazia umuhimu wa kumtumaini Yehova tunapokabiliana na hali zinazotuletea mkazo sasa na wakati ujao. Makala hii itazungumzia njia hususa zitakazotusaidia kutumia shauri linalopatikana katika andiko letu la mwaka.

^ gic. 5 Baadhi ya ndugu na dada waaminifu wanasumbuliwa na ugonjwa wa kuwa na wasiwasi au woga uliopita kiasi. Ugonjwa huo ni tatizo kubwa la afya na si aina ya mahangaiko au wasiwasi ambao Yesu alikuwa akizungumzia.

^ gic. 63 MAELEZO YA PICHA: (1) Mara kadhaa kwa siku dada huyu anasali kwa bidii kuhusu mahangaiko yake.

^ gic. 65 MAELEZO YA PICHA: (2) Akiwa kazini wakati wa mapumziko, analichunguza Neno la Mungu ili kupata hekima.

^ gic. 67 MAELEZO YA PICHA: (3) Anatafakari kuhusu mifano mizuri na mibaya inayopatikana katika Biblia.

^ gic. 69 MAELEZO YA PICHA: (4) Anabandika kwenye friji yake andiko lenye kutia moyo analotaka kukariri.

^ gic. 71 MAELEZO YA PICHA: (5) Anafurahia ushirika mzuri akiwa katika huduma.

^ gic. 73 MAELEZO YA PICHA: (6) Anaimarisha tumaini lake kwa kutafakari kuhusu wakati ujao.